Thursday, September 13, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 66


ILIPOISHIA:
Kazi iliyokuwa imesalia, ilikuwa ni kuvunja lile godauni kuangalia ndani kulikuwa na nini? Nilikuwa na shauku kubwa ya kujua kilichokuwemo mle ndani kwani kwa jinsi nilivyosikia stori za mzee huyo na mazingira ya ile ngome yake aliyokuwa akiishi, achilia mbali ulinzi wa hali ya juu, ilionesha ana mambo mengi sana maovu.
SASA ENDELEA...
Askari waliokuwa na silaha, walilizunguka godauni lote na wengine waliokuwa na vifaa maalum vya kuvunjia mageti, walisogelea geti hilo na kuseti mitambo yao, tayari kwa kazi. Kwa muda wote huo, yule mwandishi wa habari alikuwa bize kuhakikisha hakosi picha hata moja.
Alikuwa akichakarika kisawasawa, akawa anapiga picha za mnato na za video, kwa ajili ya kuwajuza wananchi juu ya kilichokuwa kinaendelea. Wakati askari hao wakijiandaa kuvunja godauni hilo, milio ya ving’ora vya magari mengi ya polisi vilisikika.
Kwa kuwa nilikuwa mwepesi, niliweza kupaa juu na kutazama upande wa kule barabarani, nikashtuka kuona magari mengi ya polisi, yakiwa naaskari wengi wenye silaha, yakija kwa kasi eneo lile. Nadhani awali Junaitha alipowapelekea taarifa juu ya oparesheni hiyo, walidhani ni tukio dogo tu lakini kilichotokea, kiliwafanya walipe tukio hilo uzito wa juu.
Binafsi hata sikuona umuhimu wa wao kufika muda huo kwa sababu tayari jeshi la mtu mmoja nilikuwa nimesafisha njia. Wale askari waliendelea na kazi yao na muda mfupi baadaye, walifanikiwa kuvunja geti hilo.

KIVURUGE WA TANDALE- 10


ILIPOISHIA
“Unanikaribishaje hivyo?” alisema huku akitanua mikono yake kama anayesema ‘njoo unikumbatie’. Basi na mimi nilifanya kama alivyotaka, nikaenda na kumkumbatia kwa nguvu, muda mfupi baadaye midomo yetu ilikuwa imegusana, hata sijui nini kilitokea, nilishtukia tu tayari tukiwa kwenye uwanja wa fundi seremala, mara mlango ukagongwa kwa nguvu.
“Ngo! Ngo! Ngooo!”
SASA ENDELEA...
“Nani tena huyo jamanii,” alisema Madam Bella huku akionesha kukasirishwa sana na kitendo cha mtu huyo kugonga. Niliamka, nikajifunga taulo na kusogea mlangoni, nikafungua kidogo na kuchungulia nje.
“Hivi unajua kwamba ni zamu yako kununua umeme?”
“Ooh! Kumbe zamu yangu imeshafika? Ok, naomba basi nikupe pesa umuagize hata mtoto akanunue.”
“Mtoto gani? Hakuna mtu hapa nyumbani, kama unavyojua wakienda shuleni nabaki peke yangu, hebui nenda kanunue kwa sababu utakatika sasa hivi, tafadhali tusije tukagombana bure,” mama mwenye nyumba alisema huku akiwa ameshika kiuno.
Haikuwa kawaida yake kuzungumza na mimi kwa namna hii, siku zote tulikuwa tukihheshimiana na kama kuna jambo lolote, alikuwa akiniambia kwa ustaarabu lakini siku hiyo alikuwa amebadilika.
Nilibamiza mlango na kurudi ndani, huku nikiwa nimepanda na jazba. Kwa alichokisema, maana yake alikuwa anataka niache kila nilichokuwa nakifanya eti nikanunue umeme, ambao kwanza hata haukuwa umekatika.
Kama hiyo haitoshi, asubuhi hiyo wakati naondoka aliniona sana lakini hakuniambia chochote kwa hiyo kama nisingerudi ingekuwaje? Niliona kama ameamua kunifanyia visa kwa makusudi ili kuniharibia mambo yangu.
“Vipi tena baba’angu,” alisema Madam Bella huku akinishika mkono kwa upole na kunirudisha uwanjani, nikamweleza kilichotokea.
“Usijali, kwani shilingi ngapi?”

Monday, September 3, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 65


ILIPOISHIA:
“Dont worry Jamal, each and everything is going to be okay!” (Usiwe na wasiwasi Jamal, kila kitu kitakuwa sawa) alisema Firyaal na kunisogelea, akanikumbatia na kunibusu mdomoni huku kila mtu akishuhudia. Sikujali, nilikuwa nampenda sana Firyaal na sikuwa tayari kuona jambo lolote baya linamtokea, hasa kabla ya mimi na yeye kukutana na kumaliza kile tulichokuwa tayari tumekianza.
SASA ENDELEA...

“Inabidi ubaki usaidiane na hawa askari, bado kuna kazi kubwa mbele yetu. Nakukumbusha tu kwamba huonekani na mtu yeyote kwa hiyo utakuwa na nafasi ya kuyafanya hata yale ambayo watu wa kawaida hawayawezi, ni lazima Loris akamatwe, umepigwa risasi na Firyaal naye amepigwa risasi, haiwezekani iwe ni kwa ajili ya kazi bure,” alisema Junaitha, sauti ambayo ilipenya vilivyo masikioni mwangu, akawa ni kama amezidi kuniongezea hasira.

