Monday, October 19, 2009

SHED NO MORE TEARS ( USILIE TENA GENEVIV) -3

Mzee Manuel Rwakatare anafanikiwa kumuokoa mwanae Geneviv kutoka kwenye mazingira ya kutisha lakini anakuwa tayari ameshachelewa “its too late…” kwani tayari Geneviv ameshaharibiwa vibaya. Kila kitu maishani mwake kimebadilika, maisha yamepoteza maana, anazidi kuuchukia ulimwengu, zaidi anawachukia wanaume… anatamani kufa kuikwepa aibu kubwa iliyoko mbele yake. Ni ndani ya siku moja tu, tayari amebakwa na wanaume watano, wanne wakiwa ni wanafunzi wahuni na mmoja akiwa ni askari polisi.
Sasa endelea…

Oooh my God! Bi Patricia alijikuta akipiga kelele baada ya kumuona mumewe akiingia ndani huku akiwa amembeba mwanae Geneviv begani akiwa hajitambui.

“What happened to my daughter,oooh…”
Kwa haraka akampokea Geneviv huku mwili wote ukimtetemeka. Akampeleka chumbani kwake na kumlaza kitandani huku mumewe akianza kuhangaika kutafuta huduma ya kwanza. Kila mtu akawa kama amechanganyikiwa, na zaidi Bi Patricia ambaye bado alikuwa hajajua nini kimemtokea mwanae. Kengele ya hatari ikalia kichwani mwa Bi Patricia wakati akiendelea kumchunguza Geneviv ambaye alikuwa hajitambui.

Kitu cha kwanza alichoshtushwa nacho ni kuona jinsi nguo za mwanae zimechanwa-chanwa. Akiwa bado anamchunguza akashtushwa na damu zilizoiloanisha sketi ya mwanae, mapigo ya moyo yakaanza kumwenda mbio…hakutaka kuamini haraka kuwa anachokihisi ndicho kilichomtokea mwanae.

Alitamani iwe ndoto lakini naye hakuweza kuubadili ukweli,akajikuta akipiga yowe kubwa na kuanza upya kuomboleza baada ya kubaini kuwa ni kweli mwanae alifanyiwa ushetani na wanaume.

“Cant believe this…I cant! Unaona ulichomsababishia mwanangu, haya furahi sasa malengo yako yametimia, ooh my Lord!”
Bi Patricia akawa anampiga-piga mumewe mgongoni huku akilia kwa uchungu. Akawa anamlalamikia kuwa yeye ndio chanzo cha yote.

“Mke wangu acha kunilaumu, mbona nimekiri makosa! Cha msingi kwa sasa tusaidiane kuokoa maisha ya geneviv, huu sio muda wa lawama.”
Bi Patricia alikuwa mgumu wa kuelewa na akazidi kulia kwa sauti kubwa kiasi cha kuwaamsha majirani ambao baada ya muda mfupi walikusanyika nje.Baada ya majadiliano ya muda mfupi,muafaka ukafikiwa kuwa Geneviv apelekwe hospitali haraka usiku huo huo.Kila mtu alimuonea huruma.

Jirani mmoja akajitolea kutoa gari lake na kwa haraka Geneviv akabadilishwa nguo na safari ya kwenda hospitali ikaanza mara moja. Japokuwa mvua kubwa ilikuwa inaendelea kunyesha hakuna aliyeonekana kujali, kila mtu akawa anahangaika kuokoa maisha ya Geneviv.

Baada ya kitambo kifupi, gari walilompakia mgonjwa likakwama kwenye matope kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha, hali iliyowalazimu mzee Rwakatare na dereva waanze kusaidiana kulitoa gari pale lilipokwama.Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, huku hali ya Geneviv ikizidi kuwa mbaya, Mzee Rwakatare akaamua kumbeba Geneviv na kuendelea na safari ya kuelekea Hospitali.

