Wednesday, October 21, 2009

MY HEART IS BLEEDING (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU) -5

Furaha ya maisha ya mzee Khalfan na familia yake inaanza kuingia doa baada ya kupokea barua ya vitisho ikiwataka kuhama ndani ya nyumba yao katika kipindi cha siku saba.
Hakuna anayetaka kuona hilo likitokea. Khalfan na mkewe wanajadiliana usiku kucha nini cha kufanya mara bada ya kupewa barua ile.
Wanaona njia muafaka ni kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi japokuwa barua ile iliwaonya juu ya kufanya kitu kama hicho.
Wanaamua kujitoa sadaka kwa kwenda kutoa taarifa polisi bila kujali nini kitakachotokea kwani wanaamini polisi ipo kwa ajili ya kuwalinda raia kama wao.
Baada ya siku saba walizopewa kuisha , polisi hawaji kuwapa msaada kama walivyowaahidi, na usiku wa manane nyumba yao inavamiwa na majambazi yenye silaha nzito a kuafanya maangamizi makubwa.
Je nini kitafuatia? twende pamoja…
***
Kulipopambazuka tu, Khalfani na mkewe wakaanza safari ya kwenda kutoa taarifa kwenye kituo kikuu cha polisi cha Blazinia “Blazinia Central police post”. Walienda na barua ile waliyoletewa kama ushahidi wao. Dakika chache baadae walikuwa wameshafika kituoni na wakashuka na kuingia ndani mpaka kaunta ambapo waliomba kukutana na mkuu wa kituo. Muda mfupi baadae wakawa ndani ya ofisi ya mkuu wa kituo, Luteni Lauden Kambi, aliyekuwa akifahamika kwa jina la utani kama “Luteni Fuvu” kutokana na ukatili wake.

Mzee Khalfan alianza kueleza kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho, na Luteni akawa anaandika kila kitu kwenye faili jeusi. Alipomaliza kueleza, Luteni Lauden Kambi aliwajibu kwa kifupi kuwa waende nyumbani kwao baada ya kuacha maelezo yote ya msingi ya mahali na mtaa wanakoishi, jeshi litawapa ulinzi baada ya siku hizo saba kupita. Aliwatoa hofu kuwa vile ni vitisho vya kawaida ambavyo vinahitaji ujasiri kuweza kukabiliana navyo. Aliwapa pia maelezo kuwa warudi siku ya sita hapo kituoni ili waambiwe nini cha kufanya. Baada ya kuridhika na maelezo waliyopewa, Khalfan na mkewe waliaga na kurudi nyumbani kwao wakiwa na matumaini makubwa ya kupewa msaada na jeshi la polisi


Siku zikawa zinasonga mbele kwa haraka mno, mara ikafika siku ya sita…yakiwa yamesalia masaa Ishirini na nne tu kabla ya siku ya mwisho waliyoambiwa kuwa wanatakiwa wawe wameondoka katika eneo lile, siku ya Jumapili. Hawakuwa na wasiwasi tena wakiamini wako salama wa kuwa walishahakikishiwa kuwa watapewa ulinzi. Walichokifanya ni kwenda kutoa ripoti Polisi siku moja kabla, yaani Jumamosi Kama walivyokuwa wameelekezwa na mkuu wa kituo cha polisi, Luteni Lauden kambi “Fuvu”.

Wakajitayarisha kwa safari ya kwenda tena Blaziniar Central Police post wakiwa na matumaini makubwa ya kupewa ulinzi. Safari hii gari lao liliendeshwa na Bi Miriam huku Khalfan akiwa ametulia siti ya pembeni. Walipofika waliomba tena kuonana na Mkuu wa kituo. Yule Askari aliyekuwa pale kaunta aliwapa taarifa kuwa Mkuu wa kituo ameanza likizo yake ya mwezi mzima kuanzia siku ya Ijumaa, yaani jana yake na kwa muda huo alikuwa ameshasafiri kurudi kwao alikoenda kuimalizia likizo yake.

Alizidi kuwaambia kuwa shughuli za ukuu wa kituo alikuwa amepewa mtu mwingine ambaye naye alikuwa safarini kikazi. Maelezo yale yalionekana kuwachanganya mno Khalfan na mkewe. Yale matumaini waliyokuwa nayo yakawa yamepotea Kama barafu inavyoyeyuka kwenye moto mkali. Walionyesha hofu na woga waziwazi vikiambatana na kupoteza matumaini Kiasi cha kumfanya yule Askari aliyewapa taarifa ile kushtuka. “Kwani kuna tatizo gani mzee! niambieni labda naweza kuwasaidia hata kama Mkuu hayupo”

Ilibidi mzee Khalfan aanze tena kueleza upya kuanzia mwanzo. Baada ya maelezo yake
yule Askari aliwaomba waongozane mpaka kwenye Ofisi ya Mkuu wa Kituo, wakatafute faili ambalo maelezo yao yalihifadhiwa pamoja ile barua waliyokuwa wameileta kama uthibitisho. Dakika chache baadae wakawa tayari ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Kituo. Yule Askari akaanza kutafuta faili lenye maelezo yao.
‘’Unasema mlikuja kutoa ripoti siku gain?” Yule askari alimhoji mzee Khalfan.
‘’Jumatatu iliyopita afande…‘’
Aliendelea kutafuta maelezo yale kwenye mafaili moja baada ya jingine.
‘’Aliweka maelezo yetu kwenye faili jeusi pamoja na ile barua’’ alizidi kusisitiza Bi Miriam huku wote wakimkodolea macho yule askari aliyekuwa akiendelea kupekua faili moja baada ya jingine. Baada ya kutafuta kwa muda mrefu karibu kila mahali, yule askari aliwageukia mzee Khalfan
na mkewe na akawaambia kuwa labda wasubiri kidogo ampigie simu bosi wake hata kama yuko likizo angewaelekeza alipolihifadhi faili lile.

Wakatoka Ofisini na kurudi kaunta ambako yule askari alinyanyua mkonga wa simu na kuanza kuongea na mkuu wa Luten Lauden Kambi. ‘’Amesema msiwe na wasiwasi, rudini nyumbani ila muache ramani ya mtaa mnakoishi, jina la mtaa, jina la balozi na namba ya nyumba eti ameshaacha maagizo na polisi watakuja kuwapa ulinzi wa kutosha kuanzia majira ya jioni.’’

Alimaliza yule Askari kuwapa maelezo aliyopewa na Mkuu wa kituo kwenye simu. Mzee Khalfan ali shusha pumzi ndefu kisha akamgeukia mkewe, wakatazamana kwa muda kisha yule askari akawapa
Karatasi kwa ajili ya kuacha maelezo ya mahali nyumba yao ilipo, jina la mtaa, jina la balozi na namba ya nyunba. Mzee Khalfan akaanza kuandika upya. Baada ya kuhakikisha kuwa maelezo waliyoyaacha ni sahihi mzee Khalfan na mkewe wakaaga na kuondoka.

Kengere ya hatari ilishalia kichwani mwa Khalfan, akahisi kuna mchezo mchafu unaotaka kuchezwa na askari wale askari. Iweje watoe maelezo mara ya pili ilhali walishahakikishiwa usalama wao?
Hakutaka kumwambia mkewe alichokihisi kwa kuogopa kumuongeza hofu. Wakapanda garini na safari ya kurudi kwao ikaanza safari hii pia hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake… kimya kimya
mpaka nyumbani.

Masaa yakawa yanazidi kuyoyoma, saa kumi jioni… kumi moja… kumi mbili, mara saa tatu usiku… nne tano kasoro… Hakukuwa na dalili yoyote ya polisi kufika eneo hilo kama walivyoahidiwa na Luten Lauden ‘’Fuvu”. Kwa muda wote huo mzee Khalfan alikuwa nje pamoja na walinzi wake watatu na wengine wawili aliwakodi kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa eneo zima la kuzunguka nyumba yao ili kulinda usalama.

‘’Boss! hao polisi uliosema watakuja tusaidiane nao kazi mbona hawaji na muda ndio unazidi kwenda? saa tano usiku sasa!’’ Alihoji mlinzi mmoja kwa niaba ya wenzake. Mzee Khalfan hakuwa na jibu la kuwapa, zaidi swali lile lilionekana kumchanganya akili. Tangu saa moja jioni alikuwa akiwapa darasa walinzi wake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha bunduki wanazotumia (magobore) yako katika hali ya utayari kwa kazi muda wowote. Alihakikisha pia kuwa bastola yake aliyoachiwa na marehemu mzee Shamsi imejaa risasi za kutosha.

Wote wakawa wamejiandaa vya kutosha wakitegemea muda wowote polisi wangefika kuungana nao kuwasubiri hao wanaotaka kuwadhulumu mali zao kwa nguvu. Walijiandaa kutoa upinzani wa kutosha kwa yeyote ambaye angethubutu kuleta ujeuri wa aina yoyote ile katika eneo lile. Bi Miriam naye alikuwa amewahi kuwaingiza watoto wake ndani mapema kuliko siku yoyote. Wakawahi kula chakula cha usiku kisha wote wakaenda kulala. Alihakikisha milango yote na madirisha yamefungwa ipasavyo.

Mzee Khalfan hakutaka kuingia ndani. Alitaka ashirikiane bega kwa bega na walinzi hata kama polisi hawatafika. Walinzi walimshauri aende ndani kwani walikuwa wakijiamini kuwa wanaweza kazi. Baada ya mabishano kidogo, hatimaye mzee Khalfan alikubali kurudi ndani huku bastola yake ikiwa mkononi “standby” kwa lolote. Muda ukazidi kuyoyoma…mara saa sita usiku… Saa saba na hatimaye saa nane.

Eneo zima lilikuwa kimya kabisa huku giza nene likiwa limetanda kila sehemu. Walinzi walikuwa waki zunguka huku huko kuhakikisha hakuna mtu anayesogelea eneo lile. Bunduki zao zilikuwa “standby” mikononi wakisaidiwa na mbwa mkubwa wa mzee Khalfan. Giza lilikuwa likizidi kushamiri na kufanya hali
ya eneo lile izidi kutisha. Ilishatimia saa tisa usiku huku bado kukiwa kimya kabisa.

Ghafla zilianza kusikika kelele za mbwa aliyekuwa akibweka na kukimbilia kwenye geti kubwa la kuingilia. Walinzi wakajua mambo yameanza, kwa umakini mkubwa nao wakaanza kunyata kuelekea kule mbwa alikokuwa anakimbilia. Alizidi kubweka na walinzi nao wakawa wanazidi kusogea kuelekea kule getini. Mara walishtukia kuona mbwa akipigwa risasi nyingi kichwani kisha akadondoka chini, Puuuh! Ile milio ya risasi ilitosha kuwamaliza kabisa ujasiri wote waliokuwa nao wale walinzi, kwani ilionekana dhahiri maadui zao wamekuja na bunduki nzito za kivita.

Hawakuelewa risasi zimetokea upande gani wakawa wanaangalia huku na huko. Wakiwa bado wanashangaa walishtukia kujikuta wote wamemulikwa na tochi kali kisha mvua ya risasi ikaanza kuwanyeshea. Sekunde chache baadae walinzi wote watano walikuwa chini wakitapatapa kukata roho baada ya shambulizi la ghafla risasi zilikuwa zimepenya vichwani mwao kisawasawa.

Kelele za shambulizi lile ziliwafanya wote waliokuwa ndani ya nyumba ya mzee Khalfan kushtuka. Watoto walianza kupiga mayowe hovyo ya kuomba msaada. Bi Miriam naye alikuwa hajitambui kwa hofu. Mzee Khalfan akapiga moyo konde na kunyanyua bastola yake, akaikamata kisawasawa. Akafungua mlango wa chumbani na kuanza kutoka huku akinyata kwa tahadhari kubwa. Mkewe alijaribu kumzuia asitoke lakini wapi! Akanyatia mpaka sebuleni. Akiwa katikati ya sebule, alishuhudia mlango wa nje ukivunjwa kwa jiwe kubwa kisha watu wapatao saba, wote wakiwa wamevalia makoti marefu meusi, usoni wakiwa wamevaa vitambaa vya kuficha sura zao (masks) , mikononi wakiwa na bunduki nzito za kivita kila mtu ya kwake wakiingia kwa kasi na kumzunguka pale aliposimama…

‘’Weka silaha chini! ‘’ Mmoja wa majambazi yale alimuamuru mzee Khalfan kwa sauti ya ukali mno. Akajikuta akitetemeka mwili mzima kiasi cha kuhisi haja ndogo ikimtoka bila ya ridhaa yake. Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kudondosha bastola yake chini kisha kuinua mikono juu kusalimu amri. Yale majambazi yakaanza kumshambulia kama mpira wa kona. Alipigwa na kitako cha bunduki kichwani akadondoka chini kama mzigo.

Yakaanza kumshushia kipigo cha nguvu kwa zamu zamu. Alijitahidi kujitetea lakini alizidiwa nguvu. Majambazi wengine wakaingia vyumbani na kuwatoa Bi Miriam na watoto wake wote. Kipigo kikaendelea kwa wote… hata mtoto wao mdogo wa mwisho ambaye na miaka miwili tu! Ikawa ni kichapo mtindo mmoja.

Mtoto wa kwanza wa Mzee Khalfan, Khaleed, ambaye kwa kipindi hicho alikuwa na miaka kumi na tatu, alifanikiwa kujificha chini ya meza kabla ya majambazi hayajamuona. Aliendelea kushuhudia jinsi baba’ake, mama’ake na wadogo zake walivyokuwa wakisulubiwa. Uchungu ulimuingia mno kiasi cha kushindwa kuvumilia. Kwa haraka alitoka chini ya meza na kunyanyua chuma kilichokuwa sakafuni, kisha akakinyanyua kwa nguvu zake zote na kukirusha kwa jambazi mmoja. Kilitua sawia kichwani kiasi cha kufanya jambazi lile lidondoke chini.

Akajikuta amedakwa juu juu kama kifaranga cha kuku mbele ya mwewe. Kisha naye akaanza kusulubiwa. Sekunde chache tu baadaye naye akawa ameloa damu mwili mzima kama wenzake. Kichapo kiliendelea mpaka wote wakawa hoi taabani. Yale majambazi yakawafunga wote kwa kamba, mikononi na miguuni na kuwajaza matambara midomoni mwao. Kisha yakaanza kuwaburuza mpaka nje ambako yalianza kuwapakiza kwenye gari yaliyokuja nayo. Yalikuwa yakiwarusha kama magunia,wakati yaiwapakia kwenye Landrover. Gari likawashwa na kuanza kuondoka kwa kasi ya ajabu kuelekea kusikojulikana. Eneo zima liliachwa likiwa limetapakaa damu na maiti tano za walinzi zikiwa zimelala chini. Ukimya ukatawala eneo zima, tena safari hii kukiwa kunatisha zaidi kwani hakuna aliyekuwa amesalia akiwa hai eneo lile.

NICOLE SCHERZINGER AMPA SHAVU SLASH




Mwanadada mkali katika anga ya muziki wa R&B kutoka kundi la The Pussycat Dolls, Nicole Scherzinger, amempa shavu la nguvu memba wa kundi la muziki wa Rock la
Guns N' Roses', aitwaye Slash ambaye anaandaa albamu ya peke yake (Solo Albam) ambayo bado hajaipa jina ila tayari singo moja inayokwenda kwa jina la "Slash & Friends" imeanza kufanya vizuri sokoni.
Wawili hao, Nicole na Slash walipanda jukwaa moja hivi karibuni huko Los Angels ambako walipiga vibao mchanganyiko kutoka makundi yote mawili, The Pussycat Dolls na Guns N' Roses'.


Nicole Scherzinger naye yuko kwenye maandalizi ya albamu ya peke yake (Solo Album) aliyoipa jina la "Her Name Is Nicole". Kiongozi huyo wa The PussyCat Dolls ameeleza kuwa hiyo haimaanishii kuwa amejitoa kutoka katika kundi lake, bali yeye bado ni memba halali wa kundi hilo na anashughulika na shughuli zote za Kundi.

MY HEART IS BLEEDING (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU)-4

Mafanikio ya haraka aliyoyapata Khalfan maishani mwake yanaanza kumletea matatizo. Baadhi ya watu wameanza kumonea wivu na wameanza kupanga mbinu za kumuangamiza. Japokuwa anajitahidi kuishi vizuri na kila mtu, maadui wanazidi kuongezeka siku baada ya siku, wengi wakiwa ni marafiki zake wa karibu.

