Thursday, December 31, 2009

HAPPY NEW YEAR 2010


I will seek elegance rather than luxury, refinement rather than fashion. I will seek to be worthy more than respectable, wealthy and not rich. I will study hard, think quietly, talk gently, and act frankly. I will listen to stars and birds, babes and sages, with an open heart. I will bear all things cheerfully, do all things bravely await occasions and hurry never. In a word I will let the spiritual, unbidden and unconscious grow up through the common.

WHY YOU WANNA GO -SEAN KINGSTON


RELYCS

It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long for you
To get close to me
Now you wanna go run away girl
Away from me
I know its got to be hard
Cuz i'm so busy
Not to mention many lonely nights
Just missin' me
Cuz ain't nothing better than you by my side (my side) x4
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took some time to
Learn to earn her trust (learn to earn her trust)
I ain't goin nowhere anytime
So you can put that on us
Pucci, Louis, Rodeo, we gon' live it up
Now you want to say goodbye
And go and mess it all up
Cuz ain't nothing better than you by my side (my side) x4

It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
Forgive me x3
I love you x3
My mom say
My pop say
My family say
They love you x3
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go
It took so long to get here
Why you wanna go (tell me girl)
Why you wanna leave me
Why you wanna go

Friday, December 11, 2009

TOFAUTI KATI YA MWANAMKE NA MWANAUME
Ni ukweli usiopingika kuwa wanaume na wanawake hatufanani. Japokuwa sote tunafahamu kuwa hatufanani, bado wengi wetu hatujajua tofauti yetu iko wapi, au ni nini. Ni kwa kosa hili kubwa, wanaume wameendelea kuamini kuwa wao ni kundi bora kuliko wanawake, huku wanawake, nao kwa kutojua ukweli, kukubali kuwa wao ni viumbe dhaifu na wanaostahili kuongozwa katika kila jambo.

Nasema tena kuwa tofauti kati ya mwanaume na mwanamke zipo na hazikwepeki, lakini ni wajibu wa kila mmoja kutambua kuwa binadamu wote ni sawa katika mantiki ya “Ubinadamu”. Kuwa mwanaume au mwanamke hakukuongezei wala kukupunguzia chochote.

Kila mmoja amekamilika kwa vile alivyo,
Na thamani yetu kama binadamu inabaki kuwa palepale. Maisha yanakuwa na maana zaidi pale mwanaume na mwanamke wanapoungana na kuishi pamoja katika muunganiko ambao kila mmoja anafahamu yeye ni nani na mwenzake ni nani. Ukifanya utafiti utagundua kuwa hata kama familia ina mafanikio makubwa kiasi gani, kama mwanaume (baba) hajajua kuwa yeye ni nani na mwenzake (mama) ni nani na anahitaji nini, familia kama hiyo haiwezi kuwa na amanai na maisha kwao yanapoteza maana kabisa.

Kwa kushindwa kuelewa sisi ni nani na wenzetu ni nani, wengi tumeendelea kuwa wahanga wa nmaisha huku kila mmoja akimsingizia mwenzake kuwa ndio sababu ya yeye kushindwa kufikia malengo. Utakuta mwanaume analalamika kuwa mke wake ndio chanzo cha yeye kutofanikiwa, huku mke nae akilalamika kuwa mumewe ndio sababu ya yeye kushindwa kufikia malengo.

Tofauti kubwa kati ya mwanamke na mwanaume kwa sehemu kubwa zipo kwenye maumbile, jinsi mwili unavyofanya kazi, utashi, homoni, hisia, mahitaji na jinsi tunavyoyatazama mambo (Perception).

Ni kutokana na ujinga wa kutojua tofauti hizi, ndio maana ndoa nyingi zinaingia kwenye matatizo na migogoro kila kukicha, kuna kuumizana kwingi ndani ya mahusiano na mwisho kutengana kwa sababu kila mmoja (Mwanaume na mwanamke) anategemea mwenzake afanye na kutenda kama yeye bila kujua kuwa hili ni jambo ambalo haliwezekani kwa kuwa tunatofautiana katika mambo kadha wa kadha.

Ni makosa makubwa kwa mwanaume kutarajia mwanamke afanye kama yeye anavyotaka, au mwanamke kutegemea mwenzi wake amfanyie kama anavyotaka. Ni vizuri kila mmoja azifahamu tofauti zilizopo ili aweze kuishi kwa amani na mwenzake. Iwapo kila mmoja atafahamu tofauti zetu zipo wapi, migogoro na mifarakano isiyo ya lazima itaepukwa kwa kiwango kikubwa sana.

Wataalamu wengi wa mambo ya jinsia wamefanya utafiti kwa miaka mingi na kwa pamoja wamebaini tofauti zifuatazo:

UELEWA WA WANAUME
Kihulka, wanaume ni viumbe wasiopenda kufundishwa wala kushauriwa kitu kwa namna ambayo itawafanya wahisi kudharauliwa au hawajui jambo. Mwanamke anaweza kumshauri vizuri sana mumewe, kwa mfano “Mshahara wako au pesa unazopata tuzitumie kidogo na nyingine zinazobaki tuweke akiba kwa ajili ya kujenga nyumba au kusomesha watoto.”

Kimantiki huu ni ushauri wa busara sana ambao wanawake wengi huwapa wenzi wao, lakini mwanaume anapoambiwa hivi na mkewe, hasa kama mke nae hajui tofauti kati yake na mumewe, matokeo huwa ni kwa mwanaume kuhisi mkewe ameona yeye hawezi kupangilia mambo vizuri na ndio maana ameamua kumfundisha. Kitakachoendelea hapa itakuwa ni ugomvi mkubwasana na pengine mwaamke atabaki kujiuliza ni wapi alipokosea mpaka mumewe amjie juu wakati ametoa ushauri ambao ni mzuri.

Kinachosababisha ugomvi hapa ni kutojua kuwa wanaume sio watu wakufundishwa kama unavyomfundisha mtoto. Ushauri kama huu unaweza kuwa mzuri na kumfanya mwanaume ajihisi ni mwenye thamani kubwa endapo ataambiwa na mkewe wakiwa faragha, wakiwa wametulia kabisa, hali ambayo itamfanya mwanaume kujiona kama shujaa.

Wanawake wanaoijua siri hii, huwashauri waume zao mambo mazuri wakiwa vyumbani mwao, tena hufanya hivi baada ya kuhakikisha wamewafurahisha vya kutosha kwa mambo mazuri kama vile kwa chakula kizuri na tendo la ndoa lililopangiliwa vizuri. Pia mwanamke anatakiwa kuanza kutoa ushauri wake kwa kumsifia mumewe kwa yale mazuri ambayo amekwisha yafanya hata kama ni machache na madogo.

Kitu kingine ambacho kihulka ni tabia ya wanaume ni kupenda kutoa au kupewa suluhisho la moja kwa moja. Mwanaume anapoamua kumweleza mkewe hukusu jambo Fulani ambalo linamtatiza, anataka kupewa suluku ya moja kwa moja na sio kuonewa huruma. Inapotokea mwanaume anamuomba ushauri mkewe na badala ya mke kumpa ufumbuzi wa nini cha kufanya anaanza kumuonea huruma na kumsikitikia, huhisi kama hadhi yake imeshushwa sana.

UELEWA WA WANAWAKE
Tofauti na wanaume, wanawake ni viumbe wanaopenda sana kuelekezwa na kufundishwa hasa na waume zao au watu wao wa karibu. Unapomuelekeza mwanamke jambo kwa upole na ukarimu, utakuwa na nafasi nzuri ya kupendwa sana na mwanamke huyo.

Wanawake pia kupenda sana kusikilizwa wanapoeleza matatizo yao. Pamoja na hayo, hupenda sana pia kusaidiwa mambo yanayowasumbua hata kama ni madogo. Utashangaa sana kwamba hata yale mambo ambayo wanaume huyaona kuwa ni kawaida na yasiyo na uzito wowote, kuwa na maana kubwa sana kwa wanawake.

Nimewahi kusimuliwa na ndugu yangu mmoja ambaye alikuwa akinisimulia insi alivyokutana na mke wake wa sasa. Alinieleza kuwa walikutana katika kituo cha daladala wakisubiri usafiri, na daladala ilipofika kutokana na msongamano wa abiria, yule mwanamke aligongwa na mwanamke mwenzake mpaka akadondosha simu na mkoba wake chini.

Ndugu yangu anasema alipoona yule mwanamke akiwa ameduwaa akiwa hajui nini cha kufanya, aliwani na kumsaidia kuokota vitu vyake chini na kumkabidhi, kisha akamsaidia kupada ndani ya daladala.
Kwa msaada huo ambao kwa mwanaume angeuona wa kawaidsa nap engine asingekumbuka hata kusema asante, yule mwanamke alijikuta akimshukuru sana ndugu yangu na walipofika mwisho wa safari, alimuomba ndugu yangu namba ya simu na huo ukawa ndio mwanzo wa uhusiano wao mpaka wakaja kufunga ndoa na kuoana.

Huo ni mfano mdogo tu wa namna wanawake wanavyopenda kusaidiwa, kusikilizwa na kuonewa huruma.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………

Kwa kutojua tofauti hii, wanaume wengi hujikuta wakiwaudhi wake zao kutokana na kuchukulia mambo kirahisi hali ambayo husababisha manun’guniko makubwa kwa wenzi wao.

Ni vizuri wanaume wakajenga utaratibu wa kuwasikiliza wake zao au wenzi wao kwa upole na umakini wa hali ya juu. Makosa ambayo wengi huyafanya bila ya wao kujua ni pamoja na kusoma gazeti au kuangalia Tv wakati mkeo anakueleza jambo akihitaji umsikilize na pengine anahitaji umpe msaada wa nini cha kufanya (Umfundishe).

Kwa mwanaume ataona ni jambo la kawaida kusoma gazeti wakati mkewe akimueleza kero zake wakati kiuhalisia wanawake hujisika vibaya sana na kuamini kuwa hawana thamani tena na ndio waume au wenzi wao hawawasikilizi kwa makini.

WANAUME HUPENDA KUSIFIWA
Miongoni mwa vitu ambavyo wanaume wanavipenda maishani mao basi ni kusifiwa. Kwa kawaida mwanaume husikia fahari kubwa sana kusifiwa, wakati mwanamke akisifiwa sana hujihisi aibu.

Mwanaume anaposifiwa hasa na mtu anayempenda kama mke wake au mpenzi wake, yuko tayari hata kufa akitaka azidi kusifiwa zaidi. Hakuna sumu kali kama mwanamke kumkosoa mwanaume, hususani mbele ya watu wengine. Hili ni kosa ambalo wanawake wengi kulifanya pia. Unakuta mke anamkosoa na kumcheka mumewe mbele ya watoto au majirani huku akiwa hana wasiwasi kabisa kuwa anafanya makosa makubwa.

Watafiti wa mambo ya mahusiano wanaeleza kuwa tatizo la wanawake kuwahosoa wanaume, huwaumiza sana wanaume kisaikolojia na ni miongoni mwa sababu inayopelekea wanaume wengi kukosa au kupungukiwa nguvu za kiume. Pia kukosolewa huku hupelekea wanaume kushindwa kujiamini hata mbele ya wanaume wenzao na huhisi kuwa thamani yao ina walakini. Hii ni sumu mbaya sana ambayo wanawake wanapaswa kuikwepa ili kudumisha uhusiano bora na wenye kudumu.

WANAWAKE HUPENDA KUONESHWA KAMA WANAPENDWA
Inawezekana ikawa ni vigumu sana kujibu swali kuwa ni kwa nini wanawake ndio wanaotakiwa kutongozwa, wakati mwanamke akimtongoza mwanaume anaonekana hajatulia. Kihulka, imani hii inatokana na ukweli kwamba mara zote wanawake ni viumbe wanaotakiwa kupendwa kwanza ndipo nao waoneshe upendo wao.

Ni vigumu sana kuishi bila kukwaruzana na mwanamke kama anahisi kuwa humpendi wala humjali. Wakati wanaume wao wanapenda sana sifa, wanawake wanapenda sana kupendwa na wako tayari kufanya lolote ili kumfurahisha mtu anayeonesha mapenzi ya hati kwao.

Ni rahisi sana kwa mwanamke kushawishika kutembea nje ya ndoa endapo atahisi kuwa mume aliyenaye hampendi kwa dhati, wahati kuna mwingine wa nje anayeonesha mapenzi ya kweli. Ukifanya utafiti, utagundua kuwa wanaume wengi huwa wepesi wa kuwatamkia wanawake kuwa wanawapenda katika siku za mwanzo za uhusiano, lakini wakishaingia ndani ya ndoa huwa ni wagumu sana kutamka neno “Nakupenda”.

Mwanamke mmoja alikuwa akitoa ushuhuda kuwa mumewe alimtamkia neno nakupenda siku moja tu wakati anamtongoza, lakini baada ya kumkubali na kuolewa naye, yapata miaka kumi na tatu sasa hajawahi kusikia tena neno hilo kutoka kwa mumewe, na hata pale yeye anapomwambia kuwa anampenda, huwa anamjibu kwa kifupi kuwa anajua kuwa anampenda.

WANAUME HUPENDA KUJITENGA WAKIWA WAMECHOKA
Kuna usemi maarufu unaotumika duniani kote unaoelezea kuwa wanaume wametokea katika sayari ya Mars wakati wanawake wanatoka katika sayari ya Venus. Msemo huu una maana kubwa sana kwamba, mara nyingi hulka za wanaume huwa zinakinzana na za wanawake. Wataalamu wanaeleza kuwa mara nyingi wanaume akili zao zinapochoka, huwa wanahitaji kukaa peke yao mpaka akili itulie ndipo waweze kuendelea na shughuli nyingine. Wanawake wengi huwa hawaliekewei hili na kwa ujinga wao hujikuta wakizidi kuwakera waume zao.

Mfano unakuta mwanaume anarudi kazini jioni kichwa kikiwa kimechoka. Badala ya mke kumpokea kwa maneno matamu yatakayomfanya uchovu wake upungue, anaanza hoja za kichokozi huku akitoa lawama kibao, mara kwa nini ulikuwa hpokeai simu, kwa nini umechelewa kurudi, ulikuwa umeongozana na nani, na kauli nyingine zilizojaa lawama.

Ni dhahiri kuwa kwa kuwa akili ya mwanaume inakuwa imeshachoka, atakuja juu kama mbogo na uwezekano wa kumpiga mwanamke wa aina hii huwa ni mkubwa. Ukichunguza kwa makini, wanawake wanaolalamika kuwa huwa wanapigwa na waume zao, wao ndio huwa sababu kubwa ya kupigwa kwao kutokana na kushindwa kuwasoma waume zao.

