Monday, August 21, 2017

The Graves of The Innocent (makaburi ya Wasio na Hatia)- 26




ILIPOISHIA:
Nilipomtazama, macho yangu na yake yaligongana, akanikazia macho, ikabidi nikwepeshe macho yangu, safari ya kurudi nyumbani ikaanza huku mara kwa mara baba akichomoza kichwa na kunitazama, jambo ambalo sikulifurahia.
SASA ENDELEA...
Bado nilikuwa na maswali mengi kuhusu huyu msichana, sikuwa najua ndani ya ile bahasha kuna nini na kwa sababu gani anaonekana kunijali kiasi hicho. Baada ya dakika kadhaa, tukawa tumeshawasili nyumbani.
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.
“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
Magari yaliposimama tu, baba alishuka haraka na kunifuata, kabla hata dereva hajanisaidia kufungua mkanda, baba alifika na kunitazama kwa macho ya ukali, safari hii nikaona kama ananionea, na mimi nikamkazia macho, tukawa tunatazamana kama majogoo yanayotaka kupigana, huku nikiificha ile bahasha asiione maana angeweza kunipokonya kama alivyofanya kwenye simu.

“Kwa nini unakuwa huelewi unapoonywa jambo? Unataka mpaka nini kitokee ndiyo ujue kwamba yule msichana ni mtu hatari kwako na kwetu sisi sote?”
“Sasa baba, unajua mimi kuna mambo mengi sana sielewi, halafu nikikuuliza hata hunipi majibu ya kuridhisha.”
“Hilo siyo jibu, umeanza kuwa na kiburi,” alisema baba kwa sauti ya chini lakini akionesha kama alikuwa amepania kuniadhibu. Sikumjibu chochote, akauma meno kwa hasira na kuelekea pale alipokuwa amesimama baba yake rahma, wakawa wanazungumza jambo. Nadhani walikuwa wananijadili.
Kiukweli, uhusiano wangu na baba ulikuwa umeingia doa kubwa na sababu ya yote, ni mambo ya ajabu yaliyokuwa yakinitokea ambayo yeye alionesha kwamba anajua kila kitu na pengine ndiyo chanzo cha yote. Bado nilikuwa na maswali mengi ambayo alipaswa kunijibu.
Swali la kwanza, nilitaka aniambie kwa nini wanakijiji wenzake kule kijijini kwetu, Chunya walikuwa wakimtuhumu kwamba ni mchawi na ndiye aliyeshiriki kwenye vifo vya watu wawili katika mazingira ya kutatanisha. Kwa macho yangu nilishuhudia akipambana na watu hao kabla ya baadaye kubainika kwamba wamekufa vifo vya ghafla.
Nilitaka aniambie ukweli, yeye ni mganga kama mwenyewe alivyokuwa akijinadi au alikuwa ni mchawi? Nilitaka pia anieleze, aliwezaje kusafiri kutoka Chunya mpaka Dar es Salaam bila kuwemo kwenye basi tulilokuwa tumepanda lakini muda wote akawa anatoke apale panapotokea tatizo, kama alivyotusaidia kuepukana na ajali mbaya zilizotaka kutokea wakati tukisafiri kutoka Chunya kuja Dar, ya kwanza ikiwa ni kwenye eneo hatari la Mlima Nyoka na la pili likiwa ni kwenye Mlima Kitonga.
Nilitaka anieleze vizuri aliwezaje kuniokoa nisigongwe na gari, lakini wakati huohuo watu wengine wote wakawa hawamuoni wala kumsikia zaidi yangu. Nilitaka aniambie, ile dawa aliyonipa niwe namnyunyizia dereva, ilikuwa na maana gani na iliwezaje kutuepusha na ajali?
“Nataka kujua nini kimetokea hapa kwa akina Rahma maana nasikia kabla sisi hatujafika walikuwa wakiishi kwa amani, mbona tangu tuingie, japo ni muda mfupi tu lakini tayari kuna mambo mengi ya ajabu yametokea? Kwa nini naona mambo ambayo watu wengine hawayaoni?”