“Lakini mvua hii ni hatari kwa mgonjwa, ukizingatia bado radi zinapiga sana, kwanini tusiendelee kulihangaikia gari?”
Dereva alitoa ushauri ambao Mzee Rwakatare alishindwa kuuafiki. Akamuinua mwanae na kumuweka begani na safari ikaendelea. Bi Geneviv naye akashuka na kuanza kuwafuata kwa kukimbia huku akizidi kulia. Dereva akabaki ameduwaa akiwaonea huruma kwa yaliyowakuta.

Baada ya safari ndefu na ngumu, hatimaye walifika kwenye hospitali ya planet Health Aid ambako walipokelewa na manesi waliokuwa zamu na upesi upesi Geneviv akawekwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kuanza kukimbizwa kuelekea wodini. Kwa haraka akaanza kupewa huduma ya kwanza. Baada ya muda mfupi alitundikiwa dripu za maji ambazo zilikuwa zikitiririka kwa kasi kuingia mishipani mwake. Saa ya ukutani ya pale hospitali ilionyesha kuwa tayari ni saa kumi ya alfajiri.

Mzee Rwakatare na mkewe wakabaki nje ya wodi wakiwa wamekaa kwenye viti sehemu ya mapokezi huku kila mmoja akiwa amejiinamia kimya. Baada ya muda mfupi nesi akatoka wodini akiwa na faili mkononi mwake na kumuita mzee Rwakatare pembeni.

“Pole mzee!” yule nesi alimpa pole mzee Rwakatare na kabla hata hajajibu kitu akaendelea kuongea…
“Mgonjwa anaendelea kupata huduma ya kwanza na muda si mrefu atazinduka. Uchunguzi wetu umebaini kuwa amebakwa, na kwa taratibu za hospitali zote nchini ni kwamba mgonjwa wa namna hii lazime apitie kituo kikuu cha polisi kuchukua PF3 kwanza ndipo atibiwe, ila kwa kuwa mgonjwa wenu alikuwa na hali mbaya tukaona ni bora tuendelee kumpa huduma ya kwanza, ila matibabu ataanza kupewa baada ya w ewe kuleta hiyo PF3”

Alimaliza kuongea yule nesi na kurudi wodini akimuacha Mzee Rwakatare ameduwaa asijue la kufanya.
Bi Patricia aliinuka haraka na kumfuata yule nesi kabla hajaingia ndani na akawa anamhoji hali ya mgonjwa.

“Maelekezo yote nimempa mzee, nenda atakueleza vizuri”
Aliongea yule nesi kwa kifupi huku akifunga mlango.

Bi Patricia alirudi kwa mumewe aliyeonekana kuchanganyikiwa, akamshika mkono na kumkalisha chini huku akiwa na shauku ya kutaka kujua yule nesi alimwambia nini.

Ukweli ni kwamba tangu usiku alipomuokoa mwanae, mzee Rwakatare alikuwa hajamwambia chochote mkewe juu ya jinsi alivyomuokoa na mazingira aliyomkuta kutokana na hali aliyokuwa nayo mkewe. Ilibidi aanze kumueleza tangu mwanzo jinsi alivyomuokoa Geneviv kabla ya kumwambia maelekezo aliyopewa na yule nesi.
Baada ya kumaliza maelezo marefu, wote walishusha pumzi ndefu wakabaki wakitazamana wasijue nini cha kufanya.

“Sasa tutafanya nini mume wangu, tukizidi kuzubaa tutampoteza mtoto wetu…please do something to save her.”
“Sasa wewe unafikiri mi ntafanya nini, Polisi siwezi kwenda kwa sababu hao ndio walioniharibia mwanangu, isitoshe nimesababisha madhara pale kituoni.Huoni kuwa nikienda nitakuwa nimejipeleka mwenyewe? I cant report anything to them. They are all rotten.”

