Wednesday, January 31, 2018

KIVURUGE WA TANDALE- 4



ILIPOISHIA:
Mara nikasikia mlango unafunguliwa, nikashtuka na kuinuka haraka kutaka kutazama ni nani aliyekuwa akiingia, nikashtuka kumuona Salma, mtoto wa kike akiwa ameingia kwenye vyoo vya wanaume, nilipomtazama vizuri alikuwa akilia, machozi yakawa yameulowanisha uso wake.
SASA ENDELEA...
Harakaharaka niliacha kila nilichokuwa nakifanya, nikalishika shati na kutaka kulivaa lakini nilikuwa nimechelewa, Salma alifunga mlango wa maliwatoni kwa ndani kisha akanisogelea mpaka mwilini, huku machozi yakiendelea kumtoka.
“Umepatwa na nini Salma?”
“Kwa nini unanitesa? Ina maana hujui kama nakupenda? Kwa nini unanitesa Ashrafu,” alisema Salma huku akipitisha mkono wake na kunishika kiunoni, akanisogelea na kujilaza kwenye kifua changu.

Tuesday, January 30, 2018

KIVURUGE WA TANDALE- 3



ILIPOISHIA:
Mara alinirushia kitu hicho, nikashtuka baada ya kugundua kuwa lilikuwa ni lile kufuli lake jeupe, likiwa na harufu f’lan hivi ‘amaizing’ kuoneshakwamba lilikua limetoka mwilini muda huohuo, akacheka sana jinsi nilivyokuwa nalitazama kwa makini huku wakati mwingine nikilisogeza kabisa kwenye pua, akasogea na kujitupa kwenye sofa huku akiinua miguu yake na kuiweka kwenye miguu yangu.
SASA ENDELEA...
“Kivurugeee!”
“Sipendi hilo jina ujue.”
“Ndiyo nimeshakuita sasa, utanifanya nini?”
“Ntakuchapaaa!”
“Huwezi,” alisema Madam Bella huku akichekacheka na kunifanyia vituko ambavyo kiukweli nilishindwa kuvivumilia. Sijui nilipata wapi ujasiri, nikapitisha mikono yangu na kukishika vizuri kiuno chake, akashtuka na kutoa mguno huku pumzi zake zikianza kubadilika, akawa anapumua kwa nguvu kama ametoka kukimbia mbio za mita mia moja.
Nilizidi kukibana kiuno chake kinene wastani katika mtindo ambao nilijua lazima utamfanya shetani wake akurupuke kutoka mafichoni kwa spidi zote.

SEVEN DAYS IN HELL (Siku Saba Kuzimu)- 58




ILIPOISHIA:
“Yule kule aliyekuwa ananguruma kama mnyama ni nani?” Firyaal aliuliza swali, nikawaona wenzake wote wakitingisha vichwa, kuunga mkono swali hilo.
“Ni stori ndefu kidogo, ngoja nitawaeleza lakini njooni kwanza huku niwape dawa,” alisema.
SASA ENDELEA...
Wote wakamfuata mpaka kule kwenye kile chumba walichokuwa wamelala, akawaamuru wote wakae kwenye mkao wa kutengeneza duara, akatoka na kuelekea chumbani kwake, aliporudi muda mfupi baadaye, alikuwa na kichupa kidogo kilichokuwa na mafuta yaliyokuwa yananukia vizuri sana, akaanza kumpaka mafuta yale kichwani na usoni mmoja baada ya mwingine.
“Itabidi mkae dakika ishirini kisha mkaoge, baada ya hapo tutakamilisha kazi ya kumzindua Shenaiza, tumeelewana?”
“Mi nasikia njaa inaniuma sana.”
“Hatutakiwi kula chchote mpaka tukamilishe kwanza kazi hii, ukishakula tu utasababisha nguvu kubwa ambazo zinatakiwa kutumika kichwani mwako, zielekezwe tumboni kwa ajili ya mmeng’enyo wa chakula, jambo linaloweza kusababisha tukakwama, tumeshakula mbuzi mzima, hatuwezi kushindwa kumalizia mkia,” alisema Junaitha akimjibu Firyaal.