WANAWAKE HUPENDA KUBEMBELEZWA WANAPOKUWA WAMECHOKA
Tofauti na wanaume ambao wakichoka hupenda kujitenga peke yao, wanawake wanapokuwa wamechoka hupendwa kubembelezwa na kufarijiwa kwa karibu. Hupenda kuwa jirani na mtu ambaye atawapa maneno matamu yatakayowafanya wasahau maswaibu na uchovu wa kutwa nzima.
Hali kuwa inakuwa mbaya katika nyumba ambayo mwanaume na mwanamke wote ni wafanyakazi. Unakuta mwanaume amerudi kazini akiwa amechoka na anahitaji muda wa kukaa peke yake mpaka akiliyake itakapotulia, upande wa pil mwanamke nae amerudi kazini akiwa amechoka sana na anahitaji kukaa jirani na mumewe kwa ajili ya kubembelezwa baada ya kazi za kutwa nzima.

Kitakachotokea hapa ni kwa mwanaume kutafuta uhuru wa kuwa peke yake. Atatoka na kwena kukaa peke yake sebuleni , ukumbini au chumbani. Kitendo hiki kitamfanya mwanamke ahisi kuwa huenda amemuuzi mumewe na ndio maana anajitenga, na ataanza kumfuatafuata kila anakokwenda. Matokeo yake ni kila mmoja kuishia kuboreka na mwenzake na hapo ndipo maudhi madogomadogo yanapoanza, na kwa wasipokuwa makini wanaweza kuishia kwenye ugomvi mkuba saa ambao chanzo chake hakieleweki.

Itaendelea
amenibarikihash@rocketmail.com
newera7113.blogspot.com
+255 (0) 768540912
STAY BLESSED YOU ALL!

Thursday, December 10, 2009

BLOOD REVENGE (Part II of My Heart Is Bleeding)







Baada ya kukaa kwa muda mrefu ndani ya kisiwa cha Zanzibar, Khaleed anapanga mikakati madhubuti ya namna ya kurudi nchini kwao, kwa ajili ya kazi moja tu! Kulipa kisasi cha damu kwa wote waliohusika na mauaji ya ndugu zake bila ya hatia.

Ilikuwa ni lazima arudi nyumbani kwao kulipa kisasi kwani damu ya ndugu zake iliyomwagika bila ya hatia ilikuwa ikimuandama muda wote, na tayari alishajiapiza tangu kipindi, kuwa lazima alipe kisasi.
‘I must revenge! The blood revenge to whoever may concern.”

Licha ya kuwa tayari Khaleed alikuwa ameanza ukurasa mpya wa maisha , hasa baada ya wazazi wake wote kufariki dunia, bado aliamini hakuna kitu ambacho kingeweza kuziba pengo la wazazi wake hapa duniani. Ni hali hii ndiyo iliyomfanya apitie mateso makubwa sana duniani kabla ya Mungu kumbariki kwa kumuangazia nuru ya maisha alipokuwa huko machimboni Mererani, alikofanikiwa kuondoka na jiwe kubwa la madini ya tanzanite, madini ambayo kwa kiasi kikubwa yaliyabadilisha maisha yake, kutoka maisha ya uchokoraa hadi kufikia kuwa milionea mtoto.

Aliendela kukaa ndani ya visiwa vya Zanzibar, kwenye hoteli moja ya kifahari iliyokuwa pembezoni mwa bahari ya hindi. Aliendelea kukaa pale kwa wiki kadhaa akiumiza kichwa namna atakavyoitekeleza operesheni aliyoipa jina la ‘Blood revenge 7113’. Muda wa jioni alikuwa akitoka na kwenda kukaa peke yake ufukweni, akiwa na kijitabu chake kidogo (Note book) akiandika kila kitu kuhusu namna ambavyo angeendesha kazi ile kubwa iliyokuwa mbele yake.

Pesa kibao alizozipata baada ya kuuza madini ya Tanzanite, zilitosha kumfanya aishi maisha aliyoyataka aliendelea kusuka mipango kwa umakini wa hali ya juu ili kuhakiksha anakamilisha zoezi lile gumu na la hatari bila ya kushtukiwa. Alikuwa akiandika majina ya watu wote waliohusuka kuiangamiza familia yao, akianza na mashetani watatu wa kundi hatari la wafanya biashara wa Holly Trinity. Aliandika majina yao kwenye kijitabu chake cheusi, akitumia kalamu nyekundu.

Aliwaandika pia watu wote walioshirikiana na The Holly Trinity, kuanzia na kamanda mkuu wa polisi wa kanda maalum, Luteni Lauden Kambi ‘Fuvu’ ambaye hkaleed alikuwa akiamini kuwa ameshiriki kwa kiwango kikubwa kwani kama angeifanyia kazi taarifa ya mapema iliyotolewa na wazazi wake, yale yote yasingetokea. Aliwaandika pia watu wengine wengi ambao kwa pamoja walitengeneza orodha ndefu ya watu ambao walikuwa wakistahili kufa kwa mikono yake.
“They deserve to die f*c them to hell” (Wanastahili kufa mashetani hawa), Khaleed aliongea kwa sauti ya juu wakati akiitazama upya ile orodha yake.

Kwa kuwa aliongea kwa sauti ya juu, bila kujua kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa amekaa jirani yake, ilibidi aanze kuvunga akiwa na lengo la kupindisha ukweli kwani hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa akiandaa mikakati kabambe ya kuua. Jirani na pale alipokuwa amekaa, pembeni alikuwa amekaa binti mmoja, ambaye kiumri walikuwa wakishabihiana na Khaleed. Kauli ile ya Khaleed “They deserve to die…’ Ilimshtua sana kiasi cha kugeuza sura yake kuelekea pale Hkaneed alipokuwa amekaa.

Aliendelea kumtazama lakini Khaleed alikuwa akijitahidi kupoteza mada baada ya kugundua kuwa alikuwa amefanya kosa kuropoka kwa sauti bila ya kujua kuwa kulikuwa na mtu pembeni yake pale ufukweni, kando ya hoteli ya kifahari aliyokuwa amefikia. Aliendelea kupunga upepo wa baharini huku mawazo mengi yakipishana akilini mwake. Yule binti aliendelea kumtazama Hkaleed kwa jicho la kumsoma, lakini Khaleed alijifanya hana habari naye.

Baada ya kuona yule binti akizidi kumtazama, Khaleed aliinuka na kuondoka pale alipokuwa amekaa na kuanza kurudi kwenye hoteli aliyokuwa amefikia. Hakutaka hata kumtazama usoni. Alipitiliza moja kwa moja mpaka chumbani kwake alikofikia ambapo alijitupa juu ya kitanda na kujilaza, huku mawazo yakizidi kupishana akilini mwake.

Kwa kadri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele, ndivyo hamu ya kulipa kisasi ilivyokuwa ikizidi kuongezeka akilini mwa Khaleed. Baaada ya kukaa kwa zaidi ya wiki tatu pale kisiwani Zanzibar, kwenye Hoteli ya kifahari aliyokuwa amefikia, safari ya kurudi nyumbani kwao Blazinia ilikuwa imekamilika. Maandalizi yote muhimu yalikuwa yamekamilika na sasa alikuwa katika hatua za mwisho kabla ya kuanza rasmi kazi yake, kazi ya kulipa kisasi cha damu.

Ikiwa ni jioni ya mwisho aliyopanga kukaa kisiwani Zanzibar, Khaleed alitoka na kwenda ufukweni kama kawaida yake, safari hii akiwa na matumaini makubwa kuwa hatimaye kazi nzito iliyokuwa mbele yake alikuwa akienda kuikamilisha. Jioni hii alionekana kuwa mchangamfu kuliko siku zote alizokaa pale hotelini. Furaha yake ilitokana na ukweli kwamba karibu taratibu zote zilikuwa zimekamilika na kilichokuwa kimesalia ilikuwa ni utekelezaji tu. Alitoka na kwenda moja kwa moja kukaa ufukweni kupunga upepo huku akichezea mchanga wa baharini.

Alikuwa akijaribu kukumbuka kila kitu kilichotokea maishani mwake mpaka akajikuta akiwa mpweke chini ya jua, akiwa hana ndugu hata mmoja aliyesalia akiwa hai. Alikumbuka kila kitu kuanzia siku ya kwanza jinamizi la mikosi lilipoanza kuiandama familia yao, akakumbuka kila kilichoendelea baada ya hapo mpaka muda ule akiwa pale ufukweni.

Kumbukumbu mbaya zilizokuwa zikipita kwa kasi ndani ya ubongo wake zilimuongeza uchungu mtimani, na akajikuta akianza kutokwa na machozi, hasa alipomkumbuka mama yake mzazi na jinsi alivyouliwa kikatili kwa kuchomwa sindano ya sumu na kumfia mikononi mwake.

Alikumbuka pia jinsi baba yake alivyouliwa kikatili kwa kupigwa risasi mbele ya macho yake, akiwa na kaka yake wa hiyari, Girbons, wakati wakijaribu kutoroka. Picha za matukio ya wadogo zake walioliwa na simba wa Gamutu usiku wa siku ya kwanza walipotekwa kutoka nyumbani kwao usiku wa manane, na mwisho kumbukumbu za kaka yake mwenye ulemavu wa ngozi ambaye mpaka muda huo alikuwa akiamini kuwa tayari ni marehemu… alishindwa kuyazuia machozi yasiuloanishe uso wake, moyo wake ulikuwa ukivuja damu.

Khaleed akijikuta akizama kwenye dimbwi zito la mawazo na hisia za maumivu makali zilizokuwa zikiuchoma mtima wake kiasi cha kutosikia wala kuona kuwa kuna mtu alikuwa akimsogelea. Alitoa kitambaa chake cha mfukoni (handkerchief) na akawa anafuta machozi, ambayo sasa yalikuwa yameuloanisha uso wake wote.

“kaka habari yako!”, Khaleed alisikia sauti laini ya kike ikimsabahi kutoka nyuma yake, lakini kutokana na halialiyokuwa nayo, hakuitikia salamu ile, na akawa anazidi kujifuta machozi.
“Kaka nakusalimu! Mbona kimya”, yule binti alirudia salamu yake na akawa anahoji kwa nini Khaleed alikuwa haitikii salamu yake. Alimsogelea kwa jirani zaidi na ndipo alipogundua kuwa alikuwa amezama kwenye hisia zilizoonekana kuuchoma moyo wake.

“Jamani pole kaka’angu, it seems you got serious problem, can I help you?” ( Inaonekana una matatizo makubwa! Naweza kukusaidia?) yule binti aliuliza kwa sauti ndogo ya upole huku akimgusa begani Khaleed. Kwa kifupi Khaleed alikuwa katika wakati mgumu sana kiasi ambacho aliona kama ni usumbufu mkubwa kwa mtu mwingine kuja kumvurugia utulivu wake, alihitaji kuwa peke yake. Alimgeukia na macho yao yakagongana. Alikuwa ni yule binti ambaye siku chache zilizopita walikuwa wamekaa jirani palepale beach ingawa hakuna ambaye alimsemesha mwenzake.

Khaleed na yule binti waliendelea kutazamana kwa dakika kadhaa bila ya kusemeshana chochote. Yule binti aliuvunja ukimya kwa kurudia kumuuliza Khaleed kama angeweza kuhutaji msaada wake.
“ Can I help you?”, aliuliza tena yule binti kwa sauti ya upole na yenye kubembeleza kanini Khaleed akaitikia kwa kichwa kuonesha kuwa alikuwa haitaji msaada wake.

Khaleed aliinuka na kuanza kuelekea kwenye hoteli aliyokuwa amefikia, akimuacha yule binti ameduwaa kwa mshangao huku akimuonea huruma. Hakugeuka nyuma mpaka aliopotelea ndani ya hoteli ya kisasa aliyokuwa amefikia kwa takribani wiki tatu sasa, tangu alipowasiri kutoka machimboni Mererani, huko Arusha Tanzania. Yule binti alimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea kabisa kwenye upeo wa macho yake.
*******
Ndani ya chumba cha hoteli ya kimataifa ya Isles Sand Resort, Khaleed alikuwa akipanga zana zake kwa ajili ya kuanza rasmi kazi yake ya kulipa kisasi, ambayo alikuwa amepanga aianze siku iliyokuwa ikifuata. Alikuwa akipanga vitu vyake vichache ndani ya mkoba wake mdogo wa rangi nyeusi.

Miongoni mwa vitu alivyokuwa anavimiliki, ilikuwepo bastola ndogo aliyofanikiwa kutoroka nayo kutoka mikononi mwa jambazi hatari huko Arusha Tanzania, aliyekuwa akifanya kazi hatari ya kuteka magari yanayosafirisha madini na vito vya thamani kutoka kwenye machimbo ya Tanzanite, huko Mererani.

“Hii itanisaidia sana! Where a metal must meet a meat” Aliongea Khaleed akimaanisha kuwa lazima risasi za mashine ile ndogo zikutane na nyama za wabaya wao.

Licha ya bastola, alikuwa na kichupa kidogo kilichokuwa ndani ya Kiboksi cheusi kilichokuwa na maandishi mekundu yaliyosomeka, ‘Ampethamine cyanide serum’. Kwa haraka alikikumbuka kiboksi kile na akakumbuka jinsi alivyokipata. Alikuwa amemuibia yule jambazi aliyemteka wakati akitoka Mererani, ambaye baadae aligeuka na kuwa rafiki yake akimtaka Khaleed aungane naye kwenye kazi yake ya ujambazi.

Alipokuwa akimuonesha vifaa vyake vya kufanyia kazi, alimuonesha pia na kile kichupa na akamueleza kuwa ile ni sumu hatari sana ambayo huchanganywa kwenye aina Fulani ya pafyumu, na inapopulizwa hewani na binadamu kuvuta hewa yake, ilikuwa ikifanya kazi katika hali ya kutisha sana. Alimpa maelekezo ya namna ya kuichanganya sumu ile na aina ya manukato yenye kemikali iitwayo “Dopamine Venule rapture” ambapo kwa pamoja mchanganyiko huo ulikuwa ukitengeneza sumu kali sana iitwayo ‘Mankind Homocidal Perfume’.

Itaendelea

amenibarikihash@rocketmail.com
newera7113.blogspot.com
+255 (0) 768540912
STAY BLESSED YOU ALL!

