Wednesday, August 16, 2017

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 15


ILIPOISHIA:
“Aisee! Mbona hii inaonekana kuwa ngoma nzito?”
“Ni ngoma nzito kwelikweli, halafu kuna huyu kijana ameingizwa kwenye mtego bila mwenyewe kujua chochote, mpaka namuonea huruma.”
SASA ENDELEA…
“Kwa akili zako unafikiri huyu kijana atakuwa ameingia kwenye mtego mwenyewe akiwa hajui chochote?”
“Hajui chochote, hata maelezo aliyokuwa anayatoa, yanaonesha kabisa hakuna anachokijua.”
“Unafikiri inawezekana mtu akaingizwa kwenye kumi na nane za Loris kama hana umuhimu? Hata kama mwenyewe hajui naamini lazima kuna jambo ambalo limefanya aingizwe kwenye huu mtego.”
“Lakini hajaingizwa na Loris mwenyewe isipokuwa binti yake.”
“Nani ambaye hajui kwamba Loris amekuwa akimtumia mwanaye kwenye kazi zake, hasa pale anapoona mambo yameanza kuwa magumu kwake?”
“Yote yanawezekana lakini taarifa za ndani zinaonesha kwamba huyu binti mwenyewe ameshachoka kumtumikia baba yake na ndiyo maana unaona anaandamwa na matatizo makubwa!”
“Unataka kusema ndiyo maana anatishiwa kuuawa?”
“Inawezekana kabisa, nahisi kuna jambo kubwa analolifahamu lakini hataki kueleza ukweli kwa sababu hata ukifuatilia maelezo aliyokuwa anayatoa, anazungumza vitu nusunusu sana.”
“Mh! Kweli hii ngoma nzito! Kwa hiyo tunafanyaje?”
“Inabidi tuwasiliane kwanza na mkuu, si unajua mtandao wa Loris unahusisha mpaka viongozi wetu?”
***
Raya alishika taulo nililokuwa nimejifunga na kulivuta kisha akalitundika pale alipoweka khanga yake, tukabaki saresare maua! Akanisogelea jirani kabisa kiasi cha kila mmoja kuanza kuzisikia pumzi za mwenzake, tukawa tunatazamana machoni huku ‘Jamal’ wangu naye akianza kufura kwa hasira.

