Monday, August 7, 2017

The Graves of The Innocent (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 15


ILIPOISHIA:
“ETI kumetokea nini kwani?” sauti ya mama yake Rahma ilisikika, akiwa ameongozana na binti yake ambaye sasa fahamu zilikuwa zimemrudia, wakiwa pamoja na mama. Nilishindwa hata cha kujibu, mate yakanikauka ghafla mdomoni.
SASA ENDELEA…
“ETI Rahma, nini kimetokea?” “Nilikuwa nimelala, ghafla nikaanza kuhisi kama naungua hivi, sijui tena kilichotokea mpaka nilipokuja kuzinduka kule sebuleni,” alisema na kunifanya nimtazame kwa macho ya mshangao.
Ni yeye pekee ndiye ageweza kuthibitisha kilichotokea lakini kwa maelezo yale, japo alizungumzia kidogo kuhusu kuhisi anaungua, bado yasingetosha kumfanya mtu aamini nilichokuwa nakizungumza. “Na hii nguo imefikaje huku?”
“Niliposhtuka usingizini, sikuwa nimevaa nguo kwa hiyo katika zile purukushani za kuwahi kuja kumuokoa dada nikasahau kuivaa na nadhani ilikuwa kwenye nguo zangu ndiyo maana ikaja kuangukia humu ndani,” nilisema.
 Sijui nilipata wapi akili za kutunga uongo mkubwa kiasi hicho. Baba alinitazama usoni, nikakwepesha macho yangu kwa sababu baba alikuwa na uwezo wa kumgundua mtu anayezungumza uongo kwa kumtazama na kwa sababu sikuwa na kawaida ya kudanganya, nilijua anaweza kunigundua kwa haraka.
Namshukuru Mungu uongo wangu ulipita, baba akaisukumia ile nguo kwangu kwa kutumia mguu wake wa kushoto. Niliinama haraka na kuiokota, nikaisunda mfukoni, kiukweli nilijisikia aibu sana kwa sababu mama alikuwepo, mama yake Rahma alikuwepo na hata Rahma mwenyewe.

