Thursday, December 31, 2009

HAPPY NEW YEAR 2010


I will seek elegance rather than luxury, refinement rather than fashion. I will seek to be worthy more than respectable, wealthy and not rich. I will study hard, think quietly, talk gently, and act frankly. I will listen to stars and birds, babes and sages, with an open heart. I will bear all things cheerfully, do all things bravely await occasions and hurry never. In a word I will let the spiritual, unbidden and unconscious grow up through the common.

WHY YOU WANNA GO -SEAN KINGSTON


RELYCS

It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long for you
To get close to me
Now you wanna go run away girl
Away from me
I know its got to be hard
Cuz i'm so busy
Not to mention many lonely nights
Just missin' me
Cuz ain't nothing better than you by my side (my side) x4
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took some time to
Learn to earn her trust (learn to earn her trust)
I ain't goin nowhere anytime
So you can put that on us
Pucci, Louis, Rodeo, we gon' live it up
Now you want to say goodbye
And go and mess it all up
Cuz ain't nothing better than you by my side (my side) x4

It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
Forgive me x3
I love you x3
My mom say
My pop say
My family say
They love you x3
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go

Friday, December 11, 2009

TOFAUTI KATI YA MWANAMKE NA MWANAUME
Ni ukweli usiopingika kuwa wanaume na wanawake hatufanani. Japokuwa sote tunafahamu kuwa hatufanani, bado wengi wetu hatujajua tofauti yetu iko wapi, au ni nini. Ni kwa kosa hili kubwa, wanaume wameendelea kuamini kuwa wao ni kundi bora kuliko wanawake, huku wanawake, nao kwa kutojua ukweli, kukubali kuwa wao ni viumbe dhaifu na wanaostahili kuongozwa katika kila jambo.

Nasema tena kuwa tofauti kati ya mwanaume na mwanamke zipo na hazikwepeki, lakini ni wajibu wa kila mmoja kutambua kuwa binadamu wote ni sawa katika mantiki ya “Ubinadamu”. Kuwa mwanaume au mwanamke hakukuongezei wala kukupunguzia chochote.

Kila mmoja amekamilika kwa vile alivyo,
Na thamani yetu kama binadamu inabaki kuwa palepale. Maisha yanakuwa na maana zaidi pale mwanaume na mwanamke wanapoungana na kuishi pamoja katika muunganiko ambao kila mmoja anafahamu yeye ni nani na mwenzake ni nani. Ukifanya utafiti utagundua kuwa hata kama familia ina mafanikio makubwa kiasi gani, kama mwanaume (baba) hajajua kuwa yeye ni nani na mwenzake (mama) ni nani na anahitaji nini, familia kama hiyo haiwezi kuwa na amanai na maisha kwao yanapoteza maana kabisa.

Kwa kushindwa kuelewa sisi ni nani na wenzetu ni nani, wengi tumeendelea kuwa wahanga wa nmaisha huku kila mmoja akimsingizia mwenzake kuwa ndio sababu ya yeye kushindwa kufikia malengo. Utakuta mwanaume analalamika kuwa mke wake ndio chanzo cha yeye kutofanikiwa, huku mke nae akilalamika kuwa mumewe ndio sababu ya yeye kushindwa kufikia malengo.

Tofauti kubwa kati ya mwanamke na mwanaume kwa sehemu kubwa zipo kwenye maumbile, jinsi mwili unavyofanya kazi, utashi, homoni, hisia, mahitaji na jinsi tunavyoyatazama mambo (Perception).

Ni kutokana na ujinga wa kutojua tofauti hizi, ndio maana ndoa nyingi zinaingia kwenye matatizo na migogoro kila kukicha, kuna kuumizana kwingi ndani ya mahusiano na mwisho kutengana kwa sababu kila mmoja (Mwanaume na mwanamke) anategemea mwenzake afanye na kutenda kama yeye bila kujua kuwa hili ni jambo ambalo haliwezekani kwa kuwa tunatofautiana katika mambo kadha wa kadha.