“Quench my thirst dear Jamal! I’m in deep love with you, take me and let me feel like a real woman!” (Nikate kiu yangu mpenzi wangu Jamal! Nipo kwenye penzi lenye kina kirefu na wewe, nichukue na unifanye nijihisi kuwa mwanamke niliyekamilika!) alisema Raya kwa sauti iliyokuwa ikisikika kama ya mtoto mchanga.
Bado sikuwa najua nifanye nini kwa sababu sitaki kusema uongo, ukiachilia mbali ukweli kwamba sikuwa na hisia za kimapenzi dhidi yake, Raya alikuwa ni msichana mzuri sana ambaye mwanaume yeyote aliyekamilika, asingeweza kumuacha, hasa katika mazingira kama yale tuliyokuwepo.
Akionesha kuwa na shauku kubwa, alinikumbatia kwa nguvu na tukagusanisha ndimi zetu, nikahisi kama mwili wangu umepigwa na shoti kali ya umeme.
Kwa kutumia mkono mmoja, alifungua bomba la maji, yakawa yanatumwagikia mithili ya watu waliokumbatiana kwenye mvua kali, hali iliyonizidishia msisimko mkali kwani japo maji yalikuwa ya baridi, joto la mwili wake lilinifanya nijihisi kama nipo kwenye ulimwengu wa tofauti kabisa.
Alifunga bomba na kuchukua sabuni, ingawa tayari nilishakuwa nimeoga, alianza upya kunipaka sabuni mwili mzima, nikazidi kusisimka pale mikono yake laini ilipokuwa ikinipaka sabuni, alipomaliza alitaka na mimi nifanye kama vile. Nikaanza kumpaka sabuni mwili mzima, kusema ukweli hakuna siku ambayo nilisisimka kama siku hiyo.
Baada ya kumaliza, alifungua tena maji, tukaoga huku mara kwa mara tukigusanisha ndimi zetu, tulipomaliza alichukua taulo na kunifuta kwa mahaba mazito kisha akanifunga kiunoni, na yeye akachukua khanga yake moja na kujifunga bila hata kujifuta.
Kwa kuwa mwili wake ulikuwa na maji, khanga ile ilishikana na ngozi ya mwili wake na kulifanya umbo lake lionekane vizuri, hasa maeneo ya kiunoni kwa nyuma ambayo yalikuwa si haba! Kwa makusudi kabisa, akatangulia mbele na kuanza kutembea kwa maringo kuelekea chumbani kwake.
Nilijikuta nikiwa kama kondoo anayepelekwa machinjioni, nikawa namfuata nyumanyuma huku macho yangu yakiwa hayabanduki kwenye mwili wake, nikimeza mate kama fisi aliyeona mfupa. Sikuelewa kilichofuatia zaidi ya kujishtukia tukiwa juu ya kitanda chake kikubwa.
Hata sikukumbuka taulo langu nililivua muda gani, achilia mbali khanga yake, zaidi ya kujikuta wote wawili tukiwa kama tulivyoletwa duniani, hakukuwa na mazungumzo tena, kilichosikika kilikuwa ni miguno ya hapa na pale wakati joto la huba likizidi kupanda kwenye mtima wa kila mmoja.
Dakika kadhaa baadaye, kila mmoja alikuwa tayari kwa pambano la kirafiki lisilo na jezi wala refa, Raya akionesha kuukamia mchezo kuliko kawaida. Kabla hata kipyenga cha kuashiria mpambano kuanza hakijalia, tayari Raya alishamkamata ‘Jamal’ wangu na kumuelekeza kwenye lango la kuingilia ngome kuu, nami nikawa mtiifu kwa kila alichokuwa anakifanya Raya.
Tofauti kabisa na nilichokuwa nimekitegemea, ‘Jamal’ wangu alikutana na ukuta mgumu wa ngome hiyo, ikabidi nimuongezee nguvu ya kusonga mbele, nikamuona Raya akiuma meno na kufumba macho yake, zoezi lililosindikizwa na miguno ambayo sikuelewa kama ilikuwa ya raha au maumivu.
Miguno ile iliniongezea hamasa, huruma zikaniishia kabisa, nikaongeza nguvu na muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa tukielea kwenye ulimwengu mwingine tofauti kabisa, ambao kwa Raya ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kuufikia. Nikiri kwamba kwa mara ya kwanza, nilijikuta nikiijutia nafsi yangu kwa kushindwa kumuelewa Raya mapema na kumpa nafasi ndani ya moyo wangu.
Haikuwa rahisi kwa msichana mrembo kama yeye, kwa umri wake, elimu yake na uwezo wa familia yao, kuwa bado hajaguswa mpaka siku hiyo. Kwangu niliiona ni zaidi ya bahati na nikaendelea kujilaumu kwa kuchelewa kusoma alama za nyakati. Tuliendelea kusakata kabumbu kwa zaidi ya dakika ishirini, Raya akijitutumua kadiri ya uwezo wake ili asionekane mgeni kabisa kwenye sanaa hiyo ya kikubwa.
Mpaka kipyenga kinalia kuashiria kumalizika kwa mpambano huo, dimba lote lilikuwa halitamaniki, ungeweza kufananisha na machinjio ya Vingunguti au ya Pugu.
“Ahsante, ahsante sana Jamal, hatimaye ndoto zangu za muda mrefu zimetimia, umenifanya nijione mwanamke niliyekamilika!” alisema Raya kwa sauti iliyokuwa inasikika kama ya mtoto mchanga, machozi yakiulowanisha uso wake. Akawa ananibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.
Kwa kuwa dimba lilishachafuka, ilibidi turudi tena bafuni, tukarudia tena kuogeshana, safari hii kwa hisia kali kuliko mwanzo kisha tukarudi kwenye chumba cha wageni ambacho kimsingi ndiyo nilichotakiwa kulala. Raya akaniganda kama ruba na hatimaye, tukajikuta tukiingia tena dimbani kwa ngwe ya lala salama. Kipyenga kilipolia kuashria kumalizika kwa dakika tisini, tulipitiwa na usingizi wa pono.
Mimi ndiyo nilikuwa wa kwanza kuzinduka, alfajiri ya siku ya pili ambapo kilichonizindua, ilikuwa ni mlio wa simu yangu iliyokuwa inaita mfululizo. Kwa taabu niliichukua simu na kutazama namba ya mpigaji. Moyo ukanilipuka baada ya kugundua kuwa alikuwa ni Shenaiza.
Nilimtazama Raya aliyekuwa bado amelala juu ya kifua changu, nikajiuliza mara mbilimbili kama nipokee au la. Mpaka simu inakata, sikuwa nimeamua nini cha kufanya, ikaanza tena kuita mfululizo ambapo nililazimika kuipokea, sauti ya Samantha ikasikika upande wa pili, ikinipa taarifa ambazo zilinishtua mno.
“Unasemaaa?” nilijikuta nikiuliza kwa sauti ya juu, iliyomzindua Raya usingizini.
Je, nini kitafuatia? Usikose Jumatatu ijayo kwenye Gazeti la Championi Jumatatu.

2 comments:

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...