Thursday, December 21, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 55


ILIPOISHIA:
“Ukitaka kuendelea kuishi, kazi ni moja tu, tunataka utuoneshe Shenaiza alipo na pia utuambie mbinu zote za kishirikina ulizomfanyia baba yake alipokuja kwako kuomba kinga ya kufanikisha mambo yake ya kishetani,” alisema Junaitha, mwanamke huyo akaanza upya kulia huku akitingisha kichwa chake, hali iliyozidi kunifanya nikose majibu. Aliendelea kulia na mara akaanza tena kutoa muungurumo kama mnyama mkali wa porini, akawa anafurukuta kwa nguvu.
SASA ENDELEA...
“Usitake kututisha hapa na ukiendelea na upuuzi wako nitakuua kwa mikono yangu mwenyewe, unajua ni kwa kiasi gani nina hasira na wewe?” alisema Junaitha kwa sauti nzito ya kunguruma, ambayo sikuwahi kumsikia hata siku moja, yule mwanamke mzee akanywea na kurudi kwenye hali yake ya kawaida lakini bado alikuwa akilia huku akitingisha kichwa, akionesha hayupo tayari kuzungumza kitu chochote.
“Wala sikulazimishi, uchaguzi ni wako, ukitaka kuendelea kuishi ni lazima uzungumze na ukitaka kufa endelea kukataa.”
“Hata nikizungumza nitakufa tu, hawezi kuniacha, ataniua.”
“Nani, unamzungumzia nani?”
Badala ya kujibu, yule mwanamke alionesha kwa ishara, Junaitha na mimi tukageuka kutazama kule alikokuwa anaonesha.
“Mungu wangu,” nilijikuta nimetamka wa sauti kubwa, Junaitha akaniwahi na kuniziba mdomo.

VYAKULA VINAVYOONGEZA NGUVU ZA KIUME




Kuongezeka kwa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa vijana na wanaume kumesababisha wengi kuhaha huku na kule kutafuta madawa makali ya kutibu tatizo hilo.
Dawa nyingi za hospitali ambazo hutumika kumaliza au kupunguza tatizo hili, zimebainika kuwa na madhara (side effects) hivyo kusababisha wataalamu kuanza kuhangaika kugundua tiba kwa njia ya vyakula.

CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la upungufu wa kiume mara nyingi husababishwa na matatizo ya kimwili au ya kisaikolojia ambapo mwanaume huwa dhaifu wakati wa tendo na wakati mwingine kushindwa kabisa kufanya chochote.

Sababu za kimwili (Physical) zinaweza kuwa ni kwa sababu mishipa ya damu inashindwa kufikisha damu yenye msukumo kwenye viungo vya uzazi.

Kuongezeka kwa kiwango cha mafuta mwilini husababisha mafuta hayo kuganda kwenye kuta za mishipa ya damu na kuzuia damu kutiririka vizuri, tatizo ambalo kitaalamu huitwa atherosclerosis.

Wednesday, December 20, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 54


ILIPOISHIA:
Kwa mbali niliwaona watu kadhaa wakiwa wamevaa nguo zilizokuwa zikifanana na zile nilizovaa, lakini kila mmoja akiwa ameinamisha kichwa kuonesha kwamba yupo usingizini. Kasi ya treni ilizidi kuongezeka na kadiri tulivyokuwa tunasonga mbele, milio ya ajabu ilianza kusikika kwa mbali, ukichanganya na muungurumo wa treni lile la ajabu, na giza totoro lililokuwepo, hali ilikuwa ya kutisha mno.
SASA ENDELEA...
“Poooh! Pooh!” honi kali ya treni ilisikika ikifuatiwa na msuguano mkali wa vyuma, nikaona watu wote waliokuwa mle ndani ya treni la ajabu wakirushwa upande wa mbele. Nilijishikilia kwa nguvu, treni likajisugua juu ya reli na kusababisha cheche nyingi ziruke, eneo lote likawa kama karakana ya kutengenezea vifaa vya chuma.
Treni liliposimama, nilishtukia nimeshashuka, hata sikumbuki nilipitia mlango gani, macho yangu yakatua kwenye kitu kilichosababisha treni hiyo ifunge breki za ghafla kiasi kile. Msichana mmoja, aliyekuwa na macho yanayong’ara kama paka awapo gizani, nywele ndefu zilizokosa matunzo na kucha kama mnyama wa porini alikuwa amekaa katikati ya reli huku akinguruma kama mnyama wa kutisha.
Sijui nilipata wapi ujasiri wa kumsogelea, kadiri nilivyokuwa nasogea mbele ndivyo msichana yule alivyozidi kutoa mlio wa kunguruma na kusababisha nipatwe na hofu kubwa mwilini. Lakini cha ajabu, eti muda huohuo nilikuwa nasikia sauti ya Junaitha ikiniambia napaswa kuishinda hofu yangu, nikazidi kumsogelea.

