Monday, February 5, 2018

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 62



ILIPOISHIA:
“Ndiyo, lakini mambo yenyewe ndiyo kama hivi, hatupati hata dakika chache za kuwa pamoja, mi nimechoka bwana,” alisema Shamila na kunisogelea mwilini, nikawa naiona hatari iliyokuwa mbele yetu endapo Junaitha atageuka na kugundua kwamba tulibaki koridoni tumesimama, tena tukiwa tumesogeleana mithili ya majogoo yanayotaka kupigana.
 SASA ENDELEA...
“Please Shamila, huu siyo muda muafaka, kama inawezekana tutafute muda baadaye,” nilisema kwa sauti ya chini, akashusha pumzi ndefu na kunitazama usoni kwa macho yake mazuri, tukaendelea kutembea lakini alionesha kweli amemaanisha kile alichokisema.
Tuliingia kwenye kile chumba ambacho tulikuwa tukikutania kila panapokuwa na shughuli maalum, Junaitha akatuelekeza kukaa kwa duara kama ilivyokuwa kawaida yetu kisha akatuambia wote tuanze kuvuta hewa kwa wingi kwa kutumia pua na kuitoa kwa kutumia mdomo.
“Inatakiwa wote tufumbe macho na tuendelee kupumua taratibu, vuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na sio kifua, unajua kuna watu wengi wanaishi lakini hawajui hata namna ya kupumua, badala yake wao wanahema,” alisema Junaitha na kuanza kutufafanulia kile alichokisema.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 61



ILIPOISHIA:
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
SASA ENDELEA...
Kila kitu kilibadilika kwa kasi kubwa mno, mvua kubwa ikaendelea kumwagika, huku wingu kubwa jeusi likitanda kila kona na kuimeza kabisa nuru iliyokuwepo, ungeweza kudhani tayari ni usiku.
“Kuna kitu kinataka kutokea siyo kizuri, hebu nifuateni haraka,” alisema Junaitha, wote tukakurupuka na kusimama, tukatoka na kuanza kumfuata Junaitha, tukiwa hatuelewi tunaenda wapi.
“Asibaki mtu nyuma, kuweni makini,” alisisitiza Junaitha huku akipiga hatua za harakaharaka, tukazidi kuelekea ndani ya nyumba hiyo, tukafika mpaka sehemu kulipokuwa na korido nyembamba, tukaenda mpaka mwisho wa korido ambako hakukuwa na mlango wala sehemu ya kupita, nikawa sielewi lengo la Junaitha.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 66



ILIPOISHIA:
“Mbona unavuja damu nyingi hapo, umepatwa na nini?” alisema Rahma, nilipojitazama pale ubavuni, nilishtuka sana baada ya kuona damu nyingi nzito zikiwa zimenitoka bila mimi mwenyewe kujua chochote na kulowanisha kabisa shati langu.
SASA ENDELEA...
Sikujua nini cha kufanya, nilitamani nirudi haraka ndani kabla mambo hayajazidi kuharibika lakini Rahma akaning’ang’ania, kwanza akitaka kujua kwa nini yule muuzaji alikuwa akinikimbia lakini pili nini kimetokea mpaka shati langu lilowe damu kiasi kile.
Kiukweli sikuwa na majibu, nikawa naendelea kuhangaika kuzuia damu isiendelee kunitoka. Rahma alivua kitenge chake na kunipa, naye akawa ni kama haelewi kilichokuwa kinaendelea.
Tukiwa tunaendelea kuhangaika, mara nilisikia ile hirizi yangu mkononi ikinibana sana, nikajua mambo yameshaharibika. Nilishaambiwa kwamba nikiona inanibana ghafla, ujue mahali nilipo kuna mtu mwenye nguvu za giza na kuna jambo baya anataka kulifanya.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 65


