Friday, August 31, 2018

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 3


ILIPOISHIA:
“Inuka na ufanye ninachokueleza, ukizingua unajua nini kitatokea,” nilisema kwa sauti ya chini lakini yenye mamlaka, yule mwanamke akakurupuka akiwa ni kama haamini kilichotokea, Suma naye akawa anatetemeka akiwa haelewi nimeingiaje pale.
SASA ENDELEA...
“Snox! Nakuomba mdogo wangu, please show me some mercy!” (Nionee huruma tafadhali) alisema Suma huku akiwa anatetemeka kuliko kawaida lakini sikumjali.
“Look at my face!” (Nitazame usoni), nilimwambia kwa Kiingereza kilichonyooka, akanitazama usoni halafu akawa ni kama ameshtuka kidogo.
“Mlikuja mkanipiga na kunijeruhi kiasi hiki, mkamteka Saima wangu na kama hiyo haitoshi, mmekuja kuchoma moto nyumba yetu. Bado unategemea kwamba nitakuonea huruma?” nilisema huku na mimi nikitetemeka kwa hasira.
”No! Nisikilize kwanza Snox,” alisema huku akiniita kwa jina langu la kazi. Watu wengi mitaani huwa wanaamini Snox ni jina langu halisi kwa sababu kila ninakoenda ndilo linalotumika lakini ukweli ni kwamba halikuwa jina langu halisi wala halikuwa na uhusiano wowote na jina langu halisi.

Thursday, August 30, 2018

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 2


ILIPOISHIA:
Bado nilikuwa nazikumbuka namba za siri nilizotumia kukifunga, macho yangu yakatua juu ya kitu kilichosababisha nitabasamu! Siyo tabasamu la furaha, la hasha! Tabasamu la kifo, tabasamu ambalo huwa linaonekana usiku wa giza totoro pekee.
SASA ENDELEA...
Unaweza kujiuliza nilikuwa nimeona nini kilichosababisha nitoe tabasamu la aina hiyo? Kihulka mimi ni mpole sana na pengine upole wangu wa nje ndiyo unaosababisha wakati mwingine watu kunionea waziwazi, wakiwa hawajui ndani ya moyo wangu kumejificha kitu.
Ilikuwa ni bunduki ninayoipenda sana, AK47 ambayo ilikuwa imekatwa kitako na mtutu na kuifanya iwe na uwezo wa kubebeka vizuri mikononi. Jinsi nilivyoipata silaha hii hatari, ambayo kisheria haitakiwi kabisa kumilikiwa na raia, isipokuwa wanajeshi tu, ni stori ndefu sana na yenye kusisimua kwelikweli.
Wakati mwingine binadamu wanakuwa wepesi wa kuwalaumu wenzao kwa matokeo ya mwisho, lakini ni wachache wanaokuwa wanaujua ukweli wa nini kinachosababisha mtu fulani akafanya tukio fulani. Sikuwahi kudhani hata mara moja kwamba itafika siku nitakuwa nikiutegemea mtutu wa bunduki kufanya kile ninachokitaka.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1


“Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!”
“Nanii?”
“Fungua!”
“Jitambulishe kwanza, wewe nani?”
“Nimesema fungua! Fungua kwa hiyari yako!”
“Huyo ni nani?”
“Shiii! Rudi ndani kalale!”
“What is going on? Please let me know!” (Nini kinaendelea? Tafadhali naomba nieleweshe).
“Ngo! Ngo! Ngo!”

Kufumba na kufumbua, kishindo kikubwa kilisikika, mlango ukaja kunibamiza kwa nguvu na kunirusha mpaka ukutani, nikajibamiza na kudondoka chini kama mzigo. Wanaume watatu waliokuwa wamevalia makoti meusi, walinifuata na kunikaba pale chini huku wakinimulika kwa tochi zenye mwanga mkali usoni.

“Tulia, vinginevyo tunakumwaga ubongo sasa hivi,” alisema mmoja kati yao, nikashtuka kusikia akikoki bunduki yake na kuninyooshea. Sikuwahi kuona bunduki halisi katika maisha yangu hata mara moja, nilizoea tu kuziona kwenye TV lakini sasa, mtutu ulikuwa ukinitazama.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...