Tuesday, December 30, 2014

PATRICK PHIRI ATIMULIWA SIMBA

Timu ya soka ya Simba, imemtimua kazi aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mzambia Patrick Phiri pamoja na msaidizi wake, Suleiman Matola kufuatia matokeo mabovu ambayo timu hiyo imeendelea kuyapata. 


Phiri aliwahi kuwa kocha wa klabu hiyo mnamo mwaka 2003-2005 kabla hajaondoka na kurudi kwao Zambia kuifundisha timu yake ya taifa mnamo 2005-2008 baada ya hapo alirejea tena kuinoa Simba  2008-2011 kabla hajatimuliwa kwa mara nyingine tena. Phiri atakumbukwa kwa mengi sana ikiwemo ya kucheza ligi kuu bila ya kufungwa hata mechi moja rekodi aliyoiweka mwaka 2010-2011.

Kutimuliwa kwa Phiri kunakuja siku chache baada ya kutimuliwa kwa kocha wa Yanga, Mbrazil Marcio Maximo.

LIKE RIHANNA LIKE JOKATE



They are bonded by a common behaviour! They love kids!

Sunday, December 28, 2014

MY REPENTANCE (KUTUBU KWANGU)- 4


ILIPOISHIA:
Kwa kuwa nilikua nimevaa taiti na sidiria tu huku juu nikiwa nimejifunga mtandio mwepesi, umbo langu lilionekana vizuri kabisa, uzalendo ukamshinda Ibrahim, akanitamkia:
“Kumbe umeumbika hivi? Loh, mpenzi wako anafaidi.” Nikacheka sana kwa furaha kwani nilichokuwa nakitaka, kilikuwa kimetimia. Tayari Ibrahim alishaanza kuonesha dalili za kunitaka kimapenzi.
SASA ENDELEA...
Unajua sisi wanawake wengi huwa tunapenda sana kusifiwa, na mtu akishaanza kukusifia, basi ukijirahisisha kwake, lazima mwisho muishie kuwa wapenzi. Baadhi ya wanaume wanaujua udhaifu wetu huu na wamekuwa wakipitia humohumo kukidhi haja za miili yao.
Basi nikazidi kuringa mtoto wa kike, nikamtoa wasiwasi kwamba hakuna mtu yeyote anayenimiliki, nipo ‘singo’.
“Unasema kweli upo singo?”
“Ndiyo, kwa nini huamini?”
“Unajua wanawake wazuri kama wewe mara nyingi huwa hawawezi kuwa singo, tena wengine wanakuwa na mpenzi zaidi ya mmoja.”
“Wala mimi sipo hivyo, wazazi wangu wakali sana na hawapendi kabisa nijihusishe na mambo hayo ndiyo maana nimeamua kuweka nguvu zangu zote kwenye masomo,” nilisema huku nikiyarembua macho yangu mazuri, kauli ambayo ilionesha kumfurahisha sana Ibrahim.
Kwa kuwa sikuwa na nguo nyingine za akiba, ilibidi nivae nguo zangu juu ya zile zilizoloana, tukatoka na Ibrahim na kuanza kutembea kuelekea kwenye gari. Tayari akili za Ibrahim zilishabadilika kabisa kwa sababu hata wakati tukitembea, alikuwa anataka nitangulie mbele kidogo halafu akawa ananitazama kwa nyuma kwa kuibia. Nililijua hilo, nikazidisha vituko.
Basi tulifika kwenye gari, tukaingia na safari ya kurudi nyumbani ikaanza, mazungumzo kati yangu na Ibrahim yalianza kubadilika taratibu, akawa ananiuliza mambo mbalimbali kuhusu maisha yangu kuanzia vitu ninavyovipenda, nisivyovipenda, ratiba yangu ya maisha ya kila siku na mambo mbalimbali kuhusu maisha yangu.

Nilimjibu kila kitu alichotaka kukijua, hatimaye tukafika Morocco. Akasimamisha gari kituoni kisha tukaagana, nilipotaka kushuka, aliniita jina langu, nikageuka na kumtazama.
“Kuna jambo nitakwambia baadaye kwenye simu, tafadhali usikatae,” alisema huku akiwa amevaa uso uliokuwa na ujumbe mzito kwangu, nilitabasamu na kumtoa wasiwasi, nikashuka.

