Tuesday, December 23, 2014

CHE GUEVARA, MAMBO 10 USIYOYAJUA!


Na Hashim Aziz
Wengi wamezoea kuiona picha yake kama alama ya ukombozi na mapinduzi ya kweli lakini ni wachache wanaomjua vizuri. Jina lake halisi anaitwa Ernesto ‘Che’ Guevara, alizaliwa Juni 14, 1928, Rosario, Argentina na yafuatayo ni mambo kumi kumhusu:
1. Alikuwa mwanaharakati na mwanamapinduzi aliyezisaidia nchi nyingi kupata uhuru kupitia vita vya msituni, zikiwemo Cuba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji na nyingine nyingi.
Ernesto Che Guevara
2. Licha ya kusumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, aliweza kusafiri sehemu mbalimbali, zikiwemo zenye baridi kali na kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kuwasaidia wanyonge.
3. Alisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Buenos Aires alikohitimu na kupata digrii (shahada) ya udaktari wa binadamu.
4. Akiwa bado anasomea udaktari, alifunga safari kwa kutumia pikipiki ambapo alisafiri umbali wa kilometa 4,500 na baadaye kilometa nyingine 8,000 kutembelea nchi mbalimbali za Amerika ya Kusini. Hali ya umaskini na ukandamizaji aliyoikuta huko ndiyo iliyomfanya awe mpiganaji wa msituni.

5. Harakati za kwanza za kimapinduzi zilizompa umaarufu, ni pale alipomsaidia Fidel Castro wa Cuba kumpindua Dikteta Fulgencio Batista wa nchi hiyo kupitia vita vya msituni akiwa mkuu wa jeshi.
6. Amewahi kufika Dar es Salaam mwaka 1966 ambapo alikutana na wapigania uhuru wa Msumbiji, Frelimo na kukubaliana kusaidiana kupigania uhuru wa nchi hiyo.
7. Baadaye aliondoka Afrika na kuelekea Bolivia kuendelea na harakati za kumtoa madarakani kiongozi aliyekuwa akitawala kimabavu nchi hiyo, René Barrientos ambapo aliunda jeshi la porini kwa ajili ya kumpindua lakini ikashindikana.
8. Baada ya kushindwa kwa mapinduzi ya Bolivia, Che Guevara alikamatwa eneo liitwalo Yuro baada ya kuzingirwa na wanajeshi wa Bolivia.
9. Baada ya kukamatwa kwake, aliteswa sana na siku chache baadaye akauawa kwa kupigwa risasi nyingi na mwanajeshi mlevi aitwaye Mario Terán.
10. Kufuatia kifo chake, mataifa mengi duniani yalitangaza siku kadhaa za maombolezo, ikiwemo Cuba ambapo Fidel Castro alitangaza siku tatu za maombolezo.  

2 comments:

  1. aendelee kupumzika kwa amani che guevara
    kamwe hawezi sahaulika mioyoni mwetu.

    ReplyDelete
  2. Kusudi tuliloletewa duniani huwa ni gumu na wengi huwa wanabadilika wanaogopa na wanasahaulika Leo Leo.

    ReplyDelete

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...