Monday, August 7, 2017

The Graves of The Innocent (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 14



ILIPOISHIA:
“MUNGU wangu,” nilijisemea, mapigo ya moyo yakiwa yananienda mbio kuliko kawaida, nikiwa sijui nini kitatokea, hasa ukizingatia kwamba nilikuwa ugenini na ndiyo kwanza tulikuwa tumewasili.
SASA ENDELEA…

ALINIACHIA huku naye akionyesha kushtuka, akashuka kitandani na kuokota khanga yake, akajifunga kivivu na kunionyesha ishara kwamba niingie kwenye kabati la nguo, nilifanya hivyo haraka, nikamsikia akifungua mlango.
“Baba amesema usije ukafunga mlango mkubwa wa nje, watachelewa kuingia ndani kwani kuna kazi wanaifanya.”
“Haya poa,” nilimsikia akizungumza na mdogo wake, akashusha pumzi ndefu na kuufunga mlango, nikamsikia safari hii akifunga kwa funguo kabisa, akaja pale kabatini na kufungua mlango, akanionyesha ishara kwamba nitoke.
Sikulaza damu, nilitoka harakaharaka nikiwa kama nilivyo, na yeye akauachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, tukawa tunatazama kama majogoo yanayotaka kupigana. Alipiga hatua moja mbele, miili yetu ikagusana, akazungusha mikono yake kwenye shingo yangu, na mimi nikiwa sijiaminiamini, nikaukumbatia ‘mlima’ wake.
Nikiri kwamba hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuwa kwenye hali kama hiyo na nilichokihisi kwenye mwili wangu, sikuwahi kukihisi kabisa tangu napata akili zangu. Ni hapo ndipo nilipoanza kuelewa kwa nini watu wengi huwa wanayasifia sana mapenzi kwamba ni matamu kuliko asali.

