Wednesday, August 19, 2015

MY REPENTANCE (KUTUBU KWANGU)- 1

Naitwa Flaviana Joel, mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nane. Nilibahatika kuolewa miaka kumi iliyopita, nikiwa bado msichana mbichi katika umri wa miaka kumi na nane tu.
Niliolewa na mume wangu kipenzi, Ibrahim au Ibra kama mwenyewe nilivyozoea kumuita ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye benki moja maarufu ambayo sitaitaja jina kwa sababu maalum, iliyopo hapa jijini Dar es Salaam.
Kabla Ibra hajanioa, tulidumu kwenye uchumba kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja, kipindi hicho nikiwa nasoma chuo kimoja cha uhasibu kilichopo Posta, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, nikiwa ndiyo kwanza nimeanza mwaka wa kwanza.
Baada ya ndoa, mimi na Ibra tulihamia Mbezi Beach kwenye nyumba yetu ambako tuliishi pamoja mpaka tulipokuja kutengana kwa sababu ambazo ndizo hasa zilizonifanya nitafute nafasi hii ya kutubu hadharani na kukiri kwa kinywa changu yote niliyowahi kuyafanya.
Nimesukumwa kuja kusimulia mkasa wangu huu kwa sababu nataka watu wajifunze kupitia maisha yangu na Ibra. Najisikia aibu sana, najikaza tu kwa sababu nataka wanawake wenzangu waelewe kilichonitokea na kamwe wasifuate njia kama ambazo mimi nilipita. Pia iwe funzo kwa wanaume, hasa wale ambao wapo ndani ya ndoa.
Nasikitika kwamba nimekuwa kikwazo kikubwa katika maisha ya Ibra, mwanaume niliyetokea kumpenda kwa moyo wangu wote lakini kwa sababu ya mapungufu ya kibinadamu ambayo nitayaelezea, nikageuka na kuwa mwiba mkali kwenye maisha yake.
Nilisema tangu awali na nitaendelea kusema kwamba sijawahi kutokea kumpenda mwanaume kama nilivyompenda Ibra ila hata sielewi ni kitu gani kilichosababisha haya yote yatokee.

HEART ATTACK (SHAMBULIO LA MOYO)- 1

MANYUNYU ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likiendelea kujikusanya angani, kuashiria mvua kubwa iliyokuwa inataka kunyesha. Japokuwa ilikuwa bado ni mapema, giza lilitanda angani na kufanya watu karibu wote kukimbilia majumbani mwao kabla mvua hiyo haijaanza kunyesha.
Radi kali na ngurumo za kutisha zilikuwa zikisikika huku na kule na kuzidi kuifanya hali kuwa tete. Manyunyu yaliongezeka na muda mfupi baadaye, mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ilianza kumwagika. Watu wote walikimbilia majumbani mwao, huku wengine wakijibanza kwenye viambaza vya nyumba na maduka kujisitiri na mvua hiyo.
“Kaka amka tunataka kufunga baa.”
“Niongeze bia moja baridi na kiroba.”
“Inamaana hii mvua wewe huisikii au?”
“We mhudumu, nimekwambia ongeza bia, kwani wewe ndiyo umenileta hapa, sitaki kuwahi kurudi nyumbani kwani moto unawaka.”
“Kivipi?”
“Naishi na mwanamke ambaye ni tatizo kubwa maishani mwangu, yaani muda mwingine natamani kujifia niepuke mateso haya,” kijana mmoja mdogo alikuwa akijibizana kilevi na mhudumu wa baa ndogo ya Mpakani. Licha ya mvua kubwa iliyokuwa inamwagika, kijana huyo hakuonekana kujali, pombe zilikuwa zimemzidi lakini bado alikuwa anataka kuendelea kunywa.