Tuesday, December 19, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 53


ILIPOISHIA:
Tukaanza kuulizana maana ya kile kilichofanyika mpaka tukafanikiwa kumuokoa Shamila ambapo Junaitha alianza kutufundisha mambo ambayo hakuna aliyekuwa akiyajua kati yetu, ambayo kama hujui ungeweza kusema ni uchawi wa hali ya juu.
“Hata ukitaka kuingia benki na kuchukua kiwango chochote cha fedha unachotaka, inawezekana, mbona rahisi tu, nitawafundisha,” alisema.
SASA ENDELEA...
“Mh!” niliguna kama ishara ya kutoamini kile alichokisema, akanigeukia na kuniambia hakuna kitu kisichowezekana chini ya jua. Alianza kutufafanulia jinsi nguvu zisizoonekana kwa macho zilivyo na uwezo wa kufanya chochote na kikatimia.
“Hujawahi kuona mtu anakunja kijiko kwa kukitazama tu au mtu anahamisha glasi ya maji kwa kuitazama tu?” alisema. Nilishawahi kusikia habari hizo lakini sikutaka kabisa kuziamini mpaka nishuhudie mwenyewe.
“Kabla ya yote nataka kujua nini kilichotokea mpaka tukafanikiwa kumuokoa Shamila?” niliuliza, nikamgeukia Shamila ambaye muda wote alikuwa kimya kabisa, akionesha bado kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.
“Eti kwani wewe ulihisi nini wakati tumekuja kukuokoa?”

Monday, December 18, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 56


ILIPOISHIA:
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
SASA ENDELEA...
Kweli nilifumba macho, baba na baba yake Rahma wakawa wanazungumza maneno fulani ambayo sikuwa nayaelewa kwa kuyarudiarudia, kisha nikaanza kusikia kama upepo mkali ukianza kuvuma kwa nguvu, sikuelewa tena kilichoendelea mpaka niliposikia baba akinitingisha kwa nguvu.
“Tumeshafika! Fumbua macho,” alisema baba, nikafumbua macho na kujikuta nikiwa kwenye mazingira tofauti kabisa. Sikuelewa tumetumia muda gani maana ninachofahamu mimi kuna umbali mrefu sana kutoka Mbeya mpaka Dar es Salaam, ni safari ya kutoka alfajiri na mapema na kufika usiku.

Thursday, December 14, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 55


ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA...
“Lakini baba...”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 52



ILIPOISHIA:
“Chukua taulo pale kabatini ingia bafuni ukaoge,” alisema akiwa amekaa juu ya kitanda kikubwa cha kisasa akihangaika kufungua zipu ya gauni alilokuwa amevaa, nikaelekea pale kwenye kabati aliponielekeza, nikachukua taulo na kuanza kuelekea kwenye lile bafu la ndani kwa ndani kule chumbani kwake.
Nililazimika kuingia na nguo zote bafuni kwani nilikuwa naona aibu kuvua hata shati mbele ya macho yake.
SASA ENDELEA...
“Sasa utaingiaje bafuni na nguo? Hebu toa ushamba wako hapa,” alisema Junaitha huku akicheka, nikajikuta nikiwa kwenye wakati mgumu sana. Japokuwa nilikuwa nimeshaingia, ilibidi nitoke, nikajikaza kisabuni na kuvua fulana niliyokuwa nimeivaa, bandeji iliyofungwa juu ya jeraha langu ikaonekana vizuri.
“Mh! Kumbe uliumia kiasi hicho, hebu njoo nikuangalie,” alisema, nikavungavunga kwa aibu mwishowe nikasogea mpaka pale kitandani alipokuwa amekaa. Akanisogelea na kuanza kunitazama vizuri pale kifuani.
“Unajisikiaje kwani?” aliniuliza huku akiligusa jeraha langu kwa juujuu.
“Sasa hivi nina afadhali kubwa,” nilimjibu, akaendelea kulitazama jeraha hilo kwa muda kisha akaniambia nisiwe na wasiwasi, kuna dawa atanipaka ambayo itanifanya nipone haraka kuliko kawaida, niliitikia kwa kutingisha kichwa.

Wednesday, December 13, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 54


ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA...
“Lakini baba...”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.
Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.
Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.
Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.
Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.
Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.
Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.
Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.
“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.
“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.
“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.
Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.
Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.
“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.
Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.
“Umeshajiandaa?”
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.
“Haya nifuate.”
“Lakini bado sijala.”
“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.
Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.
Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!
Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.
Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.
Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.
Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.
Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.
“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 51


ILIPOISHIA:
“Sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na nguvu kubwa kiasi hicho, hongera sana, utanifaa sana wewe,” alisema huku akipitisha mkono wake mmoja begani kwangu kichovu kisha akanigeukia, tukawa tunatazamana. Katika hali ambayo sikuitegemea hata kidogo, nilishangaa yule mwanamke akinibusu, tena mdomoni, nikashtuka mno.
“Hongera sana, ila inabidi upunguze mambo ya wanawake, utakuwa na nguvu zaidi ya hizi ulizonazo,” aliniambia huku akinitazama usoni.
SASA ENDELEA...
“Sijakuelewa,” nilimwambia, akashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri pale juu ya zulia. Bado si Raya, Shamila wala Firyaal waliokuwa wamezinduka.
“Utanielewa tu,” inabidi kwanza tukaoge kuondoa uchovu halafu tuwasaidie na hawa nao warudi kwenye hali yao ya kawaida, tuna kazi nyingine ya kumsaidia Shenaiza, ni lazima arudiwe na fahamu zake, tena ikiwezekana haraka iwezekanavyo,” alisema mwanamke huyo kisha akapiga miayo mfululizo na kujinyoosha.
“Kwa kawaida, kila binadamu huwa anazalisha nguvu, nadhani hilo nilishakueleza kutoka mwanzo ingawa ni wachache sana wanaolitambua hili.
“Yaani ni kama kupepesa kope, unajua ni mpaka mtu akukumbushe kwamba muda wote macho yako yanapepesa kope ndiyo unakumbuka?” alisema, nikawa sioni chochote kipya kwenye mazungumzo yake kwa sababu ni jambo ambalo nilikuwa nimeshalisikia sana maishani mwangu kwamba kila binadamu anazalisha nguvu zisizoonekana.