Ni makosa makubwa kwa mwanaume kutarajia mwanamke afanye kama yeye anavyotaka, au mwanamke kutegemea mwenzi wake amfanyie kama anavyotaka. Ni vizuri kila mmoja azifahamu tofauti zilizopo ili aweze kuishi kwa amani na mwenzake. Iwapo kila mmoja atafahamu tofauti zetu zipo wapi, migogoro na mifarakano isiyo ya lazima itaepukwa kwa kiwango kikubwa sana.

Wataalamu wengi wa mambo ya jinsia wamefanya utafiti kwa miaka mingi na kwa pamoja wamebaini tofauti zifuatazo:

UELEWA WA WANAUME
Kihulka, wanaume ni viumbe wasiopenda kufundishwa wala kushauriwa kitu kwa namna ambayo itawafanya wahisi kudharauliwa au hawajui jambo. Mwanamke anaweza kumshauri vizuri sana mumewe, kwa mfano “Mshahara wako au pesa unazopata tuzitumie kidogo na nyingine zinazobaki tuweke akiba kwa ajili ya kujenga nyumba au kusomesha watoto.”

Kimantiki huu ni ushauri wa busara sana ambao wanawake wengi huwapa wenzi wao, lakini mwanaume anapoambiwa hivi na mkewe, hasa kama mke nae hajui tofauti kati yake na mumewe, matokeo huwa ni kwa mwanaume kuhisi mkewe ameona yeye hawezi kupangilia mambo vizuri na ndio maana ameamua kumfundisha. Kitakachoendelea hapa itakuwa ni ugomvi mkubwasana na pengine mwaamke atabaki kujiuliza ni wapi alipokosea mpaka mumewe amjie juu wakati ametoa ushauri ambao ni mzuri.

Kinachosababisha ugomvi hapa ni kutojua kuwa wanaume sio watu wakufundishwa kama unavyomfundisha mtoto. Ushauri kama huu unaweza kuwa mzuri na kumfanya mwanaume ajihisi ni mwenye thamani kubwa endapo ataambiwa na mkewe wakiwa faragha, wakiwa wametulia kabisa, hali ambayo itamfanya mwanaume kujiona kama shujaa.

Wanawake wanaoijua siri hii, huwashauri waume zao mambo mazuri wakiwa vyumbani mwao, tena hufanya hivi baada ya kuhakikisha wamewafurahisha vya kutosha kwa mambo mazuri kama vile kwa chakula kizuri na tendo la ndoa lililopangiliwa vizuri. Pia mwanamke anatakiwa kuanza kutoa ushauri wake kwa kumsifia mumewe kwa yale mazuri ambayo amekwisha yafanya hata kama ni machache na madogo.

Kitu kingine ambacho kihulka ni tabia ya wanaume ni kupenda kutoa au kupewa suluhisho la moja kwa moja. Mwanaume anapoamua kumweleza mkewe hukusu jambo Fulani ambalo linamtatiza, anataka kupewa suluku ya moja kwa moja na sio kuonewa huruma. Inapotokea mwanaume anamuomba ushauri mkewe na badala ya mke kumpa ufumbuzi wa nini cha kufanya anaanza kumuonea huruma na kumsikitikia, huhisi kama hadhi yake imeshushwa sana.

UELEWA WA WANAWAKE
Tofauti na wanaume, wanawake ni viumbe wanaopenda sana kuelekezwa na kufundishwa hasa na waume zao au watu wao wa karibu. Unapomuelekeza mwanamke jambo kwa upole na ukarimu, utakuwa na nafasi nzuri ya kupendwa sana na mwanamke huyo.

Wanawake pia kupenda sana kusikilizwa wanapoeleza matatizo yao. Pamoja na hayo, hupenda sana pia kusaidiwa mambo yanayowasumbua hata kama ni madogo. Utashangaa sana kwamba hata yale mambo ambayo wanaume huyaona kuwa ni kawaida na yasiyo na uzito wowote, kuwa na maana kubwa sana kwa wanawake.

Nimewahi kusimuliwa na ndugu yangu mmoja ambaye alikuwa akinisimulia insi alivyokutana na mke wake wa sasa. Alinieleza kuwa walikutana katika kituo cha daladala wakisubiri usafiri, na daladala ilipofika kutokana na msongamano wa abiria, yule mwanamke aligongwa na mwanamke mwenzake mpaka akadondosha simu na mkoba wake chini.