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1

Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.
“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

NILIMUUA NIMPENDAYE (I KILLED MY BELOVED ONE)- 1

Jina langu naitwa Eunice, mtoto wa tatu kati ya watano wa familia ya baba yetu, mzee Ansbelt. Nilizaliwa miaka 26 iliyopita katika Kijiji cha Mtae, Lushoto mkoani Tanga lakini nimekulia jijini Dar es Salaam kwani baba yangu aliyekuwa akifanya kazi ya uhandisi katika Kampuni ya Usambara Civil Engineering, alihamishiwa kikazi jijini na akafanikiwa kujenga nyumba Tabata.
Ni hapo ndipo mimi na ndugu zangu wa tumbo moja tulipokulia hadi tulipokuwa wakubwa. Kwa kweli kwa kipindi cha utotoni, tuliishi maisha mazuri sana kwani baba yetu alikuwa akijiweza kifedha hivyo alituhudumia vizuri kwa mavazi, chakula na elimu bora.
Nakumbuka sisi ndiyo tulikuwa wa kwanza kumiliki runinga mtaani kwetu na ndiyo tulikuwa wa kwanza kupelekwa shuleni na ‘school bus’, tukisoma katika shule iliyokuwa inafundisha masomo yote kwa Kiingereza (English Medium), iliyokuwa nje kidogo ya jiji.
Mama yetu hakuwa akifanya kazi, alikuwa akishinda nyumbani kuhakikisha sisi wanaye tunapata kila tulichokihitaji, ikiwemo malezi bora. Kutokana na aina ya malezi tuliyolelewa, tulikuwa tofauti sana na watoto wengine tuliokuwa tukiishi nao mtaani kwetu.
Mimi na ndugu zangu wengine wa kike hatukuwa sawa na wasichana wengine mtaani kwetu ambao walianza kujihusisha na mapenzi wakiwa na umri mdogo, wengi wakitoka na wanaume wenye umri mkubwa, sawa na baba zao.

CRUEL WORLD (DUNIA KATILI)- 1

Mwandishi: Hashim Aziz
“Sukuma! Sukumaaa! Jikaze mwanangu... moja... mbili... tatu... haya sukumaaa!” sauti ya mkunga wa jadi, Mama Anunu ilisikika kutoka ndani ya kibanda cha nyasi na miti, akimhimiza msichana mdogo aliyekuwa na ujauzito mkubwa, Adelina kujitahidi ili hatimaye ajifungue.
Licha ya ujauzito wake kutimiza umri wa miezi kumi na moja, Adelina alishindwa kabisa kujifungua. Alishahangaika sana kwenye hospitali mbalimbali bila mafanikio, alishapewa dawa za kuongeza uchungu mara kadhaa bila mafanikio, mwisho ndipo aliposhauriwa kwenda kwa mama Anunu.
Mwanamke huyo, licha ya kuzuiwa na serikali kufanya shughuli za ukunga nyumbani kwake na badala yake akaambiwa awe anawapa washauri waende hospitali na kwenye vituo vya afya kwa usalama wao, bado aliendelea na kazi yake kwa siri, akiwasaidia wengi ambao ujauzito wao ulikuwa na matatizo na wale ambao hawakuwa na uwezo wa kusafiri mpaka hospitalini, kilometa nyingi kutoka eneo hilo.

Monday, August 3, 2015

A BOOK OF SATAN (KITABU CHA SHETANI)- 1


Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiendelea kudondoka taratibu kuashiria kumalizika kwa mvua kubwa iliyonyesha mfululizo usiku kucha. Tofauti na siku zote, watu walikuwa wachache sana barabarani japokuwa tayari kulishapambazuka. Ubaridi ulioambatana na mvua hiyo, ulimfanya kila mmoja kutamani kuendelea kuvuta shuka na kuuchapa usingizi.


“Hee! Tayari ni saa moja? Mungu wangu, nitachelewa kazini,” Edmund Katera ‘Mundi’, kijana mdogo aliyekuwa akifanya kazi katika kampuni kubwa ya mawasiliano ya Hashcom Mobile kwenye kitengo cha Teknolojia ya Mawasiliano (Information Technology) alikurupuka kutoka usingizini na kukimbilia kwenye kabati lake la nguo kwa lengo la kuchukua taulo.
Harakaharaka akatoka mpaka nje na kuchukua ndoo ya maji ya kuoga huku mswaki ukiwa mdomoni, akatembea kwa hatua za haraka mpaka bafuni ambapo alijimwagia maji bila kujali ubaridi uliokuwepo asubuhi hiyo kutokana na mvua iliyokuwa inaishia.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...