Sunday, November 8, 2009

RICK ROSE AMSHUKURU 50 CENT



California marekani
Rapa anayeandamwa na mikosi kibao kila kukicha, Rick Ross, hivi karibuni ameibuka na kudai kuwa anamshukuru sana 50 cent kwa madai kuwa ugomvi kati yao umemfanya azidi kupata umaarufu. Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari wakati wa utambulisho wa albamu yake mpya ya Triple C (Custom Cars & Cycles) Ross ameeleza kuwa beef lililodumu kwa muda mfupi kati yake na kiongozi wa G Unit limemuongezea kitu maishani mwake na akzidi kueleza kuwa kwa sasa kila kitu kiko shwari na hawana bifu tena.

Wale wote waliokuwa wanaombea ugomvi wetu uzidi kuwa mkubwa zaidi hawana nafasitena kwani tumeyamaliza kiutu uzima, alikaririwa Ross. Kuonyesha msisitizo, Ross alitumia kifungu cha Biblia kuwadiss waliokuwa wakishabikia beef lao kwa kutaja kifungu cha Biblia kutoka kitabu cha zaburi 27.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...