Monday, October 23, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 42


ILIPOISHIA:
“Una..ta..ka kufa...nya ni...ni,” sikumalizia kauli yangu, akawa tayari ameshafika pale kitandani, tukagusanisha ndimi zetu huku Shamila akionesha kweli kudhamiria kile alichokitaka. Hakuogopa kabisa kwamba pale ni wodini.
SASA ENDELEA...
Nilijaribu kumzuia lakini haikusaidia kitu, alishadhamiria na kwa ilivyoonesha, alikuwa tayari kufanya chochote ili apate alichokuwa anakitaka. Tuliendelea kugusanisha ndimi   zetu huku mikono yake laini ikitalii kwenye viunga mbalimbali vya mwili wangu, nikaanza kuhisi hali ya tofauti.
Unajua jambo ambalo nitaendelea kulisema kila siku, hakuna jambo baya kama kuyajaribu mapenzi. Wazee wetu waliosema kwamba mapenzi hayajaribiwi, walikuwa sahihi kabisa. Wakati naanza uhusiano wa kimapenzi na Shamila, nilikuwa najua kabisa kwamba tayari ninaye Raya ambaye ananipenda sana na tumeshaahidiana vitu vingi, tena kibaya zaidi mimi ndiyo nikiwa mwanaume wa kwanza maishani mwake.
Akilini mwangu nilijua kwamba hata nikimkubalia Shamila, haiwezi kuwa na tatizo lolote kwa sababu kiukweli sikuwa nimempenda kutoka ndani ya moyo wangu na nilipanga kumtumia kama daraja tu la kunifanya nipate nilichokuwa nakitaka kwa urahisi.

Hata hivyo, tangu Shamila alipoanza kua karibu na mimi, nilijikuta akiingia kwa kasi kwenye moyo wangu kuliko hata nilivyotegemea. Jambo ambalo sikuwahi kulijua tangu awali ni kwamba kumbe Shamila alikuwa mzuri kuliko Raya, kuanzia mwonekano, shepu, uchangamfu, uelewa wa mambo mpaka kwenye ufundi wa ‘uwanja wa fundi seremala’.
Ilifika mahali mwenyewe nikawa najiona kabisa kwamba nimeanza kumpenda Shamila kuliko Raya, jambo ambalo sikujua mwisho wake utakuja kuwa nini. Nawasihi kwa mara nyingine wanaume, hasa vijana kama sisi, hakuna kosa baya kama kucheza na hisia za wanawake wanaokupenda kwa wakati mmoja.
Basi Shamila aliendelea na mbwembwe, ‘Jamal’ wangu akachaji ile mbaya, nikajikuta mimi ambaye mwanzo nilikuwa navungavunga ndiyo nimekuwa nyota wa mchezo, kwa umakini wa hali ya juu nikajibinua, Shamila akawa chini mimi juu, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, kila mmoja pumzi zikimtoka kwa nguvu.
Sikuwa na muda wa kusubiri, nilianza kusakata kambumbu kwa mtindo wa kushambulia mfululizo, huku nikiwa makini nisijitoneshe jeraha langu la kifuani, Shamila akawa anayapokea mashambulizi yangu kwa miguno flan’ hivi ambayo ilizidi kunipandisha wazimu.
Ilifika mahali nikabadili mfumo wa kusakata kabumbu, nikawa nakimbia na mpira kwenye chaki kama Christiano Ronaldo vile, nikawa nahama pande zote na kumfanya Shamila apoteze ‘netiweki’, akaanza kutoa miguno kwa nguvu akiwa amesahau kabisa kwamba hatukuwa kwenye mazingira rafiki.
Niliongeza kasi, naye akaongeza kasi ya kunikaba, dakika chache baadaye nilitangaza kuzifumania nyavu zake lakini kabla sijamuwahi, na yeye alishatangaza kuzifumania zangu, ikawa ngoma droo!
Harakaharaka nilishuka pale kwenye kitanda changu na kuvaa vizuri nguo zangu ambazo hata sikumbuki nilizitupa saa ngapi sakafuni. Harakaharaka nikajiweka vizuri na kumsogelea Shamila ambaye eti tayari alikuwa ameanza kukoroma kwa mbali, akionesha kuchoshwa mno na mpambano ule wa kushtukiza.
Nikamtingisha kwa nguvu, akawa ananisukuma kama anayesema ‘niache nipumzike bwana’. Nilipozidi kumsumbua, aliinuka, naye akavaa magwanda yake, safari hii akiwa hataki kabisa kunitazama usoni. Akajizoazoa mpaka kwenye ofisi ya manesi ambako nako kulikuwa na kitanda, akajitupa kitandani.
Ilibidi mimi ndiyo niwe na kazi ya ziada ya kuondoa ushahidi wote eneo la tukio, nikaenda kufungua mapazia, nikafungua na milango na kuiweka kama inavyotakiwa kuwekwa, nikaongeza spidi ya feni na kurudi kitandani, nikajilaza huku moyoni nikijipongeza kwa kumtolea uvivu Shamila ambaye alikuwa akicheza na sharubu za simba.