Tuesday, December 12, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 53


ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA...
Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 50


ILIPOISHIA:
“Ndiyo,” nilisema kwa kujiamini, akanitazama usoni kisha akaenda mlangoni na kufungua, akawaita Raya na Firyaal, wakaingia ndani na tukakaa tena kama tulivyokuwa tumekaa mwanzo, kazi ikaanza upya huku akinisisitiza kuwa makini na kuishinda hofu ndani ya moyo wangu, nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
SASA ENDELEA...
Kazi ilianza upya, akatusisitiza kila mmoja awe anavuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na siyo kifua kama wengi tunavyopumua, pia akatutaka kuhakikisha kila mmoja akili yake aielekeza eneo la tukio.
Muda mfupi baadaye, ile hali ilianza kunitokea tena, nikawa najihisi kama naelea angani huku mwili mwingine ukiwa palepale tulipokuwa tumekaa. Hofu ilianza kunijia tena lakini nilipokumbuka maneno ya yule mwanamke, nilijitahidi kuishinda hofu.
Nikaendelea kutuliza kichwa na kufumba na kufumbua, nilijikuta nikiwa pale hospitalini nilipokuwa nimelazwa. Niliweza kuona kila kitu kilichokuwa kikiendelea, wagonjwa waliokuwa wakiingia na kutoka, manesi na madaktari waliokuwa wakikimbizana huku na kule kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano.
Upande wa Kaskazini kulikuwa na magari matatu ya polisi yaliyokuwa yamepaki huku askari wengi wenye silaha wakirandaranda huku na kule.
“Kumetokea nini kwani leo hapa?”

Monday, December 11, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 52


ILIPOISHIA:
Lakini ni hapo pia nilipokumbuka ile ajali nyingine ya bodaboda niliyoisababisha na pia nikakumbuka kisanga cha dereva wa Bajaj aliyekuwa akipaki jirani na hapo kwa akina Rahma na jinsi nilivyomkomesha asubuhi hiyo. Sikujua kama amesharudi au la na sikujua siku atakaponiona tena atasema nini.
Nikiwa nimezama kwenye dimbwi la mawazo, nilisikia mlango ukifunguliwa, Rahma akaingiza kichwa na kuchungulia ndani, macho yangu na yake yakagongana.
SASA ENDELEA...
“Togo!” aliita Rahma kwa sauti ya udadisi huku akiingia ndani na kuurudishia mlango taratibu, nikakaa vizuri kumsikiliza maana nilikuwa najua kabisa kwamba alikuwa na maswali mengi ya kuniuliza kutokana na mabadiliko makubwa niliyokuwa nayo kwa siku kadhaa zilizopita.
“Najua kwamba nalazimisha mapenzi kwako, najua kwamba unajisikia aibu kuwa na mpenzi ambaye amekuzidi umri na najua pia kwamba kama isingekuwa mimi kukuanza usingekuwa na mawazo yoyote ya kutoka kimapenzi na mimi kwa sababu hunipendi,” alisema Rahma kwa sauti ya kulalama mno, akionesha kuwa na maumivu makali ndani ya moyo wake.
“Leo nataka uniambie jambo moja tu, nimechoka kuteseka kimapenzi, kwa kipindi chote tangu nikiwa msichana mdogo nimekuwa nikijitunza na kujiheshimu sana, sasa isiwe kwa sababu nimetokea kukupenda basi ukaanza kunitesa kwa makusudi na kunidhalilisha, nataka uniambie kwamba hunitaki ili nijue moja,” alisema Rahma, safari hii machozi yakiwa yanamchuruzika na kulowanisha uso wake mzuri.
Nilijisikia kuwa na hatia kubwa ndani ya moyo wangu kwa jinsi Rahma alivyokuwa akilalamika na kulia kwa sababu yangu. Rahma hakustahili kulia kwa sababu yangu kwa sababu maskini ya Mungu hakuwahi kunifanyia jambo lolote baya na ndani ya kipindi kifupi tu nilichokaa naye, alinionesha mapenzi ya dhati kabisa kutoka moyoni mwake.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 49