Hilo halimpi hofu kabisa kwa kuwa anaamini hana kosa lolote mbele ya maulana na anaishi maisha ya haki kila siku. Familia yake nayo inazidi kukua huku mtoto wake wa kiume Khaleed akizidi kukua na kuwa na akili za kiutu uzima akiwa angali bado mdogo.

Wanaendelea kuyafurahia maisha yao na kamwe hawako tayari kuona mtu mwingine akipata taabu. Wanawasaidia wote wenye shida na Mungu anazidi kuwabariki. Lakini ghafla mambo yanaanza kwenda mrama.
Twende pamoja…
***

Baada ya miaka kadhaa kupita, walikuwa na jumla ya watoto watano, wazuri wenye furaha na afya njema. Khalfan sasa akiitwa “mzee” khalfan na mkewe Bi Miriam waliyafurahia sana maisha yao na familia yao. Muda mwingi walikuwa sambamba na watoto wao wakiwafundisha maadili mema . Utajiri ukawa unazidi kuongezeka kila kukicha, familia yao ikiwa gumzo kila kona ya mtaaa . Wengine waliendelea kuamini na kuhusisha mafanikio yale na ushirikiana , huku wengine wakiamini kwamba mzee khalfan alikuwa amebahatisha

Lakini ukweli ni kuwa juhudi na maarifa ndivyo vilivyofanya maisha yao yawe gumzo kila sehemu . Siku zikawa zinakwenda, lakini kama walivyosema waswahili penye riziki hapakosi chuki , na ili ufanikiwe zaidi unahitaji kuishi vizuri na kila mtu ingawa huwezi kukwepa kuwa na maadui, taratibu mzee Khalfan akaanza kuhisi kuwa na maadui wasiopenda mafanikio yake, alianza kuhisi marafiki zake anaoshirikiana nao katika shughuli zake za biashara wameanza kumfanyia hila kutokana na mafanikio anayoyapata, hakukosea kabisa . Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Wengi wa marafiki zake waliokuwa wakija kumtembelea pale nyumbani kwake walikuwa wakiyamezea mate mafanikio yake. Wengi walimwona kama hastahili kumiliki mali nyingi na za thamani kama alizokuwa nazo, wakaanza kupanga njama kila mmoja kwa wakati wake , wote wakitaka kumiliki mali zilizokuwa chini ya uangalizi wa khalfan na mkewe Bi Miriam. Hilo halikuwapa sana hofu khalfan na mkewe kwani waliamini Mola wao atawapigania kwa haki kwa kwa hakuna lolote baya walilomfanyia , wala hawakuwa na roho mbaya kwa mtu yeyote yule. Wote waliokuja kuomba misaada ya kimaisha walipewa walichohitaji kwa moyo wa ukarimu.

Ilikuwa ni kawaida ya familia yao kwenda kubarizi ufukweni mwa bahari kila mwisho wa wiki , siku za jumamosi na jumapili wakipendelea kukaa sehemu tulivu wakipunga upepo mwanana wa baharini huku wakibadilishana mawazo na kucheza na watoto wao.

Ilikuwa ni jumapili tulivu , majira ya jioni kabla ya jua halijazama… Khalfan na mkewe walikuwa wakirudi kutoka ufukweni walikokuwa wamekwenda kubarizi pamoja na watoto wao . Bi Miriam ndiye aliyekuwa akiendesha gari huku mumewe akiwa amekaa pembeni yake na watoto wakiendelea kucheza siti ya nyuma , baada ya muda mfupi wakawa wamefika kwenye geti la kuingia kwenye himaya yao . Bi Miriam alipiga honi mfululizo na mlinzi akatoka mbio kuja kuwafungulia.

Baada ya mlinzi kufungua mlango Bi Miriam aliingiza gari mpaka sehemu ya maegesho , akashuka na kumfungulia mumewe mlango naye akashuka kisha wakawashusha watoto wao. Kwa muda wote huo mlinzi alikuwa amesimama pembeni yao akionekana kuwa na jambo alilotaka kumwambia bosi wake, mzee Khalfani. Alisubiri wamalize kushushana ndipo ampe ujumbe aliokuwa amepewa muda mfupi uliopita kabla hawajarudi .

Khalfan aligundua kuwa mlinzi hayuko katika hali ya kawaida ikabidi amsogelee palepale alipokuwa amesimama . Mlinzi alitoa ujumbe aliokuwa amepewa na kumkabidhi mzee Khalfan, ilikuwa ni bahasha ya ukubwa wa kati iliyokuwa imefungwa vizuri. Nje ya bahasha ile hakukuwa na anuani wala jina la mtu aliyetumiwa , ila yalisomeka maandishi makubwa ya wino mwekundu “SIRI”.

Kilichomshtua khalfan ni jinsi mlinzi alivyokuwa na hofu wakati akimkabidhi ujumbe ule, alijaribu kumhoji juu ya mtu aliyeileta barua ile lakini akawa anamjibu kwa kubabaika. Alieleza kuwa muda mfupi uliopita gari ndogo nyeusi na ya kifahari ikiwa na vioo “TINTED” vya rangi nyeusi iliwateremsha wanaume wawili waliovalia makoti marefu meusi na kofia kubwa zilizoficha sura zao, mmoja akaenda mpaka pale mlangoni na mwingine akawa amebakia kwenye gari.

“Bila hata salamu akanipa bahasha na kusema nikupe wewe ukirudi!” Aliendelea kueleza mlinzi. Khalfan hakutaka kuhoji zaidi, akachukua ile bahasha na kuingia nayo ndani. Muda huo mkewe alikuwa ameshatangulia ndani na watoto akawa anaendelea kuwaandalia chakula cha jioni. Akapitiliza mpaka chumbani na kwenda kuifungua bahasha ile.

Alijikuta mikono ikianza kutetemeka alipoanza kuifungua bahasha ile akakutana na maandishi ya wino mwekundu ambayo yalisomeka vizuri. Ulikuwa ni ujumbe uliojaa vitisho na maneno ya kibabe, ukimtaka eti ‘ahame hapo nyumbani kwake yeye na familia yake yote bila kuchukua kitu chochote kwa sababu yeye Khalfan hakuwa mmiliki halali wa eneo hilo. Ujumbe ule ulizidi kutishia kwamba wanampa siku saba za kuwa ameshaondoka na onyo kali likatolewa kuwa asijaribu kutoa taarifa sehemu yoyote kwa kuwa kwa kufanya hivyo angehatarisha uhai wake.’

Alijikuta akicheka kwa dharau na kisha akatoka na ile bahasha mpaka sebuleni alikokuwa amekaa mkewe na watoto wake wakiangalia luninga. Mkewe alishtuka kumuona mumewe ameanza kubadilika, ingawa usoni alikuwa akicheka lakini alionekana kuchanganyikiwa sana akampa ule ujumbe ili na yeye ausome.

“Unatakiwa uhame hapo unapoishi wewe na familia yako bila kuchukua kitu chochote. Huna haki ya kumiliki eneo zuri kama hilo, wamiliki halali tupo na tulikuwa tunangoja muda ufike tukuambie.

Usijaribu kutoa taarifa sehemu yoyote , polisi wala jeshini kwani kwa kufanya hivyo utahatarisha usalama wako na hizo takataka zako (mkeo na watoto) unapewa siku saba za kutekeleza amri hii na ukiipuuza utaona matokeo yake”

NB. Uhai hautafutwi ila mali zinazotafutwa
By
Wamiliki

Bi Miriam alishusha pumzi ndefu baada ya kumaliza kuisoma, huku akiwa amepigwa bumbuwazi asijue nini cha kufanya. Kwa muda wote huo Khaflan alikuwa akizunguka-zunguka pale sebuleni akiwa haelewi anatafuta nini . watoto walikuwa hawana habari wakawa wanaendelea kucheza na kuruka kwenye masofa ya kisasa yaliyokuwepo pale sebuleni.

Khaflan alirudia kuisoma barua ile kisha akatoka kwa kasi kumfuata mlinzi nje. Alianza kumhoji upya ni nani aliyeleta ujumbe ule na mlinzi akarudia maelezo kama aliyoyatoa mara ya kwanza. Safari hii alionekana kuhofia zaidi baada ya kumuona bosi wake amechanganyikiwa.

Hakujua mle ndani mliandikwa nini lakini kwa hal aliyokuwa nayo bosi wake ilionyesha kuna jambo baya. Mzee Khalfan alirudi ndani na kumuelekeza mkewe awape chakula watoto haraka kisha akawalaze . Alipitiliza mpaka chumbani na kujitupa kitandani kama mzigo.

Maswali mengi yalikuwa yakipishana kichwani kama umeme wa gridi ya taifa . Alijalibu kuwaza na kuwazua ni akina nani walioleta ujumbe ule, hakupata jibu. Muda mfupi baadae mkewe akawa ameshamaliza kuwapa chakula wanae na akaenda kuwalaza kwenye chumba chao. Ama kwa hakika usiku huo ulikuwa ni usiku wa mauzauza kwao. Mpaka jogooo la kwanza linawika kuashiria mapambazuko, Khalfani na mkewe walikuwa hawajapata hata tone la usingizi.

Usiku kucha walikuwa wakijadiliana wafanye nini, hakuna aliyekuwa na jibu. Mwisho wakafikia uamuzi wa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi ingawa barua ile iliwaonya vikali juu ya uamuzi huo.
“Lakini mume wangu , si ni bora tuondoke tu tuwaachie wafanye wanachotaka ? nahofia usalama wa wanangu, tuondoke tu Mungu atatusimamia huko tuendako kwani mali hutafutwa lakini uhai hautafutwi.”
Wazo hilo halikuingia akilini mwa mzee Khalfani, kwani kufanya hivyo kungemaanisha yeye ni mwanaume dhaifu asiyeweza kuilinda familia yake aliamua kutetea msimamo wake.

”Mke wangu siko tayari hata kwa mtutu wa bunduki kuruhusu watu wengine wayaharibu maisha yetu! niamini nitafanya kila niwezalo kukulinda mke wangu na wanangu na mali zangu zote! Hakuna wa kuchukua chochote kutoka mikononi mwetu, siwezi kusalimu amri kirahisi namna hii, niamini…”

Kwa jinsi alivyokuwa akiongea kwa kujiamini, mkewe akapata imani kuwa usalama wao utalindwa kwa kila namna. Kulipopambazuka tu, mzee Khalfani na mkewe wakaanza kujiandaa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Blazinia Central Police Post”.

Walichukua barua ile kama ushahidi wa maelezo yao. Mzee Khalfan aliendesha gari lao huku mkewe akiwa pembeni yake. Hakuna aliyemsemesha mwenzake! Kila mtu alikuwa kwenye lindi zito la mawazo, maneno ya barua ile yalikuwa yakijirudiarudia vichwani mwao.
***

Kenyan building collapses, killing 6 and injuring 13; experts blame poor construction



Six people died and 14 were still missing after a three-story building collapsed on the outskirts of the country's capital, a police official said Tuesday, as experts warned that irresponsible contractors were to blame.

Policeman Samuel Mukindia said two people died while receiving treatment at a Nairobi hospital. The bodies of three men were pulled from the rubble at the building site in Kiambu. Another victim, a woman, was crushed to death. Police said 13 people were injured.

The Kenya Red Cross said 14 people were still unaccounted for after being reported missing by their relatives and friends.

Millicent Wairumu said she believed her younger brother David Wachira was trapped in the rubble. She cooked him breakfast Monday morning and asked him to work in her shop. He declined her offer, saying he wanted to earn his own money and he was already staying in her house.

"I can't reach him on his mobile phone," she wept as she dialed his number on her phone. "He should not have been here. I should have insisted he came to work for me."

Monday's disaster came barely a week after the Kenya Architectural Association said in a report that 65 percent of structures in the country were substandard.

Richard Chepkwony, a member of the Institution of Engineers of Kenya, said the organization was receiving almost daily reports of buildings collapsing because of poor construction. He said the building collapsed on Monday because of its substandard construction material and poor workmanship.

"If you grab a block of concrete, you can crack it using your hands," he said, crushing lumps of concrete between his fingers. "This is not the end of the story. We will be seeing more of this if the government does not enact laws to ensure required construction standards are met."

Building collapses are common in Africa. Corrupt planning officials, substandard materials and poor workmanship are often to blame.

Monday, October 19, 2009

MY HEART IS BLEEDING ( MOYO WANGU UNAVUJA DAMU)-3

Wakati kesi nzito inayomkabili kijana mdogo anayeshtakiwa kwa kufanya mauaji makubwa na ya kutisha ikiendelea kugusa hisia za maelfu ya watu, kitu cha ajabu kinatokea mahakamani.

Jaji mkuu Profesa Kadir Mudhihir Simba anaanguka mahakamani na kupoteza fahamu akiwa katika hatua za mwisho za kutoa hukumu. Anakimbizwa Hospitali hali yake ikiwa mbaya sana na kadri muda unavyozidi kwendahali yake inakuwa mbaya zaidi.

Huku nyuma anaacha watu wakiwa wamepigwa na bumbuwazi wakiwa hawaelewi nini kilichomsibu na tukio lile linamaanisha nini. Vurugu nyingine inazuka mahakamani lakini polisi wa kutuliza ghasia wanaidhibiti na kufankiwa kumrudisha mshtakiwa gerezani.

Watu wanaanza kufuatilia chanzo cha tukio lile miaka mingi iliyopita. Historia inaonyesha kila kitu kilivyokuwa mpaka kumsababisha kijana yule kufanya mauaji makubwa kiasi kile yaliyotikisa nchi.

Twende pamoja ufahamu chanzo...
Kwa jinsi wazazi wa Miriam, Mzee Shamsi na mkewe walivyokuwa wakimpenda mkwe wao, ilibidi wamshawishi Khalfani pamoja na mkewe Miriam wahamie nyumbani kwa Mzee Shamsi. Mzee Shamsi na mkewe hawakuwa na mtoto mwingine zaidi ya binti yao Miriam, hivyo kuondoka kwake na kumfuata mumewe, kuliwafanya wabaki wapweke sana kwenye himaya yao.

Khalfan na mkewe hawakuwa na kipingamizi chochote, wakakubali kuhamia nyumbani kwa mzee Shamsi, (Ukweni). Maisha yao yakazidi kuwa mazuri siku baada ya siku, na sasa Khalfan akawa ameachana na biashara yake ya mboga mboga na matunda.

Badala yake akawa akimsaidia mzee Shamsi kwenye shughuli zake za Biashara ya madini ya Ruby. Muda mwingi akawa akitembezwa kwenye gari ndogo aina ya “Mercedes Lexus 5 New Model” ya kisasa, akimwonyesha vitega uchumi vyake na kumwelelekeza jinsi ya kuhudumia mali zote walizokuwa nazo.

Kwa kifupi mzee Shamsi alimuamini sana Khalfan, kiasi cha kumchukulia kama mwanae wa kumzaa. Hakumficha kitu chochote, alikuwa akimpa mpaka siri zake za ndani. Aliamini kuwa kwa kuwa hakubahatika kupata mtoto wa kiume, basi khalfan ndio atakuwa mrithi wa mali zake zote akishirikiana na mkewe Miriam.

Alichokuwa akimsisitiza siku zote ni kumpenda kwa dhati mkewe, mtoto wao wa pekee Miriam. Alikuwa akimuonya pia kuwa makini sana na marafiki wa kibiashara ambao atakuwa akishirikiana nao hususani kwenye bashara ya madini kwani akili za mwanadamu hubadilika sana akiona vitu vya thamani. Nasaha alizokuwa anapewa kila siku zilimjenga upya kifikra na kumpa ujasiri kuliko ilivyokuwa mwanzo. Alijiona anaweza kufanya mambo makubwa hata kama hakuwa na elimu kubwa kichwani

Ilikuwa ni majira ya saa nne asubuhi, Miriam akiwa anamuandalia mumewe Khalfan kifungua kinywa, huku wakitaniana utani wa mume na mke! Kila mmoja alikuwa na furaha kuwa na mwenzake. Wakawa wakitaniana na kucheza kama watoto huku Miriam akiendelea kuandaa kifumgua kinywa.