Monday, January 29, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 57



ILIPOISHIA:
“Jamal! Jamal! Amka, kuna tatizo,” sauti ya Junaitha ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye usingizi fofofo, nikakurupuka nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kumetokea nini tena.
SASA ENDELEA...
“Kuna nini tena?”
“Huyu mshenzi anataka kunizidi nguvu, amka ukanisaidie,” alisema Junaitha, huku kijasho chembamba kikimtoka. Harakaharaka nikakurupuka na kuvaa bukta na fulana, nikaongozana na Junaitha ambaye tayari alishatoka na kuanza kukimbilia kule kwenye chumba chake cha siri.
Tulipokaribia nilisikia sauti za kutisha mno, yule mwanamke tuliyemteka akawa ananguruma kama mnyama wa porini huku akikwangua mlango wa chuma kwa kucha zake ngumu, akitaka kutoka.
“Nisikilize! Jamal nisikilize,” alisema Junaitha ambaye alikwama ghafla pale mlangoni.
“Tukifungua mlango atatuzidi, inabidi tuingie kwa kutumia nguvu zetu tukapambane naye hukohuko ndani, amenitia meno, si unaona,” alisema Junaitha huku akinionesha alama ya meno mkononi mwake, huku damu nyeusi zikichuruzika.

SEVEN DAYS IN HELL (Siku Saba Kuzimu)- 56



ILIPOISHIA:
Harakaharaka nikafungua mlango nikiwa ni kama siamini nilichokisikia, nikamkuta Shenaiza akihangaika kujigeuza, jambo ambalo hakuwa amelifanya kwa kipndi kirefu tangu akiwa kule hospitalini.
“Shenaiza! Shenaiza,” nilisema huku nikipiga magoti pembeni ya kitanda chake. Bado hakuwa amefumbua macho yake.
SASA ENDELEA...
Hata hivyo, japokuwa hakuwa amefumbua macho, niliona akiyapepesa kama anayetaka kuyafumbua, nikainua mikono juu kama ishara ya kumshukuru Mungu. Kumbukumbu za yote yaliyotokea kuanzia siku ya kwanza msichana huyo aliponipigia simu mpaka muda huo zilipita kwa kasi ndani ya kichwa changu.
Kila kitu kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa ambayo ungeweza kudhani ni ndoto ya kusisimua na muda si mrefu nitazinduka. Kwa kuwa Junaitha aliniambia nikamsubiri chumbani kwake, sikukaa muda mrefu ndani ya chumba hicho cha Shenaiza kwa sababu nilijua hawezi kufurahi akinikuta nikifanya tofauti na maagizo aliyonipa, nikambusu Shenaiza kwenye paji la uso kisha nikatoka na kuelekea chumbani kwa Junaitha.

KIVURUGE WA TANDALE- 2



ILIPOISHIA:
Alimpungia mkono kichokozi huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake, akatoka zake na kumuacha Ashrafu akiwa bado ameganda palepale kama barafu.
“Ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu,” alijisemea huku tabasamu hafifu likichanua kwenye uso wake, akashusha pumzi ndefu na kuinuka kuelekea kaunta kulipa.
SASA ENDELEA...
“USHALIPIWA na yule dada uliyekuwa umekaa nae,” alisema yule mhudumu aliyekuwa mapokezi.
“ooh! Ahsante,” alisema Ashrafu huku akijisikia aibu kupindukia. Kwa lugha nyepesi, alichokifanya mrembo yule ilikuwa sawa na matusi makubwa kwake, yaani akatae kumpa namba yake ya siku kisha akamlipie bili?
“Samahani, kwani wewe ni mwenyeji hapa,” Ashrafu alimuuliza yule mhudumu ambaye alikuwa bize kupokea fedha na kurudisha chenji kwa wateja wake.
“Kaka samahani, niko bize sana, naomba uniache nihudumie wateja.”
“Kwani ugomvi dada’angu? Nilitaka kukuuliza swali dogo tu.”

DOUBLE LIFE (Maisha Mara Mbili)- 2



ILIPOISHIA:
Naamua kuendelea kujilaza, vishindo vinazidi kusogea na sasa vinasikika mita chache tu kutoka pale nilipojilaza, naamua kuushinda usingizi na kuyafumbua macho yangu, napigwa na butwaa na ninachokiona mbele ya macho yangu.
SASA ENDELEA...
“Iqram! Ni wewe au naota? Ooh Mungu wangu,” msichana mrembo mwenye mchanganyiko wa damu kama chotara wa Kizungu na Kiafrika, anashuka kutoka kwenye mgongo wa farasi mkubwa mweupe aliyekuwa amesimama mita chache kutoka pale nilipokuwa nimejilaza.
Kumbe vile vishindo vilikuwa ni vya farasi huyo mkubwa lakini mzuri, kwa wale wenye mazoea ya kwenda ufukweni, hasa nyakati za jioni watakuwa mashahidi kwamba mara chache unaweza kukutana na mtu au watu waliopanda farasi, wanaokimbia nao ufukweni wakipunga upepo wa bahari.
Sikuwa nimezoea kuwaona farasi kwa karibu, nikawa namshangaa huku nikijiuliza maswali mengi ndani ya kichwa changu kuhusu mnyama huyo. Ni kama nilisahau kabisa uwepo wa msichana huyo mrembo.

