Wednesday, August 19, 2015

MY REPENTANCE (KUTUBU KWANGU)- 1

Naitwa Flaviana Joel, mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nane. Nilibahatika kuolewa miaka kumi iliyopita, nikiwa bado msichana mbichi katika umri wa miaka kumi na nane tu.
Niliolewa na mume wangu kipenzi, Ibrahim au Ibra kama mwenyewe nilivyozoea kumuita ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye benki moja maarufu ambayo sitaitaja jina kwa sababu maalum, iliyopo hapa jijini Dar es Salaam.
Kabla Ibra hajanioa, tulidumu kwenye uchumba kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja, kipindi hicho nikiwa nasoma chuo kimoja cha uhasibu kilichopo Posta, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, nikiwa ndiyo kwanza nimeanza mwaka wa kwanza.
Baada ya ndoa, mimi na Ibra tulihamia Mbezi Beach kwenye nyumba yetu ambako tuliishi pamoja mpaka tulipokuja kutengana kwa sababu ambazo ndizo hasa zilizonifanya nitafute nafasi hii ya kutubu hadharani na kukiri kwa kinywa changu yote niliyowahi kuyafanya.
Nimesukumwa kuja kusimulia mkasa wangu huu kwa sababu nataka watu wajifunze kupitia maisha yangu na Ibra. Najisikia aibu sana, najikaza tu kwa sababu nataka wanawake wenzangu waelewe kilichonitokea na kamwe wasifuate njia kama ambazo mimi nilipita. Pia iwe funzo kwa wanaume, hasa wale ambao wapo ndani ya ndoa.
Nasikitika kwamba nimekuwa kikwazo kikubwa katika maisha ya Ibra, mwanaume niliyetokea kumpenda kwa moyo wangu wote lakini kwa sababu ya mapungufu ya kibinadamu ambayo nitayaelezea, nikageuka na kuwa mwiba mkali kwenye maisha yake.
Nilisema tangu awali na nitaendelea kusema kwamba sijawahi kutokea kumpenda mwanaume kama nilivyompenda Ibra ila hata sielewi ni kitu gani kilichosababisha haya yote yatokee.

HEART ATTACK (SHAMBULIO LA MOYO)- 1

MANYUNYU ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likiendelea kujikusanya angani, kuashiria mvua kubwa iliyokuwa inataka kunyesha. Japokuwa ilikuwa bado ni mapema, giza lilitanda angani na kufanya watu karibu wote kukimbilia majumbani mwao kabla mvua hiyo haijaanza kunyesha.
Radi kali na ngurumo za kutisha zilikuwa zikisikika huku na kule na kuzidi kuifanya hali kuwa tete. Manyunyu yaliongezeka na muda mfupi baadaye, mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ilianza kumwagika. Watu wote walikimbilia majumbani mwao, huku wengine wakijibanza kwenye viambaza vya nyumba na maduka kujisitiri na mvua hiyo.
“Kaka amka tunataka kufunga baa.”
“Niongeze bia moja baridi na kiroba.”
“Inamaana hii mvua wewe huisikii au?”
“We mhudumu, nimekwambia ongeza bia, kwani wewe ndiyo umenileta hapa, sitaki kuwahi kurudi nyumbani kwani moto unawaka.”
“Kivipi?”
“Naishi na mwanamke ambaye ni tatizo kubwa maishani mwangu, yaani muda mwingine natamani kujifia niepuke mateso haya,” kijana mmoja mdogo alikuwa akijibizana kilevi na mhudumu wa baa ndogo ya Mpakani. Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inamwagika, kijana huyo hakuonekana kujali, pombe zilikuwa zimemzidi lakini bado alikuwa anataka kuendelea kunywa.

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1

Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.
“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

