Tuesday, July 25, 2017

Graves of The Innocents (Makaburi Yasiyo na Hatia)- 6


ILIPOISHIA:
Huku nikitetemeka, nilisogea mpaka pale yule mganga alipokuwa amelala, akiendelea kukoroma kwa nguvu, mimi nikamshika miguuni na baba akamshika kichwani, tukaanza kumkokota kumtoa nje ya eneo letu, tukaenda kumbwaga pembeni kabisa kwenye vichaka kisha tukarudi ndani. Ile tunaingia ndani tu, tukasikia mlango ukigongwa kwa nguvu.
SASA ENDELEA...
“Nani!”
“Fungua!”
“Sifungui mpaka mjitambulishe na mueleze shida yenu.”
“Ni mimi mzee Sifuni, mwenyekiti wa kijiji.”
“Unaonekana hauko peke yako!”
“Ndiyo, nimeongozana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya kijiji, fungua tafadhali,” baada ya mwenyekiti huyo kusema hivyo, baba alinioneshea ishara kwa mkono kwamba niende ndani kwa sababu alishahisi wale watu wamekuja kwa shari. Nikatii nilichoambiwa na kwenda chumbani lakini bado nilikuwa na shauku kubwa ya kutaka kuona kinachoendelea.
Baba alipofungua tu mlango, nilisikia wakimuamrisha jambo:
“Upo chini ya ulinzi.”
“Kwa kosa gani?”
“Kwa kumshambulia mganga wa kienyeji aliyekuwa anatimiza majukumu yake hapa kijijini kwetu.”

Monday, July 24, 2017

Seven Days In Hell (Siku Saba Kuzimu)- 6


ILIPOISHIA:
Mara simu yake ilianza kuita mfululizo, akaishika na kutazama namba ya mpigaji lakini katika hali ambayo sikuielewa, aliiachia simu hiyo, ikadondoka chini na kufunguka betri ikaangukia kivyake, mfuniko kivyake na simu nayo kivyake. Akaanza kuangua kilio kwa uchungu huku akiniomba nimsaidie, nilibaki nimepigwa na butwaa.
SASA ENDELEA…
“Nikusaidie nini Shenaiza?” nilimuuliza huku nikiiokota ile simu na kuiunganisha upya.
“Nakuomba usiniache, fanya kila kinachowezekana unitoroshe hapa hospitalini usiku huuhuu, watakuja kunimalizia,” alisema msichana huyo na kuzidi kunichanganya.
“Watakuja kukumalizia? Akina nani? Na Kwa nini tutoroke wakati hali yako bado siyo nzuri?”
“Naomba ufanye nilichokuomba mengine utaenda kuyajua mbele ya safari,” alisema msichana huyo huku akiendelea kulia.
Nikiwa bado nimeduwaa, nikiwa sijui cha kufanya, nilishtuka kumuona akichomoa sindano ya dripu aliyokuwa amechomwa mkononi mwake na kusababisha damu zianze kumtoka mkononi, akajikongoja huku akionesha kuwa na maumivu makali, akanitaka nimpe bega langu ili apate balansi ya kutembea.
Sikuwa na cha kufanya zaidi ya kukubaliana na matakwa yake, japokuwa nilikuwa najua kwamba ninachokifanya ni hatari sana lakini sikuwa na namna zaidi ya kumsaidia msichana huyo ingawa mpaka muda huo sikuwa najua nini kinachomsumbua.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 5


ILIPOSHIA:
Aliniambia Shenaiza amerejewa na fahamu na jambo la kwanza alilouliza ni kama nilikuwa nimempigia simu.
“Nimemwambia kwamba upo hapa nje, akaniomba sana akuone, lakini anazungumza kwa shida sana,” alisema nesi huyo, nikainuka na kuanza kumfuata harakaharaka kuelekea wodini.
SASA ENDELEA…
Muda mfupi baadaye, tulikuwa pembeni ya kitanda alichokuwa amelazwa msichana huyo, nesi Rozina akaniambia ananipa dakika chache za kuzungumza na mgonjwa, akatoka na kufunga mlango wa wodi hiyo. Kwa muda wote huo, macho yangu yalikuwa juu ya uso wa msichana huyo ambaye naye alikuwa akinitazama, tukawa tunatazamana.
Tofauti na nilivyofika mara ya kwanza hospitalini hapo, safari hii niliweza kumuona vizuri msichana huyo. Kitu ambacho naomba nikiseme wazi, japokuwa alikuwa kwenye maumivu makali, akiwa amefungwa bandeji kubwa kichwani na jicho lake moja likiwa limevilia damu na kuwa jekundu, Shenaiza alikuwa na sura nzuri mno.

Thursday, July 20, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 4


ILIPOISHIA:
Niliondoka kazini nikiwa ni kama nimechanganyikiwa, sikuwa namjua Shenaiza lakini sijui kwa nini nilihisi kama matatizo yake yalikuwa yakinihusu sana. Nikiwa kwenye kituo cha daladala nikiendelea kusubiri usafiri, ujumbe mfupi uliingia kwenye simu yangu, ulisomeka:
“Mwenye simu hii amelazwa Hospitali ya Amana, Ilala. Hali yake ni mbaya, hawezi kuzungumza.”
SASA ENDELEA…
“Mungu wangu,” nilisema baada ya kumaliza kuusoma ujumbe huo. Nilijaribu kuipiga tena namba hiyo, ikapokelewa lakini sauti haikuwa ya Shenaiza, akaniambia yeye ni Rozina, nesi katika hospitali ya Amana na kwamba yeye ndiye aliyekuwa akimhudumia msichana huyo.
Nilimuomba anitajie wodi aliyolazwa msichana huyo, akaniambia niende tu nikifika hospitalini hapo nipige kupitia namba hiyohiyo atakuja kunipokea. Niliita bodaboda na kumuelekeza kukimbia kadiri awezavyo kuelekea Amana. Abiria wengine waliokuwa pale kituoni wakisubiri daladala, walibaki kunishangaa lakini mwenyewe sikujali.
Nikaondoka na bodaboda huku nikimhimiza kuongeza mwendo ili tuwahi kufika. Baada ya kuhangaika sana kwenye foleni, kama ujuavyo Jiji la Dar es Salaam nyakati za jioni, hatimaye tuliwasili Amana. Nikapiga namba ya Shenaiza ambapo yule nesi alipokea tena, nikamweleza kwamba tayari nilikuwa nimefika, akaniambia nimsubiri mapokezi.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 3