Wakati hayo yakiendelea taarifa ya habari iliyokuwa inasomwa kutoka kituo maarufu cha redio, “The Bulletin FM” iliwashtua wote kiasi cha kufanya kila mtu aache alichokuwa anakifanya na kukimbilia jirani na redio ili asikie vizuri taarifa ile.

Ilikuwa ni habari mbaya ya ajali ya kutisha ya ndege iliyotokea muda mfupi uliopita. Ajali hiyo ilihusisha ndege ya kampuni ya “TRY EMIRATES” aina ya Jet B710 Sossoliso, iliyokuwa inatoka uwanja wa kimataifa wa Blazinair International Airport (BLIA) kuelekea Muscat Oman. Habari ilizidi kuelezea kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hitilafu katika moja ya injini zake, hali iliyosababisha ndege hiyo kulipuka muda mfupi baada ya kuruka, kisha ikaangukia baharini.

Kilichosikitisha ni kwamba abiria wote 67 waliokuwemo kwenye ndege walikuwa wakihofiwa kupoteza maisha katika ajali ile. Habari ilihitimishwa kwa mahojiano na watu walioshuhudia ajali ile ambapo kila aliyehojiwa alikiri kuwa hakuwahi kusikia wala kushuhudia ajali mbaya kama ile.

Khalfan na mkewe walibaki wakikodoleana macho, wasijue nini cha kufanya. Kilichowashtua ni kwamba ni asubuhi ya siku hiyo masaa machache tu yaliyopita walitoka kuwasindikiza mzee Shamsi na mkewe uwanja wa ndege, wakielekea oman kupeleka biashara yao ya madini ya Ruby.

Haikuwa kawaida kwa mzee Shamsi kusafiri na mkewe, kwani mara zote yeye aliposafiri mkewe alibaki kuwa msimamizi wa mali zao, lakini baada ya binti yao kuolewa na Khalfan Mwalukasa, shughuli zote za usimamizi wa mali zilibaki kuwa chini ya uangalizi wa Khalfan kwani walimchukulia kama mtoto wao, na kwa pamoja walikubaliana kuwa yeye ndiye atakayekuwa mrithi wa mali zao, pindi mauti yatakapowafika.

Ni masaa mawili tu yaliyopita majira ya kama saa mbili za asubuhi Khalfan na mkewe waliwasindikiza wazazi wao uwanja wa ndege na wakasubiri mpaka walipopanda ndege ya kampuni ya usafiri wa anga ya TRY EMIRATES tayari kwa safari ya Oman. Ni baada ya kuhakikisha kuwa wamepanda ndege, ndipo Khalfan na mkewe waliporudi nyumbani kuendelea na shughuli zao.

Wakiwa wanajiandaa kupata kifungua kinywa ndipo taarifa ya kusikitisha na kutia majonzi iliposikika. Hiyo ilimaanisha kuwa mzee Shamsi na mkewe walikuwa wamepoteza maisha katika ajali ile. Msiba mkubwa kiasi gani. Habari ya ajali ile iliwashtua watu wengi, ambao kwa namna moja au nyingine waliwapoteza ndugu, jamaa na marafiki zao waliokuwemo kwenye ndege ile.

Kwa Khalfan Mwalukasa, licha ya ukweli kwamba aliguswa na vifo vya wakwe zake, hii ilikuwa ni kama bahati ya mtende kuota jangwani, waswahili wanasema kufa kufaana. Ni Khalfan huyu huyu aliyekimbia kwao kutokana na ugumu wa maisha, akawa akifanya biashara ya mbogamboga na matunda, ndiye sasa alitakiwa kuwa mmiliki wa hazina ya utajiri ulioachwa na mzee Shamsi. Hakuwahi kuota wala kutegemea kuwa ipo siku atakuja kumiliki hazina kubwa ya utajiri kama ile. Kweli Mungu alikuwa ametenda miujiza katika maisha yake.

********

Siku ziwaka zinakwenda, sekunde, dakika, masaa! Mara usiku, mara mchana… mawio na machweo. Kumbukumbu ya kuwapoteza wazazi mzee Shamsi na mkewe taratibu ikaanza kupotea vichwani kwa Khalfan na mkewe Miriam. Khalfan akawa anajitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kumliwaza mkewe na kumfaya asahau yote yaliyotokea. Yeye ndiyo akawa baba na kichwa cha familia.

Mwanzoni ilimuwia vigumu kuweza kusimamia mali zote zilizoachwa na mzee Shamsi lakini kila alipokuwa akikumbuka mawaidha aliyokuwa anapewa na mzee Shamsi, akawa anajipa moyo kuwa hakuna lisilowezekana. Taratibu akawa anapata uzoefu kila siku mpya ilipokuwa ikianza. Hali hiyo ilionekana kumfariji sana mkewe, ambaye sasa akawa na uhakika kuwa kila kitu kitaendelea vizuri na kushamiri japokuwa alikuwa amepoteza wazazi wake.

Khalfan akawa anajituma kwa bidii kuhakikisha kuwa hakuna kinachomshinda.
Baada ya miezi saba tangu mzee Shamsi na mkewe wapoteze maisha katika ajali mbaya ya ndege, Miriam akiwa anarudi kutoka hospitali alikuja na habari njema kwa mumewe!

“Mume wangu, nafurahi kukuambia kuwa baada ya siku si nyingi nitakuzalia mtoto!”
“Unasema kweli mke wangu? Safi sana!” Khalfan akiwa haamini, alimkumbatia mkewe kwa nguvu… na hapo ndipo naye alipoelewa mkewe alikuwa anamaanisha nini. Mkewe alikuwa mjamzito, furaha iliyoje! Maisha yakawa kama ndio yameanza upya, muda wote wakawa wakicheza kama watoto, wakishinda kutwa nzima katika bustani za maua zilizokuwepo hapo nyumbani.

Muda ukawa unazidi kwenda, huku Khalfan akiwa anampeleka mkewe Clinic mara kwa mara, kuhakikisha anajifungua salama. Miezi ikawa inakatika, hatimaye miezi tisa ikawa imetimia. Bi Miriam akajifungua salama mtoto wa kiume, mzuri kama mama yake. Furaha katika ndoa yao ikawa imeongezeka mara dufu, na ikawa inazidi kuongezeka kila uchao.

Wakampa mtoto wao jina la Khaleed . “Mume wangu yaani furaha unayonipa maishani, sikuwahi kutegemea hata siku moja! Nakupenda sana mume wangu na Mungu azidi kuibariki ndoa yetu tudumu mpaka kifo kitakapo tutenganisha” Bi Miriam alikuwa akiongea kwa hisia nzito za mahaba kwa mumewe wakiwa na kichanga chao Khaleed, wakipunga upepo wa jioni.

Baada ya miaka miwili wakapata mtoto mwingine wa kiume, tofauti na kaka yake, yeye alifanana mno na baba yake. Watoto wakawa na afya njema, furaha na walipewa malezi bora.

Khalfan sasa akawa baba wa familia, mkewe Miriam naye akawa mama kama alivyokuwa akitamani siku zote. Waliyafurahia sana maisha yao. Muda mwingi walikuwa sambamba wakisaidiana kuwapa malezi bora watoto wao na kuwafundisha maadili mema. Utajiri nao ukawa unazidi kuongezeka kila kukicha, shamba na bustani zao za maua zikawa zinazidi kushamiri na kuwa “Evergreen” huku mazao yakistawi sana.

Wapo watu walioyahusisha mafanikio yale na imani za kishirina wakihisi kuwa huenda Khalfan Mwalukasa alikuwa akitumia nguvu za giza ili kupata mafanikio. Wapo walioanza kummezea mate wakiona kuwa hakustahili kuwa na mafanikio makubwa kama yale. Wala maneno ya walimwengu hayakuwarudisha nyuma. Walikuwa waimwamwini Mungu wao na walijitahidi kuishi vizuri na kila mtu, wakitoa misaada mingi ya kijamii kwa watu wenye shida na wanaoishi katika mazingira magumu.

Waliwasaidia pia watoto wenye shida mbalimbali hasa wale waliokuwa wakiishi kwenye mazingira magumu bada ya kufiwa na wazazi wao ama kutokana na hali duni za wazazi wao. Walijtahidi kwa kadri ya uwezo wao wote kugawana kile walichojaaliwa na Mungu kwa wale ambao hawakuwa nacho. Kadri muda ulivyokuwa unaenda wakazidi kujijengea jina na umaarufu huku kila mwenye shida akikimbilia kwao kuomba msaada.

Walifanikiwa pia kuanzisha kituo cha kulelea watoto yatima na wale wa mitaani, na wakaamua kukipa jina la “Shamsi Memorium Orphanage” ikiwa kama kumbukumbu ya mzee wao Shamsi na mkewe waliokuwa wameshatangulia mbele za haki.

Tukutane next issue!

SHED NO MORE TEARS ( USILIE TENA GENEVIV) -3

Mzee Manuel Rwakatare anafanikiwa kumuokoa mwanae Geneviv kutoka kwenye mazingira ya kutisha lakini anakuwa tayari ameshachelewa “its too late…” kwani tayari Geneviv ameshaharibiwa vibaya. Kila kitu maishani mwake kimebadilika, maisha yamepoteza maana, anazidi kuuchukia ulimwengu, zaidi anawachukia wanaume… anatamani kufa kuikwepa aibu kubwa iliyoko mbele yake. Ni ndani ya siku moja tu, tayari amebakwa na wanaume watano, wanne wakiwa ni wanafunzi wahuni na mmoja akiwa ni askari polisi.
Sasa endelea…

Oooh my God! Bi Patricia alijikuta akipiga kelele baada ya kumuona mumewe akiingia ndani huku akiwa amembeba mwanae Geneviv begani akiwa hajitambui.

“What happened to my daughter,oooh…”
Kwa haraka akampokea Geneviv huku mwili wote ukimtetemeka. Akampeleka chumbani kwake na kumlaza kitandani huku mumewe akianza kuhangaika kutafuta huduma ya kwanza. Kila mtu akawa kama amechanganyikiwa, na zaidi Bi Patricia ambaye bado alikuwa hajajua nini kimemtokea mwanae. Kengele ya hatari ikalia kichwani mwa Bi Patricia wakati akiendelea kumchunguza Geneviv ambaye alikuwa hajitambui.

Kitu cha kwanza alichoshtushwa nacho ni kuona jinsi nguo za mwanae zimechanwa-chanwa. Akiwa bado anamchunguza akashtushwa na damu zilizoiloanisha sketi ya mwanae, mapigo ya moyo yakaanza kumwenda mbio…hakutaka kuamini haraka kuwa anachokihisi ndicho kilichomtokea mwanae.

Alitamani iwe ndoto lakini naye hakuweza kuubadili ukweli,akajikuta akipiga yowe kubwa na kuanza upya kuomboleza baada ya kubaini kuwa ni kweli mwanae alifanyiwa ushetani na wanaume.

“Cant believe this…I cant! Unaona ulichomsababishia mwanangu, haya furahi sasa malengo yako yametimia, ooh my Lord!”
Bi Patricia akawa anampiga-piga mumewe mgongoni huku akilia kwa uchungu. Akawa anamlalamikia kuwa yeye ndio chanzo cha yote.

“Mke wangu acha kunilaumu, mbona nimekiri makosa! Cha msingi kwa sasa tusaidiane kuokoa maisha ya geneviv, huu sio muda wa lawama.”
Bi Patricia alikuwa mgumu wa kuelewa na akazidi kulia kwa sauti kubwa kiasi cha kuwaamsha majirani ambao baada ya muda mfupi walikusanyika nje.Baada ya majadiliano ya muda mfupi,muafaka ukafikiwa kuwa Geneviv apelekwe hospitali haraka usiku huo huo.Kila mtu alimuonea huruma.

Jirani mmoja akajitolea kutoa gari lake na kwa haraka Geneviv akabadilishwa nguo na safari ya kwenda hospitali ikaanza mara moja. Japokuwa mvua kubwa ilikuwa inaendelea kunyesha hakuna aliyeonekana kujali, kila mtu akawa anahangaika kuokoa maisha ya Geneviv.

Baada ya kitambo kifupi, gari walilompakia mgonjwa likakwama kwenye matope kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha, hali iliyowalazimu mzee Rwakatare na dereva waanze kusaidiana kulitoa gari pale lilipokwama.Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, huku hali ya Geneviv ikizidi kuwa mbaya, Mzee Rwakatare akaamua kumbeba Geneviv na kuendelea na safari ya kuelekea Hospitali.

“Lakini mvua hii ni hatari kwa mgonjwa, ukizingatia bado radi zinapiga sana, kwanini tusiendelee kulihangaikia gari?”
Dereva alitoa ushauri ambao Mzee Rwakatare alishindwa kuuafiki. Akamuinua mwanae na kumuweka begani na safari ikaendelea. Bi Geneviv naye akashuka na kuanza kuwafuata kwa kukimbia huku akizidi kulia. Dereva akabaki ameduwaa akiwaonea huruma kwa yaliyowakuta.

Baada ya safari ndefu na ngumu, hatimaye walifika kwenye hospitali ya planet Health Aid ambako walipokelewa na manesi waliokuwa zamu na upesi upesi Geneviv akawekwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kuanza kukimbizwa kuelekea wodini. Kwa haraka akaanza kupewa huduma ya kwanza. Baada ya muda mfupi alitundikiwa dripu za maji ambazo zilikuwa zikitiririka kwa kasi kuingia mishipani mwake. Saa ya ukutani ya pale hospitali ilionyesha kuwa tayari ni saa kumi ya alfajiri.

Mzee Rwakatare na mkewe wakabaki nje ya wodi wakiwa wamekaa kwenye viti sehemu ya mapokezi huku kila mmoja akiwa amejiinamia kimya. Baada ya muda mfupi nesi akatoka wodini akiwa na faili mkononi mwake na kumuita mzee Rwakatare pembeni.

“Pole mzee!” yule nesi alimpa pole mzee Rwakatare na kabla hata hajajibu kitu akaendelea kuongea…
“Mgonjwa anaendelea kupata huduma ya kwanza na muda si mrefu atazinduka. Uchunguzi wetu umebaini kuwa amebakwa, na kwa taratibu za hospitali zote nchini ni kwamba mgonjwa wa namna hii lazime apitie kituo kikuu cha polisi kuchukua PF3 kwanza ndipo atibiwe, ila kwa kuwa mgonjwa wenu alikuwa na hali mbaya tukaona ni bora tuendelee kumpa huduma ya kwanza, ila matibabu ataanza kupewa baada ya w ewe kuleta hiyo PF3”

Alimaliza kuongea yule nesi na kurudi wodini akimuacha Mzee Rwakatare ameduwaa asijue la kufanya.
Bi Patricia aliinuka haraka na kumfuata yule nesi kabla hajaingia ndani na akawa anamhoji hali ya mgonjwa.

“Maelekezo yote nimempa mzee, nenda atakueleza vizuri”
Aliongea yule nesi kwa kifupi huku akifunga mlango.

Bi Patricia alirudi kwa mumewe aliyeonekana kuchanganyikiwa, akamshika mkono na kumkalisha chini huku akiwa na shauku ya kutaka kujua yule nesi alimwambia nini.

Ukweli ni kwamba tangu usiku alipomuokoa mwanae, mzee Rwakatare alikuwa hajamwambia chochote mkewe juu ya jinsi alivyomuokoa na mazingira aliyomkuta kutokana na hali aliyokuwa nayo mkewe. Ilibidi aanze kumueleza tangu mwanzo jinsi alivyomuokoa Geneviv kabla ya kumwambia maelekezo aliyopewa na yule nesi.
Baada ya kumaliza maelezo marefu, wote walishusha pumzi ndefu wakabaki wakitazamana wasijue nini cha kufanya.

“Sasa tutafanya nini mume wangu, tukizidi kuzubaa tutampoteza mtoto wetu…please do something to save her.”
“Sasa wewe unafikiri mi ntafanya nini, Polisi siwezi kwenda kwa sababu hao ndio walioniharibia mwanangu, isitoshe nimesababisha madhara pale kituoni.Huoni kuwa nikienda nitakuwa nimejipeleka mwenyewe? I cant report anything to them. They are all rotten.”