Muda mfupi baadaye, niliona kivuli cha mtu akipita dirishani kwa nje, akaenda upande mmoja kisha muda mfupi baadaye akarudi na kusimama pale mlangoni, ilionesha kama ni mtu ambaye hakuwa na uhakika sana wa mahali anakokwenda. Kwa kuwa pale nje ya wodi za ‘private’ kulikuwa na walinzi, nilisikia wakimsemesha.
Kama kawaida yangu, nikawahi kujihami kwa kushuka pale kitandani haraka na kwenda kujibanza nyuma ya mlango ili hata kama ni miongoni mwa wale wanaoisaka roho yangu, akiingia tu niwahi kuchomoka.
Katika mahojiano yake, niligundua kwamba ni msichana, tena bado mdogo na alikuwa akitaka kuniona mimi maana niliwasikia akiwatajia mpaka jina langu. Baada ya kumhoji sana, wale walinzi walimruhusu kuingia, nadhani ni kwa sababu walishapewa maelekezo na Shamila juu ya kuwa makini na watu wanaokuja kwa lengo la kuniona. Akafungua mlango na kuanza kuangalia juu ya vitanda viwili vilivyokuwa ndani ya wodi hiyo.
“Firyaal,” nilisema baada ya kumtambua kuwa ni yule mdogo wake Shenaiza ambaye nilipewa maagizo ya kwenda nyumbani kwao kuonana naye, ambaye ndiye aliyenipa ‘hard disk’ iliyokuwa na siri nyingi kuhusu ushetani uliokuwa ukifanywa na baba yake.
“Jamal! Alisema huku akitetemeka, uso wake ukionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.
“Vipi mbona hivyo? Tulia kisha uniambie nini kinachokusumbua,” nilisema huku nikifunga mlango na kusogea naye mpaka pale kwenye kitanda changu.
“Baba anatarajiwa kurudi kesho nchini na tayari walinzi wake wamegundua kwamba kuna kitu kwenye kompyuta yake kimechomolewa, wakijua kwamba mimi na dada Shenaiza tunahusika hata sijui itakuwaje.
“Nipo chini ya miguu yako nakuomba unirudishie ile ‘hard disk’, nimefanya kazi kubwa sana kukutafuta, hospitali nzima hawajui umelazwa wodi gani,” alisema Firyaal, nikashusha pumzi ndefu na kumtazama.
“Usijali Firyaal kila kitu kitakuwa sawa,” nilimwambia na kuanza kumtuliza, nikamhakikishia kwamba kabla ya hiyo kesho, ataipata ‘hard disk’ yake, pia nikamwambia kuhusu matatizo yaliyokuwa yanamkabili dada yake.
“Tusaidie kama unaweza, najua baba akija maisha ya dada yapo hatarini sana, anaweza hata kuamuru auawe, yaani sijui baba siku hizi amekuwaje,” alisema Firyaal huku akianza kuangua kilio. Niliendelea kumtuliza huku nikitafuta mbinu ya kuwasaidia wote kwani kwa jinsi ilivyoonesha, baba yao alikuwa mtu hatari hata ndani ya familia yake mwenyewe.
Nadhani mazungumzo yetu yalimzindua Shamila aliyekuwa usingizini, akakurupuka na kutoka, akapigwa na butwaa kumuona mdogo wake Shenaiza. Alimkumbuka vizuri kwa sababu hata siku niliyoenda kuichukua ile ‘hard disk’, nilikuwa nimeongozana naye ingawa yeye alibaki ndani ya teksi.
“He, vipi imekuwaje? Binti nani amekuruhusu kuingia humu?” alihoji Shamila huku akijiweka vizuri nguo zake pamoja na nywele ambazo bado zilikuwa zimevurugika. Ilibidi nimtulize na kumweleza kilichomleta pale. Kwa bahati nzuri Shamila ni mwelewa sana, harakaharaka alielewa, kwa pamoja tukawa tunajadiliana nini cha kufanya.
“Inabidi kwanza hiyo ‘hard disk’ yake irudishwe haraka kisha baada ya hapo inabidi tufanye mpango wa kumtorosha Shenaiza wodini haraka iwezekanavyo, hayo yote yanatakiwa kufanyika usiku wa leo.
“Hata wewe hapa siyo mahali salama tena pa kuendelea kukaa, ngoja kwanza nimesahau kuuliza kitu muhimu. Wewe binti upo upande upi? Unamuunga mkono baba yako au na wewe unamsimamo kama wa dada yako?” Shamila alimuuliza swali muhimu.
Msichana huyo mdogo alituhakikishia, tena kwa kujiapiza kwamba kamwe hajawahi kumuunga mkono baba yake lakini amekuwa akikosa mtu wa kumsaidia kupambana naye.
Kauli yake hiyo ilitufurahisha sana mimi na Shamila, tukawa na uhakika kwamba sasa kazi itakuwa nyepesi kwa sababu tayari tutakuwa na mtu kutoka ndani kabisa, ambaye angetusaidia kutimiza lengo letu la kupambana na mtu huyo hatari.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...