Friday, December 26, 2014

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 3


ILIPOISHIA:
Kama hiyo haitoshi, nilimtumia ujumbe mfupi mzuri wa kumtakia usiku mwema, naye akanijibu ndani ya muda mfupi tu, nikalala na kuukumbatia mto wangu huku joto tamu likiendelea kuzunguka kwenye mwili wangu.
SASA ENDELEA...
Niseme tu wazi kwamba nilishampenda sana Ibrahim tangu nilipomuona kwa mara ya kwanza tu, na sasa nilikuwa tayari kufanya chochote, hata ikibidi kujitongozesha ilimradi awe mpenzi wangu.
Naomba watu wasinielewe vibaya kwa sababu najua kwa mila za Kitanzania, ni vigumu sana mwanamke kueleza hisia zake za kimapenzi, tumezoea kwamba sisi ni watu wa kutongozwa tu.
Wapo wengi tu ambao walikuwa wakiwapenda watu fulani ila kwa sababu ya kukosa ujasiri, wakajikuta wakiolewa na watu ambao wala hawakuwahi kuwafikiria kwenye maisha yao.
Niliamua kujitoa mhanga mtoto wa kike, nikajiapiza kuwa lazima nimpate Ibrahim. Wala kilichonizuzua halikuwa gari lake au kusikia kwamba anafanya kazi benki, walaa! Ni mapenzi ya dhati ndiyo yaliyonisukuma mpaka kupata ujasiri wa namna ile.

Niliendelea kumfikiria Ibrahim mpaka usingizi uliponipitia, kesho yake asubuhi nikawahi kuamka kama kawaida yangu na kujiandaa kwa ajili ya kwenda chuo. Nilipomaliza kuvaa, niliwaaga baba na mama kama ilivyo kawaida yangu kila siku kisha nikatoka na kuanza kutembea kuelekea kituo cha daladala.
Siku hiyo hakukuwa na mvua kama jana yake ingawa kila kona kulikuwa na matope. Kumbukumbu juu ya Ibrahim zikanijia na kujikuta nikitabasamu mwenyewe. Nilitoa simu yangu kwenye mkoba na kutafuta namba yake, nikampigia.

Wednesday, December 24, 2014

A MAN WHO SHOOT OSAMA PROBED FOR RELEASING CLASSIFIED INFORMATION

Credit: ABC News
The Navy is investigating whether a former SEAL who claimed on national television that he shot Osama bin Laden may have revealed classified information about the raid.
In November, Robert O’Neill appeared on Fox News Channel to discuss his role in the raid that killed bin Laden on May 1, 2011 in Abbotabad, Pakistan.
"The Naval Criminal Investigative Service (NCIS) is in receipt of an allegation that Mr. O'Neill may have revealed classified information to persons not authorized to receive such information,” said NCIS Public Affairs Officer Ed Buice in a statement to ABC News. “In response, NCIS has initiated an investigation to determine the merit of the allegations."
Details of the investigation were first reported Tuesday by The Daily Beast.
It is unclear how long the investigation has been underway and who allegedly received the recipients of the classified information he may have provided about the raid.
Robert O'neill
In November, O’Neill appeared on Fox and gave an interview to the Washington Post where he discussed his role in the raid and claimed that he had fired the fatal shots that killed bin Laden. The special operations news website SOFREP.com reported at the time that O’Neill was the SEAL who identified himself as “the Shooter” in a 2013 Esquire magazine article about the raid.

TRIBAL MILITANT ATTACKS KILL AT LEAST 54 IN INDIA

New Delhi (CNN) -- At least 54 people have been killed in a series of attacks by tribal militants in India's remote northeastern state of Assam, a police official said Wednesday.
The attacks involving Bodo militants took place Tuesday, Assam Police Inspector-General S.N. Singh told CNN.
The Bodo fighters, angry about a recent police crackdown that led to several arrests and the seizure of weapons, targeted members of another tribal community, said Khagen Sarma, another local police official.
Bodoland area

POZI ZA MASTAA WA BONGO INSTAGRAM

Ommy Dimpoz

Shetta

Lulu

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 2


ILIPOISHIA:
Naomba umpe namba yangu mwambie anitafute au nipe yake nijue namna ya kumfikishia mzigo wake,” alisema dereva wa ile Carina kwa sauti ya kiungwana mno.
 Nilishusha pumzi ndefu na kuachia tabasamu, nikamwambia kwamba mimi ndiyo Flaviana, nikamsikia akicheka kidogo kisha akaniuliza nipo wapi kwa wakati huo. Nilipomuelekeza, aliniambia nimsubiri hapohapo anakuja.
SASA ENDELEA... 
Kweli baada ya kama dakika tano hivi, ile Carina ilipaki upande wa pili wa barabara, akanipigia simu na kuniuliza kama nilikuwa naliona gari. Nikatoka mbiombio na kukimbia kuvuka barabara. Kwa kuwa bado mvua ilikuwa inanyesha, nilipolifikia gari lake, alinifungulia mlango, nikaingia na kukaa kwenye siti ileile niliyokuwa nimekaa awali, nikamgeukia, na yeye akanitazama, macho yetu yakagongana.