Saturday, November 21, 2009

MY HEART IS BLEEDING! (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU) -I (SWAHILI VERSION)

NOVEL MANUSCRIPT
(SWAHILI VERSION)
“Beyond The Seen Scene!… Beyond The Grave Yards… There Laid…
The Hearts That Bleeds, Hearts Of Desperately Broken Victims, The Weak!! Their Hearts Are Bleeding…, But Finally A Healing Balm For Every Wound Is Found, When The Darkness Takes Its Flight…”
My Heart Is Bleeding…
(moyo wangu unavuja damu)
Novel story by:
Aziz Hashim-Hash power
amenibarikihash@rocketmail.com

EPISODE I
SEHEMU YA KWANZA
Ilikuwa ni jumatatu ya kwanza ya mwezi Septemba, asubuhi tulivu yenye anga lililopendezeshwa na rangi ya bluu, jua la asubuhi likiwa ndio linachomoza na kuzidi kuipendezesha siku ya kwanza ya juma.
Umati mkubwa wa watu waliokuwa wamefurika katika viwanja vya mahakama kuu ulitosha kumfanya yeyote asiyejua kilichokuwa kinaendelea mahali hapo kupigwa na butwaa. Ilikuwa ni idadi kubwa kabisa ya watu kuwahi kutokea tangu mahakama hiyo ilipoanza kufanya kazi rasmi miaka kadhaa iliyopita…

Friday, November 13, 2009

My Beauty, My Grave!...Urembo wangu, kaburi langu!-1


PART II OF SHED NO MORE TEARS GENEVIV
Baada ya majeraha kupona, huacha makovu ikiwa ni alama ya maumivu yaliyopoa na kuisha. Maisha alyopitia Geneviv, yaliyojaa misukosuko na matatizo ya kila aina, hatimaye yanafikia ukingoni na Geneviv anaanza ukurasa mpya wa maisha yake. Majeraha makubwa aliyojeruhiwa mtimani na akilini mwake yanapona na kuacha makovu makubwa, makovu ambayo nayo yanafutika taratibu. Anasahau kila kitu na kwa msaada wa mama yake mpendwa anafanikiwa kurudi tena shuleni.

Lile tabasamu lilipotea kwa muda mrefu linaanza kuchanua upya usoni mwake na kuufanya uzuri wake wa asili uliopotea kwa muda mrefu kuanza kuchanua mithili ya jua la asubuhi. Ndoto zote ambazo zilikuwa zimepotea na kufutika maishani mwake mithili ya theluji juani sasa zilianza kurudi upya.
Uzuri wa sura na umbo lake vinajidhihirisha upya na kumfanya kila anayemuona kumshangaa na kumsifia kuwa amebarikiwa.

Huwezi kuamini kuwa huyu ndiye Geneviv aliyekuwa akilia na kuomboleza karibu kila siku maishani mwake kutokana na shida za dunia hii. Kila kitu kinabakia kuwa Historia na anamwachia Mungu kwani ni kwa kudra zake ndizo zilizomuwezesha kuwa hai mpaka muda huo.
********
Maisha mapya akiwa kama mwanafunzi wa sekondari, yalimfurahisha sana na akajikuta akijilaumu kwa nini alichelewa kuanza shule. Marafiki zake aliosoma nao shule ya msingi walikuwa mbele kwa kidato kimoja kutokana na yeye kupoteza mwaka mzima nyumbani kutokana na matatizo yaliyokuwa yanaiandama familia yao.

Hilo lilimtia uchungu kiasi, lakini moyoni alijiapiza kuwa ataendelea kuwa bora kuliko hata hao waliomtangulia. Baada ya muda mfupi tu tangu aandikishwe kuanza sekondari, Geneviv alishaanza kufahamika shule nzima, akijizolea marafiki wapya lukuki.

Alianza kung’ara darasani akionyesha uwezo mkubwa sana kwenye masomo, hasa elimu ya Viumbe hai (Biology), Hesabu na masomo mengine ya sayansi. Walimu wake walianza kumtabiria kuwa atakuja kuwa daktari Bingwa baadae kutokana na kuyamudu vizuri masomo ya Sayansi.

“Mama eti mwalimu kaniambia mi nafaa kuwa Daktari, Aka mi staki! Nataka kuwa mwanasheria kama baba’ake Kim ili niwatetee watoto na wanawake wanaodhulumiwa haki zao”, Aliongea Geneviv akimueleza mama yake, muda mfupi baada ya kutoka shule.

Mama yake alitabasamu na kumwambia akaze buti zaidi kwenye masomo na asijihusishe na mambo mengine kwani madhara yake alikuwa akiyafahamu vizuri. “lakini tangu unaanza darasa la kwanza ulisema unataka kuwa Daktari, Mbona leo unabadilisha maamuzi yako mwenyewe?”

Bi Patricia alimuuliza mwanae na wakawa wanapiga stori kirafiki. Geneviv alimueleza kuwa anatamani kuwa mwanasheria baada ya kugundua kuwa kuna wanawake na watoto wengi ambao wanakosa haki zao, wananyanyasika kijinsia na kuonewa kwa sababu hakuna mtu wa kuwasaidia.

Siku hizi naona umekua maana hata upeo wako wa kufikiri nao umeongezeka na unaongea mambo ya kiutu uzima zaidi, Bi Patricia alimsifia mwanae na wote wakatabasamu kwa furaha.

Maisha kwao yalikuwa ni kama yameanza upya kabisa, wakiongea na kufurahi kama zamani. Pengo kubwa lililokuwa limebakia lilikuwa ni kufiwa na baba wa familia, Bwana Rwakatare. Bi Patricia alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kuliziba pengo lile na kumfanya Geneviv asilione pengo lililokuwepo, alifanikiwa kwani Geneviv hakuona tofauti yoyote.

Kwa kawaida baada ya muda wa masomo, Geneviv na mama yake walikuwa wakienda kujumuika na watoto waliokuwa wanaishi katika mazingira magumu na mayatima, ambao kwa msaada wa Bwana Magwaza walifanikiwa kuwafungulia kituo maalum. Geneviv alikuwa akipenda kuwafundisha nyimbo za kiingereza alizofundishwa shuleni kwao.

Watoto wote walitokea kumpenda, kiasi kwamba asipoonekana hata siku moja walikuwa wakimuulizia sana mama yake, ambaye ndiye aliyekuwa mlezi mkuu wa kituo kile. Maisha yakawa yameongezeka msisimko kuliko awali. Siku zikawa zinasonga na maisha yakawa yanasogea mbele, Geneviv akizidi kukua na kupendeza zaidi.

Shuleni kwao, taratibu wanafunzi wa kiume walianza kujigonga kwa Geneviv kila mmoja akitaka awe rafiki yake. Kutokana na kumbukumbu mbaya zilizokuwa zimeanza kufutika akilini mwake juu ya ukatili aliowahi kufanyiwa na wanaume zilizimfanya awachukie wavulana kupita kawaida.

Alishajiwekea nadhiri akilini mwake kuwa kama haitawezekana kwa yeye na Kim kuja kuwa baba na mama, basi ni bora kuishi peke yake maishani mpaka atakapozeeka na kufa. Japokuwa walikuwa wametenganishwa kabisa na Kim, daima aliendelea kuwa moyoni mwake na alishamsamehe kuhusu kila kitu kilichotokea, na zaidi alimuona kama shujaa maishani mwake.

“He is my Hero! I will never Forget him” (Yeye ni Shujaa wangu! Sitamsahau maishani mwangu)
Geneviv alikuwa akiongea peke yake jioni moja akiwa amejifungia chumbani kwake akizitazama picha alizokuwa amepewa na Kim kabla hawajatenganishwa.

Kilichomfanya mpaka ashindwe kumsahau Kim ni upendo wa dhati aliomuonesha kipindi wakati wakiwa na matatizo yaliyowafanya wapteze matumaini ya kuishi, yeye na mama yake. Alikuwa akikumbuka mambo mengi ambayo Kim alimfanyia, ambayo haikuwa kawaida kwa binadamu wa kawaida kuyafanya. Alizidi kuamini kuwa Kim alikuwa ni zawadi ya kipekee kwake aliyoshushiwa kutoka mbinguni.

Kumbukumbu za matukio ya mwisho yaliyotokea na kupelekea Geneviv kutaka kujitoa roho, zilimfanya ajione kama aliyeshindwa kulpa fadhila kwa mema yote aliyotendewa na Kim. Alijikuta akimchukia sana Alice kwani aliamini yeye ndiye aliyekuwa chanzo cha yote, lakini kwa kuwa alikuwa ameamua kuanza ukurasa mpya wa maisha yake, alimsamehe kutoka moyoni mwake na akaendelea kuamini kuwa ipo siku Mungu atawakutanisha tena.

“Mama mi shuleni nasumbuliwa sana na wavulana. Everyone is seducing me! Im Bored and I don’t like them…they are devils” ( Kila mmoja ananitongoza mpaka naboreka! Siwapendi kabisa… wavulana ni mashetani), Geneviv alikuwa akimsimulia mama yake wakati wakiandaa chakula cha jioni. Ilibidi Bi Patricia acheke baada ya mwanae kumweleza.

“You are very Beatiful my Daughter, hata kama ningekuwa mimi ndio mvulana halafu nasoma darasa moja na wewe lazima ningekutaka tu”, Aliongea kwa masihara Bi Patricia na wakaishia kucheka kwa furaha. Alimtoa wasiwasi kuwa asiogope kutongozwa kwani hiyo ilikuwa ni kama sifa tosha kwa binti mrembo kama yeye, ila akamsihi kuwa asikubali kujiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote kwani hata yeye alishaona madhara yake.

“Jitulize na kazania masomo mwanangu, utampata tu atakayekufaa maishani”, Bi Patricia alizidi kumuasa mwanae. Geneviv aliitikia kwa kutingisha kichwa huku akili yake yote ikimuwaza Kim. Alijiapiza kuwa hatarudia makosa kama ya awali na akajiapiza kuwa atajitunza kwa kadri ya uwezo wake wote, ilimradi ndoto yake itimie, ya kuja kuolewa na Kim.
********


Kim alikuwa naye ameyaanza maisha mapya, akiwa mabli kabisa na kwao. Mazingira ya jii la Nairobi yalikuwa tofauti na mazingira ya nyumbani kwao, Blazinia. Shule ya sekondari ya wavulana ya Kasarani Boys Camp Nairobi aliyokuwa anasoma, ilikuwa tofauti kabisa na St Benedict Seminary aliyokuwa anasoma awali.

Japokuwa shule ilikuwa na mandhari ya kisasa, alipata shida kubwa kuzoeana na wanafunzi wenzake. Hali ya hewa nayo ilikuwa ni tatizo jingine kwake kwani alikuwa akisumbuliwa sana na tatizo la kifua kubana.

Miezi miwili aliyokaa shuleni hapo ilikuwa ni kama mwaka mzima. Licha ya kusumbuliwa na mazingira na hali ya hewa, bado akili yake ilikuwa ikimuwaza sana Geneviv. Kilichofanya amuwaze namna ile ni hisia za kushtakiwa na dhamira zilizokuwa zikitawala maisha yake. Hakuhesabu mazuri aliyowahi kumfanyia Geneviv, alichokikumbuka ilikuwa ni maumivu aliyomsababishia Geneviv mpaka akafikia hatua ya kutaka kujiua.

Alikuwa akijisikia vibaya sana kila alipokumbuka tukio lile. Alitamani kupata muda wa kumuomba msamaha Geneviv ili abakie na amani moyoni mwake, lakini hilo halikuwezekana. Umbali ulikuwa ni kigezo kikubwa kilichofanya isiwezekane.

Aliamini kuwa isingekuwa rahisi kwa geneviv kukubali kuendeleza uhusiano wao uliovunjika katika hatua za mwanzo kutokana na tukio lile, lakini alichokitaka ilikwa ni kusikia kauli ya Geneviv akimwambia kuwa amemsamehe.

Hakutaka kuendelea kumuwaza sana Geneviv kwani alijua fika kuwa ni mawazo hayohayo ndiyo yaliyomfanya akijikuta anaangukia katika tatizo kubwa la matumizi ya madawa ya kulevya. Hakutaka jambo lile lijirudie tena. Akaona njia bora ni kumsahau jumla na kumtoa kabisa mawazoni mwake. Aliamini kuwa kama Mungu wake amemsamehe basi kila kitu kilikuwa kimekwisha.

Aliamua kwa moyo mmoja kuelekeza nguvu zake zote kwenye masomo na kuzoea mazingira mapya. Licha ya kujitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote, bado hisia za ndani ziliendelea kumshtaki. Ukweli wa kuwa alikuwa amempenda Geneviv kuliko kitu chochote maishani mwake uliendelea kumtesa moyoni mwake.
Stay Tunned!

Sunday, November 8, 2009

ALICIA KEYS ALA SHAVU KWA JIGGER



New York Marekani
Baada ya kufanya vizuri sana kwenye collabo waliyoifanya pamoja, wasanii Shawn Carter Jay Z na Alicia Augello Cook Alicia Keys wanatarajia kuingia upya studio na kutengeneza Remix ya wimbo uliofanya vizuri sana sokoni wa "Empire State Of Mind", wimbo ambao utaingizwa kwenye albam mpya ya Alicia Keys itakayokwenda kwa jina la The Element of Freedom inayotarajiwa kutoka mwezi Disemba mwaka huu.

Wimbo wa Empire State of mind ultungwa na wawili hao kwa ajili ya kulisifia jiji la New York amblo ndio asili yao wote wawili. Jay Z amezaliwa na kukulia katika jiji hilo wakati Alicia Keys naye amlizaliwa na kukulia katika jiji hilo.

RICK ROSE AMSHUKURU 50 CENT



California marekani
Rapa anayeandamwa na mikosi kibao kila kukicha, Rick Ross, hivi karibuni ameibuka na kudai kuwa anamshukuru sana 50 cent kwa madai kuwa ugomvi kati yao umemfanya azidi kupata umaarufu. Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari wakati wa utambulisho wa albamu yake mpya ya Triple C (Custom Cars & Cycles) Ross ameeleza kuwa beef lililodumu kwa muda mfupi kati yake na kiongozi wa G Unit limemuongezea kitu maishani mwake na akzidi kueleza kuwa kwa sasa kila kitu kiko shwari na hawana bifu tena.

Wale wote waliokuwa wanaombea ugomvi wetu uzidi kuwa mkubwa zaidi hawana nafasitena kwani tumeyamaliza kiutu uzima, alikaririwa Ross. Kuonyesha msisitizo, Ross alitumia kifungu cha Biblia kuwadiss waliokuwa wakishabikia beef lao kwa kutaja kifungu cha Biblia kutoka kitabu cha zaburi 27.