Wale askari walipoingia, wengine ilibidi wabaki nje, wakatawanyika kule ndani kwa tahadhari kubwa na muda mfupi baaddaye, mvua nyingine ya risasi ikaanza kumwagika.
Nilishindwa kuelewa ni kwa sababu gani nyumba hiyo ilikuwa ikilindwa kiasi hicho, nikasikia sauti ya Junaitha masikioni mwangu akinielekeza kusonga mbele haraka mpaka pale walipokuwepo walinzi wengine waliokuwa wakifyatua risasi kwa kasi.

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 64


ILIPOISHIA:
“Tulia jamal, mbona una haraka, nimesema leo ndiyo leo na watu wote watatujua sisi ni akina nani. Shenaiza na Firyaal, naomba mkaze mioyo yenu maana kinachoenda kutokea kwa baba yenu siyo kizuri lakini lazima tufanye hivi,” alisema Junaitha, akawasha gari, tukaondoka huku ile difenda ikitufuata kwa nyuma.
SASA ENDELEA...
Msafara uliendelea na safari mpaka tulipofika Kurasini, tukakata kushoto na kuiacha barabara ya lami, nikaikumbuka vizuri njia hiyo kwani ndiyo tuliyopita siku ile tulipoenda nyumbani kwa akina Shenaiza.
Tulipoingia kwenye barabara hiyo, ile difenda iliyokuwa nyuma, ilituwashia taa, nikamuona Junaitha akipunguza mwendo na kupaki pembeni, ile difenda nayo ikapunguza mwendo na kusimama. Yule askari aliyekuwa na nyotanyota begani akamsogelea Junaitha.
“Kumbe mlikuwa mnamaanisha huyu mzee Loris?”
“Ndiyo, kwani maelezo yote si yanajitosheleza afande?”
“Ni hatari sana kwa kweli, hata sidhani kama itawezekana.”
“Kwani mheshimiwa, wananchi wanapoletamalalamiko kwenu, tena mazito kama haya, wakiwa na ushahidi wa kila kitu, ni nani anayeweza kuwasaidia kama siyo jeshi la polisi?”
“Wewe ni nani unayeuliza maswali ya namna hiyo? Isitoshe sizungumzi na wewe, naongea na huyu mama aliyeleta taarifa.”

KIVURUGE WA TANDALE- 9


ILIPOISHIA:
Madam Bella hakusema lolote zaidi ya kusimama, akawa anatutazama huku akionesha kushtuka sana kutokana na hali aliyotukuta maana Salma alikuwa amepeleka mkono wake shingoni kwangu kwa lengo la kunikagua ile aliyosema mwenyewe lipstiki, kwa hiyo mazingira yalionesha ni kama tulikuwa tumekumbatiana.
SASA ENDELEA...
“Yaani badala ya kufanya kazi iliyowaleta mna kazi ya kukumbatiana kwenye korido! Hivi mna akili kweli nyie?”
“Hapana Madam, nilikuwa namsaidia kumfuta madoa ya lipstiki kwenye shati lake, hebu angalia mwenyewe,” alisema Salma kwa namna ya kujihami sana.
“Lipstiki? Sasa lipstiki kwenye shati lake wewe inakuhusu nini?”
“Nisamehe Madam!”
“Ile cheki niliyokupa umeshaipeleka uhasibu?”
“Hapana bosi, ndiyo nilikuwa na...”
“Salma! Kuwa makini, kama kilichokuleta ni kazi, fanya kazi. Na wewe Ashrafu, unatakiwa kuheshimu kazi ninayokupa, yaani mimi nakutuma kitu halafu badala ya kwenda kufanya nilichokwambia unaanza kufanya mambo yako mengine.”
“Nisamehe bosi,” nilisema huku nikijitahidi kuvaa uso ambao hautamfanya Salma ashtukie chochote. Kweli hilo lilifanikiwa, Madam Bella alitoa amri ya kila mmoja kuendelea na kazi zake, harakaharaka Salma akapita mbiombio na kuelekea uhasibu na mimi nikaondoka haraka kuelekea ofisini kwangu.

KIVURUGE WA TANDALE- 8


ILIPOISHIA:
“Kumbe unajua kuimba vizuri hivyo, itabidi nikupeleke studio,” nilimchombeza, akacheka sana, tayari tulishafika maana konda alipaza sauti akisema hapo ndiyo mwisho wa gari, abiria wengine wakawa wanateremka lakini mimi nikajikuta nikipata uzito na kubaki nimekaa, naye hakuonesha kuwa na haraka sana, akawa amekaa akiwa ni kama anayenisubiri niinuke ili na yeye ainuke.
Ndani ya muda mfupi tu tayari tulishakuwa tumezoeana f’lani hivi, akili fulani ndani ya kichwa changu ikawa inaniambia ‘jaribu kutupia mistari’.
SASA ENDELEA...
“Twende basi tushuke jamani,” alisema huku akinigusa begani, nikamgeukia nakumtazama, safari hii tukiwa tumesogeleana sana maana alishaanza kuinuka.
“Mbona unaniangalia hivyo mpaka mwenzako najisikia aibu,” alisema huku akijichekesha, nikaona huo ndiyo muda mzuri wa kutekeleza kile ambacho akili yangu ilikuwa ikinituma sana.
“Wewe ni mzuri sana, hivi mumeo huwa anakusifia kila siku kabla hujatoka nyumbani?” nilimwambia, akacheka kwa nguvu na kwa kuwa abiria wote walikuwa bize kuteremka kwenye gari, hakuna aliyemjali sana, nikasimama, na yeye akasimama kwani tayari abiria walikuwa wamepungua sana ndani ya gari.
“Umejuaje kama nina mume?” aliniambia huku akinitazama kwa macho ya bashasha.
“Mwanamke mrembo kama wewe utakosaje mume?” nilizidi kumchombeza, akazidi kufurahi. Miongoni mwa udhaifu mkubwa wa wanawake, huwa wanapenda sana kusifiwa na wajanja kama sisi tunaojua namna ya kuzifikisha hizo sifa zenyewe kwa staili ya kuchombeza, huwa inakuwa rahisi sana kuwanasa.