ILIPOISHIA:
Nilihisi kama kuna kitu kinanilamba hivi, nikaanza kutetemeka huku nikiendelea kujikausha nisisababishe mtikisiko wa aina yoyote, nilipozidi kuvuta utulivu, nikahisi kuna kitu cha baridi kinatingishikatingisha upande ule niliokuwa nalambwa, mapigo ya moyo yakawa yanadunda kama nimetoka kukimbia mbio za mita mia moja.
SASA ENDELEA...
Nilitulia tuli huku nikiendelea kutetemeka, mara nikaanza kuhisi kile kitu kikitambaa na kunivuka mwili, kutoka upande mmoja kuelekea upande mwingine. Japokuwa kulikuwa na giza niliweza kukitambua vizuri kiumbe hicho kuwa alikuwa ni nyoka. Hata sijui ushujaa wa kutulia vile niliupata wapi maana kama nilivyowahi kusema, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa maishani mwangu kama nyoka.
Basi yule nyoka mdogo alinitambuka na kupotelea upande wa pili wa kitanda, nikashusha pumzi ndefu kisha kwa tahadhari kubwa nikainuka pale nilipokuwa nimelala, nikasimama kwenye uchago wa kitanda na kujivuta mpaka kwenye swichi ya taa, nikaiwasha.

Friday, February 2, 2018

Kivuruge wa Tandale- 5



ILIPOISHIA:
Sikukumbuka hata kumalizana na Shija, harakaharaka nikavuka barabara kuelekea upande ule aliokuwa amekaa yule mrembo, huku nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia anataka kuniambia nini.
“Mambo kivuruge?” alinisalimia huku akitabasamu, nikashtuka amelijulia wapi jina hilo? Uso wangu ukajawa na aibu.
SASA ENDELEA...
“Nancy!”
“Mh! Umewezaje kulikumbuka jina langu haraka hivyo?”
“Aa! Kawaida tu, unajua kitu au mtu muhimu kwenye maisha yako huwezi kumsahau kirahisi,” nilijikakamua kiume na kujaribu kuyatawala mazungumzo.
“Karibu tupate vinywaji,” alisema msichana huyo huku akinionesha sehemu ya kukaa, nikashindwa kukataa, nikajisogeza na kukaa naye meza moja, tukawa tunatazamana. Si kawaida yangu kumuonea aibu mwanamke, hata awe mzuri kiasi gani lakini siku hiyo nilijikuta nikipoteza kabisa ujasiri mbele ya Nancy.
Kulikuwa na mambo mengi ambayo yalifanya nipoteze ujasiri, kwanza siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza kukutana na msichana huyo mrembo, muda ule nilipotoka kwenda kula ‘lunch’.

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 60



ILIPOISHIA:
Junaitha alimkokota mpaka bafuni na kufunga mlango kwa ndani, nikabaki nimesimama pale koridoni. Ghafla nikaanza kusikia sauti ya Firyaal akilia kama mtu anayekabwa na kitu, nikakurupuka mpaka kwenye kile chumba walichokuwa wamelala wote, nikafunga breki za ghafla mlangoni, nikiwa siamini kile nilichokuwa nakiona.
SASA ENDELEA...
Firyaal alikuwa amejikaba shingoni kwa kutumia mikono yake miwili, macho yakiwa yamemtoka pima, akikoroma kama mtu anayeelekea kukata roho. Sikuwahi kusikia hata mara moja kama kuna mtu amewahi kufanikiwa kuyakatisha maisha yake kwa kujikaba mwenyewe lakini kwa Firyaal ilionesha kama hilo linaweza kutokea muda wowote.
Kwa kasi ya ajabu nilisukuma mlango na kwenda kumkamata Firyaal, kwa jinsi alivyokuwa na mwili ‘teketeke’, niliamini itakuwa rahisi kwangu kumtoa ile mikono yake shingoni lakini kumbe nilikuwa najidanganya.
Nilishangaa nilipomgusa Firyaal kukuta mwili wake umekakamaa na kuwa mgumu kama mti, nikaanza kuhaha kujaribu kumnasua bila mafanikio, aliendelea kukoroma huku wenzake wakiwa wamelala fofofo.