“Mbona unaongea peke yako Togo?” sauti ya Rahma ndiyo iliyonizindua kutoka kwenye dimbwi la mawazo machungu, nikashtuka sana kugundua kwamba kumbe nilikuwa nikizungumza kwa sauti huku mwenyewe nikidhani nawaza.
“Umesikia nini kwani?” nilimuuliza huku mapigo ya moyo wangu yakinienda mbio sana. Kwa bahati nzuri, kumbe sikuwa nimetamka kwa sauti mambo mengi zaidi ya kujiuliza kwa nini tangu tufike nyumbani kwa akina Rahma mambo mengi ya ajabu yalikuwa yakitokea.
“Kwani unafikiri ujio wenu ndiyo chanzo cha haya yote?” aliniuliza Rahma kwa upole huku akinishika mkono na kunielekeza tuelekee ndani maana nilikuwa nimesimama, nikiwa nimepoteza kabisa mwelekeo.
“Sisi ndiyo chanzo na pengine mimi ndiyo chanzo hasa,” nilisema kwa sauti ya unyonge, Rahma akaniambia kuna jambo zuri anataka tukazungumze chumbani kwake. Nilimkubalia, tulipoingia ndani tulipitiliza mpaka chumbani kwake.
Akina mama ilibidi waanze kuchakarika kwa sababu hata chakula cha usiku hakikuwa kimepikwa siku hiyo kwa sababu ya majanga yaliyonitokea ambapo baada ya kupata taarifa kwamba nipo hospitali nikiwa sijitambui, ilibidi nyumba nzima ije kunijulia hali. Waliingia jikoni huku ndugu zangu na wadogo zake Rahma wakikaa sebuleni kutazama runinga.
Baba na baba Rahma, kama kawaida yao wao walibaki nje wakiendelea na mazungumzo yao.
“Unataka kuniambia nini Rahma,” nilimuuliza kwa upole baada ya kumuona akifunga mlango wa chumbani kwake kwa komeo. Hakujibu kitu zaidi ya kuvua blauzi yake kisha ‘bra’, akanisogelea na kunikumbatia kwa nguvu.
Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, nilijikuta nikisisimka mno. Rahma alikuwa amejaliwa kifua kizuri mno, ambacho kwa mwanaume yeyote aliyekamilika, ilikuwa ni lazima atokwe na udenda kama fisi aliyeona mfupa.
Rahma aliendelea kunikumbatia huku akinibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu kimahaba, hali ambayo ilinichanganya kabisa kichwa changu. Taratibu alinirudisha nyuma mpaka tulipofika kwenye uwanja wa fundi seremala, akanisukumia juu yake kisha akamalizia na za chini zilizokuwa zimesalia.
Akionesha kuwa na papara za hali ya juu, alihamia kwangu na kuitoa ya juu, nikabaki kifua wazi, akahamia na ile ya chini na muda mfupi baadaye, tulikuwa ‘saresare’ maua. Bado mwili wangu haukuwa na nguvu kwa hiyo nilimuachia yeye ndiye awe ‘dairekta’ wa filamu ile ya kusisimua na kweli alikitendea haki cheo nilichompa.
Itaendelea...
Kwa ufanisi wa hali ya juu, Rahma aliitii kiu yangu, mpaka anashuka kutoka juu ya mnazi, alikuwa ameshaangua madafu kadhaa, akajitupa upande wa pili huku akinishukuru, na mimi nikawa namshukuru. Hatukuchukua raundi, kila mmoja akapitiwa na usingizi mzito.
Nadhani wangu ulikuwa mzito zaidi kwa sababu kuichwa changu kilikuwa kimebeba mambo mazito mno na alichonipa rahma ilikuwa sawa na dawa ya usingizi. Tulikuja kushtuka baadaye baada ya kusikia mlango wa chumba cha Rahma ukigongwa. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikamuamsha Rahma ambaye aliamka kichovu na kusogea karibu na mlango.
Safari hii hatukuwa na hofu tena kwani tulikuwa na ruhusa ya kukaa pamoja karibu, mimi kazi yangu ikiwa ni kuhakikisha rahma harudii tena kujaribu kuyakatisha maisha yake na Rahma kuhakikisha ananisaidia mimi mgonjwa.