KIVURUGE WA TANDALE- 7



ILIPOISHIA:
“Mungu wangu, nitasema nini nyumbani,” alisema huku akikurupuka na kuanza kutafuta nguo zake, nikaona analeta masihara, ataondokaje muda huo wakati hata kipindi cha pili kilikuwa bado?
SASA ENDELEA... 

Harakaharaka aliwasha simu yale ya bei mbaya ambayo kwa muda wote huo alikuwa ameizima. Nikamuona anavyohangaika, nadhani alikuwa akitafutwa sana kwenye simu.
“Sijui nitamwambia nini baba, sijawahi kukaa nje mpaka usiku mnene kiasi hiki.”
“Kwani wewe bado unaishi na wazazi wako?” 

“Ndiyo! Naishi na wazazi, sasa wewe ulikuwa unafikiri naishi na nani?”
“Sasa si unaweza tu kumwambia upo kwenye bethidei ya rafiki yako?”
“Hilo siyo tatizo, ilitakiwa nitoe taarifa mapema, sasa unafikiri saa saba hii naanzaje kuwaeleza kitu kama hicho? Umeniponza Ashrafu, umenisababishia matatizo,” alisema huku akianza kulia. Ilibidi niamke pale kitandani na kumfuata pale alipokuwa amesimama, nikawa najaribu kumtuliza.


“Wewe umeshakuwa mkubwa sasa, hutakiwi kuwahofia wazazi wako kwa kiasi hicho, kwani wao hawajui kwamba wewe umeshakuwa mkubwa?”
“Stop it!” alisema kwa ukali akimaanisha hataki niendelee kuzungumzia suala hilo. Kwa jinsi alivyonibadilikia, sikuwa na namna zaidi ya kumruhusu tu aondoke lakini nilifanya hivyo kwa shingo upande. 

Licha ya kazi kubwa iliyofanyika, huwezi kuamini kwamba bado mtandao ulikuwa ukisoma 4G, nikawa najitahidi kujizuia mwenyewe kwa mbinu zangu. Alivaa harakaharaka na muda mfupi baadaye, alikuwa ameshamaliza kila kitu, akanigeukia na kushtushwa na hali niliyokuwa nayo. 

“Una matatizo gani?”
“Sina tatizo lolote.”
“Mbona hivyo sasa?”
“Aah! Kawaida tu, kwani kuna tatizo?” nilisema huku na mimi nikijisikia aibu. 

KIVURUGE WA TANDALE- 6



ILIPOISHIA:
“Tumeshafika bro!” alisema yule dereva wa Ubber, kauli yake ndiyo iliyotuzindua kutoka kwenye dimbwi la huba, kucheki pembeni, kweli tayari tulikuwa Tandale kwa Mtogole.
SASA ENDELEA...
Tuliteremka kwenye Uber, kwa jinsi Nancy alivyokuwa mzuri, kitendo cha kuteremka tu pale kituoni, niliwaona wahuni kibao wakiacha kila walichokuwa wakikifanya na kuanza kutukodolea macho.
Waliokuwa wakicheza kamari waliacha, waliokuwa wakicheza singeli waliacha na hata waliokuwa wakipiga stori, wote walibaki wanatukodolea macho.
Shida moja ya kwetu ndiyo hiyo, yaani vijana wana njaa kiasi kwamba kila kitu kizuri kinachopita, wao wanaanza kuhesabu kama dili! Nilijua pale wanatupigia mahesabu ya kuja kutukaba na kuchukua viwalo vya kijanja alivyokuwa amepiga Nancy, simu yake, pochi pamoja na simu yangu.
Kwa kuwa nimeshaishi sana Tandale na najua namna ya kwenda sawa na wahuni, niliamua kuchukua tahadhari mapema kwa sababu kama tungekabwa na mrembo kama Nancy, ningekuwa nimejishushia mno hadhi.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 6


ILIPOISHIA:
Nilitafuta sehemu nzuri, upande wa nyuma kabisa wa shamba hilo kubwa, nikajificha na kuanza kupanga namna ya kwenda kutimiza azma yangu. Ilikuwa ni lazima nimuokoe Saima kwa gharama yoyote, hasa ukizingatia kwamba ndani ya tumbo lake, alikuwa na kiumbe, mwanangu mtarajiwa, ambaye angekuja kuyabadilisha kabisa maisha yangu na kunifanya na mimi nianze kuitwa baba.
SASA ENDELEA...
Nikiwa bado palepale mafichoni, usingizi ukikizonga kichwa changu kutokana na ukweli kwamba sikuwa nimelala hata kidogo usiku kucha, nilisikia muungurumo wa pikipiki zaidi ya moja kutokea upande wa nyuma wa shamba kubwa.
Nilijiweka sawa, ‘chuma’ changu nikakikamata vizuri mkononi kwa ajili ya chochote kwani japokuwa nilikuwa sehemu ambayo naujua isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kuniona, nilikuwa nafahamu vizuri jinsi Mute anavyoendesha shughuli zake. Alikuwa na intelijensia ya hali ya juu pengine kuliko hata vyombo vingi vya usalama.
Nikiri kwamba japokuwa ni kweli nilikuwa na matatizo makubwa na Mute, lakini ni yeye ndiye aliyenifundisha kila kitu nilichokuwa nakifanya. Nikiwa kwake, ndiko nilikojifunza kutumia bunduki, mbinu za mapigano ya mwilini au kwa kitaalamu ‘martial arts’, kutumia silaha nyingine mbalimbali na sehemu muhimu unazotakiwa kuwa nazo makini unapotaka kupigana na mtu, iwe ni silaha au kwa mikono.
Unajua tofauti kubwa kati ya raia wa kawaida na askari aliyepitia mafunzo, ni kwamba raia wa kawaida unaweza kuwa unajua kwamba ukimpiga ngumi usoni adui yako, utampasua na kumtoa damu au kumng’oa meno lakini hutaweza kuzuia asiendelee kupambana na wewe lakini askari anajua kabisa akikupiga sehemu gani, unaweza kudondoka na kupoteza fahamu papo hapo, au pengine kufa kabisa.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 5