Mzee Rwakatare na mkewe waliendelea kubishana kuhusu kwenda kuchukua PF3 kama walivyoelekezwa na yule nesi. Mwishowe walifikia uamuzi wa kutokwenda. Wakaamua kumueleza yule nesi ukweli kuwa mtoto wao alibakwa na Polisi haohao hivyo haikuwa na maana kwenda tena kwao kuomba kibali.

“Lakini vipimo vyetu vinaonyesha kuwa amebakwa na watu si chini ya watano, nyie mlikuwa wapi mpaka mtoto anafanyiwa ukatili mkubwa namna hii” Yule nesi alizidi kuongea kwa msisitizo huku akionekana kuwatupia lawama wazazi kwa kushindwa kumlinda binti yao.

“Nesi sio kweli, mwanangu hajabakwa na watu watano, no! mbona bado mdogo,au mmekosea vipimo…Ooh my God! I cant believe th..i…s….”
Bi Patricia alikuwa akimbishia nesi wakati akielezwa ukweli wa yaliyomkuta mwanae huku akilia. Mzee Rwakatare alibaki ameduwaa na yeye akiwa haamini alichokisikia kutoka kwa nesi.

“Anyway, cha msingi we tusaidie mtoto atibiwe,mengine tutazidi kuelekezana taratibu.”

Mzee Rwakatare aliongea kwa kukata tamaa na kwa bahati nzuri yule nesi aliwaelewa. Akarudi wodini na kuanza kumpa matibabu Geneviv ambaye fahamu zilikuwa bado hazijamrudia.

Si mzee Rwakatare wala mkewe waliokuwa tayari kuamini kuwa ni kweli mtoto wao amebakwa na watu zaidi ya watano. Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke, ikawa ni zamu ya mkewe kumbembeleza. Alikuwa akijihisi mwenye hatia kubwa sana mbele ya mwanae na mkewe na zaidi mbele ya Mungu.

Alianza kuamini sasa kuwa ni kweli pombe badala ya kupunguza matatizo ilikuwa ikiongeza.Alijilaumu sana kwa ujinga alioufanya na kumsababisha madhara makubwa namna ile.
“One mistake, five goals…F*ck me because im the source…”
Alikuwa akijisemesha peke yake kama mwendawazimu huku akijipigapiga kichwani.

****************
Mpaka inafika saa mbili asubuhi Geneviv alikuwa bado hajazinduka hali iliyoanza kuwatia hofu hata wale manesi.

“It seems she has been severely damaged in her genitals, Hydro-saline therapy is over and yet the condition is still worse. Lets call the Doctor for emergency”
(Inaonekana ameumizwa sana, dawa tulizompa zinaisha lakini bado hali ni mbaya, inabidi tumuite daktari kwa huduma ya dharula)

Wale manesi waliokuwa wanamhudumia Geneviv tangu usiku walikuwa wakijadiliana nini cha kufanya baada ya kuona hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa unaenda. Ikabidi Geneviv ahamishiwe chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U (Intensive care unit) ambako alianza kupewa huduma ya dharula ili kuokoa maisha yake.

“Inject her the Ant-spermatids serum, then add Oestrogen 20mls into Hydro-saline therapy… If this will fail to awake her, it will be out of our control”

(Mchomeni sindano ya dawa ya Ant-spermatid, kisha ongezeni mililita 20 kwenye dripu yake yenye dawa… kama bado atashindwa kuzinduka basi itakuwa nje ya uwezo wetu)

Aliongea daktari Bingwa wa magonjwa ya kina mama na watoto, Dokta Barikieli Zayumba akiwaelekeza manesi namna ya kufanya. Kwa muda wote huo, Bi Patricia na mumewe walikuwa wameshikana mikono nje wakiomba sala mfululizo, wakimuomba Mungu wao amnusuru Geneviv

Je nini kitaendelea? Geneviv atapona? Waliohusika watachukuliwa hatua gani?

OBAMA KUHALALISHA MATUMIZI YA MARIJUANA






WASHINGTON – Federal drug agents won't pursue pot-smoking patients or their sanctioned suppliers in states that allow medical marijuana, under new legal guidelines to be issued Monday by the Obama administration.

Two Justice Department officials described the new policy to The Associated Press, saying prosecutors will be told it is not a good use of their time to arrest people who use or provide medical marijuana in strict compliance with state law.

The guidelines to be issued by the department do, however, make it clear that agents will go after people whose marijuana distribution goes beyond what is permitted under state law or use medical marijuana as a cover for other crimes, the officials said.

The new policy is a significant departure from the Bush administration, which insisted it would continue to enforce federal anti-pot laws regardless of state codes.

Fourteen states allow some use of marijuana for medical purposes: Alaska, California, Colorado, Hawaii, Maine, Maryland, Michigan, Montana, Nevada, New Mexico, Oregon, Rhode Island, Vermont and Washington.

California is unique among those for the widespread presence of dispensaries — businesses that sell marijuana and even advertise their services. Colorado also has several dispensaries, and Rhode Island and New Mexico are in the process of licensing providers, according to the Marijuana Policy Project, a group that promotes the decriminalization of marijuana use.

Attorney General Eric Holder said in March that he wanted federal law enforcement officials to pursue those who violate both federal and state law, but it has not been clear how that goal would be put into practice.

A three-page memo spelling out the policy is expected to be sent Monday to federal prosecutors in the 14 states, and also to top officials at the FBI and Drug Enforcement Administration.

The memo, the officials said, emphasizes that prosecutors have wide discretion in choosing which cases to pursue, and says it is not a good use of federal manpower to prosecute those who are without a doubt in compliance with state law.

The officials spoke on condition of anonymity because they were not authorized to discuss the legal guidance before it is issued.

"This is a major step forward," said Bruce Mirken, communications director for the Marijuana Policy Project. "This change in policy moves the federal government dramatically toward respecting scientific and practical reality."

At the same time, the officials said, the government will still prosecute those who use medical marijuana as a cover for other illegal activity. The memo particularly warns that some suspects may hide old-fashioned drug dealing or other crimes behind a medical marijuana business.

In particular, the memo urges prosecutors to pursue marijuana cases which involve violence, the illegal use of firearms, selling pot to minors, money laundering or involvement in other crimes.

And while the policy memo describes a change in priorities away from prosecuting medical marijuana cases, it does not rule out the possibility that the federal government could still prosecute someone whose activities are allowed under state law.

The memo, officials said, is designed to give a sense of prosecutorial priorities to U.S. attorneys in the states that allow medical marijuana. It notes that pot sales in the United States are the largest source of money for violent Mexican drug cartels, but adds that federal law enforcement agencies have limited resources.

Medical marijuana advocates have been anxious to see exactly how the administration would implement candidate Barack Obama's repeated promises to change the policy in situations in which state laws allow the use of medical marijuana.

Soon after Obama took office, DEA agents raided four dispensaries in Los Angeles, prompting confusion about the government's plans.

___

Tuesday, October 13, 2009

KEYS TO SUCCESS- VOL 1

What “Real World” Outcomes Can you Expect?

- Money

o Direct more money into your life than ever before
o Finally get paid what you deserve
o Get recognized as a leader and ultimately have job security
o Take your personal business to the next level effortlessly and easily
o Have people calling you and approaching you for your services

- Mind

o Destroy fear in your life once and for all so that you can walk tall, with confidence and conquer everything that comes your way
o Create unbreakable self confidence in your self, your beliefs, and who you stand for being in life
o Have absolute certainty in any and all decisions you make
o Finally be stress free (wow, can you imagine what that will feel like)
o Trust your intuition, your brilliant mind and ideas.

- Body

o Effectively lose the weight and create your ideal body that you absolutely fall in love with (and so will everyone else)
o Quit smoking, drinking, overeating, or any other unhealthy habit that you have been dreaming of finally letting go of for good
o Accept yourself for who you are and truly loving every inch of your self, inside and out

- Soul

o Forgive those that have hurt you in the past so that you can be free to move forward in your life
o Find the beautiful lesson in everything that you’ve experienced in life so that you can grow faster than you ever imagined
o Honor yourself like you’ve never experienced before

- Love/Relationships

o Create an amazingly loving relationship with your partner
o Have an unbreakable trusting relationship with your kids (or your parents)
o Learn how beautiful or handsome you truly are and naturally attract a partner who showers you with love like never before

Plus so much more.

KANYE WEST, T.I WATOSA TUZO ZA BET HIP HOP AWARDS.




Wasanii mahiri wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Kanye Omari West “Kanye West” na Clifford Joseph Harris “T.I” wameshindwa kuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo za BET Hip Hop Awards ambazo kwa mwaka huu zimefanyika huko Atlanta na kuwashirikisha wakali kibao wakiwemo Jay Z, Rihhana, Ice Cube, Young Jeezy, Drake na wengineo wengi.

Katika sherehe hizo zilizofanyika kwenye ukumbi wa Atlanta Civic Center, Kanye West ambaye alikuwa ameteuliwa kuwania tuzo Tisa, hakufika ukumbini bila ya sababu yoyote, hali iliyopeleka kukosa tuzo hata moja. Kwa upande wa T.I, imefahamika kuwa alishindwa kuhudhuria sherehe hizo na kuwakilishwa na mpenzi wake Tameka "Tiny" Cottle kwa sababu anatumikia kifungo jela huko Arkansas kutokana na kukutwa na hatia ya kumiliki silaha kinyume na sheria.

SHED NO MORE TEARS GENEVIV… USILIE TENA GENEVIV -2

Baada ya vijana wa kihuni kumfanyia kitu mbaya Geneviv,wanaondoka na kumuacha akiwa amepoteza fahamu kutokana na maumivu makali aliyoyapata. Anakuja kuzinduka usiku sana na kujikuta akiwa peke yake porini,palepale chini ya mti.Hawezi hata kusimama kutokana na maumivu makali anayoyahisi…anaamua kulala hapohapo mpaka asubuhi bila kujali kuwa ni porini.
Nyumbani kwao nako baba na mama yake wameyamaliza matatizo yao kiutu uzima,lakini wanaanza tena kulumbana na kila mmoja amechanganyikiwa baada ya kuona muda unazidi kuyoyoma na usiku unaingia huku Geneviv akiwa hafahamiki aliko.
Je nini kitatokea?
Ungana nami,twende sasa…
****
Baada ya kumkosa chumbani kwake, Bi Patricia alirudi na kumpa mumewe taarifa.
“Atakuwa ameenda wapi? Maskini malaika wangu…”
Aliongea mzee Rwakatare akijifanya kumsikitikia mwanae.Kwa kifupi,zile tofauti zilizokuwepo baina ya Bi Patricia na mumewe zilionekana kama zimekwisha kabisa na sasa wote wakawa wanamfikiria binti yao Geneviv.

Muda ulizidi kwenda bila ya Geneviv kurudi nyumbani.Hawakujua yuko wapi na amepatwa na nini.
“Ningekuwa na nguvu ningeenda kumuulizia kwa wenzake,mwanangu hana tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani namna hii! Sijui kapatwa na balaa gani maskini”

aliongea Bi Patricia kwa masikitiko baada ya kuanza kuhisi kuwa huenda mwanae amepatwa na jambo baya baada ya usiku kuzidi kuingia.Mwili wake wote ulikuwa bado una maumivu kutokana na kipigo cha mumewe kiasi cha kumfanya ashindwe hata kutoka nje kwenda kumtafuta mwanae.Saa ya ukutani iliyokuwa mle chumbani ilionyesha kuwa ni tayari saa nne za usiku.
Wasiwasi ulizidi kuwaingia kiasi cha kila mtu kubaki kimya akiwaza kivyake.

“kwani alivyoondoka aliaga anakwenda wapi?”
Mzee Rwakatare aliuliza swali la kijinga kiasi cha kumkumbusha mkewe yaliyotokea asubuhi ya siku ile na kumfanya Geneviv atoroke pale nyumbani bila kuaga.
“Si ujinga wako uliokuwa unaufanya asubuhi,unafikiri mwanao bado mtoto sio, namtaka mwanangu! Amka kamtafute mwanangu…!”
Bi Patricia alianza kucharuka na kumshinikiza mumewe aende kumtafuta Geneviv.Mzee Rwakatare naye hakuweza kutoka nje kwani bado alikuwa na maumivu sehemu ya kichwani baada ya kupigwa na stuli asubuhi.Wakabaki kulaumiana wenyewe kwa wenyewe.Mzee Rwakatare alijihisi kushtakiwa na dhamira yake sana,kwani ukweli aliujua kuwa yeye ndio chanzo cha matatizo na hata kama mwanae angepatwa na jambo baya,basi yeye ndiye aliyemsababishia.Alijikuta akisononeka sana moyoni hasa baada ya kumuona mkewe akizidi kulia kwa kuomboleza.
“Mke wangu jikaze jamani,unavyolia anamchulia mwanetu,atapatwa na matatizo bure,yote tumwachie Mungu”

Mzee Rwakatare alijifanya kuongea kwa busara.Bi Patricia hakuamini kusikia maneno kama yale kutoka kwa mumewe.Ilibidi ainue macho na kumtazama usoni kwa mshangao,alihisi mumewe anamkejeli kwani tangu aachishwe kazi hakuwahi kulitaja jina la Mungu kutoka kinywani mwake zaidi ya matusi ambayo sasa alishaanza kuyazoea.

Waliendelea kutazamana kwa muda mrefu huku kila mmoja akiwa kimya.Masaa yalizidi kuyoyoma na hatimaye saa ya ukutani ikawa inasoma saa sita za usiku. Bi patricia alishindwa kujikaza na akawa anaendelea kulia kwa kilio cha kwikwi.Pia alikuwa akisali kimoyomoyo akimuomba Mungu wake amnusuru mwanae Geneviv.
****
Manyunyu ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likitanda angani kuashiria mvua kubwa inataka kunyesha.Geneviv alizinduka kutoka usingizini baada ya kuona ameanza kuloana.Aliposhtuka mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa baridi kali ya usiku huku akiwa hajajifunika kitu chochote zaidi ya nguo alizokuwa amezivaa ambazo nazo zilikuwa zimechanwachanwa. Alijaribu tena kuinuka kutoka pale chini na safari hii alifanikiwa kusimama kwani maumivu yalikuwa yamepungua kidogo.Alijaribu kuinua mguu na kupiga hatua lakini akajikuta akishindwa kutembea.
“I must die hard, I need to move out of this place”
(lazima nife kigumu,nahitaji kuondoka mahali hapa)

Alijiambia Geneviv kimoyomoyo wakati akijikaza na kuanza kupiga hatua fupifupi kuelekea barabarani ambako aliamini anaweza kupata msaada.Japokuwa alikuwa akisikia maumivu makali alijitahidi kujikongoja kiupande-upande na akawa anajongea taratibu kuelekea upande iliko barabara. Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiongezeka na kuanza kuuloanisha mwili wake mchanga.Kadri manyunyu yalivyokuwa yanaongezeka na kumloanisha ndivyo Geneviv alivyozidi kupata nguvu ya kutembea na kuongeza mwendo. Baada ya kitambo kirefu akawa amefika barabarani.

Hakutaka kupoteza muda zaidi,akaanza kuifuata barabara akiwa haelewi anakoelekea. Hakutamani tena kurudi nyumbani kwao kwani chuki dhidi ya baba yake ilizidi kukua na kumfanya amchukie kama shetani. Akiwa bado anazidi kusonga mbele akielekea asikokujua,aliona mwanga wa taa za gari likija kutokea mbele yake.Hakujua ni gari gani na lilikuwa likielekea wapi ila akapiga moyo konde na kuamua kulisimamisha.

“Haroo afande hebu simamisha ‘Defender’ ,naona kama kuna rimutu rinasimamisha gari,sijui ni rinani na rimetokea wapi usiku wote huu Mura!”

aliongea Koplo Marugu kwa Kiswahili kibovu akimuamuru dereva wake kusimamisha gari.Walikuwa wako katika doria ya usiku pamoja na askari wengine watatu waliokuwa wamekaa nyuma ya gari.