“Unasemaje?”
‘mama anauliza kama mtakula na sisi au mletewe chakula chenu huku.”
‘Ngoja nakuja mwenyewe,” alijibu Rahma wakati akizungumza na mdogo wake aliyetumwa na mama yao kuwaulizia.
‘Eti mpenzi wangu, we unapenda tukakae sebuleni au tulie hukuhuku chumbani.”
‘Utakavbyosema wewe hamna shida ila napenda zaidi tukikaa peke yetu,” nilimjibu, akanitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yameelemewa na usingizi kisha akaachia tabasamu la kichovu.
“Ngoja nikaonge kwanza,” alisema na kuchukua kitenge, akaelekea bafuni na muda mfupi baadaye, alirudi akiwa amechangamka kidogo. Ilibidi na mimi niende kuoga wakati yeye akihangaikia chakula.
Niliporudi kutoka bafuni, tayari rahma alikuwa ameleta chakula kizuri kule chumbani. Tofauti ya vyakula tulivyozoea kula kijijini na mjini ilikuwa kubwa mno. Chakula kilipikwa vizuri, yaani kwa kukitazama tu ilikuwa ni lazima mate yakutoke. Tulinawa vizuri lakini nilipotaka kuanza kula, Rahma alinikatazana na kusema anataka anilishe kidogo.
Yalikuwa ni mambo mageni kabisa, nilizoea kuona watoto wadogo au wagonjwa ambao wako mahtuti ndiyo wanalishwa, lakini eti dume mimi nilishwe? Hata hivyo sikumkatalia. Akaanza kunilisha kwa upole, huku mara kwa mara akinitazama machoni. Sijui nini kilimtokea Rahma lakini alionesha kunipenda sana, tena sana.
Mara kwa mara alikuwa akinibusu na kuniambia kwamba ananipenda sana, mpaka nikawa najisikia aibu. Sikuwa najua kabisa mambo ya kikubwa na wala sikuwa na uelewa wowote wa mahaba. Nilikuwa nikisikiasikia kwamba watu wa pwani ndiyo wataalamu wa hayo mambo.
Japo Rahma alikuwa akinilisha matonge madogo tofauti na niliyozoea lakini kiukweli nikiri kwamba nilijisikia raha ya ajabu ndani ya moyo wangu. Tulipomaliza kula, alitoa vyombo, akaja kufanya usafi kisha akafunga tena mlango.
“Itabidi mimi nikalale chumbani kwangu,” nilimwambia Rahma lakini akakataa katakata, akaniambia tutalala wote humo chumbani kwake na tutajifunika shuka moja. Japokuwa kwa nje nilikuwa navunga, ukweli ni kwamba hata mimi nilikuwa napenda sana kuwa karibu na Rahma hasa kutokana na mapenzi ya dhati aliyokuwa ananionesha.
Ile tofauti ya umri kati yetu sikuiona tena, namimi nikawa najiona mkubwa kama yeye, hata ile harufu ya undugu kati yetu nayo ilitoweka kabisa, ndani ya muda mfupi tu tuliokaa pamoja ikawa utafikiri tumeishi pamoja kwa miaka mingi tangu zamani.
 Tulipiga stori za hapa na pale, baadaye muda wa kulala ulipofika, kama ilivyokuwa mara ya kwanza, Rahma aliniganda kama ruba, tukapeana tende na halua kwa mara nyingine kabla ya kupitiwa na usingizi mzito, akiwa ameniganda kifuani kama ruba.
Nilikuja kuzinduka usiku wa manane baada ya kuhisi hali isiyo ya kawaida. Kilichoniamsha, zilikuwa ni kelele za paka waliokuwa wakipigana juu ya paa, huku wakitoa milio ya ajabu kama watoto wachanga.
Sikutaka kumuamsha Rahma, nilimtoa kifuani kwangu taratibu kisha nikashusha miguu chini, nikawa nimekaa huku nikitazama huku na kule. Sikuweza kuona chochote kutokana na giza lililokuwa limetanda usiku huo. Mara nikasikia kishindo kizito kama cha kitu kilichodondoka kutoka darini mpaka sakafuni, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kuliko kawaida.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...