Thursday, January 25, 2018

KIVURUGE WA TANDALE- 1


Saa saba na dakika zake mchana, tumbo la Ashrafu lilikuwa likiunguruma kwa kusakamwa na njaa kali, aliamua kutoka ofisini kwao ndani ya Jengo la Al- Haramain, Mtaa wa Shaurimoyo jijini Dar na kuamua kushuka kwa kuzikanyaga ngazi moja baada ya nyingine.
Kazi yake ya ufundi wa kompyuta na vifaa vya kielektroniki ilimfanya kuwa kijana maarufu sana na hii ilitokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao kwenye kazi yake kiasi cha makampuni mengi kugombea kumwajiri lakini mwenyewe akawa hataki.
Kwake aliona ni bora ajiajiri lakini kama kuna kampuni inahitaji huduma yake, inamfuata na wanafikia makubaliano kisha kazi inafanyika.
Baada ya kushuka ngazi kwa tabu hatimaye alijisogeza taratibu hadi mgahawani ambapo palijulikana kwa jina maarufu la Kwa Makofia.
Hapo alikutana na umati mkubwa hivyo kushindwa kabisa kuagiza chakula alichokuwa akihitaji hivyo aliamua kuhamia kwenye mgahawa wa jirani yake, kabla hajachukua uamuzi wa kuondoka Kwa Makofia, macho yake yalikutana na kitu kilichomfanya ashtuke kidogo.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na hatia)- 62


ILIPOISHIA:
“Ni stori ndefu Rahma ila naomba unielewe nitakachokwambia,” nilisema, nikashusha pumzi ndefu na kuamua liwalo na liwe. Nilitaka kwenda moja kwa moja, kwamba baba yake na baba yangu walikuwa wachawi. Cha ajabu, kila nilipotaka kusema hivyo, mdomo ulikuwa mzito, nikawa naumauma maneno, hali iliyosababisha anikazie macho.
SASA ENDELEA...
“Mbona sikuelewi Togo?”
“Ni kuhusu wazazi wetu.”
“Wamefanya nini?”
“Wanajihusisha na...” kabla sijamalizia nilichotaka kukisema, jambo la ajabu lilitokea. Yule muuzaji wa lile duka, alifungua mlango na kutoka huku akikimbia, cha ajabu, hakuwa amevaa nguo hata moja.
“Vipi kwani mbonaumeshtuka?”
“Umemuona?”
“Nani? Vero? Nini cha ajabu kwani?” Rahma alinishangaa sana, na mimi nikawa namshangaa. Yaani mtu atoke dukani akiwa mtupu, halafu aanze kukimbia mitaani, siyo jambo la kushangaza hilo?”

Wednesday, January 24, 2018

Double Life! (Maisha Mara Mbili)- 1


MVUA kubwa inanyesha na kila mtu anakimbilia sehemu ya kujisitiri ili asilowane lakini mimi sijali, naendelea kutembea taratibu kama hakuna chochote kinachoendelea. Mvua inazidi kumwagika kwa nguvu, radi zinapiga na upepo mkali unafanya hali iwe tete, wenye biashara ambazo zipo barabarani, wanakimbizana kuokoa mali zao zisiharibiwe na mvua hiyo, wengine wanafunga kabisa milango ya maduka yao.
Miamvuli haifui dafu kwenye mvua hii kutokana na upepo mkali, muda mfupi baadaye, mitaa yote inakuwa kimya kabisa, watu wamejibanza pembeni, wengine wakiwa wamejikunyata kutokana na baridi iliyoambatana na mvua hii.
Kwangu hali ni tofauti, kama nilivyosema, sijali chochote, naendelea kutembea taratibu kandokando ya barabara, maji machafu yanachuruzika kutoka kwenye nywele zangu nyingi na chafu mpaka kwenye nguo zangu zilizofubaa kwa uchafu.
Nina muda mrefu sijagusa maji kuusafisha mwili wangu, hali iliyonifanya niwe nanuka kama beberu, naisikia vizuri harufu mbaya inayotoka kwenye mwili wangu lakini sijali, naendelea kutembeatembea, hata sijui naelekea wapi lakini najikuta tu siwezi kukaa sehemu moja na kutulia. 
Miguuni sijavaa viatu na mgongoni nimebeba begi chafu nililoliokota kwenye jalala na kulijaza chupa tupu za maji pamoja na uchafu mwingine. Nimevaa suruali iliyochoka na kiunoni nimejifunga kwa kamba ya katani, huo ndiyo mkanda wangu, sina habari na mtu.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na hatia)- 61