Geneviv aliendelea kulipungia lile gari mikono kwa nguvu zake zote na taratibu akaanza kuliona likipunguza mwendo na kusimama karibu yake.
Liliposimama Geneviv akagundua kuwa lilikuwa ni gari la polisi,alishusha pumzi ndefu na kumshukuru Mungu wake kwani aliamini angekuwa salama mikononi mwa wanausalama wale.Hakutaka kuwaambia ukweli wa kilichomtokea kwani alijisikia vibaya kueleza kuwa amebakwa kwani alihisi ni aibu kubwa kwake.Akaamua kutunga uongo…

Baada ya lile gari kusimama,askari walishuka na kuanza kumhoji ametoka wapi na anakwenda wapi usiku wote ule,ukizingatia yeye ni mtoto wa kike na hapo alipo ni porini.
“Tulikuwa tumetoka shambani na dada,tukavamiwa na watu walioanza kutupiga mpaka wakanichania nguo.Dada alikimbia na kuniacha peke yangu huku.”

Geneviv aliongea uongo mtakatifu huku akitoa machozi na kuwafanya wale askari waamini alichokuwa anakisema.Bila hata kumhoji maswali mengi,walimpakia ndani ya Defender na kuanza kurudi naye mjini ambapo alielezwa kuwa atapewa sehemu ya kulala mpaka asubuhi ambapo ataandikisha maelezo yake kituoni ili watuhumiwa waanze kusakwa.Hakuna hata mmoja aliyehisi kuwa maelezo ya Geneviv ni uongo.

Gari likawashwa na kuanza kurudi mjini.Muda mfupi baadae tayari walikuwa wameshafika kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ambapo Geneviv alikabidhiwa kwa askari wawili wa kiume waliokuwa zamu na wale polisi wengine wakaendelea na doria. Wale askari walimpokea Geneviv na kumuweka kaunta,huku wakijifanya kumuonea huruma. Walimuonyesha sehemu ya kukaa na wao wakaendelea na shughuli zao.

“Haloo afande haka kabinti ni kazuri mno,hebu kaangalie vizuri”
wale askari walikuwa wakinong’onezana kwa sauti ya chini na mara wote wakaanza kumtolea macho Geneviv ambaye alikuwa ameanza kusinzia pale alipokaa na hakuwa na habari kama wale askari wanamtazama kwa macho ya husda.

“Aisee kweli bwana,unajua nilikuwa sijakaangalia vizuri…halafu unajua mke wangu alisafiri wiki ya pili sasa…natamani niwe fataki japo kidogo tu!”

Waliendelea kunong’ona wale askari na wakajikuta wakicheka kwa pamoja na kugongesheana mikono.Kelele za vicheko zilimshtua Geneviv aliyekuwa anasinzia kwenye kiti alichokuwa amekalia.
Mmoja kati ya wale askari aliinuka na kumfuata pale alipokuwa amekaa na kumshika begani.

“Binti naona umechoka sana, pole! amka basi nikakuonyeshe sehemu ya kulala,usiwe na wasiwasi hapa uko mikononi mwa chombo cha dola…tutakulinda mpaka asubuhi”
Aliongea yule askari akimshika mkono Geneviv na kutoka nae nje ya jengo la kituo cha polisi. Geneviv hakuwa na wasiwasi kwani aliamini kazi ya jeshi la polisi ni kuwalinda raia wake. Wakatoka na kuelekea kwenye kibanda kidogo kilichokuwa mita chache pembeni.

****

Hakuna hata mmoja kati ya Mzee Manuel Rwakatare na mkewe Bi Patricia aliyepata hata tone la usingizi. Mpaka inagonga saa nane usiku, Geneviv alikuwa hajarejea nyumbani na hakukuwa na dalili za yeye kurudi. Bi Patricia alikuwa akizidi kulia hali iliyomfanya aanze kuhisi maumivu makali ya kichwa kwani alikuwa bado hajapona. Baada ya kuona mkewe hataki kutulia, ilibidi mzee Rwakatare ajiandae kwenda kutoa taarifa polisi usiku huohuo. Na yeye alionekana kuchanganyikiwa mno, akawa anajilaumu kwa yote aliyoyafanya ambayo ndiyo yaliyopelekea kuibuka kwa tatizo hilo.

Alipiga moyo konde na kujifariji kuwa hakuna binadamu asiyekosea. Baada ya kumaliza kujiandaa alimuaga mkewe ambaye hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kumwaga machozi.Alitoka na safari ya kuelekea kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ikaanza. Ilimbidi abebe mwamvuli kwani mvua nayo ilikuwa imechachamaa kunyesha.Baada ya safari ya takribani dakika arobaini, tayari alishawasili kwenye eneo la kituo cha polisi.

Tangu asimamishwe kazi serikalini,Mzee Rwakatare alikuwa hapendi kabisa kuonekana na polisi kwa kuhofia kukamatwa kwa makosa yake ya uhujumu ambayo bado upelelezi ulikuwa unaendelea, lakini kwa sababu ya mwanae alijikuta hofu ikimuishia. Akawa anapiga hatua za taratibu kusogelea eneo la kituo.

Akiwa hatua chache kabla ya kuufikia mlango mkubwa wa kuingilia kituoni,alisikia sauti ambayo ilimfanya mapigo ya moyo yaanze kumwenda kasi mithili ya injini ya jeti.

Ilikuwa ni sauti ambayo aliitambua vizuri kuwa ni ya mwanae Geneviv ikitokea kwenye kibanda kidogo pembeni ya kituo cha polisi.
Geneviv alikuwa akilalama kwa maumivu makali aliyokuwa anayapata wakati yule askari aliyejifanya kumpeleka kulala akimuingilia kimwili kwa nguvu. Kwa mara nyingine tena, Geneviv alikuwa akibakwa,tena safari hii na Askari polisi.

Mzee Rwakatare hakutaka kuyaamini masikio yake kuwa ile sauti kweli ilikuwa ni ya Geneviv.Ikabidi asogee mpaka karibu ya kile kibanda na kuchungulia ndani kupitia tundu dogo chini ya dirisha.
Hakuyaamini macho yake kwa alichikiona…

“Sh*t, what the hell are you doin with my daughter…im gonna kill you!”
Mzee Rwakatare aliongea kwa hasira kali, na kwa nguvu zake zote aliukanyaga mlango wa kile chumba na kuingia ndani mzima-mzima.

Yule askari alishtuka kuona mlango ukivunjwa na kumharibia starehe yake.Akawa anahangaika kuvaa suruali yake vizuri.
Mzee Rwakatare alimuwahi kwa kipigo kikali cha kushtukiza mpaka yule askari akadondoka chini.Alipotazama pembeni alikiona kipande cha bomba la chuma kilichokuwachini. Alikiokota na kuanza kumuadhibu vikali yule askari kichwani mpaka akazimia.

Kwa haraka alimuinua mwanae Geneviv ambaye bado alikuwa akilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata huku damu ikimchuruzika kutoka katikati ya miguu yake.Alimuweka begani na akatoka naye kwa spidi ya ajabu na kuanza kukimbia nae kutokomea gizani.

Hakuna askari aliyeelewa kinachoendelea.Mvua nayo ilikuwa ikizidi kupamba moto na sasa zilianza kusikika radi kali zikipiga na kuufanya usiku uzidi kutisha.Mzee Rwakatare hakujali kitu,akawa anazidi kutimua mbio huku Geneviv akiwa begani.
Akiwa umbali wa mita kadhaa,alishtukia kuona anamulikwa na taa za gari lililokuwa likiingia kituo cha polisi. Kwa haraka akamrusha Geneviv chini na yeye akarukia pembeni ya barabara kwenye mtaro.

Kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha ikiambatana na ukungu,hakuna mtu yeyote kutoka kwenye lile gari aliyewaona.
Gari ambalo aliligundua kuwa ni la polisi likapita na kuingia pale kituoni.Kwa haraka aliinuka na kumnyanyua mwanae na kumuweka tena begani.Akawa anatimua mbio kurudi nyumbani kwake, safari hii akipitia njia za vichochoroni kukwepa kuonekana tena na polisi.Baada ya kama nusu saa akawa ameshafika nyumbani kwake. Geneviv alikuwa akiendelea kulalama kwa maumivu na hakuelewa kilichofuatia mpaka alipojikuta anaingizwa ndani mwao.

Bi Patricia alishtuka kusikia mlango ukigongwa.
“Nini tena jamani?” Bi Patricia aliuliza kwa sauti iliyokauka kutokana na kulia, na akawa anajikongoja kwa uchovu kwenda kufungua mlango. Alishakata tamaa ya kumuona mwanae Geneviv usiku huo.

“Fungua mke wangu!”
Aliongea mzee Rwakatare kwa sauti iliyomaanisha kuna jambo. Bi Patricia aliharakisha kufungua mlango.
“Ooooh My God!.....”
Bi Patricia alishtuka kupita kiasi.

MY HEART IS BLEEDING (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU)-2

Kijana mdogo anapandishwa kizimbani akishtakiwa kwa kosa la kuua watu wengi kwa mikono yake. Ushahidi ulishakamilika siku nyingi zilizopita kwani mshtakiwa aljisalimisha mwenyewe mikononi mwa Polisi wa kimataifa (Interpol) akiwa na vithibitisho vyote vya namna alivyoendesha mauaji yale makubwa na ya kutisha yaliyoifanya nchi nzima kuzizima kwa hofu.

Pamoja na kukutwa na hatia, mahakimu wote waliokuwa wakipangiwa kusikiliza kesi yake, walikuwa wakijitoa katika hatua za mwisho kila mmoja akitoa sababu zake binafsi. Mwishoni jaji mkuu, Profesa Kadir Mudhihir Simba anaamua kuingilia kati na kuisikiliza mwenyewe kesi ile. Hapo ndipo anapogundua kuwa kesi ile ni ngumu kupita kawaida. Ni kweli kwamba kuua ni kosa kubwa kisheria(murder), lakini sababu zilizomfanya kijana huyu mdogo kuua ndio swala lililoleta utata.

Kila mtu sasa anaanza kuwa na shauku ya kutaka kujua nini chanzo cha mauaji yale. Je ni sababu gani zilizomfanya kijana huyu mdogo kuua? Nini hatma yake? Atahukumiwa kunyongwa, kifungo cha maisha au ataachiwa huru?
Twende pamoja katika safari ndefu ya kuutafuta ukweli.
***************************
Profesa Kadir Mudhihir Simba ni hakimu mwenye uzoefu wa siku nyingi katika medani ya siasa. Alikuwa na ujuzi na utaalamu wa kutosha katika kutoa hukumu za kesi ngumu, kesi zilizoonekana kushindikana au zenye utata. Watu wote walimwamini kwani mara zote hukumu alizokuwa anazitoa zilikuwa ni zenye kuzingatia sheria na haki. Uwezo wake mkubwa wa kuchambua mambo kwa kina na busara alizokuwa nazo, vilimfanya ateuliwe kuwa jaji mkuu miaka kumi na mbili iliyopita.

Pamoja na sifa hizo zote alizokuwa nazo, kesi hii ilionekana kumchanganya sana kichwa chake na kumkosesha sana raha kiasi cha kumfanya asite kutoa hukumu. Upelelezi ulishakamilika muda mrefu kwani mshtakiwa alijisalimisha mwenyewe mikononi mwa polisi akiwa na vithibitisho vyote vya namna alivyofanya mauaji hayo makubwa na ya kutisha.

Hakukuwa na sababu yoyote ambayo ingezuia hukumu kutolewa siku hiyo, Lakini bado jaji mkuu alionekana kupoteza mwelekeo. Alitamani aiahirishe kesi ile mpaka siku nyingine, lakini alihofia kupoteza heshima ambayo alijijengea kwa raia. Sasa aligundua ni kwa nini mahakimu wote saba walioteuliwa kuisikiliza kesi ile walikuwa wakijitoa katika hatua za mwisho.

Aligeuza shingo kumtazama mshtakiwa, kisha wazee wa mahakama na mwisho umati uliokuwa umeijaza mahakama ile. Kwa mara ya kwanza tangu aanze kazi miaka mingi iliyopita, aliuhisi ugumu uliokuwa mbele yake. Japokuwa alikuwa amevaa miwani, macho yake yalionyesha dhahiri jinsi alivyokuwa akibabaika. Usingeweza kuamini kuwa huyu ndio yule jaji mkuu, Profesa Kadir Mudhihir Simba wa siku zote.

Ni kweli kabisa kwamba kuua, kwa kukusudia au bila kukusudia ni kosa kubwa mbele ya sheria, lakini sababu zilizomfanya kijana huyu mdogo kufanya mauaji makubwa kiasi kile ndilo swala lililoleta ugumu.

Jasho lilianza kumtoka kiasi cha kuamuru madirisha yote yafunguliwe na viyoyozi vyote vya mle mahakamani viwashwe. Baada ya kubabaika kwa muda mrefu, hatimaye alipiga moyo konde na kuanza kutoa hukumu.
“Kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi ya mwaka 1962, ibara ya kwanza ya makosa dhidi ya ubinadamu, kifungu kidogo cha kwanza,umepatikana na hatia ya kuua idadi kubwa ya watu kwa kukusudia. Baada ya mahakama kuridhishwa na ushahidi uliowasilishwa dhidi yako, Una..unahukum… unahu……ku……mi……w……”

Hakuna aliyeamini kilichotokea! Jaji mkuu alianza kubabaika na kushikwa na kigugumizi kikali huku jasho jingi likimtoka kama maji. Mwili wote ulikuwa umeloanishwa kwa jasho na sasa akawa anatetemeka mwili mzima. Alijitahidi kujikaza ili aendelee kusoma hukumu lakini alishindwa. Watu walikuwa wamepigwa na butwaa wakiwa wanashangaa kilichomsibu jaji yule. Alizidi kutetemeka mwili mzima na kuazna kuzitupa hovyo karatasi za jalada la hukumu na mara akadondoka kutoka kwenye kiti alichokuwa amekaa mpaka chini, kisha akawa anaporomoka kwenye ngazi. Hakika hii ilikuwa kali ya kufunga mwaka.

Ungeweza kudhani kama yanayotokea mle mahakamani ni viini macho au miujiza, lakini haikuwa hivyo. Akiwa pale chini alianza kutupa mikono na miguu huku povu lililochanganyikana na damu likimtoka puani na mdomoni. Ungeweza kuhisi anataka kukata roho. Umati wote wa watu waliokuwa mle mahakani , ulipigwa na bumbuwazi kwa mshtuko mkubwa walioupata. Ilibidi makarani wa mahakama wafanye kazi ya ziada kwa kusaidiana na watu wa huduma ya kwanza.

Waliwahi kumuinua pale chini na kumkimbiza nje akiwa juu ya machela, na muda mfupi baadae gari la wagonjwa likawa linakimbia kwa mwendo wa kasi kumuwahisha Hospitali. Mtuhumiwa bado alikuwa ametulia kizimbani na yeye akiwa amepigwa na bumbuwazi kwa yale yaliyokuwa yametokea.

Watu wakaanza kukanyagana kila mmoja akitaka ashuhudie kinachoendelea nje ya mahakama. Askari waliokuwa wamejaa mle mahakamani walifanya kazi ya ziada kuhakikisha mtuhumiwa anarudishwa gerezani. Eneo lote likazingirwa na taharuki huku hali ikiwa tete na ya kuogopesha. Polisi walifanya kazi yao kikakamavu na kuhakikisha hakuna madhara makubwa yanayotokea pale mahakamani.

Muda mfupi baadae habari kutoka Hospitali kuu ya Blaziniar zilieleza kuwa hali ya afya ya jaji Mkuu Profesa Kadir Simba ilikuwa ikizidi kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa ukienda. Kwa mujibu wa Daktari mkuu Shyroze Mahiza aliyoitoa kwa vyombo vya habari, jaji mkuu alikuwa amepatwa na mshtuko wa moyo na kusababisha mishipa ya damu iliyoko kichwani kupasuka na kuvujisha damu kwenye ubongo.

Kitaalamu hali hii iliitwa “Venule Rapture due to Hypertension Bp”, na husababisha mtu kupoteza fahamu kwa muda mrefu. Hayo ndiyo yaliyokuwa yamemtokea jaji Simba kwani aliendelea kuwa katika hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu sana.

Kila aliyemfahamu alimuonea huruma kwa yaliyompata na kila mtu akawa anajiuliza nini kimesababisha hali kama ile itokee. Kila mtu aliongea lake kwani jambo kama hilo halikuwahi kutokea hata mara moja katika historia ya nchi. Wengine waliliona kama muujiza huku wengine wakilihusisha na imani kali za kishirikina. Hali hiyo ilizua hamu na shauku ya watu kutaka kufahamu yule kijana mdogo ni nani na alikuwa ameendesha mauaji yake kwa sababu gani na katika mazingira gani. Uchunguzi wa kina ukaanza kufanywa ili kuupata uhalisia wa kesi ile.