Wednesday, October 21, 2009

MY HEART IS BLEEDING (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU) -5

Furaha ya maisha ya mzee Khalfan na familia yake inaanza kuingia doa baada ya kupokea barua ya vitisho ikiwataka kuhama ndani ya nyumba yao katika kipindi cha siku saba.
Hakuna anayetaka kuona hilo likitokea. Khalfan na mkewe wanajadiliana usiku kucha nini cha kufanya mara bada ya kupewa barua ile.
Wanaona njia muafaka ni kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi japokuwa barua ile iliwaonya juu ya kufanya kitu kama hicho.
Wanaamua kujitoa sadaka kwa kwenda kutoa taarifa polisi bila kujali nini kitakachotokea kwani wanaamini polisi ipo kwa ajili ya kuwalinda raia kama wao.
Baada ya siku saba walizopewa kuisha , polisi hawaji kuwapa msaada kama walivyowaahidi, na usiku wa manane nyumba yao inavamiwa na majambazi yenye silaha nzito a kuafanya maangamizi makubwa.
Je nini kitafuatia? twende pamoja…
***
Kulipopambazuka tu, Khalfani na mkewe wakaanza safari ya kwenda kutoa taarifa kwenye kituo kikuu cha polisi cha Blazinia “Blazinia Central police post”. Walienda na barua ile waliyoletewa kama ushahidi wao. Dakika chache baadae walikuwa wameshafika kituoni na wakashuka na kuingia ndani mpaka kaunta ambapo waliomba kukutana na mkuu wa kituo. Muda mfupi baadae wakawa ndani ya ofisi ya mkuu wa kituo, Luteni Lauden Kambi, aliyekuwa akifahamika kwa jina la utani kama “Luteni Fuvu” kutokana na ukatili wake.

Mzee Khalfan alianza kueleza kila kitu kuanzia mwanzo mpaka mwisho, na Luteni akawa anaandika kila kitu kwenye faili jeusi. Alipomaliza kueleza, Luteni Lauden Kambi aliwajibu kwa kifupi kuwa waende nyumbani kwao baada ya kuacha maelezo yote ya msingi ya mahali na mtaa wanakoishi, jeshi litawapa ulinzi baada ya siku hizo saba kupita. Aliwatoa hofu kuwa vile ni vitisho vya kawaida ambavyo vinahitaji ujasiri kuweza kukabiliana navyo. Aliwapa pia maelezo kuwa warudi siku ya sita hapo kituoni ili waambiwe nini cha kufanya. Baada ya kuridhika na maelezo waliyopewa, Khalfan na mkewe waliaga na kurudi nyumbani kwao wakiwa na matumaini makubwa ya kupewa msaada na jeshi la polisi


Siku zikawa zinasonga mbele kwa haraka mno, mara ikafika siku ya sita…yakiwa yamesalia masaa Ishirini na nne tu kabla ya siku ya mwisho waliyoambiwa kuwa wanatakiwa wawe wameondoka katika eneo lile, siku ya Jumapili. Hawakuwa na wasiwasi tena wakiamini wako salama wa kuwa walishahakikishiwa kuwa watapewa ulinzi. Walichokifanya ni kwenda kutoa ripoti Polisi siku moja kabla, yaani Jumamosi Kama walivyokuwa wameelekezwa na mkuu wa kituo cha polisi, Luteni Lauden kambi “Fuvu”.

Wakajitayarisha kwa safari ya kwenda tena Blaziniar Central Police post wakiwa na matumaini makubwa ya kupewa ulinzi. Safari hii gari lao liliendeshwa na Bi Miriam huku Khalfan akiwa ametulia siti ya pembeni. Walipofika waliomba tena kuonana na Mkuu wa kituo. Yule Askari aliyekuwa pale kaunta aliwapa taarifa kuwa Mkuu wa kituo ameanza likizo yake ya mwezi mzima kuanzia siku ya Ijumaa, yaani jana yake na kwa muda huo alikuwa ameshasafiri kurudi kwao alikoenda kuimalizia likizo yake.

Alizidi kuwaambia kuwa shughuli za ukuu wa kituo alikuwa amepewa mtu mwingine ambaye naye alikuwa safarini kikazi. Maelezo yale yalionekana kuwachanganya mno Khalfan na mkewe. Yale matumaini waliyokuwa nayo yakawa yamepotea Kama barafu inavyoyeyuka kwenye moto mkali. Walionyesha hofu na woga waziwazi vikiambatana na kupoteza matumaini Kiasi cha kumfanya yule Askari aliyewapa taarifa ile kushtuka. “Kwani kuna tatizo gani mzee! niambieni labda naweza kuwasaidia hata kama Mkuu hayupo”

Ilibidi mzee Khalfan aanze tena kueleza upya kuanzia mwanzo. Baada ya maelezo yake
yule Askari aliwaomba waongozane mpaka kwenye Ofisi ya Mkuu wa Kituo, wakatafute faili ambalo maelezo yao yalihifadhiwa pamoja ile barua waliyokuwa wameileta kama uthibitisho. Dakika chache baadae wakawa tayari ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Kituo. Yule Askari akaanza kutafuta faili lenye maelezo yao.
‘’Unasema mlikuja kutoa ripoti siku gain?” Yule askari alimhoji mzee Khalfan.
‘’Jumatatu iliyopita afande…‘’
Aliendelea kutafuta maelezo yale kwenye mafaili moja baada ya jingine.
‘’Aliweka maelezo yetu kwenye faili jeusi pamoja na ile barua’’ alizidi kusisitiza Bi Miriam huku wote wakimkodolea macho yule askari aliyekuwa akiendelea kupekua faili moja baada ya jingine. Baada ya kutafuta kwa muda mrefu karibu kila mahali, yule askari aliwageukia mzee Khalfan
na mkewe na akawaambia kuwa labda wasubiri kidogo ampigie simu bosi wake hata kama yuko likizo angewaelekeza alipolihifadhi faili lile.

Wakatoka Ofisini na kurudi kaunta ambako yule askari alinyanyua mkonga wa simu na kuanza kuongea na mkuu wa Luten Lauden Kambi. ‘’Amesema msiwe na wasiwasi, rudini nyumbani ila muache ramani ya mtaa mnakoishi, jina la mtaa, jina la balozi na namba ya nyumba eti ameshaacha maagizo na polisi watakuja kuwapa ulinzi wa kutosha kuanzia majira ya jioni.’’

Alimaliza yule Askari kuwapa maelezo aliyopewa na Mkuu wa kituo kwenye simu. Mzee Khalfan ali shusha pumzi ndefu kisha akamgeukia mkewe, wakatazamana kwa muda kisha yule askari akawapa
Karatasi kwa ajili ya kuacha maelezo ya mahali nyumba yao ilipo, jina la mtaa, jina la balozi na namba ya nyunba. Mzee Khalfan akaanza kuandika upya. Baada ya kuhakikisha kuwa maelezo waliyoyaacha ni sahihi mzee Khalfan na mkewe wakaaga na kuondoka.

Kengere ya hatari ilishalia kichwani mwa Khalfan, akahisi kuna mchezo mchafu unaotaka kuchezwa na askari wale askari. Iweje watoe maelezo mara ya pili ilhali walishahakikishiwa usalama wao?
Hakutaka kumwambia mkewe alichokihisi kwa kuogopa kumuongeza hofu. Wakapanda garini na safari ya kurudi kwao ikaanza safari hii pia hakuna aliyekuwa akimsemesha mwenzake… kimya kimya
mpaka nyumbani.

Masaa yakawa yanazidi kuyoyoma, saa kumi jioni… kumi moja… kumi mbili, mara saa tatu usiku… nne tano kasoro… Hakukuwa na dalili yoyote ya polisi kufika eneo hilo kama walivyoahidiwa na Luten Lauden ‘’Fuvu”. Kwa muda wote huo mzee Khalfan alikuwa nje pamoja na walinzi wake watatu na wengine wawili aliwakodi kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa eneo zima la kuzunguka nyumba yao ili kulinda usalama.

‘’Boss! hao polisi uliosema watakuja tusaidiane nao kazi mbona hawaji na muda ndio unazidi kwenda? saa tano usiku sasa!’’ Alihoji mlinzi mmoja kwa niaba ya wenzake. Mzee Khalfan hakuwa na jibu la kuwapa, zaidi swali lile lilionekana kumchanganya akili. Tangu saa moja jioni alikuwa akiwapa darasa walinzi wake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha bunduki wanazotumia (magobore) yako katika hali ya utayari kwa kazi muda wowote. Alihakikisha pia kuwa bastola yake aliyoachiwa na marehemu mzee Shamsi imejaa risasi za kutosha.

Wote wakawa wamejiandaa vya kutosha wakitegemea muda wowote polisi wangefika kuungana nao kuwasubiri hao wanaotaka kuwadhulumu mali zao kwa nguvu. Walijiandaa kutoa upinzani wa kutosha kwa yeyote ambaye angethubutu kuleta ujeuri wa aina yoyote ile katika eneo lile. Bi Miriam naye alikuwa amewahi kuwaingiza watoto wake ndani mapema kuliko siku yoyote. Wakawahi kula chakula cha usiku kisha wote wakaenda kulala. Alihakikisha milango yote na madirisha yamefungwa ipasavyo.

Mzee Khalfan hakutaka kuingia ndani. Alitaka ashirikiane bega kwa bega na walinzi hata kama polisi hawatafika. Walinzi walimshauri aende ndani kwani walikuwa wakijiamini kuwa wanaweza kazi. Baada ya mabishano kidogo, hatimaye mzee Khalfan alikubali kurudi ndani huku bastola yake ikiwa mkononi “standby” kwa lolote. Muda ukazidi kuyoyoma…mara saa sita usiku… Saa saba na hatimaye saa nane.

Eneo zima lilikuwa kimya kabisa huku giza nene likiwa limetanda kila sehemu. Walinzi walikuwa waki zunguka huku huko kuhakikisha hakuna mtu anayesogelea eneo lile. Bunduki zao zilikuwa “standby” mikononi wakisaidiwa na mbwa mkubwa wa mzee Khalfan. Giza lilikuwa likizidi kushamiri na kufanya hali
ya eneo lile izidi kutisha. Ilishatimia saa tisa usiku huku bado kukiwa kimya kabisa.

Ghafla zilianza kusikika kelele za mbwa aliyekuwa akibweka na kukimbilia kwenye geti kubwa la kuingilia. Walinzi wakajua mambo yameanza, kwa umakini mkubwa nao wakaanza kunyata kuelekea kule mbwa alikokuwa anakimbilia. Alizidi kubweka na walinzi nao wakawa wanazidi kusogea kuelekea kule getini. Mara walishtukia kuona mbwa akipigwa risasi nyingi kichwani kisha akadondoka chini, Puuuh! Ile milio ya risasi ilitosha kuwamaliza kabisa ujasiri wote waliokuwa nao wale walinzi, kwani ilionekana dhahiri maadui zao wamekuja na bunduki nzito za kivita.

Hawakuelewa risasi zimetokea upande gani wakawa wanaangalia huku na huko. Wakiwa bado wanashangaa walishtukia kujikuta wote wamemulikwa na tochi kali kisha mvua ya risasi ikaanza kuwanyeshea. Sekunde chache baadae walinzi wote watano walikuwa chini wakitapatapa kukata roho baada ya shambulizi la ghafla risasi zilikuwa zimepenya vichwani mwao kisawasawa.

Kelele za shambulizi lile ziliwafanya wote waliokuwa ndani ya nyumba ya mzee Khalfan kushtuka. Watoto walianza kupiga mayowe hovyo ya kuomba msaada. Bi Miriam naye alikuwa hajitambui kwa hofu. Mzee Khalfan akapiga moyo konde na kunyanyua bastola yake, akaikamata kisawasawa. Akafungua mlango wa chumbani na kuanza kutoka huku akinyata kwa tahadhari kubwa. Mkewe alijaribu kumzuia asitoke lakini wapi! Akanyatia mpaka sebuleni. Akiwa katikati ya sebule, alishuhudia mlango wa nje ukivunjwa kwa jiwe kubwa kisha watu wapatao saba, wote wakiwa wamevalia makoti marefu meusi, usoni wakiwa wamevaa vitambaa vya kuficha sura zao (masks) , mikononi wakiwa na bunduki nzito za kivita kila mtu ya kwake wakiingia kwa kasi na kumzunguka pale aliposimama…

‘’Weka silaha chini! ‘’ Mmoja wa majambazi yale alimuamuru mzee Khalfan kwa sauti ya ukali mno. Akajikuta akitetemeka mwili mzima kiasi cha kuhisi haja ndogo ikimtoka bila ya ridhaa yake. Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kudondosha bastola yake chini kisha kuinua mikono juu kusalimu amri. Yale majambazi yakaanza kumshambulia kama mpira wa kona. Alipigwa na kitako cha bunduki kichwani akadondoka chini kama mzigo.

Yakaanza kumshushia kipigo cha nguvu kwa zamu zamu. Alijitahidi kujitetea lakini alizidiwa nguvu. Majambazi wengine wakaingia vyumbani na kuwatoa Bi Miriam na watoto wake wote. Kipigo kikaendelea kwa wote… hata mtoto wao mdogo wa mwisho ambaye na miaka miwili tu! Ikawa ni kichapo mtindo mmoja.

Mtoto wa kwanza wa Mzee Khalfan, Khaleed, ambaye kwa kipindi hicho alikuwa na miaka kumi na tatu, alifanikiwa kujificha chini ya meza kabla ya majambazi hayajamuona. Aliendelea kushuhudia jinsi baba’ake, mama’ake na wadogo zake walivyokuwa wakisulubiwa. Uchungu ulimuingia mno kiasi cha kushindwa kuvumilia. Kwa haraka alitoka chini ya meza na kunyanyua chuma kilichokuwa sakafuni, kisha akakinyanyua kwa nguvu zake zote na kukirusha kwa jambazi mmoja. Kilitua sawia kichwani kiasi cha kufanya jambazi lile lidondoke chini.

Akajikuta amedakwa juu juu kama kifaranga cha kuku mbele ya mwewe. Kisha naye akaanza kusulubiwa. Sekunde chache tu baadaye naye akawa ameloa damu mwili mzima kama wenzake. Kichapo kiliendelea mpaka wote wakawa hoi taabani. Yale majambazi yakawafunga wote kwa kamba, mikononi na miguuni na kuwajaza matambara midomoni mwao. Kisha yakaanza kuwaburuza mpaka nje ambako yalianza kuwapakiza kwenye gari yaliyokuja nayo. Yalikuwa yakiwarusha kama magunia,wakati yaiwapakia kwenye Landrover. Gari likawashwa na kuanza kuondoka kwa kasi ya ajabu kuelekea kusikojulikana. Eneo zima liliachwa likiwa limetapakaa damu na maiti tano za walinzi zikiwa zimelala chini. Ukimya ukatawala eneo zima, tena safari hii kukiwa kunatisha zaidi kwani hakuna aliyekuwa amesalia akiwa hai eneo lile.

NICOLE SCHERZINGER AMPA SHAVU SLASH




Mwanadada mkali katika anga ya muziki wa R&B kutoka kundi la The Pussycat Dolls, Nicole Scherzinger, amempa shavu la nguvu memba wa kundi la muziki wa Rock la
Guns N' Roses', aitwaye Slash ambaye anaandaa albamu ya peke yake (Solo Albam) ambayo bado hajaipa jina ila tayari singo moja inayokwenda kwa jina la "Slash & Friends" imeanza kufanya vizuri sokoni.
Wawili hao, Nicole na Slash walipanda jukwaa moja hivi karibuni huko Los Angels ambako walipiga vibao mchanganyiko kutoka makundi yote mawili, The Pussycat Dolls na Guns N' Roses'.