ILIPOISHIA:
Nilikimbia na kujaribu kuruka ukuta lakini kabla sijaruka, nikasikia wale askari wakifungua milango na kuruka kwenye gari lao kwa kasi kubwa, mmoja kati yao akatoa amri ya kunitaka nisimame na kuinua mikono juu, jambo ambalo niliona kama haliwezekani.
SASA ENDELEA...
Yaani nisalimu amri kirahisi namna hiyo? Nijivalishe mwenyewe kitanzi kwenye shingo yangu? Lilikuwa ni jambo lisilowezekana kwa hiyo ilikuwa ni lazima nifanye kitu, tena haraka iwezekanavyo.
Pale nilipokuwa nimesimama, karibu na ukuta, kulikuwa na mtaro, ile inayochimbwa kandokando ya barabara. Kwa sababu maeneo mengi ya Masaki na Mikocheni yana kama asili ya majimaji, mitaro mingi iliyochimbwa ni mirefu na ina maji.
Kwa kasi ya kimbunga, nilijirusha kwenye mtaro, nikasikia risasi kadhaa zikipita mita chache kutoka pale nilipo, nikaangukia ndani ya mtaro. Kwa jinsi nilivyochukua uamuzi huo kwa kasi kubwa, nadhani hata polisi wenyewe hawakutegemea.
Katika medani za kivita, adui anapokuwa sehemu ambayo yupo chini kuliko wewe, kama kwenye shimo au handaki na ana silaha ya moto, huwa ni hatari sana kwa wewe uliyesimama juu ya ardhi kwa sababu yeye anaweza kukupiga risasi lakini wewe huwezi.

Sunday, September 2, 2018

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 4


ILIPOISHIA:
“Kumbe wakati napanda kwenye ule mti, mmoja kati ya walinzi wa eneo hilo, alikuwa ameshaniona na akawa anasubiri aone mwisho wangu. Nikiwa pale chini, nilishtukia bomba la baridi likinigusa shingoni, likifuatiwa na sauti ya ‘tulia hivyohivyo kwa usalama wako)’, nikajua nimepatikana.
SASA ENDELEA...
Miongoni mwa vitu ambavyo Mungu amenijaalia, ni kutokuwa na hofu au woga ndani ya moyo wangu na pengine hiyo ndiyo sifa iliyokuwa inawafanya watu wote wanaonijua wawe wananiogopa au kuniheshimu, yaani kama huniheshimu basi uniogope kwani sikuwa na hata chembe ya woga.
Licha ya yule mtu kunigusisha bomba ambalo bila hata kuuliza nilijua lazima litakuwa ni mtutu wa bunduki, kwa jinsi ninavyowajua walinzi wengi wa Kibongo, huwa hawafanyi kazi kwa weledi.
Unaweza ukashangaa kwa nini nasema hivyo, lakini nikiri tu kwamba nimepitia mambo mengi sana hapa duniani, mengine makubwa na ya kutisha mno ambayo hata nikikusimulia, unaweza usiamini kwa haraka utakachokisikia.
Na miongoni mwa matukio mengi niliyoyafanya, yalikuwa yakiwahusu zaidi walinzi kwa hiyo nilikuwa najua jinsi walivyo wazembe.

Friday, August 31, 2018

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 3


ILIPOISHIA:
“Inuka na ufanye ninachokueleza, ukizingua unajua nini kitatokea,” nilisema kwa sauti ya chini lakini yenye mamlaka, yule mwanamke akakurupuka akiwa ni kama haamini kilichotokea, Suma naye akawa anatetemeka akiwa haelewi nimeingiaje pale.
SASA ENDELEA...
“Snox! Nakuomba mdogo wangu, please show me some mercy!” (Nionee huruma tafadhali) alisema Suma huku akiwa anatetemeka kuliko kawaida lakini sikumjali.
“Look at my face!” (Nitazame usoni), nilimwambia kwa Kiingereza kilichonyooka, akanitazama usoni halafu akawa ni kama ameshtuka kidogo.
“Mlikuja mkanipiga na kunijeruhi kiasi hiki, mkamteka Saima wangu na kama hiyo haitoshi, mmekuja kuchoma moto nyumba yetu. Bado unategemea kwamba nitakuonea huruma?” nilisema huku na mimi nikitetemeka kwa hasira.
”No! Nisikilize kwanza Snox,” alisema huku akiniita kwa jina langu la kazi. Watu wengi mitaani huwa wanaamini Snox ni jina langu halisi kwa sababu kila ninakoenda ndilo linalotumika lakini ukweli ni kwamba halikuwa jina langu halisi wala halikuwa na uhusiano wowote na jina langu halisi.