“Pole kwa usumbufu,” aliniambia kwa sauti ya kiungwana, nikaachia tabasamu hafifu huku nikiendelea kujifuta maji ya mvua, nikwamwambia mimi ndiyo napaswa kumpa yeye pole kwani licha ya kunipa lifti bure, nilimpa kazi nyingine ya kunitafuta.
Alinipa begi langu na kuniuliza nilikokuwa nakwenda.
“Naenda chuo, pale jirani na mnara wa askari.”
“Unasomea nini?”
“Nasomea uhasibu.”
“Ooh! Safi sana, mimi pia nilisomea uhasibu pale IFM sasa hivi nafanya kazi benki,” alisema yule dereva huku na yeye akiachia tabasamu, akaniomba kama sitajali anisindikize jirani na chuo ili nisiendelee kulowa.

Nilikubali haraka na kumshukuru sana. Akawasha gari na kwenda mpaka mbele kidogo, akageuza gari na kurudi barabarani, akawa anaendesha gari taratibu huku tukipiga stori za kawaida.
Ndani ya kipindi kifupi tu nilichokaa naye, niligundua kuwa yule kaka alikuwa mtu mmoja mstaarabu sana, asiye na maneno mengi, anayejiheshimu na anayeheshimu watu wengine pia bila kujali umri, jinsia au hali ya kiuchumi.
Alinisogeza mpaka jirani na chuoni kwetu, akalitoa gari barabarani na kupaki pembeni huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Nilitaka kushuka lakini akaniambia nisubiri mvua ipungue kidogo kwani yeye hakuwa na haraka sana kwani ofisi anayofanyia kazi ni jirani na pale.

Tuesday, December 23, 2014

MREMBO APIGWA RISASI, AFARIKI

Habari zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kwamba binti huyu (pichani) ambaye bado jina na mahali anapoishi havijafahamika, amepigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi mchana wa leo, Morocco, nyuma ya makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam. 

Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio, majambazi hao walikuwa wametoka kufanya uhalifu kwenye kibanda kimoja cha M-Pesa kilichopo jirani na eneo hilo, wakati wakiondoka wakawa wanarusha risasi hovyo na moja ikampata mrembo huyu na kuyakatisha maisha yake papo hapo.
mwili wa marehemu baada ya kupigwa risasi

WE WISH YOU MARRY X-MAS

HASH POWER 7113 and Hashim's Family wishes you a prosperious festive season! Marry X- Mass

CHE GUEVARA, MAMBO 10 USIYOYAJUA!


Na Hashim Aziz
Wengi wamezoea kuiona picha yake kama alama ya ukombozi na mapinduzi ya kweli lakini ni wachache wanaomjua vizuri. Jina lake halisi anaitwa Ernesto ‘Che’ Guevara, alizaliwa Juni 14, 1928, Rosario, Argentina na yafuatayo ni mambo kumi kumhusu:
1. Alikuwa mwanaharakati na mwanamapinduzi aliyezisaidia nchi nyingi kupata uhuru kupitia vita vya msituni, zikiwemo Cuba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji na nyingine nyingi.
Ernesto Che Guevara
2. Licha ya kusumbuliwa sana na ugonjwa wa pumu, aliweza kusafiri sehemu mbalimbali, zikiwemo zenye baridi kali na kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kuwasaidia wanyonge.
3. Alisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Buenos Aires alikohitimu na kupata digrii (shahada) ya udaktari wa binadamu.
4. Akiwa bado anasomea udaktari, alifunga safari kwa kutumia pikipiki ambapo alisafiri umbali wa kilometa 4,500 na baadaye kilometa nyingine 8,000 kutembelea nchi mbalimbali za Amerika ya Kusini. Hali ya umaskini na ukandamizaji aliyoikuta huko ndiyo iliyomfanya awe mpiganaji wa msituni.

KUTUBU KWANGU (MY REPENTANCE)- 1

Naitwa Flaviana Joel, mwanamke mwenye umri wa miaka ishirini na nane. Nilibahatika kuolewa miaka kumi iliyopita, nikiwa bado msichana mbichi katika umri wa miaka kumi na nane tu.
Niliolewa na mume wangu kipenzi, Ibrahim au Ibra kama mwenyewe nilivyozoea kumuita ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye benki moja maarufu ambayo sitaitaja jina kwa sababu maalum, iliyopo hapa jijini Dar es Salaam.

Kabla Ibra hajanioa, tulidumu kwenye uchumba kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja, kipindi hicho nikiwa nasoma chuo kimoja cha uhasibu kilichopo Posta, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, nikiwa ndiyo kwanza nimeanza mwaka wa kwanza.
Baada ya ndoa, mimi na Ibra tulihamia Mbezi Beach kwenye nyumba yetu ambako tuliishi pamoja mpaka tulipokuja kutengana kwa sababu ambazo ndizo hasa zilizonifanya nitafute nafasi hii ya kutubu hadharani na kukiri kwa kinywa changu yote niliyowahi kuyafanya.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...