ILIPOISHIA:
NILISHANGAA kugundua kwamba ukiachilia mbali meseji mbili za rafiki zangu, Justice na Prosper, nyingine zote zilikuwa zimetoka kwa yule msichana aliyekosea namba ya simu, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kuzisoma, moja baada ya nyingine nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kuona ameandika nini.
SASA ENDELEA…
YA kwanza ilisomeka: “Samahani kaka Jamal naomba tuchati kama hutajali.” Nikaisoma na kuirudia zaidi ya mara mbili, sikuelewa maana ya yeye kuomba tuchati ni nini kwa sababu tayari nilishamwambia amekosea namba na mwenyewe akakiri hilo.
Hakuishia hapo, meseji nyingine ikasomeka: “Nina tatizo kubwa nilikuwa nahitaji mtu wa kumshirikisha ndiyo maana nikawa nimempigia simu ndugu yangu mmoja aitwaye Moses lakini baada ya kusikia sauti yako, naamini na wewe unaweza kuwa na busara na kunisaidia nini cha kufanya.”

Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na hatia) - 5


ILIPOISHIA:
MWANAUME mzee mwenye macho mekundu sana na midomo myeusi, akiwa amejifunga shuka refu lenye rangi nyekundu na nyeusi, kichwani akiwa amejifunga kitambaa cheusi, shingoni akiwa na hirizi kadhaa na shanga, alisimama na kunyoosha juu mkia wa mnyama ambaye sikuwa namjua, watu wote wakashangilia kwa nguvu.
SASA ENDELEA...
“Sina mengi ya kuzungumza, naomba ushirikiano wenu tuwakomeshe wachawi wa kijiji hiki,” alisema mwanaume huyo kwa Kiswahili kibovu, watu wakashangilia tena kwa nguvu kisha Mwene akaendelea na maelezo, akisisitiza kwamba kazi lazima ianze siku hiyohiyo usiku.
Baada ya maelezo marefu yaliyojaa vitisho kwa watu waliokuwa wakitajwa kuhusika na uchawi, mkutano uliahirishwa, watu wakatawanyika huku kiongozi huyo wa kijiji akiwataka watu wote kutoa ushirikiano kwa mganga Mabwanji atakapoenda kuwatembelea kwenye nyumba zao.
Hofu niliyokuwa nayo ilikuwa kubwa mno, kwa jinsi watu walivyokuwa wanatuchukia pale kijijini nilijua lazima moto utawaka. Baadhi ya wazee waliokuwa wanaheshimika pale kijijini, walianza maandalizi ya kumsaidia mganga huyo kwa kila alichokuwa anakihitaji, dawa zikaandaliwa na hatimaye muda uliokuwa ukisubiriwa na wengi ukawadia.

Makaburi ya Wasio na Hatia (The Graves of the Innocents)- 4


ILIPOISHIA:
“Naongea na wewe Togolai, ni kweli nini?” alihoji tena Madam Timbuka, safari hii akiwa amenikaribia kabisa pale nilipokuwa nimekaa, nikaanza kubabaika huku hofu kubwa ikishindwa kujificha kwenye uso wangu.
SASA ENDELEA...
“Kwamba mwalimu wetu anaumwa. Nilisikia asubuhi nikawa siamini,” nilidanganya, nikamuona mwalimu Timbuka akishusha pumzi ndefu, wanafunzi wenzangu waliokuwa wakinitazama kwa shauku, nao walionesha kuridhika na majibu yangu.
Baada ya kutoa taarifa hizo, mwalimu Timbuka alitutaka tusipige kelele bali tuutumie muda huo kujisomea, akatoka na kutuacha wote tukiwa kimya. Moyoni mwangu niliendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
“Kwa hiyo mwalimu Mwashambwa naye atakufa?” nilijiuliza moyoni wakati nikiendelea kutafakari taarifa za ugonjwa wa mwalimu wetu. Nilijaribu kuunganisha matukio, hofu ikazidi kuongezeka ndani ya moyo wangu. Bado sikutaka kuamini kwamba baba alikuwa mchawi na alikuwa akihusika na kilichokuwa kinaendelea.
Muda ulizidi kusonga mbele, hatimaye ukawadia muda wa mapumziko. Kwa kawaida, ilikuwa ikifika muda wa mapumziko, kengele inagongwa mara mbili kuashiria wanafunzi wote tutoke madarasani lakini siku hiyo, kengele iligongwa tofauti. Iligongwa mfululizo huku walimu wakiwa wameshatoka na kusimama mstarini, kila mmoja akionekana kuwa ‘siriasi’.

Wednesday, July 19, 2017

MAKABURI YA WASIO NA HATIA (GRAVES OF THE INNOCENTS)- 3


ILIPOISHIA:
Nikamuongoza baba mpaka kwenye kaburi la Alfred ambalo juu yake kulikuwa na msalaba ulioandikwa jina lake kamili, tarehe ya kuzaliwa na tarehe ya kufa kwake. Akaniambia niwe makini kwa kila atakachokuwa anakifanya, nikatingisha kichwa huku hofu kubwa ikiwa imetanda ndani ya moyo wangu kwani kiukweli nilikuwa nikiogopa sana makaburi na maiti.
SASA ENDELEA:
Baba alianza kufukuafukua ule upande wa kichwani kwenye lile kaburim akaingiza mkono mfukoni na kutoa kichupa kilichokuwa na ungaunga mweusi, akaumwaga kuanzia upande wa kichwani mpaka miguuni, kisha akaniambia tuanze kulizunguka lile kaburi kwa kuanzia kushoto kwenda kulia.
Alianza yeye, na mimi nikafuatia, tukawa tunazunguka lakini kwa kutembea kinyumenyume, baada ya kuzunguka raundi sana, nilianza kusikia kizunguzungu kikali, baba akaniambia nikae, yeye akarudi kusimama palepale alipokuwa amesimama.
“Hebu muite jina lake mara tatu kwa sauti kubwa,” alisema baba, nikawa simuelewi anamaanisha nini. Yaani mtu alishakufa siku nyingi zilizopita halafu ananiambia nimuite jina lake, tangu lini maiti ikaitika? Hata hivyo, ilibidi tu nitii kile alichoniambia, nikamuita.
Nililitaja jina lake kwa mara ya kwanza, baba akawa ananionesha ishara kwamba niongeze sauti, nikamuita kwa mara ya pili kisha kwa mara ya tatu. Cha ajabu kabisa, nilisikia akiitikia, tena niliweza kuthibitisha kabisa kwamba ni yeye kwa sababu nilikuwa naijua sauti yake na hata akizungumza neno moja tu, nakuwa nimeshamtambua.