ILIPOISHIA:
Alikuwa hanielewi kwa nini nimebadilika ghafla, nimekuwa na mambo mengi ya ajabuajabu, sioneshi kumhitaji tena kama siku za mwanzo na wala sijali hisia zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa namlinda na ndiyo maana ilikuwa lazima nifanye hivyo na njia pekee, ilikuwa ni kumshawishi naye ajiunge nasi, kazi ambayo isingekuwa nyepesi lakini nilishajipanga kumkabili.
 SASA ENDELEA...
“Rahma!” nilimuita msichana huyo baada ya kukutana naye koridoni, mimi nikitoka bafuni kuoga na yeye akitoka chumbani kwake. Tofauti na siku zote ambazo alikuwa akinichangamkia sana anaponiona, wakati mwingine hata akinifuata chumbani kwangu, siku hiyo Rahma alikuwa tofauti kabisa, alipooza na alionesha kutotaka kuzungumza chochote na mimi.
“Rahma si nakuita jamani,” nilisema baada ya kumuona amenipa mgongo, akitembea haraka kuelekea sebuleni. Licha ya kutamka maneno hayo, bado hakutaka kusimama, ikabidi nitumia nguvu kumshika mkono na kumgeuza.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 60


ILIPOISHIA:
Vijana wadogo tu kama mimi, wengine hata nawazidi lakini wanaendesha magari ya kifahari barabarani, kwa nini na mimi nisionje kidogo hata kama ni mbaya? Wakati akiendelea kunipa nasaha zake, Mkuu alinipa ishara kwamba nimfuate, harakaharaka nikainuka na kumuacha baba yake Rahma akiendelea kuongea.
SASA ENDELEA...
Alinishika mkono na kusogea pembeni na mimi, mawasiliano kati yetu kidogo yalikuwa magumu kwa sababu alikuwa akiongea maneno ya Kiswahili machache, tena yaliyopindapinda lakini muda mwingi alikuwa akizungumza lugha ambayo siielewi.
Katika yale machache niliyomuelewa, alionesha kufurahishwa na ujasiri wangu, na kuniambia kwamba japokuwa ndiyo kwanza nilikuwa nimejiunga, nilikuwa na kasi nzuri ya kujifunza. Kama alivyoniambia baba yake Rahma, kweli Mkuu aliniuliza ni zawadi gani akinipa nitafurahi?
Sikupepesa macho wala kumung’unya maneno, nikamwambia kwamba nataka dawa za kunifanya niwe tajiri. Alicheka sana, mapengo yake yakawa yanaonekana, ni hapo ndipo nikagundua kwamba kumbe naye huwa anacheka na kufurahi, ingawa sikuelewa nini hasa kilichomfurahisha.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 59


ILIPOISHIA:
Kilichotokea baada ya kufanya hivyo kwa mara ya tatu, kilinifanya nihisi kama mwili wangu unakufa ganzi kwa hofu, sijawahi kushikwa na hofu kama niliyoipata siku hiyo na kama baba asingeniwahi, huenda ningedondoka kama mzigo chini maana mwili wote uliisha nguvu. 
Japokuwa ilikuwa ni usiku, tena nikiwa sina nguo na kulikuwa na baridi kali, nilihisi kijasho chembamba kikinitoka, ama kweli duniani kuna mambo na ukishangaa ya Musa, utayaona ya Firauni.
SASA ENDELEA...
Kitendo cha kufuata maelekezo yale tu, mara kaburi lilifunuka lote, yaani ule udongo wote uliokuwa umetumika kulifukia, ukapotea kiasi kwamba kila kitu kilichokuwa ndani ya kaburi kilikuwa kikionekana.
“Ingia tukasaidiane kumtoa kwenye jeneza,” alisema baba, nikajikuta nguvu za kuendelea kusimama zimeniisha maana miguu ilikuwa ikitetemeka kuliko kawaida, nikakaa kwenye kaburi lililokuwa pembeni, uso wote ukiwa umelowa kwa machozi. 
Ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba alikuwa akiniambia kwamba bado sijakomaa kiakili na sitakiwi kuingizwa kwenye hayo mambo.
“Inuka acha kuleta mambo ya kijinga hapa, upumbavu wako ndiyo uliotufikisha hapa,” alisema baba kwa ukali, nikajikakamua na kusimama huku nikiwa bado natetemeka. Alichokifanya baba baada ya kuona kama nasuasua, alinisukumia ndani ya lile kaburi, nikaporomoka na kwenda kujibamiza kwenye jeneza.
Nilijikuta nikipiga kelele kwa sauti kubwa huku nikitafuta sehemu ya kutokea, kwa kuwa ilikuwa ni ndani ya shimo kelele zangu hata hazikufika mbali, zikawa zinajirudia na kusababishwa mwangwi. Tayari baba naye alishaingia mle kaburini, akaninyamazisha kwa ukali kama kawaida yake.