Licha ya kulimaliza hilo la kwanza kwa kuongea uongo, bado mjadala mkubwa ulibaki kwenye ishu ya mimi kusema chumba cha Rahma kilikuwa kikiwaka moto huku kukiwa hakuna dalili zozote za moto. Niliwaona baba na baba yake Rahma wakinong’onezana jambo, kisha baba yake Rahma akamnong’oneza mkewe, baba akanishika mkono na kunitoa nje, baba Rahman naye akafuatia, kwa lugha nyepesi wanaume tukatoka na kuwaacha mama Rahma, mwanaye na mama.
Tulienda mpaka nje kabisa, tukakaa kibarazani mimi nikiwa katikati, baba akanigusa begani na kunipigapiga. “Hebu sema ukweli, nini kilichotokea mpaka ukaenda kuvunja mlango na kumtoa dada yako mzobemzobe.” “Moto ulikuwa unawake, tena moto mkubwa kwelikweli.”
“Lakini wewe si unafahamu kwamba moto ukiwaka lazima uache ishara yoyote na unavyosema kwamba ulikuwa ni moto mkubwa, inawezekanaji muda huohuo sisi tuende chumbani na tusikute moto wala dalili zozote za moto?” “Aaah… eeh hata mimi ndiyo nasha…ngaa,” nilisema kwa kubabaika, maji yalikuwa yamenifika shingoni na hata sijui ningetumia lugha gani ili nieleweke.” “Umeanza kuvuta bangi kama kaka zako?” baba aliniuliza swali ambalo lilinifedhehesha sana.
Sikuwahi kutumia kilevi cha aina yoyote tofauti na kaka zangu ambao kule kijijini walikuwa na tabia ya kutembea na vijana wahuni wa kijiji ambao ilikuwa inaaminika kwamba wanavuta bangi ndiyo maana walikuwa na uwezo wa kulima mashamba makubwa bila kuchoka au kufanya kazi ngumu za migodini kwa muda mrefu. Nilitingisha kichwa kukataa, akaniambia kwamba ananiamini sana ndiyo maana ananipa upendeleo kuliko mtu yeyote kwenye familia yetu, akanitaka nisimuangushe na kama nina tatizo lolote nimwambie kuliko kumficha. Baba yake Rahma naye aliongeza kwamba wananiamini na kuna kazi kubwa mbele yetu ambayo walishakubaliana kwamba watashirikiana na mimi kwa hiyo lazima niwe makini sana.
“Haya nenda kalale,” alisema baba, nikainuka kinyonge na kuanza kutembea kuelekea ndani, huku nikijisikia vibaya sana kwa sababu niliamini nilichokifanya ilikuwa ni kwa nia njema kabisa lakini kibao kilinigeukia, nikaonekana eti mimi ni mvuta bangi! Nilijisikia vibaya sana kiukweli.
Nilipitiliza moja kwa moja mpaka chumbani, nikaingia na kujitupa kitandani na kuanza kutafakari kwa kina juu ya kilichotokea. Mambo yalikuwa yametokea kwa kasi mno, yaani siku moja ilikuwa na matukio chungu nzima, yaani kama ingekuwa ni filamu, basi nina hakika ingependwa sana.
Kutokana na uchovu wa safari na matukio yote yaliyotokea kutwa nzima, kuanzia alfajiri tulipoianza safari ya kutoka Makongorosi mpaka muda huo, tukiwa tayari ndani ya Jiji la Dar es Salaam, nilipitiwa tena usingizi mzito. Safari hii sikushtuka mpaka asubuhi na kilichoniamsha zilikuwa ni kelele za mafundi waliokuwa wakitengeneza mlango wa chumba cha Rahma.
Nikaamka na kukaa kitandani, kumbukumbu za matukio yaliyotokea jana yake zikaanza kurudi kichwani mwangu, ndugu yangu niliyelala naye alishaamka muda mrefu tu na hakuwepo chumbani kwa hiyo nilikuwa peke yangu.
“Kaka Togo! Kaka Togo,” sauti ya kike ilisikika nje ya mlango wa chumba kile, kabla sijajua cha kufanya mlango ulifunguliwa, nikakutana na sura nzuri ya Rahma, tabasamu pana likiwa limechanua usoni mwake. Aligeuka nyuma kama anayetazama kama kuna mtu anayemuangalia kisha nikamuona akiingia na kufunga mlango kwa ndani.
“Nimekuja kukuita tukanywe chai lakini pia nimekuletea zawadi,” alisema huku akinipa ‘apple’ la rangi ya kijani. Niliachia tabasamu na kulipokea, nikaanza kulila kuchangamsha mdomo kwani tangu nimeamka hata mswaki sikuwa nimepiga. Alikuja na kukaa pembeni yangu pale juu ya kitanda, akawa ananitazama kwa macho yake mazuri wakati nikilila lile tunda alilonipa.
“Samahani, eti kwani jana usiku kulitokea nini? Naomba nisamehe kama nimekusababishia matatizo.”
“Aah, kawaida tu wala usijali.” nilimjibu kwa mkato, sikutaka kujadiliana naye sana kuhusu kilichotokea, akaendelea kuniuliza maswali lakini nikawa namkatisha, nikamwambia tutazungumza vizuri kuhusu suala hilo muda muafaka ukifika.
“Samahani kama nimekuudhi,” alisema huku akiinuka na kunibusu kwenye shavu langu kisha akanikumbatia na kunibusu tena. “Usijali kabisa, wala hujaniudhi,” nilisema huku mapigo ya moyo wangu yakianza kwenda mrama.
Nikiri wazi kwamba Rahma alikuwa mzuri sana, kitendo cha kunikumbatia, kumbukumbu za tulichokifanya jana yake zilianza kujirudia ndani ya kichwa changu. Na mimi nilimkumbatia na kushika kiuno chake, nikamuona akijinyonganyonga huku akinitazama kwa macho kama vile bado alikuwa na usingizi. Hamasa niliyokuwa naipata, ilinifanya nisiogope chochote, nikaamua kuyavulia tena maji nguo, tayari kwa kuyaoga.
Muda mfupi baadaye, tulikuwa msambweni na Rahma lakini safari hii tulikuwa tukijizuia kutoa aina yoyote ya kelele kwani tulikuwa tunajua kwamba watu wote wameshaamka. Yaani ndani ya muda mfupi tu, Rahma alishaingia ndani ya moyo wangu na kunifanya nimpende sana na kuwa tayari kwa chochote.
Tuliendelea kupigiana pasi fupifupi, wakati mwingine Rahma akawa anashindwa kujizuia na kutoa miguno ya hapa na pale, tukiwa tunaendelea, tulishtuka baada ya kusikia minong’ono dirishani kwa upande wa nje. Kwa ilivyoonyesha, kuna watu walikuwa wakifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea.

“Togo,” nilisikia sauti nzito ya baba ikiniita, harakaharaka nikamtoa Rahma, kila mmoja akawa anahaha kujiweza vizuri. “Togooo,” alirudia kuniita, mapigo ya moyo yakawa yananienda mbio mno huku mdomo ukiwa mzito kufunguka. Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...