Mzee Rwakatare na mkewe waliendelea kubishana kuhusu kwenda kuchukua PF3 kama walivyoelekezwa na yule nesi. Mwishowe walifikia uamuzi wa kutokwenda. Wakaamua kumueleza yule nesi ukweli kuwa mtoto wao alibakwa na Polisi haohao hivyo haikuwa na maana kwenda tena kwao kuomba kibali.

“Lakini vipimo vyetu vinaonyesha kuwa amebakwa na watu si chini ya watano, nyie mlikuwa wapi mpaka mtoto anafanyiwa ukatili mkubwa namna hii” Yule nesi alizidi kuongea kwa msisitizo huku akionekana kuwatupia lawama wazazi kwa kushindwa kumlinda binti yao.

“Nesi sio kweli, mwanangu hajabakwa na watu watano, no! mbona bado mdogo,au mmekosea vipimo…Ooh my God! I cant believe th..i…s….”
Bi Patricia alikuwa akimbishia nesi wakati akielezwa ukweli wa yaliyomkuta mwanae huku akilia. Mzee Rwakatare alibaki ameduwaa na yeye akiwa haamini alichokisikia kutoka kwa nesi.

“Anyway, cha msingi we tusaidie mtoto atibiwe,mengine tutazidi kuelekezana taratibu.”

Mzee Rwakatare aliongea kwa kukata tamaa na kwa bahati nzuri yule nesi aliwaelewa. Akarudi wodini na kuanza kumpa matibabu Geneviv ambaye fahamu zilikuwa bado hazijamrudia.

Si mzee Rwakatare wala mkewe waliokuwa tayari kuamini kuwa ni kweli mtoto wao amebakwa na watu zaidi ya watano. Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke, ikawa ni zamu ya mkewe kumbembeleza. Alikuwa akijihisi mwenye hatia kubwa sana mbele ya mwanae na mkewe na zaidi mbele ya Mungu.

Alianza kuamini sasa kuwa ni kweli pombe badala ya kupunguza matatizo ilikuwa ikiongeza.Alijilaumu sana kwa ujinga alioufanya na kumsababisha madhara makubwa namna ile.
“One mistake, five goals…F*ck me because im the source…”
Alikuwa akijisemesha peke yake kama mwendawazimu huku akijipigapiga kichwani.

****************
Mpaka inafika saa mbili asubuhi Geneviv alikuwa bado hajazinduka hali iliyoanza kuwatia hofu hata wale manesi.

“It seems she has been severely damaged in her genitals, Hydro-saline therapy is over and yet the condition is still worse. Lets call the Doctor for emergency”
(Inaonekana ameumizwa sana, dawa tulizompa zinaisha lakini bado hali ni mbaya, inabidi tumuite daktari kwa huduma ya dharula)

Wale manesi waliokuwa wanamhudumia Geneviv tangu usiku walikuwa wakijadiliana nini cha kufanya baada ya kuona hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa unaenda. Ikabidi Geneviv ahamishiwe chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U (Intensive care unit) ambako alianza kupewa huduma ya dharula ili kuokoa maisha yake.

“Inject her the Ant-spermatids serum, then add Oestrogen 20mls into Hydro-saline therapy… If this will fail to awake her, it will be out of our control”

(Mchomeni sindano ya dawa ya Ant-spermatid, kisha ongezeni mililita 20 kwenye dripu yake yenye dawa… kama bado atashindwa kuzinduka basi itakuwa nje ya uwezo wetu)

Aliongea daktari Bingwa wa magonjwa ya kina mama na watoto, Dokta Barikieli Zayumba akiwaelekeza manesi namna ya kufanya. Kwa muda wote huo, Bi Patricia na mumewe walikuwa wameshikana mikono nje wakiomba sala mfululizo, wakimuomba Mungu wao amnusuru Geneviv

Je nini kitaendelea? Geneviv atapona? Waliohusika watachukuliwa hatua gani?

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...