Tuesday, August 8, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 9


ILIPOISHIA:
Sikupata hata muda wa kujibu chochote, Raya akanikumbatia kwa nguvu mwilini na kuanza kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu, japokuwa sikuwa tayari kwa alichokuwa anakitaka, nilijikuta kwenye wakati mgumu mno, kwani ukichanganya joto la mwili wake na uzuri aliokuwa nao, ukizingatia kwamba tulikuwa wawili tu, nilijikuta nikishindwa cha kuamua, ‘Jamal’ wangu naye akaanza usumbufu.
SASA ENDELEA…
Nilishindwa kujizuia, na mimi nikamkumbatia Raya, kitendo ambacho kilimfurahisha mno, akausogeza mdomo wake kwangu, nami nikafanya hovyohivyo, ndimi zetu zikagusana, nikamsikia akitoa migumo ambayo ilizidi kuipagawisha akili yangu.
Japokuwa sikuwa mtaalamu sana kwenye mambo ya kikubwa, nilijitahidi kadiri ya uwezo wangu kumuonesha Raya kwamba na mimi sikuwa mshamba, ‘amsha-amsha’ ziliendelea na hatimaye kipyenga kikalia kuashiria kuanza kwa mpambano wa kukata na shoka, usio na refa wala jezi, huku nikishindwa kuzidhibiti papara zangu.
Wakati nikijiandaa kusakata kabumbu, ghafla mawazo juu ya Shenaiza na kilichokuwa kinaendelea kule nyumbani kwangu yalipita kwa kasi kubwa ndani ya kichwa changu, nikashangaa ‘Jamal’ wangu ambaye muda mfupi uliopita alikuwa ngangari ile kinoma, akianza kunywea na kupoteza kabisa ukakamavu wake.