Nilitetemeka kuliko kawaida, nikawa nageuka huku na kule kwa sababu alivyoitikia, ilionesha kwamba hayupo pale kwenye kaburi bali yupo umbali wa mita kadhaa pembeni. Nikiwa bado siamini, baba alinionesha kwa kidole, akaniambia nitazame chini ya mti mkubwa wa mjohoro uliokuwa pembeni kidogo ya makaburi.

Tuesday, July 18, 2017

MAKABURI YA WASIO NA HATIA (GRAVES OF THE INNOCENTS)- 2


ILIPOISHIA:
Tulipokaribia nyumbani kwa mzee huyo, baba alinionesha ishara kwamba nisimame, nikafanya hivyo, tukawa tunasikia sauti za watu wengi wakilia kutoka nyumbani kwa mzee huyo, baba akanionesha ishara kama anayesema ‘unaona?’, nikashika mdomo kwa mshangao. Sikutaka kuamini kwamba kweli mzee Mwankuga alikuwa amefariki dunia.
SASA ENDELEA...
Nilijikuta nikishusha lile furushi la dawa na panga, nikawa nataka niende kushuhudia mwenyewe kama ni kweli lakini baba aliniambia nisithubutu kufanya hivyo, hasa kutokana na uhasama uliokuwepo kati yetu na familia hiyo. Bado niliendelea kuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kama ni kweli yule mzee amekufa.
Ilibidi baba anishike mkono, tukaenda mpaka nyumbani ambapo baba aliingia kwenye chumba chake cha uganga na kuanza kuchambua zile dawa tulizotoka nazo porini. Ni kama alijua kwamba nitamtoroka na kurudi kule msibani kwenda kushuhudia kilichotokea kwani aliniambia nikae palepale, nimuangalie jinsi alivyokuwa akichambua dawa.
Kweli nilitii maagizo yake, nikakaa pale lakini bado nilikuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kilichoendelea. Nilipomuona baba amezama kwenye kazi yake hiyo, niliinuka na kuanza kuelekea mlangoni, akaniwahi na kuniuliza ninakokwenda.

“Naenda kujisaidia baba,” nilimdanganya baba, akanitazama usoni kisha akaendelea na kazi yake. Nilitoka na kwenda chooni ambako nako nilizunguka nyuma, nikatokomea huko na kwenda kutokea upande wa pili, nyumbani kwa mzee Mwankuga.

MAKABURI YA WASIO NA HATIA (GRAVES OF THE INNOCENTS)- 1


JINA langu naitwa Togolai Mahimba, ni mtoto wa mwisho kati ya watoto saba wa baba yetu, Sinai Mahimba ambaye kwa sasa ni marehemu. Baba yetu alifariki miaka mitatu iliyopita baada ya kuugua ghafla.
Kifo chake kilitawaliwa na utata mkubwa na hata siku ya mazishi yake, kulitokea mambo mengi ya ajabu ambayo mpaka leo siwezi kuyaeleza. Ninayo mambo mengi ambayo ningependa kukusimulia ndugu msomaji lakini kwa kuanzia, naomba nikueleze mambo machache yaliyotokea kabla ya kifo cha baba yetu ambaye mimi ndiye nilikuwa mtoto anayenipenda zaidi.
Kabla hajafikwa na mauti, baba yetu alikuwa mtu maarufu sana kijijini kwetu, Makongorosi, Chunya mkoani Mbeya tulikokuwa tukiishi. Kilichofanya awe maarufu kiasi hicho, ni kazi yake ya uganga aliyokuwa anaifanya ambapo mbali na mambo mengine, alikuwa akiwafanyia matambiko wachimbaji wengi wa dhahabu ili wakiingia mgodini, wapate dhahabu kwa urahisi sambamba na wafanyabiashara wengine.

Umaarufu wa baba ulisababisha hata sisi watoto wake tuwe maarufu sana, hasa mimi ambaye muda mwingi nilikuwa nikiongozana naye kila alikokuwa anakwenda, kuanzia kwenye matambiko maporini, kwenye mazindiko migodini, kuchimba dawa msituni mpaka kilingeni kwake alikokuwa akifanyia shughuli zake za uganga.

Monday, January 2, 2017

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 2



ILIBIDI nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yeyote ili aniwahishe kabla ile ‘ambulance’ haijapotea kabisa. Nilipopiga hatua moja, nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida.
Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.
SASA ENDELEA…
“OYA mambo vipi mkubwa!” nilimsalimu dereva wa bodaboda aliyekuwa pembeni yangu kwa bashasha kubwa lakini hakuniitikia, akawa anaendelea kuifutafuta bodaboda yake.
Nilirudia kumsalimu lakini bado hakunijibu chochote na wala hakuonyesha kama ananisikia. Nilimgusa begani lakini bado ilikuwa ni kazi bure, aliendelea kufutafuta bodaboda yake, nikabaki nimepigwa na butwaa.


