Tuesday, October 13, 2009

KANYE WEST, T.I WATOSA TUZO ZA BET HIP HOP AWARDS.




Wasanii mahiri wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Kanye Omari West “Kanye West” na Clifford Joseph Harris “T.I” wameshindwa kuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo za BET Hip Hop Awards ambazo kwa mwaka huu zimefanyika huko Atlanta na kuwashirikisha wakali kibao wakiwemo Jay Z, Rihhana, Ice Cube, Young Jeezy, Drake na wengineo wengi.

Katika sherehe hizo zilizofanyika kwenye ukumbi wa Atlanta Civic Center, Kanye West ambaye alikuwa ameteuliwa kuwania tuzo Tisa, hakufika ukumbini bila ya sababu yoyote, hali iliyopeleka kukosa tuzo hata moja. Kwa upande wa T.I, imefahamika kuwa alishindwa kuhudhuria sherehe hizo na kuwakilishwa na mpenzi wake Tameka "Tiny" Cottle kwa sababu anatumikia kifungo jela huko Arkansas kutokana na kukutwa na hatia ya kumiliki silaha kinyume na sheria.

No comments:

Post a Comment

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...