Raya ambaye tayari alishajiweka tayari kupokea ‘mashuti’ ya nguvu kutoka kwangu, alishtushwa na kilichotokea, akaacha kila alichokuwa anakifanya.
“Vipi tena jaman mpenzi wangu, na..ta…ka…,” alisema Raya kwa sauti iliyokuwa ikikatakata, ikitokea kwenye matundu ya pua zake.
“Subiri kidogo,” nilisema kwa aibu kubwa, sikuwahi kutokewa na hali kama hiyo hata mara moja, nikashangaa imekuwaje? Sikupata jibu. Ili kuzuga, ilibidi niamke na kujifanya nataka kwenda maliwatoni, nikamuacha Raya amelala palepale huku akiwa kimya kabisa, akionesha kuugulia maumivu ya ndani kwa ndani.
Harakaharaka nilitoka na kuelekea choo cha ndani, nikajifungia mlango na kuanza kutafakari kuhusu kilichotokea. Nilijisikia aibu sana kwani sikujua Raya atanichukuliaje kama amenitafunia kila kitu na kuniwekea kabisa mdomoni lakini nimeshindwa kumeza. Japokuwa ulikuwa ni usiku sana na kulikuwa na baridi, nilifungulia maji ya bomba la mvua na kuanza kujimwagia. Nilisimama huku maji yakiendelea kunimwagikia kwa zaidi ya dakika tatu mpaka nikaanza kutetemeka kwa baridi.
Nikafunga bomba na kurudi chumbani ambako nilimkuta Raya amelala vilevile kama nilivyomuacha. Nikawa najisemeshasemesha ili ‘kuua soo’, nikajifuta maji na kupanda kitandani, nikamvutia Raya kifuani kwangu ambapo alikuja mzimamzima, ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe alikuwa akilia.
Lawama zake kubwa kwangu ni kwamba sikuwa nikimpenda na ndiyo maana nilimfanyia hivyo lakini kiukweli, wala sikuwa nimepanga hayo yatokee bali nilijikuta tu nikiishiwa ukakamavu.
Nikawa nambembeleza kwa maneno matamu na kwa mara ya kwanza nikamtamkia kwamba nampenda sana japokuwa nilisema vile ili kumtuliza. Alifurahi sana aliposikia maneno hayo kutoka kwangu, nikamuona akitabasamu na kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu, na mimi nikawa naonesha ushirikiano.
Niliamini safari hii nitaweza kukata kiu yake kwani ‘Jamal’ wangu naye alishaanza kuonesha ushirikiano, akawa anafura kwa hasira na kunipa matumaini makubwa kwamba nitaifuta aibu kubwa iliyokuwa inataka kunikabili.
Tuliendelea kufanya ‘warm-up’ kwa dakika kadhaa lakini safari hii Raya alionesha kutotaka kuchelewesha tena mambo, kabla hata kipyenga cha kuashiria kuanza kwa mpambano hakijalia, yeye alitaka kujianzishia mpira mwenyewe.
Katika hali ambayo sikuitegemea, mawazo juu ya Shenaiza yalijirudia tena akili mwangu, nikawa sijui nini kilichoendelea baada ya mimi kuondoka, kama ilivyokuwa mwanzo, ‘Jamal’ wangu akanywea, jambo lililomkasirisha sana Raya, safari hii akawa analia kwa sauti kama mtu aliyepokea taarifa za msiba.
“Kwa nini unanitesa hivi Jamal? Kwani mimi nina kasoro gani mpaka unifanyie hivi?” alisema huku akilia, nikaanza upya kazi ya kumbembeleza huku nikijisikia aibu kubwa ndani ya moyo wangu. Haikuwa kazi nyepesi kumtuliza Raya mpaka atulie, nikawa najaribu kujikakamua na kumfosi ‘Jamal’ wangu arudi tena mchezoni lakini ilikuwa sawa na kazi bure.
Mpaka kunapambazuka, hakuna kilichofanyika zaidi ya kubembelezana, saa kumi na moja alfajiri, wote tulipitiwa na usingizi mzito na tulipokuja kuzinduka, tayari ilikuwa ni saa moja za asubuhi. Mimi ndiye niliyekuwa wa kwanza kuzinduka, nikajaribu kujikakamua tena kuona kama angalau naweza kufanya chochote lakini ilikuwa sawa na kazi bure, Jamal wangu alikuwa amelala doro, jambo lililonifadhaisha sana.
Muda mfupi baadaye Raya naye aliamka, macho yake yakiwa yamevimba na kuwa mekundu kutokana na kulia sana, akaenda chumbani kwake na kuniacha nikijiandaa. Baada ya kumaliza kujiandaa, nilitoka hadi sebuleni ambako nilimkuta Raya akiandaa kifungua kinywa.
Ule uchangamfu aliokuwa nao kwangu uliyeyuka kama theluji iyeyukavyo juani. Nilitamani sana ajue kwamba sikuwa nimemfanyia makusudi bali lilikuwa ni jambo ambalo lipo nje ya uwezo wangu lakini haikuwezekana, alichoamini Raya ni kwamba sikuwa nampenda na nilifanya vile kumkomoa.
Tulipata kifungua kinywa kimyakimya, kwa kuwa sikuwa najua kilichotokea nyumbani kwangu usiku ule, sikuwa na muda wa kuendelea kukaa pale, nilimuaga Raya na kumwambia tutakutana kazini baadaye lakini cha ajabu, alikataa katakata kuniacha niondoke peke yangu, akaniambia atanisindikiza na kama ni kuomba ruhusa kazini, niombe ya watu wawili, mimi na yeye.
Ulikuwa ni mtihani mkubwa sana kwangu kwa sababu kwa kilichotokea kati yangu na yeye, nilihitaji kupata muda wa kukaa peke yangu na kutafakari kwa kina kilichosababisha hali ile iliyonitokea usiku.
Lakini kubwa zaidi, sikutaka kumuingiza kwenye matatizo yangu na Shenaiza, kwa kuwa nilikuwa nimeyaanza mwenyewe, nilitaka nikayamalize mwenyewe. Hata hivyo, sikutaka pia kuendelea kumuudhi, ikabidi nimkubalie ambapo tulitoka na safari ya kuelekea nyumbani kwangu ikaanza.
Tukiwa njiani nilimpigia simu bosi kazini na kumueleza kwamba nilikuwa nimepatwa na matatizo makubwa na kwamba nitachelewa kufika kazini. Sikutaka kumfafanulia kilichotokea, kwa bahati nzuri alinielewa. Nilimpigia pia simu Justice na kumtaka asizungumze chochote kazini kuhusu nilichomwambia jana yake.
“Sasa mbona umeomba ruhusa peke yako? Kwa nini usiniombee na mimi kama tulivyokubaliana?” Raya aliniuliza kwa sauti ya chini, iliyoonesha dhahiri kwamba hakuwa na furaha, Nilishindwa cha kumjibu zaidi ya kumtaka apige mwenyewe simu na kuomba ruhusa kivyake ili tusije kuonekana kwamba tumepanga kutega kazi kwa makusudi.
Kwa bahati nzuri naye alikubaliwa, tukaendelea na safari ya kuelekea kwangu kwa kutumia Bajaj ambayo Raya ndiye aliyelipa, kadiri tulivyokuwa tunazidi kukaribia kwangu ndivyo mapigo ya moyo wangu yalivyokuwa yanazidi kuongezeka, sikujua nitakutana na nini.
Nilimuelekeza dereva njia ya kupita kwani sikutaka kutokezea upande wa mbele wa mtaa niliokuwa naishi, nilitaka tutokezee uchochoroni kwa sababu za kiusalama, kweli dereva yule alinielewa na safari iliendelea. Hatimaye tukafika kwangu, tukashuka kwenye Bajaj na kumwambia yeye aondoke zake, tukaanza kupita kwenye uchochoro unaotokezea kwangu.
Tulipokaribia kufika, huku mapigo ya moyo wangu yakizidi kupiga kiasi cha kunifanya nitokwe na kijasho chembamba japokuwa bado ilikuwa ni asubuhi na kulikuwa na kibaridi, nilishtuka zaidi baada ya kuona umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika mbele ya nyumba niliyokuwa naishi.
“Mungu wangu,” nilisema huku nikifikicha macho na kutazama vizuri, kuna muda nilikuwa nahisi kwamba huenda nipo ndotoni lakini haikuwa hivyo, sikuelewa pale kwangu kuna kilichosababisha watu wajae kiasi kile.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Nifollow kwenye mitandao ya kijamii kwa:
Facebook: Hash Power
Instagram: Hashpower7113
Twitter: Hash- Power.

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...