NILIMUUA NIMPENDAYE (I KILLED MY BELOVED ONE)- 1

Jina langu naitwa Eunice, mtoto wa tatu kati ya watano wa familia ya baba yetu, mzee Ansbelt. Nilizaliwa miaka 26 iliyopita katika Kijiji cha Mtae, Lushoto mkoani Tanga lakini nimekulia jijini Dar es Salaam kwani baba yangu aliyekuwa akifanya kazi ya uhandisi katika Kampuni ya Usambara Civil Engineering, alihamishiwa kikazi jijini na akafanikiwa kujenga nyumba Tabata.
Ni hapo ndipo mimi na ndugu zangu wa tumbo moja tulipokulia hadi tulipokuwa wakubwa. Kwa kweli kwa kipindi cha utotoni, tuliishi maisha mazuri sana kwani baba yetu alikuwa akijiweza kifedha hivyo alituhudumia vizuri kwa mavazi, chakula na elimu bora.
Nakumbuka sisi ndiyo tulikuwa wa kwanza kumiliki runinga mtaani kwetu na ndiyo tulikuwa wa kwanza kupelekwa shuleni na ‘school bus’, tukisoma katika shule iliyokuwa inafundisha masomo yote kwa Kiingereza (English Medium), iliyokuwa nje kidogo ya jiji.
Mama yetu hakuwa akifanya kazi, alikuwa akishinda nyumbani kuhakikisha sisi wanaye tunapata kila tulichokihitaji, ikiwemo malezi bora. Kutokana na aina ya malezi tuliyolelewa, tulikuwa tofauti sana na watoto wengine tuliokuwa tukiishi nao mtaani kwetu.
Mimi na ndugu zangu wengine wa kike hatukuwa sawa na wasichana wengine mtaani kwetu ambao walianza kujihusisha na mapenzi wakiwa na umri mdogo, wengi wakitoka na wanaume wenye umri mkubwa, sawa na baba zao.

CRUEL WORLD (DUNIA KATILI)- 1

Mwandishi: Hashim Aziz
“Sukuma! Sukumaaa! Jikaze mwanangu... moja... mbili... tatu... haya sukumaaa!” sauti ya mkunga wa jadi, Mama Anunu ilisikika kutoka ndani ya kibanda cha nyasi na miti, akimhimiza msichana mdogo aliyekuwa na ujauzito mkubwa, Adelina kujitahidi ili hatimaye ajifungue.
Licha ya ujauzito wake kutimiza umri wa miezi kumi na moja, Adelina alishindwa kabisa kujifungua. Alishahangaika sana kwenye hospitali mbalimbali bila mafanikio, alishapewa dawa za kuongeza uchungu mara kadhaa bila mafanikio, mwisho ndipo aliposhauriwa kwenda kwa mama Anunu.
Mwanamke huyo, licha ya kuzuiwa na serikali kufanya shughuli za ukunga nyumbani kwake na badala yake akaambiwa awe anawapa washauri waende hospitali na kwenye vituo vya afya kwa usalama wao, bado aliendelea na kazi yake kwa siri, akiwasaidia wengi ambao ujauzito wao ulikuwa na matatizo na wale ambao hawakuwa na uwezo wa kusafiri mpaka hospitalini, kilometa nyingi kutoka eneo hilo.

Monday, August 3, 2015

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1


Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.


“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

Wednesday, May 27, 2015

RAY AMKANA MTOTO WA JOHARI

Msanii wa filamu za Kibongo, Raymond Kigosi 'Ray' amemkana mtoto wa mpenzi wake wa muda mrefu, Blandina Chagula 'Johari' aitwaye Maria na kusisitiza kuwa mtoto huyo si damu yake.

Ray aliulizwa kuhusu mtoto wa Johari mbele ya Chuchu, akamkana na kwenda mbali zaidi kwa kusema ni jambo la heri kujiweka mbali na watu wanaotafuta umaarufu kupitia yeye.

"Achaneni na hayo mambo, sihusiki na lolote na jambo la mtoto na sipendi kabisa kuzushiwa mambo kama hayo, watu wasinitafsiri kwa minong'ono na badala yake wafuate ninachosema, kwa sasa mwanamke wa maisha yangu ni Chuchu na ntakuwa natembea nae kila mahali ili nione hao wanasema mimi ni mpenzi wao.

Monday, May 25, 2015

WEMA: NAMPENDA ZARI

Mwanadada Wema Sepetu, amefunguka kwamba hana tatizo na Zarina Hassan 'zari' licha ya kuwa mrembo huyo anatoka na aliyekuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul 'Diamond'.
Wema aliyasema hayo usiku wa jana mei 25, 2015 katika kipindi cha Ala Za Roho kinachoongozwa na Loveness Malinzi 'diva' wakati akihojiwa.

Mmmh! Karama utaoa kweli ???

Mwanamuziki Luteni karama juzi jumamosi amemvalisha pete ya uchumba mpenz wake wa siku nyingi pia ni mwanamuziki Isabella mpanda "Bella" tukio hilo lilifanyika katika ukumbi wa klabu kakala iliyopo kigamboni jijini Dar es salaam

Tuesday, January 6, 2015

CAMERON DIAZ AND MADDEN ARE MARRIED!