Thursday, August 30, 2018

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 2


ILIPOISHIA:
Bado nilikuwa nazikumbuka namba za siri nilizotumia kukifunga, macho yangu yakatua juu ya kitu kilichosababisha nitabasamu! Siyo tabasamu la furaha, la hasha! Tabasamu la kifo, tabasamu ambalo huwa linaonekana usiku wa giza totoro pekee.
SASA ENDELEA...
Unaweza kujiuliza nilikuwa nimeona nini kilichosababisha nitoe tabasamu la aina hiyo? Kihulka mimi ni mpole sana na pengine upole wangu wa nje ndiyo unaosababisha wakati mwingine watu kunionea waziwazi, wakiwa hawajui ndani ya moyo wangu kumejificha kitu.
Ilikuwa ni bunduki ninayoipenda sana, AK47 ambayo ilikuwa imekatwa kitako na mtutu na kuifanya iwe na uwezo wa kubebeka vizuri mikononi. Jinsi nilivyoipata silaha hii hatari, ambayo kisheria haitakiwi kabisa kumilikiwa na raia, isipokuwa wanajeshi tu, ni stori ndefu sana na yenye kusisimua kwelikweli.
Wakati mwingine binadamu wanakuwa wepesi wa kuwalaumu wenzao kwa matokeo ya mwisho, lakini ni wachache wanaokuwa wanaujua ukweli wa nini kinachosababisha mtu fulani akafanya tukio fulani. Sikuwahi kudhani hata mara moja kwamba itafika siku nitakuwa nikiutegemea mtutu wa bunduki kufanya kile ninachokitaka.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1


“Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!”
“Nanii?”
“Fungua!”
“Jitambulishe kwanza, wewe nani?”
“Nimesema fungua! Fungua kwa hiyari yako!”
“Huyo ni nani?”
“Shiii! Rudi ndani kalale!”
“What is going on? Please let me know!” (Nini kinaendelea? Tafadhali naomba nieleweshe).
“Ngo! Ngo! Ngo!”

Kufumba na kufumbua, kishindo kikubwa kilisikika, mlango ukaja kunibamiza kwa nguvu na kunirusha mpaka ukutani, nikajibamiza na kudondoka chini kama mzigo. Wanaume watatu waliokuwa wamevalia makoti meusi, walinifuata na kunikaba pale chini huku wakinimulika kwa tochi zenye mwanga mkali usoni.

“Tulia, vinginevyo tunakumwaga ubongo sasa hivi,” alisema mmoja kati yao, nikashtuka kusikia akikoki bunduki yake na kuninyooshea. Sikuwahi kuona bunduki halisi katika maisha yangu hata mara moja, nilizoea tu kuziona kwenye TV lakini sasa, mtutu ulikuwa ukinitazama.

Thursday, March 29, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 63



ILIPOISHIA:
Muda mfupi baadaye, wote tulikuwa ‘saresare maua’, akanisukuma kwa nguvu kwenye uwanja wa fundi seremala, nikaangukia mgongo, akaja juu yangu kwa kasi, maandalizi ya mechi ya kirafiki isiyo na jezi wala refa yakaendelea huku akionesha kunikamia kama Simba na Yanga zinavyokamiana zinapokutana uwanjani.
SASA ENDELEA...
Kipyenga kilipolia tu, Shamila ndiye aliyekuwa wa kwanza kugusa mpira, akawa anabutua mashuti ya nguvu na kunifanya nihisi kama atanielemea na kunishinda ndani ya muda mfupi tu, jambo ambalo kwangu lingekuwa aibu kubwa.
Nikajipanga na kuanza kwenda naye sawa, akawa akipiga mashuti kwa kubutua, mimi naukontroo mpira na kumpiga chenga za mwili, wakati mwingine nikawa natambaa na chaki kama Christiano Ronaldo, jambo lililofanya kibao kigeuke, badala ya yeye kuwa ananishambulia kwa kasi, ikawa mimi ndiyo namshambulia.
Ilibidi nitumie ujuzi wa hali ya juu kuwahi kummaliza nguvu ili nimalize mchezo kwani Junaitha naye alikuwa akinisubiri na sikujua alikuwa na lengo gani. Kutokana na jinsi nilivyokuwa namshambulia Shamila kwa akili, haikuchukua muda mrefu, akatangaza kusalimu amri, akanikumbatia kwa nguvu!

Monday, February 5, 2018

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 62



ILIPOISHIA:
“Ndiyo, lakini mambo yenyewe ndiyo kama hivi, hatupati hata dakika chache za kuwa pamoja, mi nimechoka bwana,” alisema Shamila na kunisogelea mwilini, nikawa naiona hatari iliyokuwa mbele yetu endapo Junaitha atageuka na kugundua kwamba tulibaki koridoni tumesimama, tena tukiwa tumesogeleana mithili ya majogoo yanayotaka kupigana.
 SASA ENDELEA...
“Please Shamila, huu siyo muda muafaka, kama inawezekana tutafute muda baadaye,” nilisema kwa sauti ya chini, akashusha pumzi ndefu na kunitazama usoni kwa macho yake mazuri, tukaendelea kutembea lakini alionesha kweli amemaanisha kile alichokisema.
Tuliingia kwenye kile chumba ambacho tulikuwa tukikutania kila panapokuwa na shughuli maalum, Junaitha akatuelekeza kukaa kwa duara kama ilivyokuwa kawaida yetu kisha akatuambia wote tuanze kuvuta hewa kwa wingi kwa kutumia pua na kuitoa kwa kutumia mdomo.
“Inatakiwa wote tufumbe macho na tuendelee kupumua taratibu, vuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na sio kifua, unajua kuna watu wengi wanaishi lakini hawajui hata namna ya kupumua, badala yake wao wanahema,” alisema Junaitha na kuanza kutufafanulia kile alichokisema.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 61



