Thursday, August 24, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 29



ILIPOISHIA:
Nikiwa bado naendelea kuugulia, nilisikia ndugu yangu mmoja akiniita kutokea dirishani, nikafunua pazia na kuchungulia nje. Sikuyaamini macho yangu baada ya kumuona akiwa na yule msichana tuliyesafiri naye, harakaharaka nikafungua dirisha huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wangu.
SASA ENDELEA...
“Mambo Togo?”
“Safi, karibu,” nilisema huku nikitazama huku nakule. Yule ndugu yangu alikuwa amesimama pembeni akikutazama kwa zamuzamu.
“Samahani nina maongezi kidogo na wewe,” alisema. Kwa hali niliyokuwa nayo, nilikuwa nikifikiria jambo moja tu kutokakwake, mapenzi.
“Nisubiri kwa kule mbele,” nilimuelekeza huku harakaharaka nikitoka na kuelekea bafuni. Nilijimwagia maji ya baridi kwa wingi ili angalau nitulie kisha nikarudi chumbani na kuvaa nguo.
Nilijitazama tena kwenye kioo, bado nilikuwa na alama za kuvilia damu usoni lakini sikujali, akili yangu ilikuwa ikihitaji kitu kimoja tu kwa wakati huo. Nilitoka kimyakimya bila kumuaga mtu yeyote mpaka nje.
Nikamfuata yule ndugu yangu na kumwambia kwamba iwe siri yetu nitampa zawadi, nikamsisitiza kwamba asimwambie mtu yeyote. Alikubali, nikamshukuru nakumfuata yule msichana ambaye alionesha kuwa na shauku kubwa ya kuonana na mimi.
Tulitoka mpaka nje kabisa, sehemu ambayo mtu yeyote aliyekuwa ndani asingeweza kutuona, akanikumbatia kwa nguvu na kunibusu shingoni. Nilijikuta nikisisimka mno, nikawa nachekacheka tu mwenyewe.
Aliniambia kuna mahali anataka rtwende pamoja kwa sababu alikuwa na jambo muhimu lililokuwa likimsumbua ndani ya moyo wake. Nilimuuliza amepata wapi ujasiri wa kuingia mpaka kule ndani? Akaniambia ilikuwa ni muhimu sana kuonana na mimi na ndiyo maana hakujali chochote.

“Huwa unakunywa pombe?” aliniuliza, nikatingisha kichwa kumkatalia. Licha ya kujaribu mara kadhaa kunywa pombe za kienyeji tukiwa Chunya, kiukweli kichwa changu kilikuwa kibovu sana, kiufupi sikuwa na uwezo wa kuhimili pombe. Akacheka sana huku mara kwa mara akinipigapiga begani.
“Chagua sehemu ambayo unadhani inaweza kufaa kwa mazungumzo ya mimi na wewe, twende beach, Mlimani City au tutafute ‘lodge’ yoyote nzuri,” aliniuliza l;akini kati ya sehemu zote alizozitaja, ni moja tu ndiyo niliyokuwa naelewa, beach. Sikuwa najua Mlimani City ndiyo wapi na kupoje wala sikuwa najua huko ‘lodge’ ni wapi na kuna nini cha muhimu. Waliosema ushamba mzigo, hawakukosea.
Ilibidi nimuulize ili anipe ufafanuzi, akacheka sana, akaniambia Mlimani City ni kituo maalum cha kibiashara, mahali ambapo kuna maduka makubwa, mabenki, migahawa ya kisasa ya sehemu mbalimbali za starehe. Akaniambia pia kuwa neno lodge ni la Kiingereza lakini linamaanisha nyumba ya kulala wageni. Nikashtuka!
“Unamaanisha gesti?”
“Ndiyo?” alinijibu huku akinitazama kwa macho yake mazuri, ikabidi nijifanye sitaki nataka kwa sababu kule kwetu kulikuwa na stori kwamba watu wanaoingia gesti wakati hawapo safarini ni wale wahuni walioshindikana. Nikamwambia kwamba Mlimani City atanipeleka siku nyingine, akanitazama tena usoni na kuachia tabasamu pana.
Japo jibu langu halikuwa la moja kwa moja, nadhani alinielewa haraka nilikuwa namaanisha nini. Tuliingia kwenye Bajaj, nikageuka huku na kule na  nilipohakikisha hakuna aliyeniona, nilimpa ishara kwamba tuondoke.
Kwa makusudi kabisa, aliniegamia kimahaba huku mara kwa mara akiendelea kuniangushia mabusu ya hapa na pale. Yaani kama angekuwa anajua kilichokuwa ndani ya kichwa changu, kamwe asingethubutu kumwagia petroli kwenye moto.
Hatukwenda mbali sana, Bajaj ikaingia kwenye jengo moja la kisasa, getini likiwa na maandishi yaliyosomeka Sideview Hotel, tukashuka kwenye Bajaj, nikawa nashangaashangaa huku na kule, alinishika mkono bila hata wasiwasi, tukaingia mpaka ndani ambapo alimfuata dada wa mapokezi na kuanza kuzungumza naye.