Ilibidi nimsogelee dereva mwingine wa bodaboda, naye nikamsalimia kwa bashasha lakini hakunijibu, nikarudia tena na tena lakini bado hali ilikuwa ileile, nikaenda kwa watatu ambaye alikuwa akipiga stori na wenzake, naye akaonyesha kutonisikia.
“Kwani imekuwaje? Mbona sielewi kinachoendelea?” nilijisemea huku nikianza kutetemeka kwa hofu kubwa, mwisho niliamua kufanya jambo moja, nilipaza sauti kwa nguvu nikiita ‘bodabodaaa!’ niliamini yeyote ambaye atakuwa wa kwanza kuniona basi nitamchukua huyohuyo lakini wapi! Kila mmoja aliendelea na mambo yake.

Saturday, December 31, 2016

SEVEN DAYS IN HELL! (SIKU SABA KUZIMU)-1

Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.



Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.

Saturday, June 25, 2016

PENZI LILILOKUFA (DEAD LOVE)- 1

Upepo wa bahari ulikuwa ukivuma kwa nguvu na kusababisha mawimbi makubwa ya maji yawe yanapiga kwa nguvu ufukweni, yakizoa mchanga na kuupeleka bahari kisha kurudi tena.
Kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele, ndivyo upepo ulivyokuwa ukizidi kuongezeka huku wingu jeusi likianza kutanda angani. Watu wote waliokuwa wakiufurahia upepo wa baharini, sasa walianza kuuona kuwa kero kwani ulikuwa ukiambatana na baridi kali huku kijua cha jioni kilichokuwa kikiwaka, kikimezwa na wingu zito jeusi.


Watu waliokuwa wamekaa ufukweni, waliendelea kupungua kwa kasi na muda mfupi baadaye, ufukwe ulikuwa kimya kabisa huku ngurumo za hapa na pale zikianza kusikika kuashiria mvua kubwa iliyokuwa ikitaka kunyesha.


Wednesday, August 19, 2015

MY REPENTANCE (KUTUBU KWANGU)- 1

Naitwa Flaviana Joel, mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nane. Nilibahatika kuolewa miaka kumi iliyopita, nikiwa bado msichana mbichi katika umri wa miaka kumi na nane tu.
Niliolewa na mume wangu kipenzi, Ibrahim au Ibra kama mwenyewe nilivyozoea kumuita ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye benki moja maarufu ambayo sitaitaja jina kwa sababu maalum, iliyopo hapa jijini Dar es Salaam.
Kabla Ibra hajanioa, tulidumu kwenye uchumba kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja, kipindi hicho nikiwa nasoma chuo kimoja cha uhasibu kilichopo Posta, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, nikiwa ndiyo kwanza nimeanza mwaka wa kwanza.
Baada ya ndoa, mimi na Ibra tulihamia Mbezi Beach kwenye nyumba yetu ambako tuliishi pamoja mpaka tulipokuja kutengana kwa sababu ambazo ndizo hasa zilizonifanya nitafute nafasi hii ya kutubu hadharani na kukiri kwa kinywa changu yote niliyowahi kuyafanya.
Nimesukumwa kuja kusimulia mkasa wangu huu kwa sababu nataka watu wajifunze kupitia maisha yangu na Ibra. Najisikia aibu sana, najikaza tu kwa sababu nataka wanawake wenzangu waelewe kilichonitokea na kamwe wasifuate njia kama ambazo mimi nilipita. Pia iwe funzo kwa wanaume, hasa wale ambao wapo ndani ya ndoa.
Nasikitika kwamba nimekuwa kikwazo kikubwa katika maisha ya Ibra, mwanaume niliyetokea kumpenda kwa moyo wangu wote lakini kwa sababu ya mapungufu ya kibinadamu ambayo nitayaelezea, nikageuka na kuwa mwiba mkali kwenye maisha yake.
Nilisema tangu awali na nitaendelea kusema kwamba sijawahi kutokea kumpenda mwanaume kama nilivyompenda Ibra ila hata sielewi ni kitu gani kilichosababisha haya yote yatokee.

HEART ATTACK (SHAMBULIO LA MOYO)- 1

MANYUNYU ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likiendelea kujikusanya angani, kuashiria mvua kubwa iliyokuwa inataka kunyesha. Japokuwa ilikuwa bado ni mapema, giza lilitanda angani na kufanya watu karibu wote kukimbilia majumbani mwao kabla mvua hiyo haijaanza kunyesha.
Radi kali na ngurumo za kutisha zilikuwa zikisikika huku na kule na kuzidi kuifanya hali kuwa tete. Manyunyu yaliongezeka na muda mfupi baadaye, mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ilianza kumwagika. Watu wote walikimbilia majumbani mwao, huku wengine wakijibanza kwenye viambaza vya nyumba na maduka kujisitiri na mvua hiyo.
“Kaka amka tunataka kufunga baa.”
“Niongeze bia moja baridi na kiroba.”
“Inamaana hii mvua wewe huisikii au?”
“We mhudumu, nimekwambia ongeza bia, kwani wewe ndiyo umenileta hapa, sitaki kuwahi kurudi nyumbani kwani moto unawaka.”
“Kivipi?”
“Naishi na mwanamke ambaye ni tatizo kubwa maishani mwangu, yaani muda mwingine natamani kujifia niepuke mateso haya,” kijana mmoja mdogo alikuwa akijibizana kilevi na mhudumu wa baa ndogo ya Mpakani. Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inamwagika, kijana huyo hakuonekana kujali, pombe zilikuwa zimemzidi lakini bado alikuwa anataka kuendelea kunywa.