Nicole Scherzinger naye yuko kwenye maandalizi ya albamu ya peke yake (Solo Album) aliyoipa jina la "Her Name Is Nicole". Kiongozi huyo wa The PussyCat Dolls ameeleza kuwa hiyo haimaanishii kuwa amejitoa kutoka katika kundi lake, bali yeye bado ni memba halali wa kundi hilo na anashughulika na shughuli zote za Kundi.

MY HEART IS BLEEDING (MOYO WANGU UNAVUJA DAMU)-4

Mafanikio ya haraka aliyoyapata Khalfan maishani mwake yanaanza kumletea matatizo. Baadhi ya watu wameanza kumonea wivu na wameanza kupanga mbinu za kumuangamiza. Japokuwa anajitahidi kuishi vizuri na kila mtu, maadui wanazidi kuongezeka siku baada ya siku, wengi wakiwa ni marafiki zake wa karibu.

Hilo halimpi hofu kabisa kwa kuwa anaamini hana kosa lolote mbele ya maulana na anaishi maisha ya haki kila siku. Familia yake nayo inazidi kukua huku mtoto wake wa kiume Khaleed akizidi kukua na kuwa na akili za kiutu uzima akiwa angali bado mdogo.

Wanaendelea kuyafurahia maisha yao na kamwe hawako tayari kuona mtu mwingine akipata taabu. Wanawasaidia wote wenye shida na Mungu anazidi kuwabariki. Lakini ghafla mambo yanaanza kwenda mrama.
Twende pamoja…
***

Baada ya miaka kadhaa kupita, walikuwa na jumla ya watoto watano, wazuri wenye furaha na afya njema. Khalfan sasa akiitwa “mzee” khalfan na mkewe Bi Miriam waliyafurahia sana maisha yao na familia yao. Muda mwingi walikuwa sambamba na watoto wao wakiwafundisha maadili mema . Utajiri ukawa unazidi kuongezeka kila kukicha, familia yao ikiwa gumzo kila kona ya mtaaa . Wengine waliendelea kuamini na kuhusisha mafanikio yale na ushirikiana , huku wengine wakiamini kwamba mzee khalfan alikuwa amebahatisha

Lakini ukweli ni kuwa juhudi na maarifa ndivyo vilivyofanya maisha yao yawe gumzo kila sehemu . Siku zikawa zinakwenda, lakini kama walivyosema waswahili penye riziki hapakosi chuki , na ili ufanikiwe zaidi unahitaji kuishi vizuri na kila mtu ingawa huwezi kukwepa kuwa na maadui, taratibu mzee Khalfan akaanza kuhisi kuwa na maadui wasiopenda mafanikio yake, alianza kuhisi marafiki zake anaoshirikiana nao katika shughuli zake za biashara wameanza kumfanyia hila kutokana na mafanikio anayoyapata, hakukosea kabisa . Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Wengi wa marafiki zake waliokuwa wakija kumtembelea pale nyumbani kwake walikuwa wakiyamezea mate mafanikio yake. Wengi walimwona kama hastahili kumiliki mali nyingi na za thamani kama alizokuwa nazo, wakaanza kupanga njama kila mmoja kwa wakati wake , wote wakitaka kumiliki mali zilizokuwa chini ya uangalizi wa khalfan na mkewe Bi Miriam. Hilo halikuwapa sana hofu khalfan na mkewe kwani waliamini Mola wao atawapigania kwa haki kwa kwa hakuna lolote baya walilomfanyia , wala hawakuwa na roho mbaya kwa mtu yeyote yule. Wote waliokuja kuomba misaada ya kimaisha walipewa walichohitaji kwa moyo wa ukarimu.

Ilikuwa ni kawaida ya familia yao kwenda kubarizi ufukweni mwa bahari kila mwisho wa wiki , siku za jumamosi na jumapili wakipendelea kukaa sehemu tulivu wakipunga upepo mwanana wa baharini huku wakibadilishana mawazo na kucheza na watoto wao.

Ilikuwa ni jumapili tulivu , majira ya jioni kabla ya jua halijazama… Khalfan na mkewe walikuwa wakirudi kutoka ufukweni walikokuwa wamekwenda kubarizi pamoja na watoto wao . Bi Miriam ndiye aliyekuwa akiendesha gari huku mumewe akiwa amekaa pembeni yake na watoto wakiendelea kucheza siti ya nyuma , baada ya muda mfupi wakawa wamefika kwenye geti la kuingia kwenye himaya yao . Bi Miriam alipiga honi mfululizo na mlinzi akatoka mbio kuja kuwafungulia.

Baada ya mlinzi kufungua mlango Bi Miriam aliingiza gari mpaka sehemu ya maegesho , akashuka na kumfungulia mumewe mlango naye akashuka kisha wakawashusha watoto wao. Kwa muda wote huo mlinzi alikuwa amesimama pembeni yao akionekana kuwa na jambo alilotaka kumwambia bosi wake, mzee Khalfani. Alisubiri wamalize kushushana ndipo ampe ujumbe aliokuwa amepewa muda mfupi uliopita kabla hawajarudi .

Khalfan aligundua kuwa mlinzi hayuko katika hali ya kawaida ikabidi amsogelee palepale alipokuwa amesimama . Mlinzi alitoa ujumbe aliokuwa amepewa na kumkabidhi mzee Khalfan, ilikuwa ni bahasha ya ukubwa wa kati iliyokuwa imefungwa vizuri. Nje ya bahasha ile hakukuwa na anuani wala jina la mtu aliyetumiwa , ila yalisomeka maandishi makubwa ya wino mwekundu “SIRI”.

Kilichomshtua khalfan ni jinsi mlinzi alivyokuwa na hofu wakati akimkabidhi ujumbe ule, alijaribu kumhoji juu ya mtu aliyeileta barua ile lakini akawa anamjibu kwa kubabaika. Alieleza kuwa muda mfupi uliopita gari ndogo nyeusi na ya kifahari ikiwa na vioo “TINTED” vya rangi nyeusi iliwateremsha wanaume wawili waliovalia makoti marefu meusi na kofia kubwa zilizoficha sura zao, mmoja akaenda mpaka pale mlangoni na mwingine akawa amebakia kwenye gari.

“Bila hata salamu akanipa bahasha na kusema nikupe wewe ukirudi!” Aliendelea kueleza mlinzi. Khalfan hakutaka kuhoji zaidi, akachukua ile bahasha na kuingia nayo ndani. Muda huo mkewe alikuwa ameshatangulia ndani na watoto akawa anaendelea kuwaandalia chakula cha jioni. Akapitiliza mpaka chumbani na kwenda kuifungua bahasha ile.

Alijikuta mikono ikianza kutetemeka alipoanza kuifungua bahasha ile akakutana na maandishi ya wino mwekundu ambayo yalisomeka vizuri. Ulikuwa ni ujumbe uliojaa vitisho na maneno ya kibabe, ukimtaka eti ‘ahame hapo nyumbani kwake yeye na familia yake yote bila kuchukua kitu chochote kwa sababu yeye Khalfan hakuwa mmiliki halali wa eneo hilo. Ujumbe ule ulizidi kutishia kwamba wanampa siku saba za kuwa ameshaondoka na onyo kali likatolewa kuwa asijaribu kutoa taarifa sehemu yoyote kwa kuwa kwa kufanya hivyo angehatarisha uhai wake.’

Alijikuta akicheka kwa dharau na kisha akatoka na ile bahasha mpaka sebuleni alikokuwa amekaa mkewe na watoto wake wakiangalia luninga. Mkewe alishtuka kumuona mumewe ameanza kubadilika, ingawa usoni alikuwa akicheka lakini alionekana kuchanganyikiwa sana akampa ule ujumbe ili na yeye ausome.

“Unatakiwa uhame hapo unapoishi wewe na familia yako bila kuchukua kitu chochote. Huna haki ya kumiliki eneo zuri kama hilo, wamiliki halali tupo na tulikuwa tunangoja muda ufike tukuambie.

Usijaribu kutoa taarifa sehemu yoyote , polisi wala jeshini kwani kwa kufanya hivyo utahatarisha usalama wako na hizo takataka zako (mkeo na watoto) unapewa siku saba za kutekeleza amri hii na ukiipuuza utaona matokeo yake”

NB. Uhai hautafutwi ila mali zinazotafutwa
By
Wamiliki

Bi Miriam alishusha pumzi ndefu baada ya kumaliza kuisoma, huku akiwa amepigwa bumbuwazi asijue nini cha kufanya. Kwa muda wote huo Khaflan alikuwa akizunguka-zunguka pale sebuleni akiwa haelewi anatafuta nini . watoto walikuwa hawana habari wakawa wanaendelea kucheza na kuruka kwenye masofa ya kisasa yaliyokuwepo pale sebuleni.

Khaflan alirudia kuisoma barua ile kisha akatoka kwa kasi kumfuata mlinzi nje. Alianza kumhoji upya ni nani aliyeleta ujumbe ule na mlinzi akarudia maelezo kama aliyoyatoa mara ya kwanza. Safari hii alionekana kuhofia zaidi baada ya kumuona bosi wake amechanganyikiwa.

Hakujua mle ndani mliandikwa nini lakini kwa hal aliyokuwa nayo bosi wake ilionyesha kuna jambo baya. Mzee Khalfan alirudi ndani na kumuelekeza mkewe awape chakula watoto haraka kisha akawalaze . Alipitiliza mpaka chumbani na kujitupa kitandani kama mzigo.

Maswali mengi yalikuwa yakipishana kichwani kama umeme wa gridi ya taifa . Alijalibu kuwaza na kuwazua ni akina nani walioleta ujumbe ule, hakupata jibu. Muda mfupi baadae mkewe akawa ameshamaliza kuwapa chakula wanae na akaenda kuwalaza kwenye chumba chao. Ama kwa hakika usiku huo ulikuwa ni usiku wa mauzauza kwao. Mpaka jogooo la kwanza linawika kuashiria mapambazuko, Khalfani na mkewe walikuwa hawajapata hata tone la usingizi.

Usiku kucha walikuwa wakijadiliana wafanye nini, hakuna aliyekuwa na jibu. Mwisho wakafikia uamuzi wa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi ingawa barua ile iliwaonya vikali juu ya uamuzi huo.
“Lakini mume wangu , si ni bora tuondoke tu tuwaachie wafanye wanachotaka ? nahofia usalama wa wanangu, tuondoke tu Mungu atatusimamia huko tuendako kwani mali hutafutwa lakini uhai hautafutwi.”
Wazo hilo halikuingia akilini mwa mzee Khalfani, kwani kufanya hivyo kungemaanisha yeye ni mwanaume dhaifu asiyeweza kuilinda familia yake aliamua kutetea msimamo wake.

”Mke wangu siko tayari hata kwa mtutu wa bunduki kuruhusu watu wengine wayaharibu maisha yetu! niamini nitafanya kila niwezalo kukulinda mke wangu na wanangu na mali zangu zote! Hakuna wa kuchukua chochote kutoka mikononi mwetu, siwezi kusalimu amri kirahisi namna hii, niamini…”

Kwa jinsi alivyokuwa akiongea kwa kujiamini, mkewe akapata imani kuwa usalama wao utalindwa kwa kila namna. Kulipopambazuka tu, mzee Khalfani na mkewe wakaanza kujiandaa kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Blazinia Central Police Post”.

Walichukua barua ile kama ushahidi wa maelezo yao. Mzee Khalfan aliendesha gari lao huku mkewe akiwa pembeni yake. Hakuna aliyemsemesha mwenzake! Kila mtu alikuwa kwenye lindi zito la mawazo, maneno ya barua ile yalikuwa yakijirudiarudia vichwani mwao.
***

Kenyan building collapses, killing 6 and injuring 13; experts blame poor construction



Six people died and 14 were still missing after a three-story building collapsed on the outskirts of the country's capital, a police official said Tuesday, as experts warned that irresponsible contractors were to blame.

Policeman Samuel Mukindia said two people died while receiving treatment at a Nairobi hospital. The bodies of three men were pulled from the rubble at the building site in Kiambu. Another victim, a woman, was crushed to death. Police said 13 people were injured.

The Kenya Red Cross said 14 people were still unaccounted for after being reported missing by their relatives and friends.

Millicent Wairumu said she believed her younger brother David Wachira was trapped in the rubble. She cooked him breakfast Monday morning and asked him to work in her shop. He declined her offer, saying he wanted to earn his own money and he was already staying in her house.

"I can't reach him on his mobile phone," she wept as she dialed his number on her phone. "He should not have been here. I should have insisted he came to work for me."

Monday's disaster came barely a week after the Kenya Architectural Association said in a report that 65 percent of structures in the country were substandard.

Richard Chepkwony, a member of the Institution of Engineers of Kenya, said the organization was receiving almost daily reports of buildings collapsing because of poor construction. He said the building collapsed on Monday because of its substandard construction material and poor workmanship.

"If you grab a block of concrete, you can crack it using your hands," he said, crushing lumps of concrete between his fingers. "This is not the end of the story. We will be seeing more of this if the government does not enact laws to ensure required construction standards are met."

Building collapses are common in Africa. Corrupt planning officials, substandard materials and poor workmanship are often to blame.

Monday, October 19, 2009

MY HEART IS BLEEDING ( MOYO WANGU UNAVUJA DAMU)-3

Wakati kesi nzito inayomkabili kijana mdogo anayeshtakiwa kwa kufanya mauaji makubwa na ya kutisha ikiendelea kugusa hisia za maelfu ya watu, kitu cha ajabu kinatokea mahakamani.

Jaji mkuu Profesa Kadir Mudhihir Simba anaanguka mahakamani na kupoteza fahamu akiwa katika hatua za mwisho za kutoa hukumu. Anakimbizwa Hospitali hali yake ikiwa mbaya sana na kadri muda unavyozidi kwendahali yake inakuwa mbaya zaidi.

Huku nyuma anaacha watu wakiwa wamepigwa na bumbuwazi wakiwa hawaelewi nini kilichomsibu na tukio lile linamaanisha nini. Vurugu nyingine inazuka mahakamani lakini polisi wa kutuliza ghasia wanaidhibiti na kufankiwa kumrudisha mshtakiwa gerezani.

Watu wanaanza kufuatilia chanzo cha tukio lile miaka mingi iliyopita. Historia inaonyesha kila kitu kilivyokuwa mpaka kumsababisha kijana yule kufanya mauaji makubwa kiasi kile yaliyotikisa nchi.