Alimwambia anahitaji chumba kwa siku nzima mpaka kesho yake. Nilishangaa kwa nini anataka tukae mpaka kesho yake wakati anajua mimi ni mgeni na nilikuwa chini ya wazazi wangu. Hata hivyo, sikutaka kumhoji chochote mpaka nipate nilichokuwa nakitaka.
Alitoa pochi yake na kuhesabu fedha, akampa yule mhudumu, akatoka na funguo na kwenda kutuonesha chumba chenyewe. Kilikuwa chumba kizuri mno, yaani pengine kuliko vyumba vya kwenye majumba ya watu wengi sana. Picha niliyokuwa nimeijenga kichwani mwangu mwanzoni, nilitegemea chumba kitakuwa kama vile vya gesti za kijiji, kitanda kidogo chenye kunguni na kilicholegea, godoro chafu na jembamba sambamba na mashuka makuukuu.
Kitanda kilikuwa kikubwa, juu yake kikiwa kimetandikwa kwa mashuka meupe na mito mikubwa mizuri, chini kikiwa kimepigwa marumaru safi nyeupe, huku taa zenye mwanga fulani mzuri zikizidi kuyapendezesha mandhari ya chumba hicho, nikawa nashangaashangaa.
Sikuwa na habari kwamba mwenzangu bila hata kuzungumza kile alichosema tunataka kuzungumza, ameshaanza kufaanya kazi nyingine. Alikuwa tayari ameshavua blauzi yake na kubaki na bra, akawa anahaha kufungua suruali yake iliyokuwa imembanana kulichora vilivyo umbo lake. Nilijikuta nikitetemeka mwenyewe, hata sijui ni kwa nini, nikampa mgongo.
“Togo! Mimi mwenzio na...ku..pe...” alishindwa kumalizia alichotaka kukisema, akagusanisha mdomo wake na wangu huku mikono yake ikiwa imenibana kisawasawa kwenye kifua chake kilichosheheni. Kwa kuwa rahma alikuwa amenipa ‘twisheni’ ya mambo hayo, na mimi sikutaka kubaki nyuma, nilimpa ushirikiano, tukawa tunaelea kwenye ulimwengu tofauti kabisa.
Ile halai niliyokuwa naisikia mwanzo, safari hii ilizidi mno, yaani nikawa naona kama nachelewa. Tofauti na Rahma, huyu yeye hakuwa na aibu kabisa na kila alichokuwa anakifanya, alikuwa akifanya kwa kujiamini. Akaninyonyoa manyoya yote kama kuku aliyechinjwa huku na yeye akifanya hivyohivyo, muda mfupi baadaye, tukawa ‘saresare’ maua.
“Togoo!” aliniita kwa mshtuko huku akiwa amepigwa na butwaa iliyochanganyikana na furaha.
“Kumbe upo hivi,” alisema huku akinitazama kwa macho yake kama anasikia usingizi, sikuelewa kauli yake hiyo ilikuwa ikimaanisha nini, lakini aliendelea kunimwagia sifa lukuki kwamba siku ya kwanza aliponiona tu aligundua kwamba nina sifa za kipekee ambazo wanaume wengine hawana.
Sikutilia sana maanani kile alichokuwa anakisema, akili yangu ilikuwa ikiwaza jambo moja tu. Muda mfupi baadaye, tuliianza safari huku mimi nikiwa ndiyo kiongozi wa msafara. Unajua kama una kiu kali ya maji, hata ukipewa jagi zima unaweza kulifakamia lote mpaka liishe. Hicho ndicho kilichotokea kwangu.
Ghafla nilishangaa akianza kugeuza macho na kutupatupa mikono na miguu kama mtu anayetaka kukata roho, haraka nikashuka chini na kuanza kumtingisha kwa nguvu huku nikishindwa hata namna ya kumuita maana kiukweli sikuwa nalijua jina lake.
Kadiri nilivyokuwa namtingisha ndivyo alivyozidi kulegea, mara akatulia huku macho yake yakiwa yamegeuka na kutazama upande wa juu. Nilijaribu kusikiliza mapigo ya moyo wake lakini hayakuwa yakipiga na hakuwa akipumua.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikianza kutafuta nguo zangu, harakaharaka nikavaa huku kijasho chembamba kikinitoka, nikawa najiuliza nini cha kufanya maana tayari ulishakuwa msala. Hakuna ambaye angeamini kwamba msichana huyo amekufa mwenyewe, wangejua kwamba nimemuua, nilijikuta nikitetemeka mno.
Akili niliyoipata, ilikuwa ni kuondoka haraka hotelini hapo bila mtu yeyote kujua. Nilichukua shuka na kumfunika kisha nikafungua mlango. Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu, nilitoka na kuurudishia mlango, harakaharaka nikawa natembea kuelekea nje.
Kwa bahati nzuri, nilipofika pale mapokezi, yule dada hakuwepo, nikatoka kimyakimya mpaka nje, nikaelekea lilipo geti kubwa huku nikijitahidi kuvaa tabasamu la uongo ili walinzi wa hoteli hiyo wasishtukie chochote.
“Aroo! We kijana... Aroo wewe,” nilisikia sauti ya mlinzi wa nje ya geti la hoteli hiyo akiniita, moyo ukalipuka paah!
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...