ILIPOISHIA:
Ndani ya dakika mbili tangu tukae mkao huo, kuna mambo ya ajabu yalianza kunitokea, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kwenda mbio kuliko kawaida kutokana na kile nilichokuwa nakishuhudia.
SASA ENDELEA...
Nilianza kuona ile hali kama ambayo ilinitokea siku ile nilipovamiwa barabarani na kujeruhiwa vibaya na baadaye kuingia kwenye ulimwengu wa tofauti, nikawa najihisi kwamba japokuwa nilikuwa nimekaa pale chini na wenzangu, taswira nyingine ya mwili wangu ilikuwa ikianza kupaa juu na kuelea angani, nikawa sielewi nini kinachotaka kutokea.
Cha ajabu ni kwamba, yule aliyekuwa akianza kupaa ndiyo alikuwa mimi kwa sababu nilikuwa najitambua kabisa, nikainamisha kichwa na kutazama chini, nikajiona nikiwa nimekaa pale juu ya zulia, nikiwa nimeshikana mikono na yule mwenyeji wetu, Raya na Firyaal, jambo ambalo lilisababisha hofu kubwa ndani ya moyo wangu.
“Noo! Sitaki kufa tena, sitakiii,” nilisema kwa sauti ya juu, nikashtukia nikiporomoka kutoka pale juu nilipokuwa nikielea, nikaanguka chini kama furushi na kujibamiza sakafuni kwa kishindo.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 51


ILIPOISHIA:
Lakini ni hapo pia nilipokumbuka ile ajali nyingine ya bodaboda niliyoisababisha na pia nikakumbuka kisanga cha dereva wa Bajaj aliyekuwa akipaki jirani na hapo kwa akina Rahma na jinsi nilivyomkomesha asubuhi hiyo. Sikujua kama amesharudi au la na sikujua siku atakaponiona tena atasema nini.
Nikiwa nimezama kwenye dimbwi la mawazo, nilisikia mlango ukifunguliwa, Rahma akaingiza kichwa na kuchungulia ndani, macho yangu na yake yakagongana.
SASA ENDELEA...
“Togo!” aliita Rahma kwa sauti ya udadisi huku akiingia ndani na kuurudishia mlango taratibu, nikakaa vizuri kumsikiliza maana nilikuwa najua kabisa kwamba alikuwa na maswali mengi ya kuniuliza kutokana na mabadiliko makubwa niliyokuwa nayo kwa siku kadhaa zilizopita.
“Najua kwamba nalazimisha mapenzi kwako, najua kwamba unajisikia aibu kuwa na mpenzi ambaye amekuzidi umri na najua pia kwamba kama isingekuwa mimi kukuanza usingekuwa na mawazo yoyote ya kutoka kimapenzi na mimi kwa sababu hunipendi,” alisema Rahma kwa sauti ya kulalama mno, akionesha kuwa na maumivu makali ndani ya moyo wake.
“Leo nataka uniambie jambo moja tu, nimechoka kuteseka kimapenzi, kwa kipindi chote tangu nikiwa msichana mdogo nimekuwa nikijitunza na kujiheshimu sana, sasa isiwe kwa sababu nimetokea kukupenda basi ukaanza kunitesa kwa makusudi na kunidhalilisha, nataka uniambie kwamba hunitaki ili nijue moja,” alisema Rahma, safari hii machozi yakiwa yanamchuruzika na kulowanisha uso wake mzuri.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 48


ILIPOISHIA:
“Nakupenda Jamal,” alisema kisha akanibusu kwenye shavu langu la upande wa kushoto, mwili wote ukasisimka tena, nikakosa hata cha kujibu zaidi ya mimi kumkumbatia pia na kumbusu, uvuguvugu wa joto la mwili wake ukanifanya nitamani niendelee kumkumbatia lakini nilipokumbuka mtihani mzito uliokuwa mbele yangu, nilimuachia, nikatoka haraka na kwenda kumuamsha Raya, harakaharaka tukaanza kujiandaa.
SASA ENDELEA...
Muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa tumeshamaliza kujiandaa, mimi na Raya tukasaidiana kumbeba Shenaiza ambaye bado alikuwa haelewi chochote kinachoendelea, Firyaal akaenda kuwasha gari. Ilibidi kila kitu kifanyike harakaharaka kama Shamila alivyotuambia.
Kwa bahati nzuri tulifanikiwa kutoka salama, tukafunga milango yote na kuiacha funguo mahali alipokuwa ametuelekeza Shamila. Kwa kuwa bado ilikuwa ni asubuhi, hakukuwa na foleni sana barabarani, safari ya kuelekea Kimara Temboni ikaanza.
Ilibidi nimuombe Raya simu yake kwa ajili ya kumpigia yule mtu ambaye Shamila aliniambia kwamba ni ndugu yake ambaye ndiye angeenda kutupokea na kutupa hifadhi. Namshukuru Mungu kwamba nilivyopiga mara moja tu, alipokea, tukazungumza na kuelewana.
Nikawa namuelekeza Firyaal kama na mimi nilivyoelekezwa na yule mwenyeji wetu, kwa bahati nzuri tulipofika Kimara Temboni tu, mwanamke wa makamo, mweupe na mnene kiasi, alitupokea. Yeye alikuwa amepanda bodaboda, akatonesha ishara kwamba tumfuate, Firyaal ambaye alikuwa na uzoefu wa kutosha wa kuendesha gari, akawa anamfuata.