Credits: E! News
The couple tied the knot Monday night at Diaz's Beverly Hills home after a whirlwind courtship and blink-and-you-missed-it engagement.
All told, we hear that about 100 guests were in attendance and, while a massive tent was set up in the yard, the ceremony took place inside the house. Friends and family filed into the reception tent after the I-dos.
Word just got out today that the super-stealth duo were planning on taking the plunge, boggling more than a few minds since Diaz, 42, and Madden, 35, just stepped out as a couple (and an unconfirmed couple at that) last May.
 The Good Charlotte rocker popped the question a few days before Christmas.
But maybe they started planning when they met, because the big celebration didn't have the look of an 11th-hour affair.

JIMBO LA KILOSA; MAPIGANO, HUDUMA MBOVU ZA KIJAMII NI TATIZO SUGU


Na Hashim Aziz
Kilosa ni moja kati ya wilaya zinazounda Mkoa wa Morogoro ikiwa na jumla ya wakazi 26,060 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002. Pia ni jimbo la uchaguzi linaloongozwa na mwanasiasa mkongwe, Mustapha Mkulo kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Mkullo (kulia)
Wiki iliyopita, Uwazi lilifunga safari mpaka kwenye jimbo hilo ambapo mwandishi wetu alifanikiwa kuzungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali yakiwemo Mtendeni, Mkwateni, Magomeni, Kibaoni, Manzese A, Manzese B, Uhindini, Mazinyungu na maeneo mengine mengi ambapo alizungumza na wananchi walioeleza matatizo yao.
MATATIZO YA WANANCHI
Katika ziara hiyo, Uwazi lilibaini matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi wa jimbo hilo, kubwa ikiwa ni mapigano ya mara kwa mara kati ya jamii za wakulima na wafugaji wanaogombea ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji, kama ilivyobainika pia katika Jimbo la Mvomero ambalo pia lilitembelewa hivi karibuni.
Mkullo
Wakulima wanalalamika kwamba wafugaji wa Kimasai,

IDI AMINI DADA; MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU

Wengi wanamkumbuka kutokana na ukatili wake kipindi alipokuwa madarakani na vita kali ya kugombea mpaka iliyopiganwa kati ya nchi yake ya Uganda dhidi ya Tanzania, enzi hizo ikiwa chini ya Rais Julius Kambarage Nyerere.
Anaitwa Idi Amini Dada, Rais wa tatu wa Uganda aliyeingia madarakani baada ya kumpindua Rais Milton Obote na yafuatayo ni mambo kumi usiyoyajua kuhusu dikteta huyu.
1. Katika kipindi alichokuwa madarakani, kutoka 1971 hadi 1979, inakadiriwa kwamba aliwaua kikatili zaidi ya watu laki tano waliokuwa wakienda kinyume na amri zake.

2. Aliwahi kuwa mwenyekiti wa OAU (Organisation of African Unity) na alikuwa na ndoto za kuiunganisha Afrika kuwa nchi moja ili aitawale, kama alivyokuwa akiwaza rafiki yake mkubwa, Muammar Gaddafi.
3. Alikuwa na elimu ndogo aliyoipata kwenye Shule ya Kiislamu ya Bombo na inaelezwa kuwa baadaye aliacha shule akiwa hajui vizuri kuandika wala kusoma.
4. Mpaka anakufa, historia ya maisha yake haikuwa ikifahamika vizuri. Wachambuzi wanaeleza kuwa alizaliwa Koboko mwaka 1925, kutoka kabila la Kakwa.

Monday, January 5, 2015

BOKO HARAM FIGHTERS OVERPOWER MULTINATIONAL FORCE


Boko Haram Islamic extremists have overpowered a multinational military force and seized its key base on Nigeria's border with Chad, according to residents who took to canoes to escape.

Scores of soldiers and civilians were killed, while others drowned in Lake Chad, Nigerians taking refuge in a Chadian village said in cell phone calls Sunday night. They said insurgents fired rocket-propelled grenades and automatic assault rifles and hurled explosives.
Boko Haram

"They came in their hundreds driving several Hilux patrol vehicles, trucks and some were on motorcycles and immediately began to throw explosives and bombs," fisherman Audu Labbo told The Associated Press.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...