Twende pamoja ufahamu chanzo...
Kwa jinsi wazazi wa Miriam, Mzee Shamsi na mkewe walivyokuwa wakimpenda mkwe wao, ilibidi wamshawishi Khalfani pamoja na mkewe Miriam wahamie nyumbani kwa Mzee Shamsi. Mzee Shamsi na mkewe hawakuwa na mtoto mwingine zaidi ya binti yao Miriam, hivyo kuondoka kwake na kumfuata mumewe, kuliwafanya wabaki wapweke sana kwenye himaya yao.

Khalfan na mkewe hawakuwa na kipingamizi chochote, wakakubali kuhamia nyumbani kwa mzee Shamsi, (Ukweni). Maisha yao yakazidi kuwa mazuri siku baada ya siku, na sasa Khalfan akawa ameachana na biashara yake ya mboga mboga na matunda.

Badala yake akawa akimsaidia mzee Shamsi kwenye shughuli zake za Biashara ya madini ya Ruby. Muda mwingi akawa akitembezwa kwenye gari ndogo aina ya “Mercedes Lexus 5 New Model” ya kisasa, akimwonyesha vitega uchumi vyake na kumwelelekeza jinsi ya kuhudumia mali zote walizokuwa nazo.

Kwa kifupi mzee Shamsi alimuamini sana Khalfan, kiasi cha kumchukulia kama mwanae wa kumzaa. Hakumficha kitu chochote, alikuwa akimpa mpaka siri zake za ndani. Aliamini kuwa kwa kuwa hakubahatika kupata mtoto wa kiume, basi khalfan ndio atakuwa mrithi wa mali zake zote akishirikiana na mkewe Miriam.

Alichokuwa akimsisitiza siku zote ni kumpenda kwa dhati mkewe, mtoto wao wa pekee Miriam. Alikuwa akimuonya pia kuwa makini sana na marafiki wa kibiashara ambao atakuwa akishirikiana nao hususani kwenye bashara ya madini kwani akili za mwanadamu hubadilika sana akiona vitu vya thamani. Nasaha alizokuwa anapewa kila siku zilimjenga upya kifikra na kumpa ujasiri kuliko ilivyokuwa mwanzo. Alijiona anaweza kufanya mambo makubwa hata kama hakuwa na elimu kubwa kichwani

Ilikuwa ni majira ya saa nne asubuhi, Miriam akiwa anamuandalia mumewe Khalfan kifungua kinywa, huku wakitaniana utani wa mume na mke! Kila mmoja alikuwa na furaha kuwa na mwenzake. Wakawa wakitaniana na kucheza kama watoto huku Miriam akiendelea kuandaa kifumgua kinywa.

Wakati hayo yakiendelea taarifa ya habari iliyokuwa inasomwa kutoka kituo maarufu cha redio, “The Bulletin FM” iliwashtua wote kiasi cha kufanya kila mtu aache alichokuwa anakifanya na kukimbilia jirani na redio ili asikie vizuri taarifa ile.

Ilikuwa ni habari mbaya ya ajali ya kutisha ya ndege iliyotokea muda mfupi uliopita. Ajali hiyo ilihusisha ndege ya kampuni ya “TRY EMIRATES” aina ya Jet B710 Sossoliso, iliyokuwa inatoka uwanja wa kimataifa wa Blazinair International Airport (BLIA) kuelekea Muscat Oman. Habari ilizidi kuelezea kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hitilafu katika moja ya injini zake, hali iliyosababisha ndege hiyo kulipuka muda mfupi baada ya kuruka, kisha ikaangukia baharini.

Kilichosikitisha ni kwamba abiria wote 67 waliokuwemo kwenye ndege walikuwa wakihofiwa kupoteza maisha katika ajali ile. Habari ilihitimishwa kwa mahojiano na watu walioshuhudia ajali ile ambapo kila aliyehojiwa alikiri kuwa hakuwahi kusikia wala kushuhudia ajali mbaya kama ile.

Khalfan na mkewe walibaki wakikodoleana macho, wasijue nini cha kufanya. Kilichowashtua ni kwamba ni asubuhi ya siku hiyo masaa machache tu yaliyopita walitoka kuwasindikiza mzee Shamsi na mkewe uwanja wa ndege, wakielekea oman kupeleka biashara yao ya madini ya Ruby.

Haikuwa kawaida kwa mzee Shamsi kusafiri na mkewe, kwani mara zote yeye aliposafiri mkewe alibaki kuwa msimamizi wa mali zao, lakini baada ya binti yao kuolewa na Khalfan Mwalukasa, shughuli zote za usimamizi wa mali zilibaki kuwa chini ya uangalizi wa Khalfan kwani walimchukulia kama mtoto wao, na kwa pamoja walikubaliana kuwa yeye ndiye atakayekuwa mrithi wa mali zao, pindi mauti yatakapowafika.

Ni masaa mawili tu yaliyopita majira ya kama saa mbili za asubuhi Khalfan na mkewe waliwasindikiza wazazi wao uwanja wa ndege na wakasubiri mpaka walipopanda ndege ya kampuni ya usafiri wa anga ya TRY EMIRATES tayari kwa safari ya Oman. Ni baada ya kuhakikisha kuwa wamepanda ndege, ndipo Khalfan na mkewe waliporudi nyumbani kuendelea na shughuli zao.

Wakiwa wanajiandaa kupata kifungua kinywa ndipo taarifa ya kusikitisha na kutia majonzi iliposikika. Hiyo ilimaanisha kuwa mzee Shamsi na mkewe walikuwa wamepoteza maisha katika ajali ile. Msiba mkubwa kiasi gani. Habari ya ajali ile iliwashtua watu wengi, ambao kwa namna moja au nyingine waliwapoteza ndugu, jamaa na marafiki zao waliokuwemo kwenye ndege ile.

Kwa Khalfan Mwalukasa, licha ya ukweli kwamba aliguswa na vifo vya wakwe zake, hii ilikuwa ni kama bahati ya mtende kuota jangwani, waswahili wanasema kufa kufaana. Ni Khalfan huyu huyu aliyekimbia kwao kutokana na ugumu wa maisha, akawa akifanya biashara ya mbogamboga na matunda, ndiye sasa alitakiwa kuwa mmiliki wa hazina ya utajiri ulioachwa na mzee Shamsi. Hakuwahi kuota wala kutegemea kuwa ipo siku atakuja kumiliki hazina kubwa ya utajiri kama ile. Kweli Mungu alikuwa ametenda miujiza katika maisha yake.

********

Siku ziwaka zinakwenda, sekunde, dakika, masaa! Mara usiku, mara mchana… mawio na machweo. Kumbukumbu ya kuwapoteza wazazi mzee Shamsi na mkewe taratibu ikaanza kupotea vichwani kwa Khalfan na mkewe Miriam. Khalfan akawa anajitahidi kwa kadri ya uwezo wake wote kumliwaza mkewe na kumfaya asahau yote yaliyotokea. Yeye ndiyo akawa baba na kichwa cha familia.

Mwanzoni ilimuwia vigumu kuweza kusimamia mali zote zilizoachwa na mzee Shamsi lakini kila alipokuwa akikumbuka mawaidha aliyokuwa anapewa na mzee Shamsi, akawa anajipa moyo kuwa hakuna lisilowezekana. Taratibu akawa anapata uzoefu kila siku mpya ilipokuwa ikianza. Hali hiyo ilionekana kumfariji sana mkewe, ambaye sasa akawa na uhakika kuwa kila kitu kitaendelea vizuri na kushamiri japokuwa alikuwa amepoteza wazazi wake.

Khalfan akawa anajituma kwa bidii kuhakikisha kuwa hakuna kinachomshinda.
Baada ya miezi saba tangu mzee Shamsi na mkewe wapoteze maisha katika ajali mbaya ya ndege, Miriam akiwa anarudi kutoka hospitali alikuja na habari njema kwa mumewe!

“Mume wangu, nafurahi kukuambia kuwa baada ya siku si nyingi nitakuzalia mtoto!”
“Unasema kweli mke wangu? Safi sana!” Khalfan akiwa haamini, alimkumbatia mkewe kwa nguvu… na hapo ndipo naye alipoelewa mkewe alikuwa anamaanisha nini. Mkewe alikuwa mjamzito, furaha iliyoje! Maisha yakawa kama ndio yameanza upya, muda wote wakawa wakicheza kama watoto, wakishinda kutwa nzima katika bustani za maua zilizokuwepo hapo nyumbani.

Muda ukawa unazidi kwenda, huku Khalfan akiwa anampeleka mkewe Clinic mara kwa mara, kuhakikisha anajifungua salama. Miezi ikawa inakatika, hatimaye miezi tisa ikawa imetimia. Bi Miriam akajifungua salama mtoto wa kiume, mzuri kama mama yake. Furaha katika ndoa yao ikawa imeongezeka mara dufu, na ikawa inazidi kuongezeka kila uchao.

Wakampa mtoto wao jina la Khaleed . “Mume wangu yaani furaha unayonipa maishani, sikuwahi kutegemea hata siku moja! Nakupenda sana mume wangu na Mungu azidi kuibariki ndoa yetu tudumu mpaka kifo kitakapo tutenganisha” Bi Miriam alikuwa akiongea kwa hisia nzito za mahaba kwa mumewe wakiwa na kichanga chao Khaleed, wakipunga upepo wa jioni.

Baada ya miaka miwili wakapata mtoto mwingine wa kiume, tofauti na kaka yake, yeye alifanana mno na baba yake. Watoto wakawa na afya njema, furaha na walipewa malezi bora.

Khalfan sasa akawa baba wa familia, mkewe Miriam naye akawa mama kama alivyokuwa akitamani siku zote. Waliyafurahia sana maisha yao. Muda mwingi walikuwa sambamba wakisaidiana kuwapa malezi bora watoto wao na kuwafundisha maadili mema. Utajiri nao ukawa unazidi kuongezeka kila kukicha, shamba na bustani zao za maua zikawa zinazidi kushamiri na kuwa “Evergreen” huku mazao yakistawi sana.

Wapo watu walioyahusisha mafanikio yale na imani za kishirina wakihisi kuwa huenda Khalfan Mwalukasa alikuwa akitumia nguvu za giza ili kupata mafanikio. Wapo walioanza kummezea mate wakiona kuwa hakustahili kuwa na mafanikio makubwa kama yale. Wala maneno ya walimwengu hayakuwarudisha nyuma. Walikuwa waimwamwini Mungu wao na walijitahidi kuishi vizuri na kila mtu, wakitoa misaada mingi ya kijamii kwa watu wenye shida na wanaoishi katika mazingira magumu.

Waliwasaidia pia watoto wenye shida mbalimbali hasa wale waliokuwa wakiishi kwenye mazingira magumu bada ya kufiwa na wazazi wao ama kutokana na hali duni za wazazi wao. Walijtahidi kwa kadri ya uwezo wao wote kugawana kile walichojaaliwa na Mungu kwa wale ambao hawakuwa nacho. Kadri muda ulivyokuwa unaenda wakazidi kujijengea jina na umaarufu huku kila mwenye shida akikimbilia kwao kuomba msaada.

Walifanikiwa pia kuanzisha kituo cha kulelea watoto yatima na wale wa mitaani, na wakaamua kukipa jina la “Shamsi Memorium Orphanage” ikiwa kama kumbukumbu ya mzee wao Shamsi na mkewe waliokuwa wameshatangulia mbele za haki.

Tukutane next issue!

SHED NO MORE TEARS ( USILIE TENA GENEVIV) -3

Mzee Manuel Rwakatare anafanikiwa kumuokoa mwanae Geneviv kutoka kwenye mazingira ya kutisha lakini anakuwa tayari ameshachelewa “its too late…” kwani tayari Geneviv ameshaharibiwa vibaya. Kila kitu maishani mwake kimebadilika, maisha yamepoteza maana, anazidi kuuchukia ulimwengu, zaidi anawachukia wanaume… anatamani kufa kuikwepa aibu kubwa iliyoko mbele yake. Ni ndani ya siku moja tu, tayari amebakwa na wanaume watano, wanne wakiwa ni wanafunzi wahuni na mmoja akiwa ni askari polisi.
Sasa endelea…

Oooh my God! Bi Patricia alijikuta akipiga kelele baada ya kumuona mumewe akiingia ndani huku akiwa amembeba mwanae Geneviv begani akiwa hajitambui.

“What happened to my daughter,oooh…”
Kwa haraka akampokea Geneviv huku mwili wote ukimtetemeka. Akampeleka chumbani kwake na kumlaza kitandani huku mumewe akianza kuhangaika kutafuta huduma ya kwanza. Kila mtu akawa kama amechanganyikiwa, na zaidi Bi Patricia ambaye bado alikuwa hajajua nini kimemtokea mwanae. Kengele ya hatari ikalia kichwani mwa Bi Patricia wakati akiendelea kumchunguza Geneviv ambaye alikuwa hajitambui.

Kitu cha kwanza alichoshtushwa nacho ni kuona jinsi nguo za mwanae zimechanwa-chanwa. Akiwa bado anamchunguza akashtushwa na damu zilizoiloanisha sketi ya mwanae, mapigo ya moyo yakaanza kumwenda mbio…hakutaka kuamini haraka kuwa anachokihisi ndicho kilichomtokea mwanae.

Alitamani iwe ndoto lakini naye hakuweza kuubadili ukweli,akajikuta akipiga yowe kubwa na kuanza upya kuomboleza baada ya kubaini kuwa ni kweli mwanae alifanyiwa ushetani na wanaume.

“Cant believe this…I cant! Unaona ulichomsababishia mwanangu, haya furahi sasa malengo yako yametimia, ooh my Lord!”
Bi Patricia akawa anampiga-piga mumewe mgongoni huku akilia kwa uchungu. Akawa anamlalamikia kuwa yeye ndio chanzo cha yote.

“Mke wangu acha kunilaumu, mbona nimekiri makosa! Cha msingi kwa sasa tusaidiane kuokoa maisha ya geneviv, huu sio muda wa lawama.”
Bi Patricia alikuwa mgumu wa kuelewa na akazidi kulia kwa sauti kubwa kiasi cha kuwaamsha majirani ambao baada ya muda mfupi walikusanyika nje.Baada ya majadiliano ya muda mfupi,muafaka ukafikiwa kuwa Geneviv apelekwe hospitali haraka usiku huo huo.Kila mtu alimuonea huruma.

Jirani mmoja akajitolea kutoa gari lake na kwa haraka Geneviv akabadilishwa nguo na safari ya kwenda hospitali ikaanza mara moja. Japokuwa mvua kubwa ilikuwa inaendelea kunyesha hakuna aliyeonekana kujali, kila mtu akawa anahangaika kuokoa maisha ya Geneviv.