Friday, November 17, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 50


ILIPOISHIA:
Sijisifii lakini ukweli ni kwamba katika suala la mbio, nilikuwa na uwezo mkubwa sana, dakika chache baadaye nikawa nimeshatokomea kwenye mashamba ya mikorosho na minazi, kelele za wale watu waliokuwa wakinifukuza zikiwa bado zinaendelea kusikika, sauti ya baba ikasikika tena masikioni mwangu lakini safari hii, ilikuwa na maelezo ambayo yalinimaliza kabisa nguvu, nikajua mwisho wangu umewadia. Niliujutia sana uamuzi wangu wa kujipeleka mwenyewe kwenye mdomo wa mamba.
SASA ENDELEA...
“Inabidi uvue nguo zote na kukimbia kuelekea upande wa Magharibi mpaka uvuke barabara ya lami kisha kimbia mpaka utakapoukuta mti mkubwa wa mbuyu, uzunguke mara saba kisha fumba macho, usifumbue mpaka nitakapokwambia,” sauti ya baba ilisikika masikioni mwangu.
Yaani nivue nguo zote na kuanza kukimbia nikiwa mtupu? Kibaya zaidi, upande huo wa Magharibi aliokuwa anausema ilikuwa ni kulekule nilikokuwa nakimbia. Kwa lugha nyepesi nilitakiwa kuanza upya kukimbia kurudi kule nilikotoka, safari hii nikiwa mtupu! Ilikuwa ni zaidi ya mtihani.
Kitu pekee nilichokuwa nakihitaji, ilikuwa ni kuokoa na balaa hilo kwani kwa jinsi wale wazee waliokuwa wakinikimbiza walivyokuwa na hasira, kama wangenitia mikononi mwao sijui nini kingetokea. Ilibidi nipige moyo konde, harakaharaka nikavua nguo zote na viatu, nikavikunja na kuvitia kwapani.

Thursday, October 26, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 49


ILIPOISHIA:
Nilipofika, na mimi nilijifanya ni mwombolezaji wa kawaida tu, nikawasalimia baadhi ya watu kisha nikajichanganya na waombolezaji wengine. Ghafla nilishtuka baada ya kuona kitu ambacho sikukitarajia, nikahisi kijasho chembamba kikianza kunitoka, mara hirizi yangu ikaanza kunibana kwa nguvu, kufumba na kufumbua kamba yake ikakatika, ikadondoka chini!
SASA ENDELEA...
“Mungu wangu!” nilijikuta nimetamka kwa sauti, hali iliyofanya watu wote washtuke, hata wale ambao hawakuwa wameniona nikiwasili eneo hilo, waligeuka na kunitazama, nikajihisi mwili ukiishiwa nguvu na kunyong’onyea kama nimepigwa na shoti ya umeme.
Sikujua nifanye nini kwa wakati huo, watu wakawa bado wamenikazia macho, kila mtu akiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua mimi ni nani na nini kimetokea mpaka nikashtuka kiasi hicho.
“Wasalimu watu wote kwa heshima kisha wape pole,” nilisikia sauti ya baba masikioni mwangu, ghafla nikajikuta nimepata nguvu na kuwa na imani kubwa kwamba hata iweje, baba ameshajua kinachoendelea kwa hiyo atanisaidia.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 47


ILIPOISHIA:
“Nataka nikalale na dada Shenaiza,” alisema kwa sauti ya kudeka huku akinisogelea na kujilaza kifuani kwangu, nikapitisha mkono wangu na kumshika kiunoni, nikamuona akiruka kama aliyepigwa na shoti ya umeme.
SASA ENDELEA...
“No! Usifanye hivyo,” alisema Firyaal huku akinitoa mkono kwa staili ya ‘sitaki nataka’, nikamvutia kwangu na kusababisha tuwe tunatazamana katika umbali usiozidi nchi tano, kiasi cha kila mmoja kuwa anazisikia pumzi za mwenzake.
“This is not the right time,” (Huu siyo muda muafaka) alisema huku akiipitisha mikono yake na kunishika shingoni, kwa mara nyingine nikamshika kiunoni, akashtuka tena, safari hii kwa nguvu zaidi na kufumba macho yake mazuri, tukagusanisha ndimi zetu na kuanza kuwaiga njiwa wanavyoyalisha makinda yao.
Jambo la ajabu lilitokea kwenye hisia zangu, nikawa nahisi kama nipo kwenye ulimwengu mwingine wa tofauti kabisa, tuliendelea kugandana kama ruba kwa sekunde chache, kelele za kitasa cha chumba alichokuwa amelala Raya ndizo zilizotushtua.
Harakaharaka nikamuachia Firyaal na kumuonesha kwa ishara kwamba aende chumbani alikokuwa amelala dada yake, kweli alifanya hivyo, akakimbia kwa kunyata wakati mimi nikienda kumfungulia Raya.