Ndugu yangu anasema alipoona yule mwanamke akiwa ameduwaa akiwa hajui nini cha kufanya, aliwani na kumsaidia kuokota vitu vyake chini na kumkabidhi, kisha akamsaidia kupada ndani ya daladala.
Kwa msaada huo ambao kwa mwanaume angeuona wa kawaidsa nap engine asingekumbuka hata kusema asante, yule mwanamke alijikuta akimshukuru sana ndugu yangu na walipofika mwisho wa safari, alimuomba ndugu yangu namba ya simu na huo ukawa ndio mwanzo wa uhusiano wao mpaka wakaja kufunga ndoa na kuoana.

Huo ni mfano mdogo tu wa namna wanawake wanavyopenda kusaidiwa, kusikilizwa na kuonewa huruma.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………

Kwa kutojua tofauti hii, wanaume wengi hujikuta wakiwaudhi wake zao kutokana na kuchukulia mambo kirahisi hali ambayo husababisha manun’guniko makubwa kwa wenzi wao.

Ni vizuri wanaume wakajenga utaratibu wa kuwasikiliza wake zao au wenzi wao kwa upole na umakini wa hali ya juu. Makosa ambayo wengi huyafanya bila ya wao kujua ni pamoja na kusoma gazeti au kuangalia Tv wakati mkeo anakueleza jambo akihitaji umsikilize na pengine anahitaji umpe msaada wa nini cha kufanya (Umfundishe).

Kwa mwanaume ataona ni jambo la kawaida kusoma gazeti wakati mkewe akimueleza kero zake wakati kiuhalisia wanawake hujisika vibaya sana na kuamini kuwa hawana thamani tena na ndio waume au wenzi wao hawawasikilizi kwa makini.

WANAUME HUPENDA KUSIFIWA
Miongoni mwa vitu ambavyo wanaume wanavipenda maishani mao basi ni kusifiwa. Kwa kawaida mwanaume husikia fahari kubwa sana kusifiwa, wakati mwanamke akisifiwa sana hujihisi aibu.

Mwanaume anaposifiwa hasa na mtu anayempenda kama mke wake au mpenzi wake, yuko tayari hata kufa akitaka azidi kusifiwa zaidi. Hakuna sumu kali kama mwanamke kumkosoa mwanaume, hususani mbele ya watu wengine. Hili ni kosa ambalo wanawake wengi kulifanya pia. Unakuta mke anamkosoa na kumcheka mumewe mbele ya watoto au majirani huku akiwa hana wasiwasi kabisa kuwa anafanya makosa makubwa.

Watafiti wa mambo ya mahusiano wanaeleza kuwa tatizo la wanawake kuwahosoa wanaume, huwaumiza sana wanaume kisaikolojia na ni miongoni mwa sababu inayopelekea wanaume wengi kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume. Pia kukosolewa huku hupelekea wanaume kushindwa kujiamini hata mbele ya wanaume wenzao na huhisi kuwa thamani yao ina walakini. Hii ni sumu mbaya sana ambayo wanawake wanapaswa kuikwepa ili kudumisha uhusiano bora na wenye kudumu.

WANAWAKE HUPENDA KUONESHWA KAMA WANAPENDWA
Inawezekana ikawa ni vigumu sana kujibu swali kuwa ni kwa nini wanawake ndio wanaotakiwa kutongozwa, wakati mwanamke akimtongoza mwanaume anaonekana hajatulia. Kihulka, imani hii inatokana na ukweli kwamba mara zote wanawake ni viumbe wanaotakiwa kupendwa kwanza ndipo nao waoneshe upendo wao.

Ni vigumu sana kuishi bila kukwaruzana na mwanamke kama anahisi kuwa humpendi wala humjali. Wakati wanaume wao wanapenda sana sifa, wanawake wanapenda sana kupendwa na wako tayari kufanya lolote ili kumfurahisha mtu anayeonesha mapenzi ya hati kwao.

Ni rahisi sana kwa mwanamke kushawishika kutembea nje ya ndoa endapo atahisi kuwa mume aliyenaye hampendi kwa dhati, wahati kuna mwingine wa nje anayeonesha mapenzi ya kweli. Ukifanya utafiti, utagundua kuwa wanaume wengi huwa wepesi wa kuwatamkia wanawake kuwa wanawapenda katika siku za mwanzo za uhusiano, lakini wakishaingia ndani ya ndoa huwa ni wagumu sana kutamka neno “Nakupenda”.