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1

Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.
“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

NILIMUUA NIMPENDAYE (I KILLED MY BELOVED ONE)- 1

Jina langu naitwa Eunice, mtoto wa tatu kati ya watano wa familia ya baba yetu, mzee Ansbelt. Nilizaliwa miaka 26 iliyopita katika Kijiji cha Mtae, Lushoto mkoani Tanga lakini nimekulia jijini Dar es Salaam kwani baba yangu aliyekuwa akifanya kazi ya uhandisi katika Kampuni ya Usambara Civil Engineering, alihamishiwa kikazi jijini na akafanikiwa kujenga nyumba Tabata.
Ni hapo ndipo mimi na ndugu zangu wa tumbo moja tulipokulia hadi tulipokuwa wakubwa. Kwa kweli kwa kipindi cha utotoni, tuliishi maisha mazuri sana kwani baba yetu alikuwa akijiweza kifedha hivyo alituhudumia vizuri kwa mavazi, chakula na elimu bora.
Nakumbuka sisi ndiyo tulikuwa wa kwanza kumiliki runinga mtaani kwetu na ndiyo tulikuwa wa kwanza kupelekwa shuleni na ‘school bus’, tukisoma katika shule iliyokuwa inafundisha masomo yote kwa Kiingereza (English Medium), iliyokuwa nje kidogo ya jiji.
Mama yetu hakuwa akifanya kazi, alikuwa akishinda nyumbani kuhakikisha sisi wanaye tunapata kila tulichokihitaji, ikiwemo malezi bora. Kutokana na aina ya malezi tuliyolelewa, tulikuwa tofauti sana na watoto wengine tuliokuwa tukiishi nao mtaani kwetu.
Mimi na ndugu zangu wengine wa kike hatukuwa sawa na wasichana wengine mtaani kwetu ambao walianza kujihusisha na mapenzi wakiwa na umri mdogo, wengi wakitoka na wanaume wenye umri mkubwa, sawa na baba zao.

CRUEL WORLD (DUNIA KATILI)- 1

Mwandishi: Hashim Aziz
“Sukuma! Sukumaaa! Jikaze mwanangu... moja... mbili... tatu... haya sukumaaa!” sauti ya mkunga wa jadi, Mama Anunu ilisikika kutoka ndani ya kibanda cha nyasi na miti, akimhimiza msichana mdogo aliyekuwa na ujauzito mkubwa, Adelina kujitahidi ili hatimaye ajifungue.
Licha ya ujauzito wake kutimiza umri wa miezi kumi na moja, Adelina alishindwa kabisa kujifungua. Alishahangaika sana kwenye hospitali mbalimbali bila mafanikio, alishapewa dawa za kuongeza uchungu mara kadhaa bila mafanikio, mwisho ndipo aliposhauriwa kwenda kwa mama Anunu.
Mwanamke huyo, licha ya kuzuiwa na serikali kufanya shughuli za ukunga nyumbani kwake na badala yake akaambiwa awe anawapa washauri waende hospitali na kwenye vituo vya afya kwa usalama wao, bado aliendelea na kazi yake kwa siri, akiwasaidia wengi ambao ujauzito wao ulikuwa na matatizo na wale ambao hawakuwa na uwezo wa kusafiri mpaka hospitalini, kilometa nyingi kutoka eneo hilo.

Monday, August 3, 2015

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1


Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.


“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

Wednesday, May 27, 2015

RAY AMKANA MTOTO WA JOHARI

Msanii wa filamu za Kibongo, Raymond Kigosi 'Ray' amemkana mtoto wa mpenzi wake wa muda mrefu, Blandina Chagula 'Johari' aitwaye Maria na kusisitiza kuwa mtoto huyo si damu yake.

Ray aliulizwa kuhusu mtoto wa Johari mbele ya Chuchu, akamkana na kwenda mbali zaidi kwa kusema ni jambo la heri kujiweka mbali na watu wanaotafuta umaarufu kupitia yeye.

"Achaneni na hayo mambo, sihusiki na lolote na jambo la mtoto na sipendi kabisa kuzushiwa mambo kama hayo, watu wasinitafsiri kwa minong'ono na badala yake wafuate ninachosema, kwa sasa mwanamke wa maisha yangu ni Chuchu na ntakuwa natembea nae kila mahali ili nione hao wanasema mimi ni mpenzi wao.

Monday, May 25, 2015

WEMA: NAMPENDA ZARI

Mwanadada Wema Sepetu, amefunguka kwamba hana tatizo na Zarina Hassan 'zari' licha ya kuwa mrembo huyo anatoka na aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul 'Diamond'.
Wema aliyasema hayo usiku wa jana mei 25, 2015 katika kipindi cha Ala Za Roho kinachoongozwa na Loveness Malinzi 'diva' wakati akihojiwa.

Mmmh! Karama utaoa kweli ???

Mwanamuziki Luteni karama juzi jumamosi amemvalisha pete ya uchumba mpenz wake wa siku nyingi pia ni mwanamuziki Isabella mpanda "Bella" tukio hilo lilifanyika katika ukumbi wa klabu kakala iliyopo kigamboni jijini Dar es salaam

Tuesday, January 6, 2015

CAMERON DIAZ AND MADDEN ARE MARRIED!


Credits: E! News
The couple tied the knot Monday night at Diaz's Beverly Hills home after a whirlwind courtship and blink-and-you-missed-it engagement.
All told, we hear that about 100 guests were in attendance and, while a massive tent was set up in the yard, the ceremony took place inside the house. Friends and family filed into the reception tent after the I-dos.
Word just got out today that the super-stealth duo were planning on taking the plunge, boggling more than a few minds since Diaz, 42, and Madden, 35, just stepped out as a couple (and an unconfirmed couple at that) last May.
 The Good Charlotte rocker popped the question a few days before Christmas.
But maybe they started planning when they met, because the big celebration didn't have the look of an 11th-hour affair.

JIMBO LA KILOSA; MAPIGANO, HUDUMA MBOVU ZA KIJAMII NI TATIZO SUGU


Na Hashim Aziz
Kilosa ni moja kati ya wilaya zinazounda Mkoa wa Morogoro ikiwa na jumla ya wakazi 26,060 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002. Pia ni jimbo la uchaguzi linaloongozwa na mwanasiasa mkongwe, Mustapha Mkulo kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Mkullo (kulia)
Wiki iliyopita, Uwazi lilifunga safari mpaka kwenye jimbo hilo ambapo mwandishi wetu alifanikiwa kuzungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali yakiwemo Mtendeni, Mkwateni, Magomeni, Kibaoni, Manzese A, Manzese B, Uhindini, Mazinyungu na maeneo mengine mengi ambapo alizungumza na wananchi walioeleza matatizo yao.
MATATIZO YA WANANCHI
Katika ziara hiyo, Uwazi lilibaini matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi wa jimbo hilo, kubwa ikiwa ni mapigano ya mara kwa mara kati ya jamii za wakulima na wafugaji wanaogombea ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji, kama ilivyobainika pia katika Jimbo la Mvomero ambalo pia lilitembelewa hivi karibuni.
Mkullo
Wakulima wanalalamika kwamba wafugaji wa Kimasai,