Baada ya kitambo kifupi, gari walilompakia mgonjwa likakwama kwenye matope kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha, hali iliyowalazimu mzee Rwakatare na dereva waanze kusaidiana kulitoa gari pale lilipokwama.Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, huku hali ya Geneviv ikizidi kuwa mbaya, Mzee Rwakatare akaamua kumbeba Geneviv na kuendelea na safari ya kuelekea Hospitali.

“Lakini mvua hii ni hatari kwa mgonjwa, ukizingatia bado radi zinapiga sana, kwanini tusiendelee kulihangaikia gari?”
Dereva alitoa ushauri ambao Mzee Rwakatare alishindwa kuuafiki. Akamuinua mwanae na kumuweka begani na safari ikaendelea. Bi Geneviv naye akashuka na kuanza kuwafuata kwa kukimbia huku akizidi kulia. Dereva akabaki ameduwaa akiwaonea huruma kwa yaliyowakuta.

Baada ya safari ndefu na ngumu, hatimaye walifika kwenye hospitali ya planet Health Aid ambako walipokelewa na manesi waliokuwa zamu na upesi upesi Geneviv akawekwa juu ya kitanda cha wagonjwa na kuanza kukimbizwa kuelekea wodini. Kwa haraka akaanza kupewa huduma ya kwanza. Baada ya muda mfupi alitundikiwa dripu za maji ambazo zilikuwa zikitiririka kwa kasi kuingia mishipani mwake. Saa ya ukutani ya pale hospitali ilionyesha kuwa tayari ni saa kumi ya alfajiri.

Mzee Rwakatare na mkewe wakabaki nje ya wodi wakiwa wamekaa kwenye viti sehemu ya mapokezi huku kila mmoja akiwa amejiinamia kimya. Baada ya muda mfupi nesi akatoka wodini akiwa na faili mkononi mwake na kumuita mzee Rwakatare pembeni.

“Pole mzee!” yule nesi alimpa pole mzee Rwakatare na kabla hata hajajibu kitu akaendelea kuongea…
“Mgonjwa anaendelea kupata huduma ya kwanza na muda si mrefu atazinduka. Uchunguzi wetu umebaini kuwa amebakwa, na kwa taratibu za hospitali zote nchini ni kwamba mgonjwa wa namna hii lazime apitie kituo kikuu cha polisi kuchukua PF3 kwanza ndipo atibiwe, ila kwa kuwa mgonjwa wenu alikuwa na hali mbaya tukaona ni bora tuendelee kumpa huduma ya kwanza, ila matibabu ataanza kupewa baada ya w ewe kuleta hiyo PF3”

Alimaliza kuongea yule nesi na kurudi wodini akimuacha Mzee Rwakatare ameduwaa asijue la kufanya.
Bi Patricia aliinuka haraka na kumfuata yule nesi kabla hajaingia ndani na akawa anamhoji hali ya mgonjwa.

“Maelekezo yote nimempa mzee, nenda atakueleza vizuri”
Aliongea yule nesi kwa kifupi huku akifunga mlango.

Bi Patricia alirudi kwa mumewe aliyeonekana kuchanganyikiwa, akamshika mkono na kumkalisha chini huku akiwa na shauku ya kutaka kujua yule nesi alimwambia nini.

Ukweli ni kwamba tangu usiku alipomuokoa mwanae, mzee Rwakatare alikuwa hajamwambia chochote mkewe juu ya jinsi alivyomuokoa na mazingira aliyomkuta kutokana na hali aliyokuwa nayo mkewe. Ilibidi aanze kumueleza tangu mwanzo jinsi alivyomuokoa Geneviv kabla ya kumwambia maelekezo aliyopewa na yule nesi.
Baada ya kumaliza maelezo marefu, wote walishusha pumzi ndefu wakabaki wakitazamana wasijue nini cha kufanya.

“Sasa tutafanya nini mume wangu, tukizidi kuzubaa tutampoteza mtoto wetu…please do something to save her.”
“Sasa wewe unafikiri mi ntafanya nini, Polisi siwezi kwenda kwa sababu hao ndio walioniharibia mwanangu, isitoshe nimesababisha madhara pale kituoni.Huoni kuwa nikienda nitakuwa nimejipeleka mwenyewe? I cant report anything to them. They are all rotten.”

Mzee Rwakatare na mkewe waliendelea kubishana kuhusu kwenda kuchukua PF3 kama walivyoelekezwa na yule nesi. Mwishowe walifikia uamuzi wa kutokwenda. Wakaamua kumueleza yule nesi ukweli kuwa mtoto wao alibakwa na Polisi haohao hivyo haikuwa na maana kwenda tena kwao kuomba kibali.

“Lakini vipimo vyetu vinaonyesha kuwa amebakwa na watu si chini ya watano, nyie mlikuwa wapi mpaka mtoto anafanyiwa ukatili mkubwa namna hii” Yule nesi alizidi kuongea kwa msisitizo huku akionekana kuwatupia lawama wazazi kwa kushindwa kumlinda binti yao.

“Nesi sio kweli, mwanangu hajabakwa na watu watano, no! mbona bado mdogo,au mmekosea vipimo…Ooh my God! I cant believe th..i…s….”
Bi Patricia alikuwa akimbishia nesi wakati akielezwa ukweli wa yaliyomkuta mwanae huku akilia. Mzee Rwakatare alibaki ameduwaa na yeye akiwa haamini alichokisikia kutoka kwa nesi.

“Anyway, cha msingi we tusaidie mtoto atibiwe,mengine tutazidi kuelekezana taratibu.”

Mzee Rwakatare aliongea kwa kukata tamaa na kwa bahati nzuri yule nesi aliwaelewa. Akarudi wodini na kuanza kumpa matibabu Geneviv ambaye fahamu zilikuwa bado hazijamrudia.

Si mzee Rwakatare wala mkewe waliokuwa tayari kuamini kuwa ni kweli mtoto wao amebakwa na watu zaidi ya watano. Mzee Rwakatare alishindwa kuyazuia machozi yasimtoke, ikawa ni zamu ya mkewe kumbembeleza. Alikuwa akijihisi mwenye hatia kubwa sana mbele ya mwanae na mkewe na zaidi mbele ya Mungu.

Alianza kuamini sasa kuwa ni kweli pombe badala ya kupunguza matatizo ilikuwa ikiongeza.Alijilaumu sana kwa ujinga alioufanya na kumsababisha madhara makubwa namna ile.
“One mistake, five goals…F*ck me because im the source…”
Alikuwa akijisemesha peke yake kama mwendawazimu huku akijipigapiga kichwani.

****************
Mpaka inafika saa mbili asubuhi Geneviv alikuwa bado hajazinduka hali iliyoanza kuwatia hofu hata wale manesi.

“It seems she has been severely damaged in her genitals, Hydro-saline therapy is over and yet the condition is still worse. Lets call the Doctor for emergency”
(Inaonekana ameumizwa sana, dawa tulizompa zinaisha lakini bado hali ni mbaya, inabidi tumuite daktari kwa huduma ya dharula)

Wale manesi waliokuwa wanamhudumia Geneviv tangu usiku walikuwa wakijadiliana nini cha kufanya baada ya kuona hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya kadri muda ulivyokuwa unaenda. Ikabidi Geneviv ahamishiwe chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U (Intensive care unit) ambako alianza kupewa huduma ya dharula ili kuokoa maisha yake.

“Inject her the Ant-spermatids serum, then add Oestrogen 20mls into Hydro-saline therapy… If this will fail to awake her, it will be out of our control”

(Mchomeni sindano ya dawa ya Ant-spermatid, kisha ongezeni mililita 20 kwenye dripu yake yenye dawa… kama bado atashindwa kuzinduka basi itakuwa nje ya uwezo wetu)

Aliongea daktari Bingwa wa magonjwa ya kina mama na watoto, Dokta Barikieli Zayumba akiwaelekeza manesi namna ya kufanya. Kwa muda wote huo, Bi Patricia na mumewe walikuwa wameshikana mikono nje wakiomba sala mfululizo, wakimuomba Mungu wao amnusuru Geneviv

Je nini kitaendelea? Geneviv atapona? Waliohusika watachukuliwa hatua gani?

OBAMA KUHALALISHA MATUMIZI YA MARIJUANA






WASHINGTON – Federal drug agents won't pursue pot-smoking patients or their sanctioned suppliers in states that allow medical marijuana, under new legal guidelines to be issued Monday by the Obama administration.

Two Justice Department officials described the new policy to The Associated Press, saying prosecutors will be told it is not a good use of their time to arrest people who use or provide medical marijuana in strict compliance with state law.

The guidelines to be issued by the department do, however, make it clear that agents will go after people whose marijuana distribution goes beyond what is permitted under state law or use medical marijuana as a cover for other crimes, the officials said.

The new policy is a significant departure from the Bush administration, which insisted it would continue to enforce federal anti-pot laws regardless of state codes.

Fourteen states allow some use of marijuana for medical purposes: Alaska, California, Colorado, Hawaii, Maine, Maryland, Michigan, Montana, Nevada, New Mexico, Oregon, Rhode Island, Vermont and Washington.

California is unique among those for the widespread presence of dispensaries — businesses that sell marijuana and even advertise their services. Colorado also has several dispensaries, and Rhode Island and New Mexico are in the process of licensing providers, according to the Marijuana Policy Project, a group that promotes the decriminalization of marijuana use.

Attorney General Eric Holder said in March that he wanted federal law enforcement officials to pursue those who violate both federal and state law, but it has not been clear how that goal would be put into practice.

A three-page memo spelling out the policy is expected to be sent Monday to federal prosecutors in the 14 states, and also to top officials at the FBI and Drug Enforcement Administration.

The memo, the officials said, emphasizes that prosecutors have wide discretion in choosing which cases to pursue, and says it is not a good use of federal manpower to prosecute those who are without a doubt in compliance with state law.

The officials spoke on condition of anonymity because they were not authorized to discuss the legal guidance before it is issued.

"This is a major step forward," said Bruce Mirken, communications director for the Marijuana Policy Project. "This change in policy moves the federal government dramatically toward respecting scientific and practical reality."

At the same time, the officials said, the government will still prosecute those who use medical marijuana as a cover for other illegal activity. The memo particularly warns that some suspects may hide old-fashioned drug dealing or other crimes behind a medical marijuana business.

In particular, the memo urges prosecutors to pursue marijuana cases which involve violence, the illegal use of firearms, selling pot to minors, money laundering or involvement in other crimes.

And while the policy memo describes a change in priorities away from prosecuting medical marijuana cases, it does not rule out the possibility that the federal government could still prosecute someone whose activities are allowed under state law.

The memo, officials said, is designed to give a sense of prosecutorial priorities to U.S. attorneys in the states that allow medical marijuana. It notes that pot sales in the United States are the largest source of money for violent Mexican drug cartels, but adds that federal law enforcement agencies have limited resources.

Medical marijuana advocates have been anxious to see exactly how the administration would implement candidate Barack Obama's repeated promises to change the policy in situations in which state laws allow the use of medical marijuana.

Soon after Obama took office, DEA agents raided four dispensaries in Los Angeles, prompting confusion about the government's plans.

___

Tuesday, October 13, 2009

KEYS TO SUCCESS- VOL 1

What “Real World” Outcomes Can you Expect?

- Money

o Direct more money into your life than ever before
o Finally get paid what you deserve
o Get recognized as a leader and ultimately have job security
o Take your personal business to the next level effortlessly and easily
o Have people calling you and approaching you for your services

- Mind

o Destroy fear in your life once and for all so that you can walk tall, with confidence and conquer everything that comes your way
o Create unbreakable self confidence in your self, your beliefs, and who you stand for being in life
o Have absolute certainty in any and all decisions you make
o Finally be stress free (wow, can you imagine what that will feel like)
o Trust your intuition, your brilliant mind and ideas.

- Body

o Effectively lose the weight and create your ideal body that you absolutely fall in love with (and so will everyone else)
o Quit smoking, drinking, overeating, or any other unhealthy habit that you have been dreaming of finally letting go of for good
o Accept yourself for who you are and truly loving every inch of your self, inside and out

- Soul

o Forgive those that have hurt you in the past so that you can be free to move forward in your life
o Find the beautiful lesson in everything that you’ve experienced in life so that you can grow faster than you ever imagined
o Honor yourself like you’ve never experienced before

- Love/Relationships

o Create an amazingly loving relationship with your partner
o Have an unbreakable trusting relationship with your kids (or your parents)
o Learn how beautiful or handsome you truly are and naturally attract a partner who showers you with love like never before

Plus so much more.

KANYE WEST, T.I WATOSA TUZO ZA BET HIP HOP AWARDS.




Wasanii mahiri wa muziki wa Hip Hop nchini Marekani, Kanye Omari West “Kanye West” na Clifford Joseph Harris “T.I” wameshindwa kuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo za BET Hip Hop Awards ambazo kwa mwaka huu zimefanyika huko Atlanta na kuwashirikisha wakali kibao wakiwemo Jay Z, Rihhana, Ice Cube, Young Jeezy, Drake na wengineo wengi.

Katika sherehe hizo zilizofanyika kwenye ukumbi wa Atlanta Civic Center, Kanye West ambaye alikuwa ameteuliwa kuwania tuzo Tisa, hakufika ukumbini bila ya sababu yoyote, hali iliyopeleka kukosa tuzo hata moja. Kwa upande wa T.I, imefahamika kuwa alishindwa kuhudhuria sherehe hizo na kuwakilishwa na mpenzi wake Tameka "Tiny" Cottle kwa sababu anatumikia kifungo jela huko Arkansas kutokana na kukutwa na hatia ya kumiliki silaha kinyume na sheria.

SHED NO MORE TEARS GENEVIV… USILIE TENA GENEVIV -2

Baada ya vijana wa kihuni kumfanyia kitu mbaya Geneviv,wanaondoka na kumuacha akiwa amepoteza fahamu kutokana na maumivu makali aliyoyapata. Anakuja kuzinduka usiku sana na kujikuta akiwa peke yake porini,palepale chini ya mti.Hawezi hata kusimama kutokana na maumivu makali anayoyahisi…anaamua kulala hapohapo mpaka asubuhi bila kujali kuwa ni porini.
Nyumbani kwao nako baba na mama yake wameyamaliza matatizo yao kiutu uzima,lakini wanaanza tena kulumbana na kila mmoja amechanganyikiwa baada ya kuona muda unazidi kuyoyoma na usiku unaingia huku Geneviv akiwa hafahamiki aliko.
Je nini kitatokea?
Ungana nami,twende sasa…
****
Baada ya kumkosa chumbani kwake, Bi Patricia alirudi na kumpa mumewe taarifa.
“Atakuwa ameenda wapi? Maskini malaika wangu…”
Aliongea mzee Rwakatare akijifanya kumsikitikia mwanae.Kwa kifupi,zile tofauti zilizokuwepo baina ya Bi Patricia na mumewe zilionekana kama zimekwisha kabisa na sasa wote wakawa wanamfikiria binti yao Geneviv.