Mwanamke mmoja alikuwa akitoa ushuhuda kuwa mumewe alimtamkia neno nakupenda siku moja tu wakati anamtongoza, lakini baada ya kumkubali na kuolewa naye, yapata miaka kumi na tatu sasa hajawahi kusikia tena neno hilo kutoka kwa mumewe, na hata pale yeye anapomwambia kuwa anampenda, huwa anamjibu kwa kifupi kuwa anajua kuwa anampenda.

WANAUME HUPENDA KUJITENGA WAKIWA WAMECHOKA
Kuna usemi maarufu unaotumika duniani kote unaoelezea kuwa wanaume wametokea katika sayari ya Mars wakati wanawake wanatoka katika sayari ya Venus. Msemo huu una maana kubwa sana kwamba, mara nyingi hulka za wanaume huwa zinakinzana na za wanawake. Wataalamu wanaeleza kuwa mara nyingi wanaume akili zao zinapochoka, huwa wanahitaji kukaa peke yao mpaka akili itulie ndipo waweze kuendelea na shughuli nyingine. Wanawake wengi huwa hawaliekewei hili na kwa ujinga wao hujikuta wakizidi kuwakera waume zao.

Mfano unakuta mwanaume anarudi kazini jioni kichwa kikiwa kimechoka. Badala ya mke kumpokea kwa maneno matamu yatakayomfanya uchovu wake upungue, anaanza hoja za kichokozi huku akitoa lawama kibao, mara kwa nini ulikuwa hpokeai simu, kwa nini umechelewa kurudi, ulikuwa umeongozana na nani, na kauli nyingine zilizojaa lawama.

Ni dhahiri kuwa kwa kuwa akili ya mwanaume inakuwa imeshachoka, atakuja juu kama mbogo na uwezekano wa kumpiga mwanamke wa aina hii huwa ni mkubwa. Ukichunguza kwa makini, wanawake wanaolalamika kuwa huwa wanapigwa na waume zao, wao ndio huwa sababu kubwa ya kupigwa kwao kutokana na kushindwa kuwasoma waume zao.

WANAWAKE HUPENDA KUBEMBELEZWA WANAPOKUWA WAMECHOKA
Tofauti na wanaume ambao wakichoka hupenda kujitenga peke yao, wanawake wanapokuwa wamechoka hupendwa kubembelezwa na kufarijiwa kwa karibu. Hupenda kuwa jirani na mtu ambaye atawapa maneno matamu yatakayowafanya wasahau maswaibu na uchovu wa kutwa nzima.
Hali kuwa inakuwa mbaya katika nyumba ambayo mwanaume na mwanamke wote ni wafanyakazi. Unakuta mwanaume amerudi kazini akiwa amechoka na anahitaji muda wa kukaa peke yake mpaka akiliyake itakapotulia, upande wa pil mwanamke nae amerudi kazini akiwa amechoka sana na anahitaji kukaa jirani na mumewe kwa ajili ya kubembelezwa baada ya kazi za kutwa nzima.

Kitakachotokea hapa ni kwa mwanaume kutafuta uhuru wa kuwa peke yake. Atatoka na kwena kukaa peke yake sebuleni , ukumbini au chumbani. Kitendo hiki kitamfanya mwanamke ahisi kuwa huenda amemuuzi mumewe na ndio maana anajitenga, na ataanza kumfuatafuata kila anakokwenda. Matokeo yake ni kila mmoja kuishia kuboreka na mwenzake na hapo ndipo maudhi madogomadogo yanapoanza, na kwa wasipokuwa makini wanaweza kuishia kwenye ugomvi mkuba saa ambao chanzo chake hakieleweki.

Itaendelea
amenibarikihash@rocketmail.com
newera7113.blogspot.com
+255 (0) 768540912
STAY BLESSED YOU ALL!

Thursday, December 10, 2009

BLOOD REVENGE (Part II of My Heart Is Bleeding)







Baada ya kukaa kwa muda mrefu ndani ya kisiwa cha Zanzibar, Khaleed anapanga mikakati madhubuti ya namna ya kurudi nchini kwao, kwa ajili ya kazi moja tu! Kulipa kisasi cha damu kwa wote waliohusika na mauaji ya ndugu zake bila ya hatia.