ILIPOISHIA:
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
SASA ENDELEA...
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
“Asibaki mtu nyuma, kuweni makini,” alisisitiza Junaitha huku akipiga hatua za harakaharaka, tukazidi kuelekea ndani ya nyumba hiyo, tukafika mpaka sehemu kulipokuwa na korido nyembamba, tukaenda mpaka mwisho wa korido ambako hakukuwa na mlango wala sehemu ya kupita, nikawa sielewi lengo la Junaitha.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 66



ILIPOISHIA:
“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.
SASA ENDELEA...
Sikujua nini cha kufanya, nilitamani nirudi haraka ndani kabla mambo hayajazidi kuharibika lakini Rahma akaning’ang’ania, kwanza akitaka kujua kwa nini yule muuzaji alikuwa akinikimbia lakini pili nini kimetokea mpaka shati langu lilowe damu kiasi kile.
Kiukweli sikuwa na majibu, nikawa naendelea kuhangaika kuzuia damu isiendelee kunitoka. Rahma alivua kitenge chake na kunipa, naye akawa ni kama haelewi kilichokuwa kinaendelea.
Tukiwa tunaendelea kuhangaika, mara nilisikia ile hirizi yangu mkononi ikinibana sana, nikajua mambo yameshaharibika. Nilishaambiwa kwamba nikiona inanibana ghafla, ujue mahali nilipo kuna mtu mwenye nguvu za giza na kuna jambo baya anataka kulifanya.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 65


ILIPOISHIA:
Nilihisi kama kuna kitu kinanilamba hivi, nikaanza kutetemeka huku nikiendelea kujikausha nisisababishe mtikisiko wa aina yoyote, nilipozidi kuvuta utulivu, nikahisi kuna kitu cha baridi kinatingishikatingisha upande ule niliokuwa nalambwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kama nimetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
SASA ENDELEA...
Nilitulia tuli huku nikiendelea kutetemeka, mara nikaanza kuhisi kile kitu kikitambaa na kunivuka mwili, kutoka upande mmoja kuelekea upande mwingine. Japokuwa kulikuwa na giza niliweza kukitambua vizuri kiumbe hicho kuwa alikuwa ni nyoka. Hata sijui ushujaa wa kutulia vile niliupata wapi maana kama nilivyowahi kusema, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa maishani mwangu kama nyoka.
Basi yule nyoka mdogo alinitambuka na kupotelea upande wa pili wa kitanda, nikashusha pumzi ndefu kisha kwa tahadhari kubwa nikainuka pale nilipokuwa nimelala, nikasimama kwenye uchago wa kitanda na kujivuta mpaka kwenye swichi ya taa, nikaiwasha.

Friday, February 2, 2018

Kivuruge wa Tandale- 5



ILIPOISHIA:
Sikukumbuka hata kumalizana na Shija, harakaharaka nikavuka barabara kuelekea upande ule aliokuwa amekaa yule mrembo, huku nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia anataka kuniambia nini.
“Mambo kivuruge?” alinisalimia huku akitabasamu, nikashtuka amelijulia wapi jina hilo? Uso wangu ukajawa na aibu.
SASA ENDELEA...
“Nancy!”
“Mh! Umewezaje kulikumbuka jina langu haraka hivyo?”
“Aa! Kawaida tu, unajua kitu au mtu muhimu kwenye maisha yako huwezi kumsahau kirahisi,” nilijikakamua kiume na kujaribu kuyatawala mazungumzo.
“Karibu tupate vinywaji,” alisema msichana huyo huku akinionesha sehemu ya kukaa, nikashindwa kukataa, nikajisogeza na kukaa naye meza moja, tukawa tunatazamana. Si kawaida yangu kumuonea aibu mwanamke, hata awe mzuri kiasi gani lakini siku hiyo nilijikuta nikipoteza kabisa ujasiri mbele ya Nancy.
Kulikuwa na mambo mengi ambayo yalifanya nipoteze ujasiri, kwanza siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza kukutana na msichana huyo mrembo, muda ule nilipotoka kwenda kula ‘lunch’.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 60



ILIPOISHIA:
Junaitha alimkokota mpaka bafuni na kufunga mlango kwa ndani, nikabaki nimesimama pale koridoni. Ghafla nikaanza kusikia sauti ya Firyaal akilia kama mtu anayekabwa na kitu, nikakurupuka mpaka kwenye kile chumba walichokuwa wamelala wote, nikafunga breki za ghafla mlangoni, nikiwa siamini kile nilichokuwa nakiona.
SASA ENDELEA...
Firyaal alikuwa amejikaba shingoni kwa kutumia mikono yake miwili, macho yakiwa yamemtoka pima, akikoroma kama mtu anayeelekea kukata roho. Sikuwahi kusikia hata mara moja kama kuna mtu amewahi kufanikiwa kuyakatisha maisha yake kwa kujikaba mwenyewe lakini kwa Firyaal ilionesha kama hilo linaweza kutokea muda wowote.
Kwa kasi ya ajabu nilisukuma mlango na kwenda kumkamata Firyaal, kwa jinsi alivyokuwa na mwili ‘teketeke’, niliamini itakuwa rahisi kwangu kumtoa ile mikono yake shingoni lakini kumbe nilikuwa najidanganya.
Nilishangaa nilipomgusa Firyaal kukuta mwili wake umekakamaa na kuwa mgumu kama mti, nikaanza kuhaha kujaribu kumnasua bila mafanikio, aliendelea kukoroma huku wenzake wakiwa wamelala fofofo.