Monday, January 15, 2018

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 58


ILIPOISHIA:
Sikuyaamini macho yangu kugundua kwamba tulikuwa Mlandizi, tena jirani kabisa na pale ile ajali ilipotokea. Nilipotazama upande wa pili wa barabara, niliwaona watu wengi wakiwa wamekaa na kuuzunguka moto, pale kwenye ile nyumba iliyokuwa na msiba wa kwanza wa yule mtoto, moyo ukashtuka sana nikikumbuka kilichotokea.
“Mbona umeshtuka,” baba aliniuliza.
SASA ENDELEA...
Sikumjibu zaidi ya kumuonesha kidole kwenye ile nyumba ambapo bado watu walikuwa wakiendelea kuota moto huku wakipiga stori za hapa na pale msibani. Baba wala hakuhangaika hata kugeuka, akanitaka kuelekeza akili zangu kwenye jambo lililotupeleka pale kwani muda ulikuwa umetutupa mkono.
Ilionesha baba alikuwa anaelewa kila kitu kilichokuwa kikiendelea, nikawa najiuliza ameyajuaje yote hayo? Kiukweli sikupata jibu, baba Rahma naye wala hakujishughulisha na chochote na wale watu kama baba.
“Onesha aliangukia wapi? Unatupotezea muda,” alisema baba, nikawa najaribu kuvuta kumbukumbu, nikawa natembea pembeni ya barabara kuelekea pale yule dereva wa bodaboda alipodondokea, wakawa wananifuata kwa nyuma.
“Nadhani ni hapa.”

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 57


ILIPOISHIA:
Ni kama fahamu zake zilikuwa zimemrejea kwani alishtuka sana kuniona ndani ya chumba chake, akageuka huku na kule huku akijaribu kujitoa kwenye mikono yangu kwa hofu kubwa.
“Togoo! Umeingiaje humu?” aliniuliza kwa sauti ya juu, nikasikia mlango wa chumba cha pili ukifunguliwa kuashiria kwamba kuna mtu alikuwa amesikia na sasa anatoka.
SASA ENDELEA...
“Nimekwisha!” nilijisema huku nikigeuka huku na kule, sikumuona baba wala baba yale Rahma, Sadoki akanibadilikia na kunishika kwa nguvu ii nisipate nafasi ya kukimbia.
Akili za haraka, zilinituma kutumia nguvu zangu kujiokoa na kwa kuwa nilikuwa na ile kinga yangu ya hirizi mkononi, nilipiga mguu wa kushoto chini huku nikiwa nimevibana vidole gumba na vile vya mwisho. Hii ni mbinu niliyofundishwa ya kutaka kupotea kwenye macho ya watu, yaani unakuwepo sehemu hiyohiyo lakini huonekani.
Nilipofanya hivyo, nilishtukia nikiwa mwepesi kama upepo, Sadoki akabaki ameduwaa kwani japokuwa alikuwa amenishika, alishtukia nikiyeyuka mikononi mwake, giza nene likatanda chumba kizima.
Mara mlango ulianza kugongwa kwa nguvu, Sadoki akaenda kuufungua maana alikuwa amefunga kwa komeo kwa ndani, mama yake Sadoki akaingia mbiombio akiwa ameshika kibatari.
“Una nini Sadoki?”
“Mama! Nimemuona Togo kwa macho yangu, hata sijui ameingiaje humu ndani wakati milango ilikuwa imefungwa.”

Mbinu za Kumtongoza Mwanamke Umpendaye

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...