Ilikuwa ni lazima arudi nyumbani kwao kulipa kisasi kwani damu ya ndugu zake iliyomwagika bila ya hatia ilikuwa ikimuandama muda wote, na tayari alishajiapiza tangu kipindi, kuwa lazima alipe kisasi.
‘I must revenge! The blood revenge to whoever may concern.”

Licha ya kuwa tayari Khaleed alikuwa ameanza ukurasa mpya wa maisha , hasa baada ya wazazi wake wote kufariki dunia, bado aliamini hakuna kitu ambacho kingeweza kuziba pengo la wazazi wake hapa duniani. Ni hali hii ndiyo iliyomfanya apitie mateso makubwa sana duniani kabla ya Mungu kumbariki kwa kumuangazia nuru ya maisha alipokuwa huko machimboni Mererani, alikofanikiwa kuondoka na jiwe kubwa la madini ya tanzanite, madini ambayo kwa kiasi kikubwa yaliyabadilisha maisha yake, kutoka maisha ya uchokoraa hadi kufikia kuwa milionea mtoto.

Aliendela kukaa ndani ya visiwa vya Zanzibar, kwenye hoteli moja ya kifahari iliyokuwa pembezoni mwa bahari ya hindi. Aliendelea kukaa pale kwa wiki kadhaa akiumiza kichwa namna atakavyoitekeleza operesheni aliyoipa jina la ‘Blood revenge 7113’. Muda wa jioni alikuwa akitoka na kwenda kukaa peke yake ufukweni, akiwa na kijitabu chake kidogo (Note book) akiandika kila kitu kuhusu namna ambavyo angeendesha kazi ile kubwa iliyokuwa mbele yake.

Pesa kibao alizozipata baada ya kuuza madini ya Tanzanite, zilitosha kumfanya aishi maisha aliyoyataka aliendelea kusuka mipango kwa umakini wa hali ya juu ili kuhakiksha anakamilisha zoezi lile gumu na la hatari bila ya kushtukiwa. Alikuwa akiandika majina ya watu wote waliohusuka kuiangamiza familia yao, akianza na mashetani watatu wa kundi hatari la wafanya biashara wa Holly Trinity. Aliandika majina yao kwenye kijitabu chake cheusi, akitumia kalamu nyekundu.

Aliwaandika pia watu wote walioshirikiana na The Holly Trinity, kuanzia na kamanda mkuu wa polisi wa kanda maalum, Luteni Lauden Kambi ‘Fuvu’ ambaye hkaleed alikuwa akiamini kuwa ameshiriki kwa kiwango kikubwa kwani kama angeifanyia kazi taarifa ya mapema iliyotolewa na wazazi wake, yale yote yasingetokea. Aliwaandika pia watu wengine wengi ambao kwa pamoja walitengeneza orodha ndefu ya watu ambao walikuwa wakistahili kufa kwa mikono yake.
“They deserve to die f*c them to hell” (Wanastahili kufa mashetani hawa), Khaleed aliongea kwa sauti ya juu wakati akiitazama upya ile orodha yake.

Kwa kuwa aliongea kwa sauti ya juu, bila kujua kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa amekaa jirani yake, ilibidi aanze kuvunga akiwa na lengo la kupindisha ukweli kwani hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa akiandaa mikakati kabambe ya kuua. Jirani na pale alipokuwa amekaa, pembeni alikuwa amekaa binti mmoja, ambaye kiumri walikuwa wakishabihiana na Khaleed. Kauli ile ya Khaleed “They deserve to die…’ Ilimshtua sana kiasi cha kugeuza sura yake kuelekea pale Hkaneed alipokuwa amekaa.

Aliendelea kumtazama lakini Khaleed alikuwa akijitahidi kupoteza mada baada ya kugundua kuwa alikuwa amefanya kosa kuropoka kwa sauti bila ya kujua kuwa kulikuwa na mtu pembeni yake pale ufukweni, kando ya hoteli ya kifahari aliyokuwa amefikia. Aliendelea kupunga upepo wa baharini huku mawazo mengi yakipishana akilini mwake. Yule binti aliendelea kumtazama Hkaleed kwa jicho la kumsoma, lakini Khaleed alijifanya hana habari naye.