Wednesday, October 25, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 48


ILIPOISHIA:
Nilichopanga kichwani, ni kuchukua maelekezo vizuri kwa yule mtu aliyesema marehemu ni jirani yake kisha kwenda kwanza mpaka eneo la ajali na baada ya hapo, nitakwenda Tumbi kujionea hali ya mgonjwa na hiyo maiti kama nitapata nafasi. Nilikuwa na shauku kubwa ya kujua kila kitu maana moyo wangu ulikuwa na hatia kubwa, hasa kutokana na jinsi taarifa za ajali ile zilivyowaumiza mioyo abiria wengi.
SASA ENDELEA...
Safari iliendelea na hatimaye tukawasili Kibaha, gari liliposimama tu, nilimuwahi yule abiria aliyekuwa akisimulia kuhusu ile ajali, nikamsalimu na kumuomba anielekeze ulipo msiba kwa sababu aliyefariki ni ndugu yangu.
“Ni Mlandizi, ukishuka tu pale kituoni, uliza mtu yeyote eti kwenye msiba wa mtoto aliyekufa kwenye ajali ni wapi? Huwezi kupoteza, mtoto alikuwa anafahamika sana yule kutokana na jinsi alivyokuwa na heshima,” alisema yule abiria, nikamshukuru.
Nilipoachana naye, nilimfuata dereva ili anielekeze sehemu gari lilipopata ajali kwani kuna muda nilimsikia akisema kwamba eneo hilo ni baya sana, ajali huwa zinatokea mara kwa mara. Eneo lenyewe nilikuwa nalifahamu lakini sikujua naweza kufikaje.

Seven Days ih Hell (Siku Saba Kuzimu)- 46


ILIPOISHIA:
“Ulisema unasomea IT, hebu chukua ile laptop pale uje hapa unisaidie kitu,” nilimtega, naye ni kama alikuwa akiisubiri nafasi hiyo, harakaharaka aliinuka pale alipokuwa amekaa, akaenda kuchukua laptop ya Shamila na kuja nayo kwenye lile kochi nililokuwa nimekaa, akaja kukaa karibu kabisa na mimi kiasi cha kunifanya niwe nalisikia joto la mwili wake, lililonakshiwa kwa manukato mazuri aliyokuwa amejipulizia.
Mara mlango wa jikoni ukafunguliwa.
SASA ENDELEA...
“Vipi?” Shamila aliuliza huku akiwa ni kama ameshtuka f’lani hivi kuniona nikiwa nimekaa jirani namna ile na Firyaal.
“Kuna kazi namuelekeza anisaidie.”
“Ooh! Tena huyo atakufaa zaidi, si amesema anajuajua mambo ya IT?”
“Ndiyo japo bado sijathibitisha,” nilisema huku nikijifanya kumkandamiza Firyaal ili kuua soo, naye ni kama alijua kilichokuwa ndani ya akili yangu, akatulia kiasi cha kufanya iwe vigumu kwa Shamila kuelewa kilichokuwa kikiendelea kati yangu na msichana huyo mdogo lakini mrembo.
Akaenda kwenye friji na kuchukua baadhi ya vifaa kisha akarudi jikoni, akaniacha nikiwa bize nikijifanya namuelekeza kitu Firyaal ambaye naye alikuwa akiitikia kwa umakini, alipoingia jikoni tukatazamana.

Tuesday, October 24, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 47


ILIPOISHIA:
“Broo vipi unaenda?” alisema huku akisimamisha Bajaj yake jirani kabisa na pale nilipokuwa nimesimama, nadhani kwa sababu ya kigiza kile cha alfajiri hakuwa ameniona vizuri, aliniponisemesha na mimi kumtazama usoni, niliona jinsi alivyoshtuka, akataka kuondoa Bajaj yake haraka lakini alishachelewa.
SASA ENDELEA...
Nilishika bomba la Bajaj yake na kuingia, nikakaa siti ya nyuma, akawa ni kama amepagawa maana hakujua kama akimbie na Bajaj au aiache akimbie kwa miguu.
“Simama kwa usalama wako,” niliongea kwa sauti ya mamlaka, nikamuona jinsi alivyokuwa akihangaika, kijasho chembamba. Hakuwa tayari kusimama, inaonesha alikuwa akiniogopa sana, nilichoamua kukifanya ilikuwa ni kumtumia kutimiza mahitaji yangu.
Nilivuta pumzi ndefu na kuzibana kama baba alivyonielekeza, nikaweka utulivu kidogo kisha nikamuamrisha kunipeleka Ubungo. Nilifanya hivyo kwa kuzungumza moyoni maana ndivyo nilivyoelekezwa, nikamuona akizidi kuichochea Bajaj yake.
Hata hivyo, njia aliyokuwa anapita, ilikuwa ni ileile tuliyoipita jana wake wakati tukielekea Ubungo kupanda magari ya kwenda Kibaha. Alizidi kuongeza kasi, akawa anakimbia kama mshale, mwenyewe alidhani ananikimbia lakini kumbe tayari nilishaingia ndani ya akili yake.
Huwa si kawaida ya Bajaj kukimbia spidi kubwa na kuyapita magari lakini siku hiyo iliwezekana. Baada ya dakika kadhaa za kukimbia kwa kasi kubwa kwenye lami, hatimaye tuliwasili Ubungo, nikavuta tena pumzi na kumpa amri ya kusimama kwenye kituo cha mafuta.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 45