Mbinu Nyepesi za Kujitibu Upungufu wa Nguvu za Kiume

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 64



ILIPOISHIA:
Tukiwa tunaendelea kuchanja mbuga, baba akiwa mbele na baba yake Rahma akiwa nyuma, mara tulianza kusikia sauti za ajabu kutoka ndani ya pori lile, huku kukiwa na purukushani kubwa, mapigo ya moyo wangu yalilipuka na kuanza kunienda mbio kuliko kawaida.
SASA ENDELEA...
“Nakufaaa! Naku...fa...aa,” sauti ya mwanamke ilisikika, aliporudia mara ya pili kuimba msaada, sauti yake ilikuwa ikikwamakwama na muda mfupi baadaye akaanza kukoroma kuonesha kwamba mtu au watu waliokuwa wakitaka kumdhuru tayari walishafanikisha lengo lao.
Tofauti na hali niliyokuwa nayo mimi, baba na baba yake Rahma hawakuonesha kushtuka chochote, yaani ilikuwa ni kama hakuna kilichotokea na wala hakuna aliyeshughulika kwa chochote.
Muda mfupi baadaye, harufu ya damu mbichi ilitawala eneo lote lile, milio ya bundi na midege mingine ya ajabu ikazidi kuifanya hali iwe ya kutisha mno. Baba aliendelea kupiga hatua ndefundefu, hukumoyo wangu ukiwa umepondwapondwa kwa hofu na mshtuko, na mimi nikawa naongeza mwendo, miguu yangu ikitetemeka kuliko kawaida.

Thursday, February 1, 2018

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 59



ILIPOISHIA:
Maneno yake yalinipa nguvu sana, akaniambia kwamba aliwalaza usingizi mzito kwa makusudi wale wengine ili tukamalizie kazi ya kumzindua Shenaiza lakini akanipa taarifa ambazo zilinishtua mno. Aliniambia baba yake Shenaiza amejizatiti vilivyo kwa nguvu za nje na ndani na ili tufanikishe azma yetu, ilikuwa ni lazima mtu mmoja kati yetu afe.
“Afe?”
“Ndiyo, lazima afe mtu kwenye kafara.”
SASA ENDELEA...
“Sasa mambo ya makafara yanaingiaje tena hapa? Kama ni hivyo basi mimi najitoa.”
“Ukijitoa maana yake wewe ndiyo utakufa. Wasiwasi wa nini na wewe ni mwanaume? Hebu acha woga, nitakufundisha cha kufanya wala usiwe na wasiwasi,” alisema Junaitha lakini kiukweli alikuwa amenichanganya mno.
Mmoja kati yetu lazima afe? Nani sasa! Kama siyo mimi ni nani? Raya? Haiwezekani. Shenaiza? Hapana. Shamila? Noo! Au Firyaal? Nilijiuliza maswali mengi ambayo yote hayakuwa na majibu. Nilichokifanya ilikuwa ni kujaribu kupambana na hofu ambayo sasa ilikuwa inanitafuna ndani kwa ndani.

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 63



ILIPOISHIA:
“Nimepata salamu zako kwamba umechagua kuwa tajiri, ombi lako limekubaliwa lakini kuna masharti inatakiwa kabla siku zako saba hazijaisha, uwe umeshaanza kuyafuata, vinginevyo utakufa,” alisema yule mwanamke, macho yakanitoka pima.
SASA ENDELEA...
Nilijiweka vizuri pale chini nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kusikia ataniambia nini, akanitazama machoni kisha akashusha pumzi ndefu na kunisogelea.
“Kwa nini umeamua kupita njia hii?” aliniuliza kwa sauti ya upole, nikashindwa kuelewa alikuwa anamaanisha nini.
“Unalingana na kijana wangu ambaye mwezi wa kumi na mbili angekuwa anatimiza miaka 21, makosa yangu yamesababisha niishi maisha ya kujuta kila siku, sitaki mtu mwingine apite njia kama niliyowahi kupita mimi na kusababisha nimpoteze mwanangu kipenzi,” alisema lakini wala maneno yake hayakuniingia akilini.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...