Baada ya kuona yule binti akizidi kumtazama, Khaleed aliinuka na kuondoka pale alipokuwa amekaa na kuanza kurudi kwenye hoteli aliyokuwa amefikia. Hakutaka hata kumtazama usoni. Alipitiliza moja kwa moja mpaka chumbani kwake alikofikia ambapo alijitupa juu ya kitanda na kujilaza, huku mawazo yakizidi kupishana akilini mwake.

Kwa kadri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele, ndivyo hamu ya kulipa kisasi ilivyokuwa ikizidi kuongezeka akilini mwa Khaleed. Baaada ya kukaa kwa zaidi ya wiki tatu pale kisiwani Zanzibar, kwenye Hoteli ya kifahari aliyokuwa amefikia, safari ya kurudi nyumbani kwao Blazinia ilikuwa imekamilika. Maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika na sasa alikuwa katika hatua za mwisho kabla ya kuanza rasmi kazi yake, kazi ya kulipa kisasi cha damu.

Ikiwa ni jioni ya mwisho aliyopanga kukaa kisiwani Zanzibar, Khaleed alitoka na kwenda ufukweni kama kawaida yake, safari hii akiwa na matumaini makubwa kuwa hatimaye kazi nzito iliyokuwa mbele yake alikuwa akienda kuikamilisha. Jioni hii alionekana kuwa mchangamfu kuliko siku zote alizokaa pale hotelini. Furaha yake ilitokana na ukweli kwamba karibu taratibu zote zilikuwa zimekamilika na kilichokuwa kimesalia ilikuwa ni utekelezaji tu. Alitoka na kwenda moja kwa moja kukaa ufukweni kupunga upepo huku akichezea mchanga wa baharini.

Alikuwa akijaribu kukumbuka kila kitu kilichotokea maishani mwake mpaka akajikuta akiwa mpweke chini ya jua, akiwa hana ndugu hata mmoja aliyesalia akiwa hai. Alikumbuka kila kitu kuanzia siku ya kwanza jinamizi la mikosi lilipoanza kuiandama familia yao, akakumbuka kila kilichoendelea baada ya hapo mpaka muda ule akiwa pale ufukweni.

Kumbukumbu mbaya zilizokuwa zikipita kwa kasi ndani ya ubongo wake zilimuongeza uchungu mtimani, na akajikuta akianza kutokwa na machozi, hasa alipomkumbuka mama yake mzazi na jinsi alivyouliwa kikatili kwa kuchomwa sindano ya sumu na kumfia mikononi mwake.

Alikumbuka pia jinsi baba yake alivyouliwa kikatili kwa kupigwa risasi mbele ya macho yake, akiwa na kaka yake wa hiyari, Girbons, wakati wakijaribu kutoroka. Picha za matukio ya wadogo zake walioliwa na simba wa Gamutu usiku wa siku ya kwanza walipotekwa kutoka nyumbani kwao usiku wa manane, na mwisho kumbukumbu za kaka yake mwenye ulemavu wa ngozi ambaye mpaka muda huo alikuwa akiamini kuwa tayari ni marehemu… alishindwa kuyazuia machozi yasiuloanishe uso wake, moyo wake ulikuwa ukivuja damu.

Khaleed akijikuta akizama kwenye dimbwi zito la mawazo na hisia za maumivu makali zilizokuwa zikiuchoma mtima wake kiasi cha kutosikia wala kuona kuwa kuna mtu alikuwa akimsogelea. Alitoa kitambaa chake cha mfukoni (handkerchief) na akawa anafuta machozi, ambayo sasa yalikuwa yameuloanisha uso wake wote.

“kaka habari yako!”, Khaleed alisikia sauti laini ya kike ikimsabahi kutoka nyuma yake, lakini kutokana na halialiyokuwa nayo, hakuitikia salamu ile, na akawa anazidi kujifuta machozi.
“Kaka nakusalimu! Mbona kimya”, yule binti alirudia salamu yake na akawa anahoji kwa nini Khaleed alikuwa haitikii salamu yake. Alimsogelea kwa jirani zaidi na ndipo alipogundua kuwa alikuwa amezama kwenye hisia zilizoonekana kuuchoma moyo wake.

