Tuesday, August 15, 2017

The Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 21


ILIPOISHIA:
Hakuwa na nguo yoyote mwilini zaidi ya kipande cha sanda alichokuwa amefunikwa kuanzia juu kidogo ya mapaja mpaka kifuani ambacho nacho kilikuwa na damudamu. Baba akanitazama usoni, na mimi nikamtazama nikiwa na shauku kubwa ya kusikia kile atakachoniambia. Nilikuwa tayari kwa chochote ilimradi Rahma apone.
SASA ENDELEA...
“Mlichokifanya mkidhani ni siri yenu ndicho unachotakiwa kukifanya hapa,” alisema baba huku akigeuka na kuanza kutoka. Ilibidi nimshike mkono na kumvuta, sikuwahi kumfanyia baba hivyo hata siku moja lakini siku hiyo nilijikuta tu nikifanya hivyo.
“Baba!”
“Ambacho huelewi ni nini? Kama unataka apone fanya nilichokwambia na wakati wa tendo hakikisha hiyo sanda huivui,” alisema baba kisha akatingisha kichwa kuonesha kwamba niendelee, akanifinjia kijicho na kuachia tabasamu hafifu. Nilijikuta nikiogopa pengine kuliko kipindi chochote maishani mwangu.
Yaani mtu anaumwa kiasi kile, yupo kwenye hatua za mwisho za kukata roho, halafu eti naambiwa nifanye naye mapenzi, tena mwili wake ukiwa umelowa damu na mimi nikiwa nimevalishwa sanda! Moyo wangu ulipigwa na ganzi.