MANY YEARS AGO-MIAKA MINGI ILIYOPITA
Khalfan Mwalukasa alikuwa ni mzaliwa wa mkoa wa Nyanda, uliopo kusini mwa nchi ya Blazinia. Alikuwa ni mtoto wa kipekee katika familia yao, na akiwa bado kijana aliamua kuondoka nyumbani kwa wazazi wake na kwenda kujaribu kutafuta maisha katika nchi jirani ya Tanzania. Hata hivyo alipofika Tanzania aligundua kuwa maisha yalikuwa magumu zaidi kuliko kwao Blazinia.

Alichokifanya aliamua kwenda kwenye visiwa vya jirani vilivyokuwa vikipakana na nchi yake, visiwa vya Banaland vilivyokuwa katika bahari ya Hindi. Visiwa hivi vilikuwa ni sehemu ya nchi yake hivyo hakukuwa na haja ya kuwa na Passport au viza ya kusafiria. Ilimgharimu kiasi kidogo tu cha pesa kupanda meli na siku chache baadae akawa tayari ndani ya visiwa vya Banaland.

Kwa kuwa kilichomtoa kwao na kukimbilia ugenini ilikuwa ni kutafuta ahueni ya maisha , hakutaka kuchagua kazi kwani hata hivyo hakuwa amejaaliwa kusoma kutokana na wazazi wake kuwa na hali duni ya kimaisha. Alijiwekea dhamira ya kufanya kazi yoyote ambayo ingepatikana ilimradi tu imuingizie kipato. Bahati nzuri alipata kazi ya kuuza genge la mbogamboga na matunda.

Moyo wa kujituma, heshima kwa wakubwa na wadogo na busara alizokuwa nazo vilimfanya aweze kuishi kwa amani japokuwa alikuwa mbali na wazazi wake. Muda mfupi baadae alifanikiwa kufungua biashara yake mwenyewe na akaanza rasmi kujitegemea. Alifanikiwa kupanga chumba kimoja mitaa ya uswahili na taratibu akaanza kutengamaa kimaisha.

Mara zote alikuwa akijikumbusha kuwa kilichompeleka pale ilikuwa ni kutafuta maisha, aliahidi kufanya kila alichoweza ili afanikiwe maishani ikiwa ni pamoja na kujiepusha na mambo ambayo alihisi yangezuia ndoto zake.

Baada ya takribani mwaka mmoja kupita, alikuwa ameshajijengea jina miongoni mwa wafanyabiashara wa mbogamboga na matunda. Aliipenda kazi yake, na faida ndogo aliyokuwa akiipata alikuwa akitumia vizuri na kujiwekea akiba. Wateja wake wengi walikuwa ni wanawake lakini kwa kuwa alikuwa akifahamu alichokuwa anakifanya, hakujihusisha nao zaidi ya uteja wa kawaida.

Miongoni mwa wateja wake, alikuwepo binti mmoja aliyekuwa na asili kama ya mchanganyiko wa damu mbili tofauti. Alionekana kuwa na mchanganyiko wa kibantu na watu wa visiwa vya ushelisheli. Mchanganyiko huu ulimfanya awe na mvuto wa kimahaba kuliko wasichana wengine wa rika lake.

Miriam, tofauti na wateja wengine, alikuwa akipenda sana kupiga stori na Khalfan Mwalukasa. Hata baada ya kuhudumiwa kila alichokuwa akihitaji, bado alikuwa akifurahia kuendelea kuongea na Khalfani bila kujali kama alikuwa akichelewa nyumbani kwao.

Japokuwa alishindwa tu kueleza wazi hisia zake, Miriam alitokea kumpenda Khalfani Mwalukasa lakini alishindwa kumwambia bayana kwa hofu ya kueleweka vibaya. Akawa anaendelea kuumia mtimani siku hadi siku huku akijitahidi kumuonyeshea kwa vitendo kuwa alimhitaji awe baba wa watoto wake. Khalfani Mwalukasa alishaelewa kilichokuwa mawazoni mwa mteja wake Miriam, lakini hakutaka kuwa na papara hasa ukizingatia kilichompeleka kule ilikuwa ni kutafuta maisha na sio mapenzi.

Pamoja na kujifanya mgumu, Khalfani naye alijikuta taratibu akianza kuvutiwa na urembo wa binti Miriam aliyekuwa na haiba ya kike haswaa…mrefu kama twiga, uso wake wa duara ukiwa umepambwa na macho madogo ambayo muda wote yalikuwa kama yana usingizi, huku sura yake ikiwa imejawa na tabasamu tamu muda wote. Taratibu alijikuta uzalendo ukimshinda na mara wakajikuta tayari wamezama kwenye dimbwi la mahaba.

“Khalfani hivi kweli utanioa? Au ndio unataka kunitumia mwisho uniache niteseke?”
Miriam alikuwa akimuuliza huku sauti yake ikwa imejawa na huba.
“Ningependa uwe wangu wa maisha Miriam, lakini hali yangu nadhani we mwenyewe unaiona…itakuwa ni maajabu kwa muuza mboga kumuoa mtoto wa milionea kama wewe, haitawezekana”

Khalfani alikuwa akijitetea mbele ya Miriam, lakini baada ya mazungumzo marefu, Miriam alimtoa wasiwasi kuwa yeye hakuhitaji chochote kutoka kwake, zaidi ya kumhitaji awe baba watoto wake bila kuzingatia hali yake ya kimaisha wala kipato.

Moto wa mapenzi ukaanza kukolea kwenye mioyo ya wawili hawa na baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, hatimaye Miriam alimpeleka “mumewe mtarajiwa” kumtanbulisha kwa wazazi wake. Miriam alikuwa akiishi na wazazi wake wote wawili, Mzee Nurdin Shamsi na mkewe. Walibarikiwa kuwa na maisha mazuri ya kitajiri, utajiri ambao ulitokana na biashara aliyokuwa anaifanya mzee Nurdin Shamsi ya madini ya Ruby. Alikuwa akinunua Ruby kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo na kuisafirisha mpaka nchi za uarabuni (U.A.E). Biashara hiyo ilimuingizia pesa nyingi sana zlizomuwezesha yeye na familia yake kuwa na maisha ya juu.

Alifanikiwa kujenga nyumba nzuri ya kifahari pembezoni mwa fukwe za bahari ya Hindi alikokuwa akiishi na familia yake. Alinunua pia eneo kubwa kuzunguka nyumba yake, alilolipendezesha kwa bustani nzuri za maua, viunga vya minazi na karafuu. Eneo zima lilikuwa likipendeza mithili ya Edeni ndogo.

Baada ya kutambulishwa kwa wazazi wa Miriam, Khalfani Mwalukasa aliendelea kuonyesha nidhamu na heshima ya hali ya juu kwa kila mtu, hali ambayo iliwavutia sana wazazi wa Miriam na kuwafanya wamkubalie kwa moyo mkunjufu kumposa binti yao.

Baada ya kutoa posa, taratibu za ndoa zilianza kuandaliwa na siku chache baadae Khalfan Mwalukasa akawa mume halali wa Miriam Shamsi. Wakayaanza maisha mapya ya ndoa. Kwa kuwa umri wa mzee Shamsi na mkewe ulikuwa umekwenda, na Miriam ndio alikuwa mtoto wao pekee, kitendo cha yeye kuolewa na kwenda kuishi kwa mumewe kiliwafanya wawe wapweke sana. Ikabidi mzee Shamsi amshawishi Khalfan Mwalukasa na mkewe wahamie katika jumba lao la kifahari ili waendelee kuishi wote pamoja. Khalfani alijadiliana na mkewe na wakakubaliana kuhamia nyumbani kwa kina Miriam (Ukweni).

Khalfani akayaanza maisha mapya ndani ya jumba la kifahari, maisha ambayo hakuwahi kuyaota. Alikuwa amebadili sana mazingira, kutoka kuwa muuza mboga na matunda akiishi uswahilini, mpaka kuwa mume wa binti tajiri akiishi ndani ya paradiso ndogo. Alimshukuru Mungu wake na kuahidi kuwa atampenda mkewe kwa moyo wake wote.

“Daima nitakuenzi mke wangu, na kamwe sitakufanya utoe machozi ya uchungu, bali utatoa machozi ya furaha”
Khalfan alikuwa akimpa maneno matamu ya huba mkewe jioni moja wakiwa wameketi kwenye moja ya bustani nzuri zilizokuwa ndani ya kasri la mzee Shamsi. Ndoa yao changa ikatawaliwa na upendo na mahaba ya dhati.

Victory over the world!

Grace and peace to you from God our Father and the Lord Jesus Christ, who gave himself for our sins to rescue us from the present evil age, according to the will of our God and Father

Galatians 1:3,4 NIV

__________________

I have given them thy word; and the world hath hated them, because they are not of the world, even as I am not of the world. I pray not that thou shouldest take them out of the world, but that thou shouldest keep them from the evil. They are not of the world, even as I am not of the world. Sanctify them through thy truth: thy word is truth.

John 17:14-17 KJV

__________________

For whatever is born of God overcomes the world; and this is the victory that overcomes the world, our faith. Who is it that overcomes the world but he who believes that Jesus is the Son of God?

1 John 5:4,5 RSV

__________________

Thanks be unto God for His wonderful gift:
Jesus Christ, the only begotten Son of God
is the object of our faith; the only faith
that saves is faith in Him.

Monday, October 12, 2009


HOLLY SCRIPTURES
So the LORD God said to the serpent, "Because you have done this, "Cursed are you above all the livestock and all the wild animals! You will crawl on your belly and you will eat dust all the days of your life. And I will put enmity between you and the woman, and between your offspring and hers; he will crush your head, and you will strike his heel."

Genesis 3:14,15 NIV

Eternal Life...Only One Way

"For God so loved the world that he gave his one and only Son, that whoever believes in him shall not perish but have eternal life. For God did not send his Son into the world to condemn the world, but to save the world through him. Whoever believes in him is not condemned, but whoever does not believe stands condemned already because he has not believed in the name of God's one and only Son.

This is the verdict: Light has come into the world, but men loved darkness instead of light because their deeds were evil. Everyone who does evil hates the light, and will not come into the light for fear that his deeds will be exposed. But whoever lives by the truth comes into the light, so that it may be seen plainly that what he has done has been done through God."

John 3:16-21 NIV

Sunday, October 11, 2009


JOIN MY WORLD OF TEARS BY READING THESE TWO STORIES, "SHED NO MORE TEARS GENEVIV!" AND "MY HEART IS BLEEDING!"
AUTHOR- AZIZ HASHIM
...all rights reserved

 

SHED NO MORE TEARS GENEVIV… USILIE TENA GENEVIV

Na Aziz Hashim-Hash power


UTANGULIZI
Geneviv ni binti mdogo ambaye amezaliwa katika familia yenye maisha mazuri sana.Mungu amemjaalia kuwa na sura nzuri yenye mvuto.Bahati mbaya kuzaliwa kwake akiwa na sura nzuri na urembo usio na kifani kunamfanya apate mateso makubwa sana kutoka kwa wanaume ambao kila mmoja akiwemo hata baba yake mzazi wanamtumia kimapenzi na baadae kumuacha akipata mateso makubwa mno.

Uzuri ambao Mungu alimjaalia unageuka kuwa sumu kali ambayo inammaliza taratibu mpaka anakaribia kupoteza uhai wake, akiwa katika hatua za mwisho kabisa za uhai wake.Ni mateso,maumivu, machozi,majeraha mtimani na kilio ndivyo vinavyotawala maisha yake.Anaichukia dunia,anawachukia wanaume…hawezi kulipa kisasi,anachoweza kufanya ni kutoa machozi muda wote,analia lakini hakuna anayemsikia! Anapokaribia kukata pumzi anasikia sauti ikimfariji…Shed no more tears Geneviv!

Ungana nami ufahamu mkasa mzima
SEHEMU YA KWANZA
Ilikuwa ni alfajiri tulivu,miale ya jua ikianza kuchomoza kwa mbali kuashiria mwanzo wa siku mpya,siku ya jumatatu.Milio ya ndege wa angani waliokuwa wakiimba na kurukaruka kutoka tawi moja hadi tawi jingine juu ya miti waliufanya mwanzo wa siku uwe wakuvutia sana.Jua lilikuwa likizidi kuchomoza huku nuru yake ikilifukuzia mbali giza la alfajiri.Wakati kukizidi kupambazuka,upande wa pili alikuwepo binti mdogo aliyekuwa amejilaza chini ya mti mkubwa,mahali ambapo yamekuwa makazi yake kwa muda mrefu sasa,akishinda kutwa nzima akiwa amejilaza chini kivulini na giza likiingia alikuwa akilala na kujifunika kipande cha gunia palepale mpaka asubuhi.Mwili wake wote ulikuwa umejawa na vidonda vilivyokuwa vinatoa usaha na kumsababishia maumivu makali kupita kiasi.Harufu kali ya majeraha yaliyokuwa yakiendelea kuuozesha mwili wake na harufu ya haja kubwa aliyokuwa anajisaidia hapo hapo, vilipafanya pale chini ya mti panuke mithili ya mzoga wa mnyama aliyejifia.
Binti yule mdogo hakuwa na msaada wowote,hakuweza hata kuinuka kutoka pale chini alipokuwa amelala…alichoweza ilikuwa ni kufumba na kufumbua macho na kufukuza nzi waliokuwa wakivizonga vidonda vyake.Alishakata tamaa ya kuishi na alionekana kama anayengojea pumzi yake ya mwisho ikatike aondokane na mateso makali yaliyokuwa yanamuandama.Kwake maisha yalipoteza maana kabisa,aliichukia dunia na vyote vilivyomo ndani yake.Mara kwa mara alikuwa akimkufuru Muumba wake kwa kumsababishia mateso makali kiasi kile kwani aliamini anateseka kwa sababu Mungu alimuumba akiwa mrembo kupita kiasi. Aliamini anapata mateso makali kiasi kile kwa sababu ya uzuri wake aliopendelewa na Mungu,na huo ndio ulikuwa ukweli.Miaka michache tu aliyoishi duniani ilikuwa ni kama karne nzima kwani alipitia mateso makubwa sana ambayo kama angepata nafasi ya kuusimulia ulimwengu hakika kila mtu angemwonea huruma na kudondosha machozi.Aliendelea kuwaza akiwa amelala pale chini huku macho yake yakilitazama jua lililokuwa linazidi kuchomoza na kuanza kuwa kali.
Dunia aliiona kama shimo la hewa na zaidi aliwachukia wanaume.Aliapa kuwa kama angepata nafasi ya kulipa kisasi,angewateketeza wanaume wote duniani.Aliamini wanaume ni mashetani kwa waliyomfanyia na akazidi kukufuru dini kwa kumlaumu Mungu kwa kuwaumba wanaume.
“ I hate the world,I hate men…”
alijisemea Geneviv pale chini alipolala kwa sauti ya kunong’ona.

Kumbukumbu zake zilimrudisha nyuma alipokuwa bado mdogo.
Aliyakumbuka maisha ya furaha aliyoishi na familia yake kabla mambo hayajaanza kubadilika.Alishindwa kuyazuia machozi ambayo yalianza kuuloanisha uso wake mchanga uliochakazwa na mateso… soo many tears…hakika alitia huruma.

Geneviv alikuwa ni mtoto wa kipekee kwenye familia ya mzee Manuel Rwakatare na Bi. Patricia mahiza.Alizaliwa kwenye familia yenye uwezo mkubwa kifedha, baba yake akiwa ni Afisa utumishi katika wizara ya Madini na nishati huku mama yake akiwa Katibu Muhtasi katika ofisi ya waziri mkuu wa Nchini Blaziniar.Tangu anazaliwa maisha yalikuwa mazuri kupita kiasi huku wazazi wake wakijitahidi kumpatia kila alichokihitaji.Waliishi kama wako peponi huku pesa kwao ikiwa sio tatizo.
Uzuri aliojaaliwa Geneviv ulianza kuonekana tangu akiwa mdogo hali ambayo ilizidi kuwaongezea fahari mzee Rwakatare na mkewe.Kila aliyemuona mtoto Geneviv alishindwa kujizuia kumsifia.Sura yake iliyokuwa na mchanganyiko safi wa baba na mama ulizidi kumfanya aonekane kama malaika…

“you have beared a very cute angel sir,congrats!”
(umezaa mtoto mzuri sana mzee,hongera sana)
Hiyo ilikuwa ni kauli kutoka kwa mmoja kati ya wafanyakazi wenzake mzee Rwakatare akimsifia kwa kuzaa mtoto mzuri kiasi kile.
Bi Patricia naye alikuwa akipokea sifa kila alipopita na mwanae hali iliyozidi kumpa kichwa na kumfanya ajione kama mama wa malaika.