ILIPOISHIA:
Nguo maalum aliyofunikwa upande wa kichwani, ilifanya iwe vigumu kwa mtu yeyote kumtambua, tukaendelea kusonga mbele mpaka tulipofika kwenye geti la kutokea nje ya hospitali, hapo tukakumbana na kipingamizi ambacho hakuna aliyekitegemea, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Haroo! Mnaenda wapi usiku? Harafu hao wagonjwa mbona mumewafunika sura, wafunueni, hima,” alisema askari aliyekuwa amevalia sare maalum, mkononi akiwa ameshika bunduki. Ilibidi Shamila atumie mbinu ya ziada kumtuliza kwani tayari alishaonesha wasiwasi nao.
“Kamanda, ina maana hata mimi hunijui? Hiki hapa ni kitambulisho changu, naitwa Shamila, nawapeleka wagonjwa wangu hapo kwenye maabara za Lancet hapo nje kwenye kipimo cha MRI, si unajua humu ndani hakuna na isitoshe kesho asubuhi kutakuwa na foleni kubwa sana,” alisema Shamila kwa lafudhi laini ambayo ilimfanya yule mlinzi awe anamtazama tu usoni.
“Ooh! Nesi Shamira, kumbe ni wewe, basi wapereke ila ukitoka basi uje hapa nina mazungumzo na wewe kidogo sawa nesi,” alisema mlinzi huyo kwa lafudhi ambayo ilionesha dhahiri kwamba ni Mkurya, kwa kutambua udhaifu wake, Shamila alimbania kijicho kimoja, akawa anachekacheka mwenyewe na kwenda kufungua geti.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na hatia)- 46


ILIPOISHIA:
Tangu nizaliwe, sikuwahi kuchinja hata kuku tu, achilia mbali ndege tuliokuwa tukiwawinda kule kijijini kwetu lakini sasa eti nilikuwa natakiwa nimchinje binadamu, mtoto asiye na hatia yoyote ili nifaulu mtihani na kuwa mwanachama kamili, nilijikuta nikitetemeka kuliko kawaida.
Nilikichomoa kisu pale kiunoni nilipokiweka, mikono ikawa inatetemeka kuliko kawaida, nikawa namtazama mtoto yule usoni, nilijikuta nikiingiwa na huruma isiyo ya kawaida.
SASA ENDELEA...
Kisu kikadondoka na kwenda kujikita kwenye udongo. Nikamuona Mkuu akinikata jicho la ukali, akatembea kwa hatua zenye vishindo vizito mpaka pale nilipokuwa nimesimama, akainama kwa tabu na kukichomoa kile kisu, akanishikisha mkononi.
Baada ya hapo aliingiza mkono kwenye kimkoba chake kidogo cha ngozi, akatoa kichupa kilichokuwa na ungaunga mweusi, akamimina kwenye viganja vya mikono yake kisha akanipulizia usoni bila kusema chochote, nikapiga chafya mbili mfululizo kisha nikaanza kuona kama akili zangu zinabadilika jinsi ya ufanyaji kazi wake.
Hata sijui nini kiliendelea lakini baadaye akili zangu zilipokuja kukaa sawa, nilikuwa nimeshika kisu kwa nguvu huku mwili wangu ukiwa umetapakaa damu, watu wote wakawa wanashangilia kwa nguvu.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 44


ILIPOISHIA:
Ilibidi Raya abaki palepale hospitalini mpaka usiku ili iwe rahisi kufanya kazi yetu, muda ukazidi kuyoyoma na hatimaye giza likaingia, ule muda tuliokuwa tukiusubiri kwa hamu ukawa umewadia.
SASA ENDELEA...
“Tunakusikiliza wewe Shamila!”
“Yaah! Inabidi mnisikilize kwa makini vinginevyo hakuna kitakachofanikiwa.”
“Tunaanzia wapi?” nilimuuliza Shamila huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio.
“Tulia Jamal, mbona una haraka namna hiyo,” alisema Shamila, nikashusha pumzi ndefu na kutulia, hakuna muda ambao nilikuwa nahitaji msaada wake kama huo na kubwa zaidi, sikuwa mimi tu ambaye nilikuwa nahitaji msaada wake, bali Shenaiza pia.
Shamila aliingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo, muda mfupi baadaye alitoka akiwa na gauni jingine, akampa Raya na kumuelekeza kuingia kule ndani kwenda kubadilisha nguo. Kweli akatii alichoambiwa, muda mfupi baadaye akatoka akiwa ndani ya mavazi ya kinesi, usingeweza kumtambua kwamba hakuwa nesi.

Monday, October 23, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 43


ILIPOISHIA:
Kauli yake hiyo ilitufurahisha sana mimi na Shamila, tukawa na uhakika kwamba sasa kazi itakuwa nyepesi kwa sababu tayari tutakuwa na mtu kutoka ndani kabisa, ambaye angetusaidia kutimiza lengo letu la kupambana na mtu huyo hatari.
SASA ENDELEA...
“Kwa hiyo tunaanzia wapi?” nilimuuliza Shamila, akawa ni kama anayetafakari kitu kisha akaniambia ameshapata majibu.
“Ngoja niende kwanza na huyu binti nikampe hiyo hard disk yake,” alisema Shamila.
“Utaweza kuichomoa kwenye kompyuta?”
“Mimi naweza, nasomea Information Technology niko mwaka wa pili,” alisema Firyaal ambaye alikuwa amefanana sana na Shenaiza, yaani hata bila kuuliza ungemjua tu kwamba ni ndugu yake.
“Sijamaliza kukopi data ninazozihitaji lakini.”
“Nitakusaidia pia, ninayo ‘back up’ kubwa tu nyumbani, naweza kuhamisha data zote na kukuletea,” alisema msichana huyo, nikawa namtazama usoni kwani aliyokuwa akiyasema hayakuwa yakifanana na umri wake.
Kwa kumtazama alionekana kama msichana mdogo ambaye kwa makadirio ungeweza kudhani yupo kidato cha pili au cha tatu lakini kumbe tayari alishafika kidato cha sita na sasa alikuwa chuoni.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 42