“Nakupenda Rahma na sinba cha kufanya zaidi ya kukusaidia, namuomba Mungu anisamehe na akusamehe pia na wewe,” nilisema huku machozi yakinilengalenga. Hali aliyokuwa nayo Rahma pale kitandani ilikuwa ya kuhuzunisha mno, nikaamua kupiga moyo konde na kuivaa roho ya kinyama.
Ilikuwa ni lazima niivae roho ya kinyama kwa sababu vinginevyo ningemuonea huruma Rahma kutokana na hali aliyokuwa nayo na pengine huruma yangu ndiyo ingekuwa tiketi yake ya kuendelea kuzimu.
Niliifunua ile sanda kwa mbele na kuacha uwazi, nikafumba macho na kuanza kuvuta hisia za jinsi mimi na Rahma tulivyokuwa tukiogelea kwenye dimbwi la mahaba, kwa mbali hisia zikaanza kunijia. Sikutaka kufumbua macho kabisa, niliendelea kufumba macho, nikapapasa na kupanda juu ya kile kitanda, mapigo ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida.
Nilipiga magoti na kumuweka rahma katikati yangu, nikakisogeza kile kitambaa cha sanda pembeni, nikaendelea kuvuta hisia huku machozi mengi yakinitoka na muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nikiogelea kwenye dimbwi la damu. Niliendelea kujikaza kisabuni, nikawa napiga mbizi hivyohivyo huku nikiendelea kulia.
Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishtuka baada ya Rahma kuzinduka na kunikamata mikono yangu kwa nguvu, ikabidi nifumbue macho, nikamuona amefumbua macho yake huku akijiuma midomo kama aliyekuwa akitaka kuzungumza kitu.
‘Ongeza spidi, dawa inakaribia kufanya kazi,” nilisikia sauti ya baba, sijjui hata ilitokea wapi kwani chumba kilikuwa kimefungwa na hata pazia lilikuwa limefunikwa. Nilijisikia aibu sana lakini sikuwa na cha kufanya, nilizidisha kasi ya kile nilichokuwa nakifanya, nikashangaa Rahma akiniachia mikono na kunikumbatia kifuani huku akianza kuangua kilio.
Sikujali damu zilizokuwa zimeulowanisha karibu mwili wake wote na pale kitandani, niliendelea kufanya kile nilichoagizwa na ghafla, nilimuona Rahma akianza kukakamaa mwili wake, nikazidi kuongeza kasi.
“Kuna kitu kitamtoka mdomoni, hakikisha unakikamata,” alisema baba, nikashtuka maana kauli yake ilimaanisha hicho kitakachomtoka kitakuwa na uhai, sasa tangu lini mtu akatoa kiumbe chenye uhai kutoka mdomoni?
Ghafla rahma alifumbua mdomo huku mwili wake wote ukiwa umekakamaa, nikashtukia kiumbe cha ajabu kama panya mweusi lakini asiye na manyoya mwilini akichungulia kutoka mdomoni, nilishtuka mno kiasi cha kunifanya nishindwe kuendelea kufanya kile nilichokuwa.
Ghafla kile kiumbe kiliruka kutoka mdomoni na kuangukia juu ya kitanda, nikasikia sauti ya baba akinisisitiza kwamba lazima nihakikishe nakikamata. Ilikuwa panya siyo panya, chura siyo chura yaani hata sijui nikielezeeje maana kichwa na kiwiliwili kilikuwa kama panya lakini hakuwa na manyoya wala mkia na hata kutembea kwake hakikuwa akikimbia kama panya bali kilikuwa kikiruka kama chura.
Nilijikuta nikipiga moyo konde, moyo wa kijasiri ukanivaa, nikaruka kutoka pale kitandani mpaka chini, nikakirukia kile kiumbe na kufanikiwa kukidaka kwenye mikono yangu lakini cha ajabu, kilipasukia mikononi mwangu, nikashtukia nimeshika mabonge ya damu.
“Safi sana!” baba alisema huku akiingia akiwa ameongozana na baba yake Rahma ambaye naye alianza kunipongeza, wakawa wananipigia makofi. Bado nilijihisi kama nipo ndotoni, sikuelewa kile kiumbe kimepotelea wapi tena na kuniacha na mabonge ya damu mikononi, nikawa natetemeka kuliko kawaida.
“Harakaharaka baba alitoa kitambaa cheupe, akanifuta yale mabonge ya damu na kukiweka kile kitambaa kwenye mfuko mweusi, akatoa wembe, akanichanja kwenye paji la uso, eneo nywele zinapoanzia na kutoa dawa kwenye kichupa, akanipaka na kuisugua kwa nguvu. Dawa ilikuwa ikiuma mno, akarudia kunipongeza kisha akaniambia kazi imekwisha, nimsaidie rahma kumsafisha na kusaficha chumba chote, wakatoka tena huku wote wakionesha kuwa na furaha kubwa mioyoni mwao.
“Togo!”
“Naam Rahma!”
“Nini kimetokea?” alisema Rahma huku akiinuka kitandani, akawa anashangaa kila kitu.
“Ni stori ndefu, naomba twende kwanza ukaoge,” nilimwambia, harakaharaka nikamuona akiinuka na kukimbilia khanga yake, akajifunga huku akionekana kunionea aibu. Hakuwa Rahma yule ambaye muda mfupi uliopita alikuwa akikaribia kukata roho, alishabadilika na kuchangamka utafikiri hakuna kilichotokea.
Baada ya kujifunga khanga, alisogea kwenye dressing table na kujitazama, nikamuona jinsi alivyoshtuka.
“Mungu wangu, mbona nimelowa damu hivi? Halafu mbona na wewe umelowa damu? Kwani nini kimetokea?” alihoji Rahma, ikabidi nivae tabasamu la uongo ili kumuondolea hofu moyoni. Nakumbuka baba amewahi kunifundisha kwamba njia nzuri ya kuishi na wanawake, ni pale wanapoonekana kulichukulia tatizo kwa ukubwa, wewe lirahisishe.
Hatua hiyo kweli ilifanikiwa sana, kwani licha ya mshtuko aliokuwa nao, aliponiona mimi nikitabasamu, Rahma aliamini kwamba kilichotokea hakikuwa tatizo kubwa, nikamshika mkono na kutaka kutoka naye tuelekee bafuni.
“Hiki nini ulichovaa?” aliniuliza, nikamtazama usoni na kumuomba anipe khanga nyingine na mimi nijifunge.
“Hujanijibu lakini.”
“Mbona una haraka ya kujua mambo yote mara moja? Nimekwambia nitakueleza kila kitu, kuwa mpole.”
“Halafu mimi si nilitaka kujiua?” alisema akiwa ni kama ameanza kurudiwa na fahamu zake, nikachukua khanga mwenyewe na kumshika mkono kumpeleka bafuni maana niliona akili yake bado ina mawenge.
“Utumie ile sabuni niliyokuwa kuogea wewe na yeye,” baba alisema, wote tukageuka na kuwatazama, kumbe walikuwa wakituangalia, wakiwa ni kama hawaamini kama Rahma yule aliyekuwa akikaribia kunusa umauti, ndiyo yule aliyekuwa akitembea mwenyewe.
“Nilifungua mlango wa bafuni, nikamtanguliza Rahma, nikamuona akitaka kujifungia mlango lakini nilisukuma na kuingia.
“Wanatuona, unafikiri baba na mama watatuelewaje?”
“Wao ndiyo wamenipa kazi ya kukusaidia kwa hiyo usiwe na wasiwasi,” nilisema huku nikifunga mlango kwa ndani, rahma akawa ananitazama kwa macho yenye maswali mengi bila majibu.
“Unatakiwa kuoga kwa kutumia hii sabuni,” nilisema huku nikimpa kile kijiwe cha ajabu nilichopewa an baba, ambacho nilikiacha humohumo bafuni, Rahma akawa bado anashangaashangaa, ilibidi nimdogeze kwenye bomba, nikafungulia maji, yakaanza kumwagikia ambapo alionekana kama kuanza kuzinduka.
“Kile nilichokiona mle bafuni na kuhisi kama naoga damu, ndicho kilichokuwa kinatokea muda huo kwani maji yaliyokuwa yakichuruzika kutoka kwenye mwili wa Rahma, yalikuwa damu tupu, nikavuta kumbukumbu na kuhisi labda kile kilichonitokea kilikuwa na uhusiano na tukio hilo.
Nilijifungua ile sanda, na mimi nikabaki kama Rahma, nikasogea pale kwenye bomba, maji yakawa yanatumwagikia, chini damu zikawa zinaendelea kutiririka kuelekea kwenye bomba la kutolea maji machafu. Nilimshika mikono Rahma, nikamvutia kwenye kifua changu, tukawa tunatazamana huku maji yakiendelea kutumwagikia, nikajikuta nikitamani kumbusu mdomoni.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...