Ni hapo pia ndipo nilipoelewa kwa nini watu wengine hufikia hatua hata ya kutoana roho, baada ya mmoja kugundua kwamba anatembea na mkewe au mpenzi wake. Dakika chache baadaye, nilikuwa nahema kama nataka kukata roho, ufundi wa mikono yake kuvinjari kwenye mwili wangu, ulinifanya mara kwa mara niwe natoa miguno ambayo sikuwahi kuitoa kabla.
Hata sikukumbuka nilifikaje kwenye uwanja wake wa fundi seremala, nilikuja tu kushtukia yeye yuko juu yangu nikiwa nimelala chali, huku nikiendelea kupumua kwa fujo, mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana na ‘Togolai’ akiwa anazidi kuongeza hasira kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele.
Kwa ufundi wa hali ya juu, alimuelekeza njia ya kupita, nikajikuta nikianza kuzungumza kama bubu, maneno hayatoki wala hayaeleweki, kucheka natamani lakini muda huohuo natamani kupiga chafya, ilikuwa ni hali ya ajabu mno. Safari iliendelea, mwanzo alikuwa akipiga hatua fupifupi lakini baadaye nikaanza kumuona akinogewa na kuongeza huku akitoa ukelele fulani ulioongeza raha kubwa kwenye masikio yangu.
Baadaye ilibidi tubadilishane magoli kwenye mechi ile ya kirafiki isiyo na refa wala jezi, yeye akawa anapeleka mashambulizi Kaskazini mwa uwanja na mimi napeleka Kusini.
Japokuwa hata danadana sikuwa najua kupiga na siku hiyo ndiyo ilikuwa ya kwanza, nilijitahidi kuonyesha kiwango kwa sababu nimewahi kusikia kwamba ukicheza chini ya kiwango, huwa unadharaulika mbele ya viumbe hawa.
Akaongeza mno kasi ya mashambulizi kisha akanikaba kwa nguvu shingoni kama wanavyofanya wale watu wanaopora simu au fedha, akanishikilia kwa nguvu na kunibana, na mimi nikaongeza kasi, nikajisikia hali fulani hivi nzuri sana, akazidi kunibana kisha akaniachia na kudondokea upande wa pili, jasho likiwa limemlowanisha chapachapa na mimi nikiwa hoi bin taaban, nilijikuta nikicheka mwenyewe kwa furaha.
Hakuzungumza jambo lolote kwa dakika kadhaa, baadaye aliinuka na kukaa kitandani, akawa ananitazama kama ambaye haamini kitu fulani.
“Una miaka mingapi?”
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Kwa nje unaonekana mdogo lakini wewe ni zaidi ya mwanaume,” alisema na kunikumbatia tena, akaanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu huku akiniambia kwamba ananipenda na anaomba nisimuache ila uhusiano wetu uwe wa siri.
Bado sikuwa naelewa alichokimaanisha, akaendelea na uchokozi wake na hata sijui nini kilitokea lakini muda mfupi baadaye, nilishtukia tukiwa tena dimbani, safari hii kidogo nikawa sina ugeni na uwanja pamoja na mchezo wenyewe.
Mpambano mkali uliendelea mpaka baadaye ambapo ile hali iliyotutokea mwanzo ilitokea tena, tena kwa kila mtu. Safari hii, alipoangukia upande wa pili, haukupita muda mrefu akaanza kukoroma.
Kwa kuwa muda ulikuwa umeenda sana, harakaharaka niliinuka na kuvaa nguo zangu nikaenda kufungua mlango na kutoka huku nikinyata, nikaenda mpaka kwenye mlango wa kile chumba ambacho nitalala na ndugu yangu mmoja.
Kwa bahati nzuri, mlango haukuwa umefungwa, nikaingia mpaka ndani, tayari ndugu yangu naye alikuwa akikoroma, nikajilaza kitandani huku nikisikia uchovu wa kiwango cha juu, karibu kila sehemu kwenye mwili wangu ilikuwa inauma.
Tabasamu pana lilikuwa limechanua kwenye uso wangu, hasa kumbukumbu ya nilichotoka kukifanya ilipokuwa inanijia. Sasa na mimi nilijihisi kuwa mwanaume niliyekamilika. Bado nilikuwa siamini jinsi nilivyoweza kuuangusha mbuyu kwa shoka moja, haukupita muda mrefu nilipitiwa na usingizi.
“Motooo! Jamani moto… nakufaaaa,” sauti za mtu aliyekuwa akipiga kelele kuomba msaada, ndizo zilizonishtua kutoka kwenye usingizi mzito, nikakurupuka huku mapigo yangu ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida, nikatoka mpaka koridoni.
Sikuamini macho yangu kusikia sauti ile ilikuwa ikitoka kwenye kile chumba ambacho usiku huo mimi na yule dada tulilambishana asali. Moto ulikuwa umekolea kiasi kwamba hata sehemu ya kupita haikuwa ikionekana.
Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kufika eneo hilo kwa sababu sikumkuta mtu mwingine yeyote, nikaona nikisema niende kuwaamsha baba na mama, dada wa watu anaweza kufa bure, nikapiga moyo konde na kuukanyaga mlango ambao ulikuwa ukiwaka moto, ukaangukia ndani.
Sikujali kuhusu moshi mzito uliokuwa umetanda kwani tayari nilikuwa na uzoefu wa kucheza kwenye moshi kwani kule kijijini ilikuwa kama tunataka kwenda kupakua asali kwenye mzinga, lazima tuwashe moto kwa kutumia miti inayotoa moshi mzito. Nilibana pumzi, nikaenda mpaka pale kitandani ambapo nilimkuta akiwa ameanza kuishiwa pumzi kutokana na kuvuta moshi mwingi.
Kwa kuwa mwili wangu ulikuwa na nguvu, si unajua tena maisha ya kijijini yanakufanya uwe ‘ngangari’ kutokana na kazi ngumu, nilimbeba na kutoka naye mpaka koridoni, moto ukawa unazidi kuwaka lakini kilichonishangaza sana ni kwamba haukuwa ukisambaa kwenye vyumba vingine.
Nikiwa koridoni, mikononi nikiwa nimembeba yule dada ambaye alishapoteza fahamu, nilikutana na baba na mwenyeji wake pamoja na mama na mwenyeji wake.
“Kuna nini tena? Rahma kapatwa na nini?” aliuliza baba yake, ni hapo ndipo nilipojua kwamba kumbe jina lake anaitwa Rahma. Sikuweza kuwajibu kwa sababu walikuwa wanamuona hali aliyokuwa nayo, baba yake na baba wakanipokea na kumkimbiza mpaka sebuleni, feni zote zikawashwa.
“Kumetokea nini?”
“Moto.”
“Motoo?”
“Ndiyo, chumbani kwake kunawaka moto,” nilisema huku nikishangaa kwa nini walikuwa wakiniuliza mara mbilimbili jambo ambalo lilikuwa wazi. Harakaharaka walielekea kule chumbani wakati mama yake akihangaika kumpa huduma ya kwanza lakini muda mfupi baadaye, walirudi mbiombio.
“Umesema chumbani kwake kunawaka moto?”
“Ndiyo, alikuwa anapiga kelele za kuomba msaada ndiyo nikaamka na kwenda kumsaidia, nilisema, nikaona baba na mwenyeji wake wakitazamana, sikuelewa walikuwa wanamaanisha nini. Ilibidi haraka nirudi kule chumbani kwake ili kuangalia moto umefikia wapi.
Cha ajabu, mpaka nafika mlangoni hakukuwa na moto wala dalili za moto isipokuwa mlango ulikuwa umevunjwa na nakumbuka vizuri mimi ndiye niliyeukanyaga kwa nguvu ukavunjika.
Huku nikiwa nimepigwa na butwaa, niliingia ndani ambako muda mfupi uliopita moto mkubwa ulikuwa umetanda kila sehemu lakini cha ajabu kila kitu kilikuwa sehemu yake, nikageuka huku nikiwa siamini, nikakutana na baba na mwenyeji wake ambao kumbe walikuwa nyuma yangu wakinitazama.
“Ulimaanisha chumba hiki au kingine?”
“Hikihiki, nashangaa sijui imekuwaje, kwani nyie hamjasikia kelele za kuomba msaada?”
“Mimi nimesikia kelele za mlango kuvunjwa tu, basi.”
“Mungu wangu,” nilisema kwa hofu kubwa, nikijihisi kama nipo kwenye ndoto ya kutisha.
“Na vipi kuhusu hii?” baba aliniuliza, huku akinionyeshea nguo yangu ya ndani iliyokuwa pale chini ya kitanda cha Rahma. Kumbe wakati muda ule navaa nguo zangu, niliisahau si unajua tena maisha ya kijijini kuvaa hiyo kitu hasa kwa sisi wanaume siyo kitu cha lazima sana? Aibu ya mwaka ilikuwa imenifika.
“Eti kumetokea nini kwani?” sauti ya mama yake Rahma ilisikika, akiwa ameongozana na binti yake ambaye sasa fahamu zilikuwa zimemrudia, wakiwa pamoja na mama. Nilishindwa hata cha kujibu, mate yakanikauka ghafla mdomoni.

Je, nini kitafuatia? Usikose Jumatatu kwenye Gazeti la Championi Jumatatu.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...