ILIPOISHIA:
“Una..ta..ka kufa...nya ni...ni,” sikumalizia kauli yangu, akawa tayari ameshafika pale kitandani, tukagusanisha ndimi zetu huku Shamila akionesha kweli kudhamiria kile alichokitaka. Hakuogopa kabisa kwamba pale ni wodini.
SASA ENDELEA...
Nilijaribu kumzuia lakini haikusaidia kitu, alishadhamiria na kwa ilivyoonesha, alikuwa tayari kufanya chochote ili apate alichokuwa anakitaka. Tuliendelea kugusanisha ndimi   zetu huku mikono yake laini ikitalii kwenye viunga mbalimbali vya mwili wangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti.
Unajua jambo ambalo nitaendelea kulisema kila siku, hakuna jambo baya kama kuyajaribu mapenzi. Wazee wetu waliosema kwamba mapenzi hayajaribiwi, walikuwa sahihi kabisa. Wakati naanza uhusiano wa kimapenzi na Shamila, nilikuwa najua kabisa kwamba tayari ninaye Raya ambaye ananipenda sana na tumeshaahidiana vitu vingi, tena kibaya zaidi mimi ndiyo nikiwa mwanaume wa kwanza maishani mwake.
Akilini mwangu nilijua kwamba hata nikimkubalia Shamila, haiwezi kuwa na tatizo lolote kwa sababu kiukweli sikuwa nimempenda kutoka ndani ya moyo wangu na nilipanga kumtumia kama daraja tu la kunifanya nipate nilichokuwa nakitaka kwa urahisi.

Tuesday, September 26, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 45


ILIPOISHIA:
Kitu cha mwisho nilichokumbuka, wakati nataka kufumbua macho nilimuona yule mwanamke aliyekuwa kwenye usukani, akikunja usukani ghafla kama aliyeona kitu cha hatari mbele na sasa anataka kukikwepa, ndipo kikafuatia kile kishindo.
“Nenda haraka, hakikisha unamtoa mtoto kwenye gari na kuja naye hapa, pale kwenye gari ulipomtoa utaweka hiki,” alisema baba huku akinipa kipande cha mgomba.
SASA ENDELEA...
“Nikikamatwa je?”
“Nenda, hakuna mtu yeyote atakayekukamata wala kukuona, usiongee chochote na mtu yeyote, hata wakikusemesha usijibu,” alisema baba. Basi huku nikitetemeka, nilitoka na kile kipande cha mgomba, nikatembea harakaharaka mpaka pale barabarani.
Lile gari dogo lilikuwa limepata ajali mbaya na kupinduka, matairi yakiwa juu, likiwa limegeukia kule lilikotokea. Kwa mtu yeyote lazima angejiuliza sana kilichosababisha ajali hiyo kwa sababu kwanza lilikuwa ni eneo la tambarare na hakukuwa na kona wala tuta lolote.
Damu zilikuwa zimetapakaa kuanzia barabarani mpaka kando ya barabara, pale gari hilo lilipokuwa limepinduka. Ilibidi nifanye kile nilichoambiwa kabla watu hawajaanza kujaa. Niliinama kwenye upande aliokuwa amekaa yule mtoto, nikakitingisha kioo ambacho kilishapasuka kwa sehemu kubwa, kikamwagika chote kwenye lami.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 41


ILIPOISHIA:
“Habari za saizi nesi,” Raya alimsalimia Shamila kwa unyenyekevu, jambo ambalo hakuwahi kulifanya kabla. Shamila naye akajibu kwa uchangamfu, nikabaki njia panda. Sikujua walizungumza nini muda ule mpaka wakamaliza tofauti zao. Raya akaja mpaka pale kitandani na kunibusu mdomoni, Shamila akageuka na kulishuhudia tukio hilo.
SASA ENDELEA...
Alipogundua kwamba namtazama, harakaharaka Shamila alijifanya kama hakuwa ameona chochote.
“Leo nimekupikia chakula kizuuri, naamini utakipenda,” alisema Raya huku akianza kuniandalia chakula. Nikawa nimetulia pale kitandani huku akilini mwangu mawazo mengi yakipita. Nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari sana ambao sasa ilikuwa ni lazime nifanye kila kinachowezekana kujikomboa.
Njia pekee ambayo ingenisaidia, ilikuwa ni kuhakikisha baba yake Shenaiza na kundi lake lote wanafikishwa mbele ya sheria na mamia ya watu ambao maisha yao yalikuwa hatarini, wanaokolewa kutoka kwenye shimo la mauti.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...