”Atawasumbua sana vijana wa kiume akikua huyu,kama wewe ulivyonisumbua kipindi nakutafuta darling…”
Mzee Rwakatare alimtania mkewe wakati wakipata chakula cha jioni na mtoto wao Geneviv.Bi Patricia alitabasamu huku akimbusu mumewe shavuni.
Siku zikawa zinasonga kwa kasi huku Geneviv akizidi kukua na kupendeza zaidi, urembo wake ukizidi kujionyesha dhahiri hali iliyomfanya aonekane tishio mbele ya kila aliyemtazama.
Alipotimiza miaka saba wazazi wake wakaona bora wamuanzishe shule.Akatafutiwa shule nzuri yenye hadhi ya kimataifa, st Benard Blaziniar academy,shule iliyokuwa ikisifika kwa kutoa elimu bora kwa nadharia na vitendo.Baada ya taratibu zote kukamilika Geneviv akaanza shule.Aliahidi kwa wazazi wake kuwa atasoma kwa bidii mpaka afike chuo kikuu.

“I want to be a doctor daddy! I want to heal the world…”
(Nataka kuwa daktari baba,nataka kuuponya ulimwengu)
Geneviv alikuwa akimwambia baba yake asubuhi wakiwa ndani ya gari lao akimpeleka shule.

“Sure! Go for it and you can be what you you want to be”
(Hakika utakuwa kama unavyotaka kuwa ukijipangia malengo vizuri na kuyatekeleza)

Mzee Rwakatare alikuwa akimtia ujasiri bintiye kuwa anaweza kuwa daktari ikiwa atajiwekea malengo madhubuti ya kusoma kwa bidii.
“Let education be your only heritage daughter coz when everything has gone the future still remain dark”
(Ikazanie sana elimu ndio iwe urithi pekee maishani mwako, vitu vyote vitakapopita, maarifa yatabaki kuwa mwanga pekee wa maisha yako)

Baada ya kumfikisha shule,Geneviv alipokelewa na mwalimu na kuelekezwa utaratibu wa Shule.Ilikuwa ni furaha isiyo kifani kwa Geneviv kuanza shule.Alikuwa amechoka kufungiwa ndani kila siku,akaona huo ndio muda muafaka wa kuanza kufurahi na wenzake.Alijiwekea nadhiri ya kusoma kwa kadri ya uwezo wake wote ili azidi kuwafurahisha wazazi wake na kutimiza ndoto yake.
Baada ya siku chache tu tangu Geneviv ajiunge na Shule ya st Bernard Blaziniar, wanafunzi karibu wote na walimu walishamfahamu kutokana na uzuri aliojaaliwa.Wengine wakambatiza jina na kuanza kumuita “Cute Angel”. Usingepata shida kumtafuta kwani kila kona ya shule alifahamika. Akapata marafiki wengi huku wavulana anaosoma nao Grade one (darasa la kwanza) wakijigonga kila mmoja akitaka awe mchumba wake.
“Geneviv njoo tudimbedimbe mi niwe baba wewe uwe mama” aliongea mwanafunzi mmoja aliyeitwa Kim darasani na kusababisha darasa zima licheke.
Ukiacha uzuri na shani alivyokuwa navyo Geneviv,pia alitokea kuwa mwelewa “Bright” darasani hali ilyomfanya azidi kuwa kivutio kwa walimu wake na wanafunzi.
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda mbele umaarufu wa Geneviv ukawa unaongezeka.
Nyumbani nako hali ilizidi kuwa shwari huku baba yake mzee Manuel Rwakatare na mkewe bi Patricia wakizidi kuonyeshana mapenzi motomoto. Amani na upendo vikazidi kutawala ndani ya familia ya mzee Rwakatare hali iliyozidi kumpa furaha Geneviv.Akawa anazidi kukua vizuri kimwili, kiakili na kiroho, kwani alifundishwa pia kumcha Mungu.

****************************************

Katika kipindi hiki chote, baba yake alikuwa bado ni mfanyakazi wa wizara ya madini na nishati huku akipokea mshahara mnono na marupurupu yaliyomfanya aweze kuyamudu maisha ya familia yake kwa kiwango cha juu kabisa.Alianzisha vitega uchumi vingi nchini Blaziniar na katika nchi jirani ya Tanzania.Pamoja na kwamba alipata mshahara mkubwa na mke wake naye alikuwa akipokea mshahara mnono, bado siri ya utajiri wao uliokuwa unazidi kukua kila ilipoitwa leo haikufahamika.Kwa makadirio ya haraka ilitosha kusema kwamba mafanikio makubwa aliyokuwa nayo mzee Manuel Rwakatare yalizidi kipato chake halisi.
Mambo yakaanza kubadilika ofisini kwake mara baada ya Raisi mpya, mhe. James Kahungo “the JK”, kuingia ikulu ya Blaziniar.Raisi huyu mpya mwana mageuzi halisi aliwataka watumishi wote wa wizara zote nyeti kuorodhesha mali walizokuwa wanazimiliki na kueleza namna walivyozipata.

Tofauti na maraisi wengine ambao nao walikuwa wakitoa mkwara kama huo bila kusimamia utekelezaji, James kahungo alionyesha kudhamiria kiuhakika kuwapunguza wahujumu nchi.Miezi mitatu tu tangu aingie madarakani,watumishi zaidi ya mia tatu walisimamishwa kazi kwa kosa la ubadhirifu na kujilimbikizia mali kinyume na sheria ya nchi ya Blaziniar.

Kivumbi kikahamia kwenye wizara ya Madini na Nishati ambako uozo mkubwa ulifichuliwa wa hujuma nzito zilizokuwa zikifanyika.Mzee manuel Rwakatare, baba yake Geneviv naye akawa miongoni mwa waliokumbwa na Ufagio wa chuma.Alisimamishwa kazi baada ya kugundulika kuwa ameingiza hasara ya mamilioni ya pesa kwenye ofisi yake.Mahakama ikaamuru mali zake zote isipokuwa nyumba aliyokuwa anaishi zitaifishwe ili kufidia deni alilokuwa anadaiwa.
Ilikuwa vigumu sana kwa mzee Manuel Rwakatare kukabiliana na hali halisi.Alishazoea kucheza na mamiloni ya pesa,leo ghafla anafukuzwa kazi na mali zake zote kufilisiwa! hakutaka kuamini haraka kuwa ni kweli yamemkuta. Akaanza kuhangaika kwa waganga kutafuta ni nani aliyemloga bila mafanikio…akaanza pia kwenda kuroga usiku na mchana ili arudishwe kazini lakini wapi! Mwisho akajikuta akiishiwa mbinu. Mkewe bi Patricia akawa anajitahidi kumfariji mumewe na kumtuliza kwa maneno matamu lakini hgakufanikiwa.

“Mume wangu yote tumwachie mungu, mshahara wangu utatosha kutufanya tuishi vizuri na mwanetu atasoma bila shida, wewe kinachokuumiza ni nini? Calm down please my Huz, everything gonna be alright”
Bi patricia alikuwa akimbembeleza mumewe usiku baada ya kuona hali ya mumewe inazidi kuwa mbaya, chakula hali wala usingizi hapati.Pamoja na kujaribu kumfariji usiku kucha kila siku, bado haikusaidia kitu.Mzee Rwakatare alikuwa amekata tamaa kabisa…kila kitu kilipoteza maana kwake.Akaona njia bora ya kutoa mawazo na mfadhaiko ni kunywa pombe! Akaanza kidogokidogo kunywa pombe,kumbe ndio alikuwa anaongeza matatizo.

Maisha yakaanza kubadilika kwa kasi ya ajabu, kutoka kwenye umilionea hadi kwenye ufukara. Akiba ya Pesa zilizokuwa zimesalia akawa anazitumia kunywea pombe…”From Hero to Zero”

ndivyo wambea wa mitaani walivyoanza kumuita na kumbeza baada ya habari kuzagaa karibu kila kona ya nchi juu ya kufukuzwa kwake kazi.Ni katika kipindi hiki Geneviv alikuwa akijiandaa kufanya mtihani wa mwisho wa kuhitimu elimu ya msingi. Hakufahamu mara moja ni nini kimemtokea baba yake kwani muda mwingi alikuwa yuko shule akijiandaa na mitihani.
“Mama mbona dadii siku hizi haendi kazini?”
Geneviv aliuliza swali ambalo lilikuwa kama msumari wa moto kwa Bi Patricia. Ilibidi atumie uongo kumridhisha Geneviv kuficha aibu ya mumewe.
“Dadii yuko likizo mwanangu,ameamua kupumzika nyumbani”

Geneviv hakuridhika na jibu hilo lakini kwa jinsi alivyozisoma hisia za mama yake kwa haraka akajua lazima kuna kitu ambacho mama yake anamficha.Akauliza swali lingine ambalo nalo lilikuwa gumu…

“Lakini mbona siku hizi anachelewa sana kurudi nyumbani na akija anakuwa ananuka pombe…kwani ameanza lini kunywa Pombe? Mwalimu shuleni ametufundisha kuwa kunywa pombe ni vibaya na ni tabia hatarishi,sasa mbona baba ameanza kunywa?”
Geneviv alikuwa akiendelea kumshambulia mama yake kwa maswali mfululizo ambayo yote Bi. Patricia alishindwa kuyajibu.

“Basi mngoje akirudi umuulize mwenyewe maana mimi nashindwa kuyajibu.”

Alijitetea Bi Patricia na kabla hata hajamalizia ,wote walisikia mlango ukigongwa kwa nguvu,wakajua baba mwenye nyumba karudi.Geneviv akanyanyuka na kukimbilia mlangoni kwenda kumfungulia baba yake.
Tofauti na alivyozoea kumuona,mzee Rwakatare alikuwa tofauti kabisa,hali iliyomfanya Geneviv arudi nyuma kwa hofu…
“Whats wrong with you daddy?”
Aliuliza Geneviv kwa sauti iliyokuwa ikitetemeka kwa hofu.Mzee Rwakatare alikuwa amelewa kupita kiasi ,akishindwa hata kutembea vizuri kiasi cha kujiegemeza kwenye mlango kama mgonjwa,ile Geneviv anafungua tu mlango,mzee Rwakatare alidondokea kwa ndani na kuanguka sakafuni kama gunia …Puuh!

“Daddy! Are you sick? Mama njoo umuone daddy…”

alipaza sauti kwa nguvu Geneviv na kuanza kukimbilia ndani alikomuacha mama yake.Alikuwa ameshtuka kupita kiasi akidhani baba yake amepatwa na jambo baya.Hakujua kuwa Starehe ya pombe ndiyo iliyomfanya awe vile.
Hata kabla ya kumuona,Bi Patricia alishajua kilichomsibu mumuwe.Alichokifanya ni kumtuliza mwanae Geneviv ambaye alionekana kuchanganyikiwa,akampeleka chumbani kwake na kumsihi alale mpaka asubuhi na kumhakikishia kuwa baba yake hakuwa na tatizo lolote.Kweli Geneviv alikubali kulala kwa shingo upande huku maswali mengi yasiyo na majibu yakipishana kichwani mwake.

Baada ya kuhakikisha Geneviv ametulia Bi Patricia alirudi mlangoni na kumkuta mumewe akiwa bado palepale chini akikoroma kutokana na kuzidiwa na pombe.Kwa upole alimuinua na kumpeleka chumbani kwao.Alimvua nguo na kumpeleka bafuni ili angalau azinduke baada ya kuoga maji ya baridi.Kweli alifanikiwa kwani baada ya kummwagia maji mengi ya baridi Fahamu zilimrudia na pombe zikamuisha kichwani.Baada ya kumuogesha vizuri,Bi Patricia alimshika mkono mumewe na kumpeleka chumbani ambapo alimlaza vizuri na kumuacha apumzike.

Alipohakikisha kuwa kila kitu kimetulia Bi Patricia alienda chumbani kwa mwanae Geneviv.Alimkuta akiwa bado hajalala.Alikuwa amejikunja kitandani huku ameukumbatia mto wake.Aligundua namna mwanae alivyopatwa na mshtuko kwa kumuona baba yake katika hali ile.Akaamua kumfariji na kumfanya asahau kila kitu.Alianza kumfanyia utani kama walivyozoea kufanyiana kila siku na baada ya muda mfupi Geneviv alikuwa tayari ameshasahau yote yaliyotokea,wakawa wanacheka kwa furaha.

Kelele za vicheko zilimshtua mzee Rwakatare ambaye aliamka na kuanza upya kuvaa nguo.Japokuwa pombe ilikuwa imepungua lakini bado akili yake ilikuwa haijatulia.Alifikiri mkewe na mwanae wanamcheka yeye kwa sababu amelewa sana,kumbe haikuwa hivyo.Akajikuta hasira zikianza kumpanda na mara akainuka na kuanza kufoka kwa sauti. Bi Patricia aliposikia mumewe anafoka alitoka haraka na kumucha Geneviv akijiandaa kulala.Akawa anatembea kwa haraka kuelekea chumbani kwao, kabla hata hajafika akamuona mumewe akitoka kwa jazba chumbani.Wakakutana mlangoni…

”Mnachekacheka nini na mwanao? mnanicheka mimi sio? Sasa leo mtanijua!”
Aliongea kwa ukali mno mzee Rwakatare, akimfokea mkewe kama mtoto mdogo.Bi patricia alibaki ameduwaa akimshangaa mumewe.Tangu waoane karibu miaka kumi na tano iliyopita hakuwahi kumuona mumewe akiwa katika hali kama ile. Bila hata kusubiri mkewe ajitetee mzee Rwakatare akaanza Kurusha ngumi na mateke kama anapigana na mwanaume mwenzake.Mkewe akaamua kukimbilia chumbani bila ya kupiga kelele hata kidogo akihofia mwanae Geneviv angejifunza kitu kibaya.
Alipoingia chumbani alitaka kuwahi kujifungia kwa ndani lakini Mzee Rwakatare akamuwahi na kuusukuma mlango kwa nguvu.Akaingia na kuufunga mlango kwa ndani.Kilichoendelea humo ikawa ni kipigo mtindo mmoja.Bi Patricia alijitahidi kujitetea lakini wapi…baadae akaanguka chini na kupoteza fahamu baada ya kuzidiwa na maumivu huku damu nyingi zikimtoka puani na mdomoni.Baada ya kuona mkewe amedondoka na kupoteza fahamu,mzee Rwakatare akatoka na kuufunga mlango kwa nje.Akahamia kwenye chumba anacholala mwanae.