IDI AMINI DADA; MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU

Wengi wanamkumbuka kutokana na ukatili wake kipindi alipokuwa madarakani na vita kali ya kugombea mpaka iliyopiganwa kati ya nchi yake ya Uganda dhidi ya Tanzania, enzi hizo ikiwa chini ya Rais Julius Kambarage Nyerere.
Anaitwa Idi Amini Dada, Rais wa tatu wa Uganda aliyeingia madarakani baada ya kumpindua Rais Milton Obote na yafuatayo ni mambo kumi usiyoyajua kuhusu dikteta huyu.
1. Katika kipindi alichokuwa madarakani, kutoka 1971 hadi 1979, inakadiriwa kwamba aliwaua kikatili zaidi ya watu laki tano waliokuwa wakienda kinyume na amri zake.

2. Aliwahi kuwa mwenyekiti wa OAU (Organisation of African Unity) na alikuwa na ndoto za kuiunganisha Afrika kuwa nchi moja ili aitawale, kama alivyokuwa akiwaza rafiki yake mkubwa, Muammar Gaddafi.
3. Alikuwa na elimu ndogo aliyoipata kwenye Shule ya Kiislamu ya Bombo na inaelezwa kuwa baadaye aliacha shule akiwa hajui vizuri kuandika wala kusoma.
4. Mpaka anakufa, historia ya maisha yake haikuwa ikifahamika vizuri. Wachambuzi wanaeleza kuwa alizaliwa Koboko mwaka 1925, kutoka kabila la Kakwa.

Monday, January 5, 2015

BOKO HARAM FIGHTERS OVERPOWER MULTINATIONAL FORCE


Boko Haram Islamic extremists have overpowered a multinational military force and seized its key base on Nigeria's border with Chad, according to residents who took to canoes to escape.

Scores of soldiers and civilians were killed, while others drowned in Lake Chad, Nigerians taking refuge in a Chadian village said in cell phone calls Sunday night. They said insurgents fired rocket-propelled grenades and automatic assault rifles and hurled explosives.
Boko Haram

"They came in their hundreds driving several Hilux patrol vehicles, trucks and some were on motorcycles and immediately began to throw explosives and bombs," fisherman Audu Labbo told The Associated Press.

Tuesday, December 30, 2014

PATRICK PHIRI ATIMULIWA SIMBA

Timu ya soka ya Simba, imemtimua kazi aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mzambia Patrick Phiri pamoja na msaidizi wake, Suleiman Matola kufuatia matokeo mabovu ambayo timu hiyo imeendelea kuyapata. 


Phiri aliwahi kuwa kocha wa klabu hiyo mnamo mwaka 2003-2005 kabla hajaondoka na kurudi kwao Zambia kuifundisha timu yake ya taifa mnamo 2005-2008 baada ya hapo alirejea tena kuinoa Simba  2008-2011 kabla hajatimuliwa kwa mara nyingine tena. Phiri atakumbukwa kwa mengi sana ikiwemo ya kucheza ligi kuu bila ya kufungwa hata mechi moja rekodi aliyoiweka mwaka 2010-2011.

Kutimuliwa kwa Phiri kunakuja siku chache baada ya kutimuliwa kwa kocha wa Yanga, Mbrazil Marcio Maximo.

LIKE RIHANNA LIKE JOKATE



They are bonded by a common behaviour! They love kids!

Sunday, December 28, 2014

MY REPENTANCE (KUTUBU KWANGU)- 4


ILIPOISHIA:
Kwa kuwa nilikua nimevaa taiti na sidiria tu huku juu nikiwa nimejifunga mtandio mwepesi, umbo langu lilionekana vizuri kabisa, uzalendo ukamshinda Ibrahim, akanitamkia:
“Kumbe umeumbika hivi? Loh, mpenzi wako anafaidi.” Nikacheka sana kwa furaha kwani nilichokuwa nakitaka, kilikuwa kimetimia. Tayari Ibrahim alishaanza kuonesha dalili za kunitaka kimapenzi.
SASA ENDELEA...
Unajua sisi wanawake wengi huwa tunapenda sana kusifiwa, na mtu akishaanza kukusifia, basi ukijirahisisha kwake, lazima mwisho muishie kuwa wapenzi. Baadhi ya wanaume wanaujua udhaifu wetu huu na wamekuwa wakipitia humohumo kukidhi haja za miili yao.
Basi nikazidi kuringa mtoto wa kike, nikamtoa wasiwasi kwamba hakuna mtu yeyote anayenimiliki, nipo ‘singo’.
“Unasema kweli upo singo?”
“Ndiyo, kwa nini huamini?”
“Unajua wanawake wazuri kama wewe mara nyingi huwa hawawezi kuwa singo, tena wengine wanakuwa na mpenzi zaidi ya mmoja.”
“Wala mimi sipo hivyo, wazazi wangu wakali sana na hawapendi kabisa nijihusishe na mambo hayo ndiyo maana nimeamua kuweka nguvu zangu zote kwenye masomo,” nilisema huku nikiyarembua macho yangu mazuri, kauli ambayo ilionesha kumfurahisha sana Ibrahim.
Kwa kuwa sikuwa na nguo nyingine za akiba, ilibidi nivae nguo zangu juu ya zile zilizoloana, tukatoka na Ibrahim na kuanza kutembea kuelekea kwenye gari. Tayari akili za Ibrahim zilishabadilika kabisa kwa sababu hata wakati tukitembea, alikuwa anataka nitangulie mbele kidogo halafu akawa ananitazama kwa nyuma kwa kuibia. Nililijua hilo, nikazidisha vituko.
Basi tulifika kwenye gari, tukaingia na safari ya kurudi nyumbani ikaanza, mazungumzo kati yangu na Ibrahim yalianza kubadilika taratibu, akawa ananiuliza mambo mbalimbali kuhusu maisha yangu kuanzia vitu ninavyovipenda, nisivyovipenda, ratiba yangu ya maisha ya kila siku na mambo mbalimbali kuhusu maisha yangu.

