Friday, November 17, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 50


ILIPOISHIA:
Sijisifii lakini ukweli ni kwamba katika suala la mbio, nilikuwa na uwezo mkubwa sana, dakika chache baadaye nikawa nimeshatokomea kwenye mashamba ya mikorosho na minazi, kelele za wale watu waliokuwa wakinifukuza zikiwa bado zinaendelea kusikika, sauti ya baba ikasikika tena masikioni mwangu lakini safari hii, ilikuwa na maelezo ambayo yalinimaliza kabisa nguvu, nikajua mwisho wangu umewadia. Niliujutia sana uamuzi wangu wa kujipeleka mwenyewe kwenye mdomo wa mamba.
SASA ENDELEA...
“Inabidi uvue nguo zote na kukimbia kuelekea upande wa Magharibi mpaka uvuke barabara ya lami kisha kimbia mpaka utakapoukuta mti mkubwa wa mbuyu, uzunguke mara saba kisha fumba macho, usifumbue mpaka nitakapokwambia,” sauti ya baba ilisikika masikioni mwangu.
Yaani nivue nguo zote na kuanza kukimbia nikiwa mtupu? Kibaya zaidi, upande huo wa Magharibi aliokuwa anausema ilikuwa ni kulekule nilikokuwa nakimbia. Kwa lugha nyepesi nilitakiwa kuanza upya kukimbia kurudi kule nilikotoka, safari hii nikiwa mtupu! Ilikuwa ni zaidi ya mtihani.
Kitu pekee nilichokuwa nakihitaji, ilikuwa ni kuokoa na balaa hilo kwani kwa jinsi wale wazee waliokuwa wakinikimbiza walivyokuwa na hasira, kama wangenitia mikononi mwao sijui nini kingetokea. Ilibidi nipige moyo konde, harakaharaka nikavua nguo zote na viatu, nikavikunja na kuvitia kwapani.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...