Kitendo cha Geneviv kumuona baba yake akiingia chumbani mwake kilimfanya moyo umlipuke kwa hofu.Alishasikia ugomvi uliokuwa unaendelea chumbani kwa wazazi wake, akajua sasa ni zamu yake.Tangu aanze kuwa na akili hakuwahi kupigwa hata kibao na baba yake,akabaki akisubiri aone kitakachomtokea.
Mzee Rwakatare baada ya kumuona mwanae akiwa amejawa na hofu kiasi kile,anajikuta nguvu zikimuishia na kuanza kumuomba msamaha mwanae.Geneviv alishindwa kuelewa nini lengo la baba yake na akabaki akimkodolea macho huku akishindwa kuificha hofu yake.Mzee Rwakatare akawa mpole ghafla na akasogea na kukaa karibu na geneviv juu ya kitanda chake.Bado Geneviv akawa anatetemeka mwili mzima kiasi cha kufanya kijasho chembamba kimtoke na kuiloanisha Night dress ndogo aliyokuwa ameivaa.Dakika kama tatu zikapita huku wakiwa bado wanatazamana,mwishoni Geneviv alishindwa kujizuia na kumuuliza baba yake kwa sauti ya kutetemeka,

“Where is my mum,Why do you act like this to us?
(Mama yangu yuko wapi,kwanini unatufanyia hivi)

Kwa mara ya kwanza Mzee Rwakatare akaligundua kosa alilolifanya,akajikuta akikosa jibu la kumpa mwanae…akiwa bado anajikanyaga, Geneviv alimsukuma kwa nguvu na kukimbilia chumbani aliko mama yake,alipofika mlangoni akakuta mlango umefungwa kwa funguo, akawa anagonga kwa nguvu akimtaka mama yake amfungulie…akiwa bado anagonga,akaona kitu chini ya mlango ambacho kinamshtua mno.Aliona michirizi mikubwa ya damu ikichuruzika kupitia chini ya mlango kutoka ndani ya chumba alimo mama yake.Nguvu zikamuishia na taratibu akakaa chini na kuzigusa zile damu akiwa bado haamini.
“Dady, did you kill my mother? I hate you… “

Geneviv aliongea kwa sauti kubwa na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada kwa majirani.Mzee Rwakatare akiwa amechanganyikiwa akatokea mlango wa nyuma na kutokomea gizani akielekea kusikojulikana.Geneviv akazidi kupiga mayowe yaliyowaamsha majirani ambao ndani ya muda mfupi walikusanyika kutaka kujua kumetokea nini.

Geneviv akisaidiana na majirani waliuvunja mlango na kufanikiwa kuingia chumbani ambako walimkuta mama yake akiwa amelala chini huku damu nyingi zikimtoka puani na mdomoni.Uso mzima ulikuwa umevimba kiasi cha kutotambulika…Geneviv akajikuta mwili wote ukimlegea akiwa haamini alichokiona, ghafla na yeye akaanguka na kupoteza fahamu.

************************************************
Bi patricia alikuja kurudiwa na fahamu baada ya siku mbili.Alipofumbua macho tu,sauti ya kwanza kuisikia ilikuwa ni ya mwanae Geneviv aliyekuwa amekaa pembeni yake akilia huku akisali kwa sauti ya chini, ndani ya wodi ya upasuaji ya hospitali ya Planet Health Aid.Kumbukumbu za matukio yote yaliyompata zilikuwa zimepotea kutokana na majeraha makubwa aliyokuwa ameyapata sehemu za kichwani na kifuani.
“Hapa ni wapi?” Aliuliza Bi Patricia huku akizishangaa dripu za maji na dawa zilizokuwa zinatiririka kuingia mishipani mwake.Kitendo cha kufumbua macho na kuuliza hapo ni wapi kilimshtua Geneviv aliyekuwa amezama kwenye kilio na Sala ya kumuombea mama yake.

“She is awake, Nurse Please come quick, my mother is back into her counciousness”

Aliongea Geneviv kwa sauti kubwa huku akiwa na furaha na akakimbia mpaka kwenye chumba cha nesi aliyekuwa anamhudumia mama yake.Sekunde chache baadae Geneviv alirudi akiwa ameongozana na nesi. Bi Patricia alikuwa bado akijaribu kukumbuka ni nini kilichomtokea mpaka akawa hapo.
Geneviv akawa anamshukuru Mungu kwa kumrejeshea fahamu mama yake huku machozi yakizidi kumiminika kwenye mashavu yake laini.Nesi alimtumliza Geneviv kwa kumwambia kuwa mgonjwa anahitaji kupumzika zaidi kwani alipata majeraha makubwa hivyo kelele zingemuongezea maumivu.Geneviv alielewa haraka na akatulia kimya akimtazama mama yake usoni alikokuwa amefungwa bandeji kubwa.

“Pole mum, My dad is a devil,I hate him…”
Aliongea Geneviv huku akimpiga busu mama yake.Hapo Bi Patricia akaanza kukumbuka yaliyomtokea mpaka akawa hpo hospitalini.Aliumia sana moyoni mwake, na kilichomuumiza haikuwa majeraha na maumivu aliyoyapata, aliumizwa zaidi na Geneviv ambaye aliyashuhudia yote na kujifunza kitu kibaya akilini mwake.
“Don’t cry for me Geneviv, im okay and everything is fine, Pray God for your daddy, don’t hate him.”
Aliongea Bi Patricia kwa taabu akimsihi binti yake kuchukulia kawaida yote yaliyotokea na kuzidi kumwomba Mungu kwani yeye ndiye mweza wa yote.
Bi Patricia aliendelea kutibiwa kwa siku kadhaa na hali yake ilipokuwa nzuri akaruhusiwa kurudi nyumbani.

Kwa siku zote alizokuwa Hospitalini, mumewe hakuwahi kuja hata mara moja kumjulia hali yake.Msaidizi mkubwa akawa ni mwanae pekee Geneviv ambaye ilibidi aache kwenda shule kwa takribani wiki mbili akimhudumia mama yake.Kipindi ambacho Geneviv alikuwa haendi shule, wenzake ndio walikuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kufanya mtihani wa mwisho wa kumalizia elimu ya msingi.
Aliendelea kumuomba Mungu amsimamie katika wakati mgumu aliokuwa nao.Kwa kipindi chote hicho Mzee Manuel Rwakatare alikuwa hafahamiki yuko wapi kwani hata nyumbani kwake alikuwa hakanyagi.
“Mum why cant we report dad on police station for the pain he has caused you?”
(mama kwanini usimshitaki baba polisi kwa maumivu aliyokusababishia?)
Aliuliza Geneviv wakati akimpoozea mama yake uji.Pamoja na maumivu aliyosababishiwa na mumewe,Bi Patricia bado alikuwa anampenda na alishamsamehe kwa yote yaliyotokea.
“Mwanangu Geneviv,matatizo ya kifamilia humalizwa na wanafamilia wenyewe kwa msaada wa Mungu baba wa Mbinguni,kwenda polisi ni kuongeza matatizo kwani hawatatusaidia chochote.Mungu anatufundisha kuwapenda wanaotufanyia mabaya, kusamehe
na kusahau kama yeye anavyotusamehe dhambi zetu,nakuomba usimchukie baba yako,msamehe kwani ni shetani ndio anamtumia kwa sasa,jifunze kusamehe…”

Bi Patricia alikuwa akimpa darasa zito binti yake kwani alionekana kuanza kumchukia baba yake.Wakiwa bado wanaendelea na mazungumzo yao, walisikia mlango ukigongwa kwa nguvu.Wakajua “Simba mtu amerudi”. Geneviv akainuka na kwenda kufungua mlango.Alikuwa ni baba yake,mzee Rwakatare.Japokuwa ilikuwa ni asubuhi,alionekana ameshalewa kama mtu aliyelala kwenye kilabu cha pombe.Bila hata salamu, mzee Rwakatare aliingia mpaka ndani alikomkuta mkewe akinywa uji alioandaliwa na mwanae.

“Karibu mume wangu,habari za asubuhi!” alimpokea kwa moyo mkunjufu mumewe.Mzee Rwakatare hakujibu kitu, akaanza kufoka.Safari hii alikuja na hoja mpya akimtuhumu mkewe kuwa anatembea na bosi wake na ndio maaana wakaandaa njama za kumfukuzisha kazi. Bi patricia hakujibu kitu akawa anamtazama mumewe usoni kwa huruma. Geneviv alikuwa amesimama mlangoni akishuhudia yote yaliyokuwa yakiendelea. Ghafla mzee Rwakatare alimvamia mkewe pale alipokuwa amelala akiuguza majeraha yake ya kupigwa ambayo yalikuwa bado hayajapona.
“Si naongea na wewe? Mbona hunijibu…kiburi sio?”
Kabla hata Bi Patricia hajajibu lolote, alishtukia akipigwa kibao kizito usoni, damu zikaanza kumtoka masikioni,puani na mdomoni.
Geneviv alishindwa kuvumilia kitendo kile alichokiona.kwa nguvu zake zote akaibeba stuli iliyokuwa mbele yake na kuinyanyua juu, kisha akaishusha kwa nguvu kichwani kwa baba yake.Ilitua kisawasawa utosini na kumfanya mzee Rwakatare apige yowe kubwa kisha akadondoka chini na kutulia kimya…alipoteza fahamu.

“Umefanya nini Geneviv, si nilikwambia usilipe ubaya kwa ubaya?” aliongea Bi patricia huku akijikongoja kuamka kitandani na kumuinamia mumewe pale chini huku akijifuta damu zilizokuwa zinavuja baada ya kupigwa kibao na mumewe.
Geneviv alibaki akimshangaa mama yake, Pamoja na maumivu yote aliyokuwa anapewa na mumewe bado alikuwa akimtetea!
“No mum,no mum, it pain my heart, cant tolerate to see this…im walking away”
Aliongea Geneviv na kuanza kukimbia kuelekea nje akiwa haelewi anakokwenda. Hakukusudia kumuumiza baba yake,lakini pia hakuweza kuvumilia kuona mateso aliyokuwa anayapata mama yake.
Hakukumbuka hata kuvaa viatu,akatoka hivyohivyo huku akikimbia kama aliyerukwa na akili.Alikimbia umbali mrefu sana mpaka akaanza kuhisi mwili wote ukiishiwa nguvu.Akatafuta mti wenye kivuli na kujitupa chini huku machozi yakimtoka kama chemchemi.Taratibu usingizi ukaanza kumpitia…

****************************************

Mzee Rwakatare alikuja kushtuka baada ya masaa manne tangu alipopoteza fahamu kwa kupigwa na kitu kizito kichwani. Alijikuta amelala chumbani kwake huku mkewe Bi Patricia akimpepelea kwa kanga yake na kiyoyozi alichokisogeza karibu kabisa na kitanda.
“Pole mume wangu, nisamehe kwani mimi ndio chanzo cha yote”
Alikuwa akiongea Bi Patricia kwa sauti ya chini huku machozi yakimtoka. Mzee Rwakatare alifumbua macho akiwa hakumbuki kilichomtokea, alichokihisi ni maumivu makali sehemu ya utosini.
“What happened to me!” Alihoji mzee Rwakatare kwa sauti ya chini,mkewe hakumjibu kitu, akabaki akimtazama usoni kwa huruma.Baada ya muda kumbukumbu zikaanza kumrudia upya.Alikumbuka kila kitu kuanzia siku ya kwanza alipompiga na kumjeruhi vibaya mkewe na kisha kumtelekeza chumbani akiwa amepoteza fahamu.Alikumbuka alivyoshinda kwenye baa za pombe kwa wiki mbili mfululizo huku akiwa hajui mkewe anaendeleaje ingawa alisikia kuwa alikuwa amelazwa.Alikumbuka pia jinsi alivyoingia kwa vurugu asubuhi hiyo na kuanza kumpiga upya mkewe japokuwa alijua kabisa kuwa bado hajapona.Kumbukumbu zake ziliishia hapo…
“What happened to me?....” alirudia swali lake lilelile lakini Bi Patricia hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kububujikwa na machozi.Kilichomshangaza Mzee Rwakatare ni kule kuzinduka na kujikuta yuko mikononi mwa mkewe.kwa matukio aliyokuwa anamfanyia aliamini isingekuwa rahisi kwa mkewe kuendelea kumpenda na kumjali kiasi kile.Alipomtazama tena usoni,aligundua mkewe alikuwa na makovu makubwa ambayo ni yeye ndiye aliyemsababishia.Alijikuta dhamira yake ikimshtaki kwa uovu aliomfanyia mkewe waliyetoka naye mbali kimaisha.
“Patricia…”
Bi Patricia alishtuka kumsikia mumewe akilitaja jina lake kwani tangu wampate mtoto wao Geneviv, mumewe aliacha kabisa kumuita jina lake…akitumia zaidi mama Geneviv au My Darling!
“Abee mume wangu!” aliitikia Bi Patricia kwa adabu huku akijifuta machozi.
“Naomba nisamehe mke wangu.Najua nimeuumiza sana moyo wako Darling, Najua nimekufanya ulie sana mke wangu…I know…I know! But please 4give me…I will never hurt you again.”
Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke.Alimvuta mkewe na kumkumbatia kwa nguvu.Bi Patricia hakujibu kitu zaidi ya kumwambia kuwa yote alimwachia Mungu na alishamsamehe kwa sababu anampenda.

“Mwanangu Geneviv yuko wapi? Hebu mwite nimuombe msamaha sababu najua yeye ndiye aliyeumia zaidi”.
“Ngoja nimuangalie chumbani kwake…Aliinuka Bi Patricia kwa kujikongoja na kuelekea chumbani kwa Geneviv.Alishajua kuwa hayupo ila alitaka tu kwenda kuhakikisha.”

*********************************************


“Oyaa washkaji eeeh…huyu si ndo yule Cute Angel Geneviv wa sculi kwetu?”
“Ndo mwenyewe mwana! Halafu mi nilikuwa namtamani siku kibao useme ndio alikuwa ananimwaga kila nikimuaproch!”
“Hata mimi nilikuwa namlia taiming siku kibao ila nilikuwa namgwaya si unajua mtoto mwenyewe alivyo juu!”
“Leo kajilengesha kwenye 18 zetu…ful kujisevia”

Hayo yalikuwa ni mazungumzo ya vijana wanne waliokuwa wametoka porini kuvuta bangi baada ya kutoroka shule.Walimkuta Geneviv akiwa amelala chini ya mti kutokana na uchovu wa kukimbia juani akitoroka kwao baada ya kumjeruhi baba yake kwa kumpiga na stuli mpaka akapoteza fahamu wakati akimpiga mama yake.

Akiwa usingizini alisikia sauti za watu wakichekelea kwa furaha.Aliposhtuka alikuta vijana wapatao wanne wamemzunguka na kabla hata hajakaa sawa alijikuta akivamiwa mwilini na kubanwa pale chini kiasi cha kushindwa hata kufurukuta.Mmoja alimziba mdomo huku wengine wakimvua nguo.Kufumba na kufumbua nguo alizokuwa amezivaa zilichanwachanwa na kumuacha akiwa mtupu.Akajua kilichokuwa kinataka kutokea.

Hakuna kitu alichokuwa anakiogopa maishani mwake kama kubakwa.Tangu awe mkubwa hakuwahi kumjua mwanaume hata siku moja na aliapa kujitunza mpaka atakapokuja kuolewa.Hakuwa tayari kuamini kuwa usichana aliokuwa akiutunza kama yai ndio ulikuwa unatolewa kwa aibu na maumivu makubwa namna ile.Alijitahidi kufurukuta lakini wapi,akataka kupiga mayowe ya kuomba msaada lakini hakuweza…akashuhudia kijana wa kwanza akifungua zipu yake na kumuinamia pale chini.Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kufumba macho huku akiuma meno.Kilichofuatia ikawa ni maumivu makali kupita kiasi ambayo hakuwahi kuyapata maishani mwake.

Baada ya yule wa kwanza kumaliza, alishuhudia wa pili akijiandaa…akajua huo ndio ulikuwa mwisho wake.Alijikaza mpaka naye akamaliza, akashuhudia watatu naye akijiandaa…akajikuta fahamu zikimtoka polepole kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata.
Wale vijana waliendelea kumfanyia ushetani ule Geneviv kwa zamu zamu mpaka wote wanne walipotosheka baada ya kurudia karibu mara tatu tatu.Wakamuacha akiwa amepoteza fahamu wakitokomea kusikojulikana.
Geneviv alikuja kushtuka baada ya kuhisi baridi kali ikimpiga.Aliposhtuka akajikuta yuko palepale chini ya mti, huku nguo zake zikiwa zimechanwachanwa.Alitaka kuinuka,maumivu makali yakamrudisha chini.Akawa anajaribu kukumbuka kilichomtokea,akapeleka mkono wake kwenye ikulu yake changa,kulikuwa kumeharibiwa vibaya mno…ndipo hapo kumbukumbu zilipomrudia,alikuwa amebakwa.Alibaki amepigwa na bumbuwazi akitamani hiyo iwe ndoto lakini haikuwa hivyo,ukweli ukabaki kuwa palepale,alibakwa.
Alijaribu tena kuinuka,lakini safari hii alisikia maumivu makali kupita kiasi.Akajilaza chali huku akilia kilio cha kuomboleza.Alijikuta akimchukia mno baba yake mzee Rwakatare kwani bila yeye asingepatwa na tukio baya namna ile.
“I hate my daddy! I hate men, they are Devils”

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...