Nilimjibu kila kitu alichotaka kukijua, hatimaye tukafika Morocco. Akasimamisha gari kituoni kisha tukaagana, nilipotaka kushuka, aliniita jina langu, nikageuka na kumtazama.
“Kuna jambo nitakwambia baadaye kwenye simu, tafadhali usikatae,” alisema huku akiwa amevaa uso uliokuwa na ujumbe mzito kwangu, nilitabasamu na kumtoa wasiwasi, nikashuka.

Friday, December 26, 2014

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 3


ILIPOISHIA:
Kama hiyo haitoshi, nilimtumia ujumbe mfupi mzuri wa kumtakia usiku mwema, naye akanijibu ndani ya muda mfupi tu, nikalala na kuukumbatia mto wangu huku joto tamu likiendelea kuzunguka kwenye mwili wangu.
SASA ENDELEA...
Niseme tu wazi kwamba nilishampenda sana Ibrahim tangu nilipomuona kwa mara ya kwanza tu, na sasa nilikuwa tayari kufanya chochote, hata ikibidi kujitongozesha ilimradi awe mpenzi wangu.
Naomba watu wasinielewe vibaya kwa sababu najua kwa mila za Kitanzania, ni vigumu sana mwanamke kueleza hisia zake za kimapenzi, tumezoea kwamba sisi ni watu wa kutongozwa tu.
Wapo wengi tu ambao walikuwa wakiwapenda watu fulani ila kwa sababu ya kukosa ujasiri, wakajikuta wakiolewa na watu ambao wala hawakuwahi kuwafikiria kwenye maisha yao.
Niliamua kujitoa mhanga mtoto wa kike, nikajiapiza kuwa lazima nimpate Ibrahim. Wala kilichonizuzua halikuwa gari lake au kusikia kwamba anafanya kazi benki, walaa! Ni mapenzi ya dhati ndiyo yaliyonisukuma mpaka kupata ujasiri wa namna ile.

Niliendelea kumfikiria Ibrahim mpaka usingizi uliponipitia, kesho yake asubuhi nikawahi kuamka kama kawaida yangu na kujiandaa kwa ajili ya kwenda chuo. Nilipomaliza kuvaa, niliwaaga baba na mama kama ilivyo kawaida yangu kila siku kisha nikatoka na kuanza kutembea kuelekea kituo cha daladala.
Siku hiyo hakukuwa na mvua kama jana yake ingawa kila kona kulikuwa na matope. Kumbukumbu juu ya Ibrahim zikanijia na kujikuta nikitabasamu mwenyewe. Nilitoa simu yangu kwenye mkoba na kutafuta namba yake, nikampigia.

Wednesday, December 24, 2014

A MAN WHO SHOOT OSAMA PROBED FOR RELEASING CLASSIFIED INFORMATION

Credit: ABC News
The Navy is investigating whether a former SEAL who claimed on national television that he shot Osama bin Laden may have revealed classified information about the raid.
In November, Robert O’Neill appeared on Fox News Channel to discuss his role in the raid that killed bin Laden on May 1, 2011 in Abbotabad, Pakistan.
"The Naval Criminal Investigative Service (NCIS) is in receipt of an allegation that Mr. O'Neill may have revealed classified information to persons not authorized to receive such information,” said NCIS Public Affairs Officer Ed Buice in a statement to ABC News. “In response, NCIS has initiated an investigation to determine the merit of the allegations."
Details of the investigation were first reported Tuesday by The Daily Beast.
It is unclear how long the investigation has been underway and who allegedly received the recipients of the classified information he may have provided about the raid.
Robert O'neill
In November, O’Neill appeared on Fox and gave an interview to the Washington Post where he discussed his role in the raid and claimed that he had fired the fatal shots that killed bin Laden. The special operations news website SOFREP.com reported at the time that O’Neill was the SEAL who identified himself as “the Shooter” in a 2013 Esquire magazine article about the raid.

TRIBAL MILITANT ATTACKS KILL AT LEAST 54 IN INDIA

New Delhi (CNN) -- At least 54 people have been killed in a series of attacks by tribal militants in India's remote northeastern state of Assam, a police official said Wednesday.
The attacks involving Bodo militants took place Tuesday, Assam Police Inspector-General S.N. Singh told CNN.
The Bodo fighters, angry about a recent police crackdown that led to several arrests and the seizure of weapons, targeted members of another tribal community, said Khagen Sarma, another local police official.
Bodoland area

POZI ZA MASTAA WA BONGO INSTAGRAM

Ommy Dimpoz

Shetta

Lulu

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 2


ILIPOISHIA:
Naomba umpe namba yangu mwambie anitafute au nipe yake nijue namna ya kumfikishia mzigo wake,” alisema dereva wa ile Carina kwa sauti ya kiungwana mno.
 Nilishusha pumzi ndefu na kuachia tabasamu, nikamwambia kwamba mimi ndiyo Flaviana, nikamsikia akicheka kidogo kisha akaniuliza nipo wapi kwa wakati huo. Nilipomuelekeza, aliniambia nimsubiri hapohapo anakuja.
SASA ENDELEA... 
Kweli baada ya kama dakika tano hivi, ile Carina ilipaki upande wa pili wa barabara, akanipigia simu na kuniuliza kama nilikuwa naliona gari. Nikatoka mbiombio na kukimbia kuvuka barabara. Kwa kuwa bado mvua ilikuwa inanyesha, nilipolifikia gari lake, alinifungulia mlango, nikaingia na kukaa kwenye siti ileile niliyokuwa nimekaa awali, nikamgeukia, na yeye akanitazama, macho yetu yakagongana.

“Pole kwa usumbufu,” aliniambia kwa sauti ya kiungwana, nikaachia tabasamu hafifu huku nikiendelea kujifuta maji ya mvua, nikwamwambia mimi ndiyo napaswa kumpa yeye pole kwani licha ya kunipa lifti bure, nilimpa kazi nyingine ya kunitafuta.
Alinipa begi langu na kuniuliza nilikokuwa nakwenda.
“Naenda chuo, pale jirani na mnara wa askari.”
“Unasomea nini?”
“Nasomea uhasibu.”
“Ooh! Safi sana, mimi pia nilisomea uhasibu pale IFM sasa hivi nafanya kazi benki,” alisema yule dereva huku na yeye akiachia tabasamu, akaniomba kama sitajali anisindikize jirani na chuo ili nisiendelee kulowa.