Mbinu Nyepesi za Kujitibu Upungufu wa Nguvu za Kiume

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 64



ILIPOISHIA:
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Nakufaaa! Naku...fa...aa,” sauti ya mwanamke ilisikika, aliporudia mara ya pili kuimba msaada, sauti yake ilikuwa ikikwamakwama na muda mfupi baadaye akaanza kukoroma kuonesha kwamba mtu au watu waliokuwa wakitaka kumdhuru tayari walishafanikisha lengo lao.
Tofauti na hali niliyokuwa nayo mimi, baba na baba yake Rahma hawakuonesha kushtuka chochote, yaani ilikuwa ni kama hakuna kilichotokea na wala hakuna aliyeshughulika kwa chochote.
Muda mfupi baadaye, harufu ya damu mbichi ilitawala eneo lote lile, milio ya bundi na midege mingine ya ajabu ikazidi kuifanya hali iwe ya kutisha mno. Baba aliendelea kupiga hatua ndefundefu, hukumoyo wangu ukiwa umepondwapondwa kwa hofu na mshtuko, na mimi nikawa naongeza mwendo, miguu yangu ikitetemeka kuliko kawaida.

Thursday, February 1, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 59



ILIPOISHIA:
Maneno yake yalinipa nguvu sana, akaniambia kwamba aliwalaza usingizi mzito kwa makusudi wale wengine ili tukamalizie kazi ya kumzindua Shenaiza lakini akanipa taarifa ambazo zilinishtua mno. Aliniambia baba yake Shenaiza amejizatiti vilivyo kwa nguvu za nje na ndani na ili tufanikishe azma yetu, ilikuwa ni lazima mtu mmoja kati yetu afe.
“Afe?”
“Ndiyo, lazima afe mtu kwenye kafara.”
SASA ENDELEA...
“Sasa mambo ya makafara yanaingiaje tena hapa? Kama ni hivyo basi mimi najitoa.”
“Ukijitoa maana yake wewe ndiyo utakufa. Wasiwasi wa nini na wewe ni mwanaume? Hebu acha woga, nitakufundisha cha kufanya wala usiwe na wasiwasi,” alisema Junaitha lakini kiukweli alikuwa amenichanganya mno.
Mmoja kati yetu lazima afe? Nani sasa! Kama siyo mimi ni nani? Raya? Haiwezekani. Shenaiza? Hapana. Shamila? Noo! Au Firyaal? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu. Nilichokifanya ilikuwa ni kujaribu kupambana na hofu ambayo sasa ilikuwa inanitafuna ndani kwa ndani.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 63



ILIPOISHIA:
“Nimepata salamu zako kwamba umechagua kuwa tajiri, ombi lako limekubaliwa lakini kuna masharti inatakiwa kabla siku zako saba hazijaisha, uwe umeshaanza kuyafuata, vinginevyo utakufa,” alisema yule mwanamke, macho yakanitoka pima.
SASA ENDELEA...
Nilijiweka vizuri pale chini nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia ataniambia nini, akanitazama machoni kisha akashusha pumzi ndefu na kunisogelea.
“Kwa nini umeamua kupita njia hii?” aliniuliza kwa sauti ya upole, nikashindwa kuelewa alikuwa anamaanisha nini.
“Unalingana na kijana wangu ambaye mwezi wa kumi na mbili angekuwa anatimiza miaka 21, makosa yangu yamesababisha niishi maisha ya kujuta kila siku, sitaki mtu mwingine apite njia kama niliyowahi kupita mimi na kusababisha nimpoteze mwanangu kipenzi,” alisema lakini wala maneno yake hayakuniingia akilini.

Wednesday, January 31, 2018

KIVURUGE WA TANDALE- 4



ILIPOISHIA:
Mara nikasikia mlango unafunguliwa, nikashtuka na kuinuka haraka kutaka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia, nikashtuka kumuona Salma, mtoto wa kike akiwa ameingia kwenye vyoo vya wanaume, nilipomtazama vizuri alikuwa akilia, machozi yakawa yameulowanisha uso wake.
SASA ENDELEA...
Harakaharaka niliacha kila nilichokuwa nakifanya, nikalishika shati na kutaka kulivaa lakini nilikuwa nimechelewa, Salma alifunga mlango wa maliwatoni kwa ndani kisha akanisogelea mpaka mwilini, huku machozi yakiendelea kumtoka.
“Umepatwa na nini Salma?”
“Kwa nini unanitesa? Ina maana hujui kama nakupenda? Kwa nini unanitesa Ashrafu,” alisema Salma huku akipitisha mkono wake na kunishika kiunoni, akanisogelea na kujilaza kwenye kifua changu.

Tuesday, January 30, 2018

KIVURUGE WA TANDALE- 3



ILIPOISHIA:
Mara alinirushia kitu hicho, nikashtuka baada ya kugundua kuwa lilikuwa ni lile kufuli lake jeupe, likiwa na harufu f’lan hivi ‘amaizing’ kuoneshakwamba lilikua limetoka mwilini muda huohuo, akacheka sana jinsi nilivyokuwa nalitazama kwa makini huku wakati mwingine nikilisogeza kabisa kwenye pua, akasogea na kujitupa kwenye sofa huku akiinua miguu yake na kuiweka kwenye miguu yangu.
SASA ENDELEA...
“Kivurugeee!”
“Sipendi hilo jina ujue.”
“Ndiyo nimeshakuita sasa, utanifanya nini?”
“Ntakuchapaaa!”
“Huwezi,” alisema Madam Bella huku akichekacheka na kunifanyia vituko ambavyo kiukweli nilishindwa kuvivumilia. Sijui nilipata wapi ujasiri, nikapitisha mikono yangu na kukishika vizuri kiuno chake, akashtuka na kutoa mguno huku pumzi zake zikianza kubadilika, akawa anapumua kwa nguvu kama ametoka kukimbia mbio za mita mia moja.
Nilizidi kukibana kiuno chake kinene wastani katika mtindo ambao nilijua lazima utamfanya shetani wake akurupuke kutoka mafichoni kwa spidi zote.