“Jamani pole kaka’angu, it seems you got serious problem, can I help you?” ( Inaonekana una matatizo makubwa! Naweza kukusaidia?) yule binti aliuliza kwa sauti ndogo ya upole huku akimgusa begani Khaleed. Kwa kifupi Khaleed alikuwa katika wakati mgumu sana kiasi ambacho aliona kama ni usumbufu mkubwa kwa mtu mwingine kuja kumvurugia utulivu wake, alihitaji kuwa peke yake. Alimgeukia na macho yao yakagongana. Alikuwa ni yule binti ambaye siku chache zilizopita walikuwa wamekaa jirani palepale beach ingawa hakuna ambaye alimsemesha mwenzake.

Khaleed na yule binti waliendelea kutazamana kwa dakika kadhaa bila ya kusemeshana chochote. Yule binti aliuvunja ukimya kwa kurudia kumuuliza Khaleed kama angeweza kuhutaji msaada wake.
“ Can I help you?”, aliuliza tena yule binti kwa sauti ya upole na yenye kubembeleza kanini Khaleed akaitikia kwa kichwa kuonesha kuwa alikuwa haitaji msaada wake.

Khaleed aliinuka na kuanza kuelekea kwenye hoteli aliyokuwa amefikia, akimuacha yule binti ameduwaa kwa mshangao huku akimuonea huruma. Hakugeuka nyuma mpaka aliopotelea ndani ya hoteli ya kisasa aliyokuwa amefikia kwa takribani wiki tatu sasa, tangu alipowasiri kutoka machimboni Mererani, huko Arusha Tanzania. Yule binti alimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kabisa kwenye upeo wa macho yake.
*******
Ndani ya chumba cha hoteli ya kimataifa ya Isles Sand Resort, Khaleed alikuwa akipanga zana zake kwa ajili ya kuanza rasmi kazi yake ya kulipa kisasi, ambayo alikuwa amepanga aianze siku iliyokuwa ikifuata. Alikuwa akipanga vitu vyake vichache ndani ya mkoba wake mdogo wa rangi nyeusi.

Miongoni mwa vitu alivyokuwa anavimiliki, ilikuwepo bastola ndogo aliyofanikiwa kutoroka nayo kutoka mikononi mwa jambazi hatari huko Arusha Tanzania, aliyekuwa akifanya kazi hatari ya kuteka magari yanayosafirisha madini na vito vya thamani kutoka kwenye machimbo ya Tanzanite, huko Mererani.

“Hii itanisaidia sana! Where a metal must meet a meat” Aliongea Khaleed akimaanisha kuwa lazima risasi za mashine ile ndogo zikutane na nyama za wabaya wao.

Licha ya bastola, alikuwa na kichupa kidogo kilichokuwa ndani ya Kiboksi cheusi kilichokuwa na maandishi mekundu yaliyosomeka, ‘Ampethamine cyanide serum’. Kwa haraka alikikumbuka kiboksi kile na akakumbuka jinsi alivyokipata. Alikuwa amemuibia yule jambazi aliyemteka wakati akitoka Mererani, ambaye baadae aligeuka na kuwa rafiki yake akimtaka Khaleed aungane naye kwenye kazi yake ya ujambazi.

Alipokuwa akimuonesha vifaa vyake vya kufanyia kazi, alimuonesha pia na kile kichupa na akamueleza kuwa ile ni sumu hatari sana ambayo huchanganywa kwenye aina Fulani ya pafyumu, na inapopulizwa hewani na binadamu kuvuta hewa yake, ilikuwa ikifanya kazi katika hali ya kutisha sana. Alimpa maelekezo ya namna ya kuichanganya sumu ile na aina ya manukato yenye kemikali iitwayo “Dopamine Venule rapture” ambapo kwa pamoja mchanganyiko huo ulikuwa ukitengeneza sumu kali sana iitwayo ‘Mankind Homocidal Perfume’.

Itaendelea

amenibarikihash@rocketmail.com
newera7113.blogspot.com
+255 (0) 768540912
STAY BLESSED YOU ALL!

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...