Muda ulizidi kwenda bila ya Geneviv kurudi nyumbani.Hawakujua yuko wapi na amepatwa na nini.
“Ningekuwa na nguvu ningeenda kumuulizia kwa wenzake,mwanangu hana tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani namna hii! Sijui kapatwa na balaa gani maskini”

aliongea Bi Patricia kwa masikitiko baada ya kuanza kuhisi kuwa huenda mwanae amepatwa na jambo baya baada ya usiku kuzidi kuingia.Mwili wake wote ulikuwa bado una maumivu kutokana na kipigo cha mumewe kiasi cha kumfanya ashindwe hata kutoka nje kwenda kumtafuta mwanae.Saa ya ukutani iliyokuwa mle chumbani ilionyesha kuwa ni tayari saa nne za usiku.
Wasiwasi ulizidi kuwaingia kiasi cha kila mtu kubaki kimya akiwaza kivyake.

“kwani alivyoondoka aliaga anakwenda wapi?”
Mzee Rwakatare aliuliza swali la kijinga kiasi cha kumkumbusha mkewe yaliyotokea asubuhi ya siku ile na kumfanya Geneviv atoroke pale nyumbani bila kuaga.
“Si ujinga wako uliokuwa unaufanya asubuhi,unafikiri mwanao bado mtoto sio, namtaka mwanangu! Amka kamtafute mwanangu…!”
Bi Patricia alianza kucharuka na kumshinikiza mumewe aende kumtafuta Geneviv.Mzee Rwakatare naye hakuweza kutoka nje kwani bado alikuwa na maumivu sehemu ya kichwani baada ya kupigwa na stuli asubuhi.Wakabaki kulaumiana wenyewe kwa wenyewe.Mzee Rwakatare alijihisi kushtakiwa na dhamira yake sana,kwani ukweli aliujua kuwa yeye ndio chanzo cha matatizo na hata kama mwanae angepatwa na jambo baya,basi yeye ndiye aliyemsababishia.Alijikuta akisononeka sana moyoni hasa baada ya kumuona mkewe akizidi kulia kwa kuomboleza.
“Mke wangu jikaze jamani,unavyolia anamchulia mwanetu,atapatwa na matatizo bure,yote tumwachie Mungu”

Mzee Rwakatare alijifanya kuongea kwa busara.Bi Patricia hakuamini kusikia maneno kama yale kutoka kwa mumewe.Ilibidi ainue macho na kumtazama usoni kwa mshangao,alihisi mumewe anamkejeli kwani tangu aachishwe kazi hakuwahi kulitaja jina la Mungu kutoka kinywani mwake zaidi ya matusi ambayo sasa alishaanza kuyazoea.

Waliendelea kutazamana kwa muda mrefu huku kila mmoja akiwa kimya.Masaa yalizidi kuyoyoma na hatimaye saa ya ukutani ikawa inasoma saa sita za usiku. Bi patricia alishindwa kujikaza na akawa anaendelea kulia kwa kilio cha kwikwi.Pia alikuwa akisali kimoyomoyo akimuomba Mungu wake amnusuru mwanae Geneviv.
****
Manyunyu ya mvua yalianza kudondoka huku wingu zito likitanda angani kuashiria mvua kubwa inataka kunyesha.Geneviv alizinduka kutoka usingizini baada ya kuona ameanza kuloana.Aliposhtuka mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa baridi kali ya usiku huku akiwa hajajifunika kitu chochote zaidi ya nguo alizokuwa amezivaa ambazo nazo zilikuwa zimechanwachanwa. Alijaribu tena kuinuka kutoka pale chini na safari hii alifanikiwa kusimama kwani maumivu yalikuwa yamepungua kidogo.Alijaribu kuinua mguu na kupiga hatua lakini akajikuta akishindwa kutembea.
“I must die hard, I need to move out of this place”
(lazima nife kigumu,nahitaji kuondoka mahali hapa)

Alijiambia Geneviv kimoyomoyo wakati akijikaza na kuanza kupiga hatua fupifupi kuelekea barabarani ambako aliamini anaweza kupata msaada.Japokuwa alikuwa akisikia maumivu makali alijitahidi kujikongoja kiupande-upande na akawa anajongea taratibu kuelekea upande iliko barabara. Manyunyu ya mvua yalikuwa yakiongezeka na kuanza kuuloanisha mwili wake mchanga.Kadri manyunyu yalivyokuwa yanaongezeka na kumloanisha ndivyo Geneviv alivyozidi kupata nguvu ya kutembea na kuongeza mwendo. Baada ya kitambo kirefu akawa amefika barabarani.

Hakutaka kupoteza muda zaidi,akaanza kuifuata barabara akiwa haelewi anakoelekea. Hakutamani tena kurudi nyumbani kwao kwani chuki dhidi ya baba yake ilizidi kukua na kumfanya amchukie kama shetani. Akiwa bado anazidi kusonga mbele akielekea asikokujua,aliona mwanga wa taa za gari likija kutokea mbele yake.Hakujua ni gari gani na lilikuwa likielekea wapi ila akapiga moyo konde na kuamua kulisimamisha.

“Haroo afande hebu simamisha ‘Defender’ ,naona kama kuna rimutu rinasimamisha gari,sijui ni rinani na rimetokea wapi usiku wote huu Mura!”

aliongea Koplo Marugu kwa Kiswahili kibovu akimuamuru dereva wake kusimamisha gari.Walikuwa wako katika doria ya usiku pamoja na askari wengine watatu waliokuwa wamekaa nyuma ya gari.

Geneviv aliendelea kulipungia lile gari mikono kwa nguvu zake zote na taratibu akaanza kuliona likipunguza mwendo na kusimama karibu yake.
Liliposimama Geneviv akagundua kuwa lilikuwa ni gari la polisi,alishusha pumzi ndefu na kumshukuru Mungu wake kwani aliamini angekuwa salama mikononi mwa wanausalama wale.Hakutaka kuwaambia ukweli wa kilichomtokea kwani alijisikia vibaya kueleza kuwa amebakwa kwani alihisi ni aibu kubwa kwake.Akaamua kutunga uongo…

Baada ya lile gari kusimama,askari walishuka na kuanza kumhoji ametoka wapi na anakwenda wapi usiku wote ule,ukizingatia yeye ni mtoto wa kike na hapo alipo ni porini.
“Tulikuwa tumetoka shambani na dada,tukavamiwa na watu walioanza kutupiga mpaka wakanichania nguo.Dada alikimbia na kuniacha peke yangu huku.”

Geneviv aliongea uongo mtakatifu huku akitoa machozi na kuwafanya wale askari waamini alichokuwa anakisema.Bila hata kumhoji maswali mengi,walimpakia ndani ya Defender na kuanza kurudi naye mjini ambapo alielezwa kuwa atapewa sehemu ya kulala mpaka asubuhi ambapo ataandikisha maelezo yake kituoni ili watuhumiwa waanze kusakwa.Hakuna hata mmoja aliyehisi kuwa maelezo ya Geneviv ni uongo.

Gari likawashwa na kuanza kurudi mjini.Muda mfupi baadae tayari walikuwa wameshafika kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ambapo Geneviv alikabidhiwa kwa askari wawili wa kiume waliokuwa zamu na wale polisi wengine wakaendelea na doria. Wale askari walimpokea Geneviv na kumuweka kaunta,huku wakijifanya kumuonea huruma. Walimuonyesha sehemu ya kukaa na wao wakaendelea na shughuli zao.

“Haloo afande haka kabinti ni kazuri mno,hebu kaangalie vizuri”
wale askari walikuwa wakinong’onezana kwa sauti ya chini na mara wote wakaanza kumtolea macho Geneviv ambaye alikuwa ameanza kusinzia pale alipokaa na hakuwa na habari kama wale askari wanamtazama kwa macho ya husda.

“Aisee kweli bwana,unajua nilikuwa sijakaangalia vizuri…halafu unajua mke wangu alisafiri wiki ya pili sasa…natamani niwe fataki japo kidogo tu!”

Waliendelea kunong’ona wale askari na wakajikuta wakicheka kwa pamoja na kugongesheana mikono.Kelele za vicheko zilimshtua Geneviv aliyekuwa anasinzia kwenye kiti alichokuwa amekalia.
Mmoja kati ya wale askari aliinuka na kumfuata pale alipokuwa amekaa na kumshika begani.

“Binti naona umechoka sana, pole! amka basi nikakuonyeshe sehemu ya kulala,usiwe na wasiwasi hapa uko mikononi mwa chombo cha dola…tutakulinda mpaka asubuhi”
Aliongea yule askari akimshika mkono Geneviv na kutoka nae nje ya jengo la kituo cha polisi. Geneviv hakuwa na wasiwasi kwani aliamini kazi ya jeshi la polisi ni kuwalinda raia wake. Wakatoka na kuelekea kwenye kibanda kidogo kilichokuwa mita chache pembeni.

****

Hakuna hata mmoja kati ya Mzee Manuel Rwakatare na mkewe Bi Patricia aliyepata hata tone la usingizi. Mpaka inagonga saa nane usiku, Geneviv alikuwa hajarejea nyumbani na hakukuwa na dalili za yeye kurudi. Bi Patricia alikuwa akizidi kulia hali iliyomfanya aanze kuhisi maumivu makali ya kichwa kwani alikuwa bado hajapona. Baada ya kuona mkewe hataki kutulia, ilibidi mzee Rwakatare ajiandae kwenda kutoa taarifa polisi usiku huohuo. Na yeye alionekana kuchanganyikiwa mno, akawa anajilaumu kwa yote aliyoyafanya ambayo ndiyo yaliyopelekea kuibuka kwa tatizo hilo.

Alipiga moyo konde na kujifariji kuwa hakuna binadamu asiyekosea. Baada ya kumaliza kujiandaa alimuaga mkewe ambaye hakumjibu kitu zaidi ya kuendelea kumwaga machozi.Alitoka na safari ya kuelekea kituo kikuu cha polisi cha Blaziniar ikaanza. Ilimbidi abebe mwamvuli kwani mvua nayo ilikuwa imechachamaa kunyesha.Baada ya safari ya takribani dakika arobaini, tayari alishawasili kwenye eneo la kituo cha polisi.

Tangu asimamishwe kazi serikalini,Mzee Rwakatare alikuwa hapendi kabisa kuonekana na polisi kwa kuhofia kukamatwa kwa makosa yake ya uhujumu ambayo bado upelelezi ulikuwa unaendelea, lakini kwa sababu ya mwanae alijikuta hofu ikimuishia. Akawa anapiga hatua za taratibu kusogelea eneo la kituo.

Akiwa hatua chache kabla ya kuufikia mlango mkubwa wa kuingilia kituoni,alisikia sauti ambayo ilimfanya mapigo ya moyo yaanze kumwenda kasi mithili ya injini ya jeti.

Ilikuwa ni sauti ambayo aliitambua vizuri kuwa ni ya mwanae Geneviv ikitokea kwenye kibanda kidogo pembeni ya kituo cha polisi.
Geneviv alikuwa akilalama kwa maumivu makali aliyokuwa anayapata wakati yule askari aliyejifanya kumpeleka kulala akimuingilia kimwili kwa nguvu. Kwa mara nyingine tena, Geneviv alikuwa akibakwa,tena safari hii na Askari polisi.

Mzee Rwakatare hakutaka kuyaamini masikio yake kuwa ile sauti kweli ilikuwa ni ya Geneviv.Ikabidi asogee mpaka karibu ya kile kibanda na kuchungulia ndani kupitia tundu dogo chini ya dirisha.
Hakuyaamini macho yake kwa alichikiona…

“Sh*t, what the hell are you doin with my daughter…im gonna kill you!”
Mzee Rwakatare aliongea kwa hasira kali, na kwa nguvu zake zote aliukanyaga mlango wa kile chumba na kuingia ndani mzima-mzima.

Yule askari alishtuka kuona mlango ukivunjwa na kumharibia starehe yake.Akawa anahangaika kuvaa suruali yake vizuri.
Mzee Rwakatare alimuwahi kwa kipigo kikali cha kushtukiza mpaka yule askari akadondoka chini.Alipotazama pembeni alikiona kipande cha bomba la chuma kilichokuwachini. Alikiokota na kuanza kumuadhibu vikali yule askari kichwani mpaka akazimia.

Kwa haraka alimuinua mwanae Geneviv ambaye bado alikuwa akilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapata huku damu ikimchuruzika kutoka katikati ya miguu yake.Alimuweka begani na akatoka naye kwa spidi ya ajabu na kuanza kukimbia nae kutokomea gizani.

Hakuna askari aliyeelewa kinachoendelea.Mvua nayo ilikuwa ikizidi kupamba moto na sasa zilianza kusikika radi kali zikipiga na kuufanya usiku uzidi kutisha.Mzee Rwakatare hakujali kitu,akawa anazidi kutimua mbio huku Geneviv akiwa begani.
Akiwa umbali wa mita kadhaa,alishtukia kuona anamulikwa na taa za gari lililokuwa likiingia kituo cha polisi. Kwa haraka akamrusha Geneviv chini na yeye akarukia pembeni ya barabara kwenye mtaro.

Kutokana na mvua kubwa iliyokuwa inaendelea kunyesha ikiambatana na ukungu,hakuna mtu yeyote kutoka kwenye lile gari aliyewaona.
Gari ambalo aliligundua kuwa ni la polisi likapita na kuingia pale kituoni.Kwa haraka aliinuka na kumnyanyua mwanae na kumuweka tena begani.Akawa anatimua mbio kurudi nyumbani kwake, safari hii akipitia njia za vichochoroni kukwepa kuonekana tena na polisi.Baada ya kama nusu saa akawa ameshafika nyumbani kwake. Geneviv alikuwa akiendelea kulalama kwa maumivu na hakuelewa kilichofuatia mpaka alipojikuta anaingizwa ndani mwao.

Bi Patricia alishtuka kusikia mlango ukigongwa.
“Nini tena jamani?” Bi Patricia aliuliza kwa sauti iliyokauka kutokana na kulia, na akawa anajikongoja kwa uchovu kwenda kufungua mlango. Alishakata tamaa ya kumuona mwanae Geneviv usiku huo.

“Fungua mke wangu!”
Aliongea mzee Rwakatare kwa sauti iliyomaanisha kuna jambo. Bi Patricia aliharakisha kufungua mlango.
“Ooooh My God!.....”
Bi Patricia alishtuka kupita kiasi.

THE DARKEST HOURS (SAA ZA GIZA TOTORO)- 1

Mtunzi: Hashim Aziz (Hashpower) 0719401968 “Ngo! Ngo! Ngo! Fungua!” “Nanii?” “Fungua!” “Jitambulishe kwanza, wewe nani?” “Nimese...