SEVEN DAYS IN HELL (Siku Saba Kuzimu)- 58




ILIPOISHIA:
“Yule kule aliyekuwa ananguruma kama mnyama ni nani?” Firyaal aliuliza swali, nikawaona wenzake wote wakitingisha vichwa, kuunga mkono swali hilo.
“Ni stori ndefu kidogo, ngoja nitawaeleza lakini njooni kwanza huku niwape dawa,” alisema.
SASA ENDELEA...
Wote wakamfuata mpaka kule kwenye kile chumba walichokuwa wamelala, akawaamuru wote wakae kwenye mkao wa kutengeneza duara, akatoka na kuelekea chumbani kwake, aliporudi muda mfupi baadaye, alikuwa na kichupa kidogo kilichokuwa na mafuta yaliyokuwa yananukia vizuri sana, akaanza kumpaka mafuta yale kichwani na usoni mmoja baada ya mwingine.
“Itabidi mkae dakika ishirini kisha mkaoge, baada ya hapo tutakamilisha kazi ya kumzindua Shenaiza, tumeelewana?”
“Mi nasikia njaa inaniuma sana.”
“Hatutakiwi kula chchote mpaka tukamilishe kwanza kazi hii, ukishakula tu utasababisha nguvu kubwa ambazo zinatakiwa kutumika kichwani mwako, zielekezwe tumboni kwa ajili ya mmeng’enyo wa chakula, jambo linaloweza kusababisha tukakwama, tumeshakula mbuzi mzima, hatuwezi kushindwa kumalizia mkia,” alisema Junaitha akimjibu Firyaal.

Monday, January 29, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 57



ILIPOISHIA:
“Jamal! Jamal! Amka, kuna tatizo,” sauti ya Junaitha ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye usingizi fofofo, nikakurupuka nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kumetokea nini tena.
SASA ENDELEA...
“Kuna nini tena?”
“Huyu mshenzi anataka kunizidi nguvu, amka ukanisaidie,” alisema Junaitha, huku kijasho chembamba kikimtoka. Harakaharaka nikakurupuka na kuvaa bukta na fulana, nikaongozana na Junaitha ambaye tayari alishatoka na kuanza kukimbilia kule kwenye chumba chake cha siri.
Tulipokaribia nilisikia sauti za kutisha mno, yule mwanamke tuliyemteka akawa ananguruma kama mnyama wa porini huku akikwangua mlango wa chuma kwa kucha zake ngumu, akitaka kutoka.
“Nisikilize! Jamal nisikilize,” alisema Junaitha ambaye alikwama ghafla pale mlangoni.
“Tukifungua mlango atatuzidi, inabidi tuingie kwa kutumia nguvu zetu tukapambane naye hukohuko ndani, amenitia meno, si unaona,” alisema Junaitha huku akinionesha alama ya meno mkononi mwake, huku damu nyeusi zikichuruzika.

SEVEN DAYS IN HELL (Siku Saba Kuzimu)- 56



ILIPOISHIA:
Harakaharaka nikafungua mlango nikiwa ni kama siamini nilichokisikia, nikamkuta Shenaiza akihangaika kujigeuza, jambo ambalo hakuwa amelifanya kwa kipndi kirefu tangu akiwa kule hospitalini.
“Shenaiza! Shenaiza,” nilisema huku nikipiga magoti pembeni ya kitanda chake. Bado hakuwa amefumbua macho yake.
SASA ENDELEA...
Hata hivyo, japokuwa hakuwa amefumbua macho, niliona akiyapepesa kama anayetaka kuyafumbua, nikainua mikono juu kama ishara ya kumshukuru Mungu. Kumbukumbu za yote yaliyotokea kuanzia siku ya kwanza msichana huyo aliponipigia simu mpaka muda huo zilipita kwa kasi ndani ya kichwa changu.
Kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa ambayo ungeweza kudhani ni ndoto ya kusisimua na muda si mrefu nitazinduka. Kwa kuwa Junaitha aliniambia nikamsubiri chumbani kwake, sikukaa muda mrefu ndani ya chumba hicho cha Shenaiza kwa sababu nilijua hawezi kufurahi akinikuta nikifanya tofauti na maagizo aliyonipa, nikambusu Shenaiza kwenye paji la uso kisha nikatoka na kuelekea chumbani kwa Junaitha.

KIVURUGE WA TANDALE- 2



ILIPOISHIA:
Alimpungia mkono kichokozi huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake, akatoka zake na kumuacha Ashrafu akiwa bado ameganda palepale kama barafu.
“Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu,” alijisemea huku tabasamu hafifu likichanua kwenye uso wake, akashusha pumzi ndefu na kuinuka kuelekea kaunta kulipa.
SASA ENDELEA...
“USHALIPIWA na yule dada uliyekuwa umekaa nae,” alisema yule mhudumu aliyekuwa mapokezi.
“ooh! Ahsante,” alisema Ashrafu huku akijisikia aibu kupindukia. Kwa lugha nyepesi, alichokifanya mrembo yule ilikuwa sawa na matusi makubwa kwake, yaani akatae kumpa namba yake ya siku kisha akamlipie bili?
“Samahani, kwani wewe ni mwenyeji hapa,” Ashrafu alimuuliza yule mhudumu ambaye alikuwa bize kupokea fedha na kurudisha chenji kwa wateja wake.
“Kaka samahani, niko bize sana, naomba uniache nihudumie wateja.”
“Kwani ugomvi dada’angu? Nilitaka kukuuliza swali dogo tu.”

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...