Sunday, November 8, 2009

ALICIA KEYS ALA SHAVU KWA JIGGER



New York Marekani
Baada ya kufanya vizuri sana kwenye collabo waliyoifanya pamoja, wasanii Shawn Carter Jay Z na Alicia Augello Cook Alicia Keys wanatarajia kuingia upya studio na kutengeneza Remix ya wimbo uliofanya vizuri sana sokoni wa "Empire State Of Mind", wimbo ambao utaingizwa kwenye albam mpya ya Alicia Keys itakayokwenda kwa jina la The Element of Freedom inayotarajiwa kutoka mwezi Disemba mwaka huu.

Wimbo wa Empire State of mind ultungwa na wawili hao kwa ajili ya kulisifia jiji la New York amblo ndio asili yao wote wawili. Jay Z amezaliwa na kukulia katika jiji hilo wakati Alicia Keys naye amlizaliwa na kukulia katika jiji hilo.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...