Nilikubali haraka na kumshukuru sana. Akawasha gari na kwenda mpaka mbele kidogo, akageuza gari na kurudi barabarani, akawa anaendesha gari taratibu huku tukipiga stori za kawaida.
Ndani ya kipindi kifupi tu nilichokaa naye, niligundua kuwa yule kaka alikuwa mtu mmoja mstaarabu sana, asiye na maneno mengi, anayejiheshimu na anayeheshimu watu wengine pia bila kujali umri, jinsia au hali ya kiuchumi.
Alinisogeza mpaka jirani na chuoni kwetu, akalitoa gari barabarani na kupaki pembeni huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Nilitaka kushuka lakini akaniambia nisubiri mvua ipungue kidogo kwani yeye hakuwa na haraka sana kwani ofisi anayofanyia kazi ni jirani na pale.

Tuesday, December 23, 2014

MREMBO APIGWA RISASI, AFARIKI

Habari zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kwamba binti huyu (pichani) ambaye bado jina na mahali anapoishi havijafahamika, amepigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi mchana wa leo, Morocco, nyuma ya makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam. 

Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, majambazi hao walikuwa wametoka kufanya uhalifu kwenye kibanda kimoja cha M-Pesa kilichopo jirani na eneo hilo, wakati wakiondoka wakawa wanarusha risasi hovyo na moja ikampata mrembo huyu na kuyakatisha maisha yake papo hapo.
mwili wa marehemu baada ya kupigwa risasi

WE WISH YOU MARRY X-MAS

HASH POWER 7113 and Hashim's Family wishes you a prosperious festive season! Marry X- Mass

CHE GUEVARA, MAMBO 10 USIYOYAJUA!


Na Hashim Aziz
Wengi wamezoea kuiona picha yake kama alama ya ukombozi na mapinduzi ya kweli lakini ni wachache wanaomjua vizuri. Jina lake halisi anaitwa Ernesto ‘Che’ Guevara, alizaliwa Juni 14, 1928, Rosario, Argentina na yafuatayo ni mambo kumi kumhusu:
1. Alikuwa mwanaharakati na mwanamapinduzi aliyezisaidia nchi nyingi kupata uhuru kupitia vita vya msituni, zikiwemo Cuba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji na nyingine nyingi.
Ernesto Che Guevara
2. Licha ya kusumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, aliweza kusafiri sehemu mbalimbali, zikiwemo zenye baridi kali na kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kuwasaidia wanyonge.
3. Alisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Buenos Aires alikohitimu na kupata digrii (shahada) ya udaktari wa binadamu.
4. Akiwa bado anasomea udaktari, alifunga safari kwa kutumia pikipiki ambapo alisafiri umbali wa kilometa 4,500 na baadaye kilometa nyingine 8,000 kutembelea nchi mbalimbali za Amerika ya Kusini. Hali ya umaskini na ukandamizaji aliyoikuta huko ndiyo iliyomfanya awe mpiganaji wa msituni.

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 1

Naitwa Flaviana Joel, mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nane. Nilibahatika kuolewa miaka kumi iliyopita, nikiwa bado msichana mbichi katika umri wa miaka kumi na nane tu.
Niliolewa na mume wangu kipenzi, Ibrahim au Ibra kama mwenyewe nilivyozoea kumuita ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye benki moja maarufu ambayo sitaitaja jina kwa sababu maalum, iliyopo hapa jijini Dar es Salaam.

Kabla Ibra hajanioa, tulidumu kwenye uchumba kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja, kipindi hicho nikiwa nasoma chuo kimoja cha uhasibu kilichopo Posta, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, nikiwa ndiyo kwanza nimeanza mwaka wa kwanza.
Baada ya ndoa, mimi na Ibra tulihamia Mbezi Beach kwenye nyumba yetu ambako tuliishi pamoja mpaka tulipokuja kutengana kwa sababu ambazo ndizo hasa zilizonifanya nitafute nafasi hii ya kutubu hadharani na kukiri kwa kinywa changu yote niliyowahi kuyafanya.

Wednesday, November 5, 2014

MBINU 10 ZA KUFUFUA PENZI LILILOKUFA

HASH POWER 7113
NI matumaini yangu kwamba msomaji wangu uko poa. Ni wiki nyngine tunapokutana kwenye busati letu ambapo tunajuzana na kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu uhusiano wa kimapenzi.
Nakushukuru wewe unayetuma ujumbe mfupi ukitoa maoni, kuchangia au kutaka ushauri kuhusu mambo mbalimbali, hata kama hujajibiwa elewa kwamba ujumbe wako umefika na utafanyiwa kazi.
Mada ya leo ni maalum kwa watu ambao tayari mpo kwenye uhusiano wa kimapenzi, iwe ni wapenzi wa muda mrefu, wachumba au wanandoa.
DALILI ZA PENZI LILILOKUFA
Umewahi kuhisi kwamba penzi lako limefikia mwisho japo bado upo na mpenzi wako, mchumba au mumeo/mkeo? Yaani upoupo tu, zile hisia tamu za mapenzi

MMEGOMBANA NA MPENZI WAKO? FUATA MBINU HIZI KURUDISHA MAPENZI

HASH POWER 7113
Kugombana ni jambo ambalo halikwepeki katika uhusiano wa kimapenzi. Upo ugomvi ambao ni wa kawaida na huisha kirahisi lakini upo ugomvi ambao huwa mkubwa na kama ukitokea na ukashindwa kujua nini cha kufanya kuweka mambo sawa, husababisha ufa kwenye penzi lenu.

Leo tutazungumzia mambo ya muhimu ya kufanya inapotokea wewe na mpenzi wako mmeingia katika ugomvi mkubwa, mmetoleana maneno machafu au hata kupigana.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...